SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu used za bei rahisi za madaraja ya kati na juu

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

July 6, 2023

Kuna simu za bei kubwa ambazo zilizotoka miaka ya nyuma na kwa sasa hazipatikani zikiwa mpya

Matoleo yake yalikuwa yanalenga watumiaji wanaopenda vitu vya gharama hivyo kuwa na vitu vingi vizuri

Vitu vingine havipo kwenye matoleo ya simu za miaka ya karibuni

Kwenye orodha hii kuna simu kali used za bei rahisi ambazo zilitamba miaka ya nyuma na zinaweza kutumika mpaka sasa bila tatizo

Utafahamu na bei ya kila simu

1- Apple iPhone 11

Simu ya apple iPhone 11 ni simujanja ya mwaka 2019

Ipo kwenye kundi la daraja la kwanza kwa wakati huo iliokuwa inatoka

Pamoja na kuwa ina miaka minne uwezo wa utendaji ni mkubwa

iphone 11

Na pia ina eSim kitu ambacho hakipo kwenye simu nyingi mpya za 2023

Pitia hapa, kujua maana ya esim na ufanyaji kazi wake

Inatumia processor yenye nguvu inayoweza kufungua kwa wepesi gemu nyingi nzito

Processor yake ya Apple A13 Bionic inazizidi simu nyingi za android mpya ikiwemo simu zote mpya za infinix 2023

Hii simu inaweza kupokea mfumo mpya kabisa wa iOS 17 hivyo maisha yake ni marefu

Bei ya iphone 11 used kwa hapa Tanzania ni shilingi 700,000 kwa ya GB 64

2- Apple iPhone 11 Pro

Simu ya Apple iPhone 11 Pro pia ilitoka miaka minne iliyopita

Kiuwezo inashindana na kuzizidi simu nyingi za android toka makampuni mbalimbali za uundaji wa simu

Inatumia chip yenye nguvu pia ya Apple A13 Bionic

iPhone 11 Pro haipitishi maji kama ikizama kwenye kina mpaka cha mita 4 kwa muda wa nusu saa

iphone 11 pro

Imeundwa kwa bodi ngumu inayotumia kioo cha Gorilla

Na pia ina uwezo wa kutumia eSIM

Kioo chake ni aina cha OLED chenye HDR10 na Dolby Vision

HDR10 na Dolby Vision huboresha muonekano wa vitu kwa kuipa skrini uwezo kuonyesha rangi nyingi kwa kila pixel moja ya kioo

Kama ukitazama simu ya Redmi Note 12 ya 2023 huwezi kukuta teknolojia hii

Hivyo bei ya iphone 11 pro used imechangamka kidogo kwani infika shilingi 1,200,000

3- Apple iPhone X

Simu ya iPhone X ni ya mwaka 2017 kwa maana ina miaka zaidi ya mitano tangu itoke

Ni simu ya 4G na yenye water proof kwani inaweza kuzuia maji kupenya kwa muda wa nusu iwapo imezama kwenye kina cha mita 1

Kamera zake zinatoa picha nzuri na zinaweza kurekodi video za 4k kwa fremu 60

iphone x

Yapo matoleo ya daraja la kati ya 2023 yenye kamera ambazo zinarekodi video za full hd pekee bila 4K mfano Tecno Spark 10 Pro

Hii inaifanya iphone x kuwa bado inaendana na teknolojia za sasa pamoja na umri mkubwa

Changamoto yenyewe inapokea toleo la iOS 16 haiwezi kupata iOS 17

Hata iOS 16 ni kama bado mpya maana ilikuja na iPhone 14 Pro Max hivyo uhai wake bado ni mkubwa

Bei ya iPhone X ya GB 256 ni shilingi 650,000 na ya GB 64 inauzwa laki tano

4- Apple iPhone XR

Kiubora iPhone X ni nzuri kuliko Apple iPhone XR iliyotoka mwaka 2018

Hata hivyo iPhone XR bado ni simu nzuri kwa mwaka 2023 ukilinganisha na bei yake na simu zingine za android

Kioo cha XR ni cha IPS LCD chenye resolution ya 828 x 1792 pixels

Ukiangalia ni resolution ndogo

Upande wa memori kuna ya GB 64, 128 na 256 huku RAM yake ikiwa ni GB 3

Kiuhalisia kiwango cha RAM ni kidogo ila processor yake ina nguvu kubwa

Kamera yake ipo moja ambayo kiuwezo kwa simu za sasa inaendana na simu nyingi zenye kamera nzuri za bei rahisi

Bei ya iphone xr used ya GB 64 ni shilingi 550,000

5- Samsung Galaxy S10

Samsung Galaxy S10 ni simu ya 4G ya mwaka 2019

Ni smartphone yenye memori ya GB 128 hadi GB 256 na ya GB 6 AU 8

Ina viwango vya IP68 vinavyoashilia uwezo wa kuzuia maji kuingia ndani ya simu kama ikizama

Kioo chake kina resolution kubwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi kwa usahihi kwani ni cha amoled

samsung galaxy s10

Betri yake ni ndogo kwa viwango vya sasa kwani ina 3400mAh hivyo ukaaji wa chaji sio mkubwa kivile

Kamera zake ni nzuri kutokana na uwepo wa teknolojia kama ya dual pixel pdaf inayofanya simu kulenga kitu kwa ustadi

Pia kamera za galaxy S10 zinarekodi video za 4K, na kioo chake pia kina HDR10+

Kitu kinachofanya muonekano wa vitu kuwa wa uharisia sababu ya usahihi wa kiwango kikubwa cha rangi

Inakuja na toleo la android 9 ila inaweza kupokea mpaka toleo la android 12 pekee

Hii simu  inaizidi Oppo Reno7 ya mwaka 2022

Bei ya Samsung Galaxy S10 used ya GB 128 ni shilingi 600,000

6- Samsung Galaxy S10+

Simu ya Samsung Galaxy S10+ ni ya mwaka 2019 na yenyewe pia

Ina ufanano na galaxy s10 isipokuwa samsung s10 plus ni ndefu na betri yake ni kubwa na ina ubora wa ziada kwenye kamera

Na memori zake zinaenda mpaka 1TB(gb 1000)

Kamera yake inaweza kurekodi video za 4K kwa kutumia hdr10+

samsung galaxy s10+

Uwepo wa HDR10+ inafanya muonekano wa kitu kinachopigwa picha kuwa na uharisia kwa kiwango kikubwa

Fahamu: Maana ya HDR na matumizi yake

Ukubwa wa betri ya samsung galaxy s10+ ni 4100mAh

Simu za madaraja ya kati zinaweza izidi hii simu kwenye kasi ya kuchaji

Kwani kasi ya galaxy s10 plus ni wati 15

Bei ya Samsung Galaxy S10+ used ni shilingi 650,000

7- Samsung Galaxy S10 5G

Samsung Galaxy S10 5g ndio simujanja ya kwanza kuwa na 5G mwaka 2019

Betri yake ni kubwa lenye ujazo wa 4500mAh hivyo ukaaji wa chaji ni mkubwa

Inatumia kioo cha amoled kama ilivyo kwa samsung zingine za bei kubwa

samsung galaxy s10 5g

Kwenye kamera na mambo mengine inaendana na Samsung S10 Plus

Tofauti kubwa ni network kwa maana ina 5G na betri pia ukubwa wa kimo kwa sababu ina inchi 6.7

Bei ya samsung galaxy s10 5g used ni shilingi 650,000

8- Google Pixel 3

Google Pixel 3 ni simu ya mwaka 2018 kutoka kwa kampuni ya Google

Ukubwa wa betri ni 2915mAh hivyo haikai sana na chaji

Pamoja na ukweli kuwa ni simu ya kitambo ila upande wa kamera ina mfumo mzuri

Kamera ipo moja yenye megapixel 12.5 na ina teknolojia ya dual pixel pdaf inayofanya kamera kulenga kitu vizuri hata kikiwa kinakimbia

Hii kamera inaweza kurekodi video za 4K na ina OIS inayotuliza kamera wakati wa kurekodi

Kasi ya chaji ni wati 18

Upande wa memori unaweza ipata ya GB 64 au GB 128

Hii simu inakubali mpaka android 12 ambayo pia inatumiwa na baadhi ya simu za mwaka 2023

Bei ya Google Pixel 3 used kwa sasa ni shilingi 285,000, ni bei ukizingatia simu za google pixel huwa na kamera nzuri

9- Google Pixel 3a

Simu ya Google Pixel 3a ilitoka mwaka 2019 baada yaa pixel 3

Ni simu inayotumia kioo chenye ufanisi wa kuonyesha vitu kwa rangi sahihi

Hii inatokana na kioo chake kuwa cha OLED ambacho kina resolution ya 1080 x 2220 pixels

Betri yake na yenyewe sio kubwa kwani ina 3000mAh hivyo ukaaji wa chaji sio wa kiwango kikubwa

Utendaji wake ni wastani kwa sababu chip inayotumia ni Snapdragon 670

Ila ina toleo la aina moja tu upande wa memori ambayo  ni GB 64

Hata Google Pixel 3a inazidiwa ubora na mtangulizi wake pixel 3

Bei ya Google Pixel 3a used ni shilingi 265,000

10- Google Pixel 4

Simu ya Google Pixel 4 ni simu iliyoingia sokoni mnamo mwaka 2019

Ni simu ya 4G ambayo kwenye kioo imewekewa kioo kigumu cha Gorilla Glass 5

Ina viwango vya IP68 vinavyoonyesha uwezo wa simu kuzia maji kupenya ndani ya simu kama ikizama

Skrini ni ya oled yenye refresh rate ya 90Hz hivyo unapotashi simu inafanya vitu kwa haraka

google pixel 4

Kwa mara ya kwanza simu inakuja na android 10 ila inapokea Android 13 ambayo ndio toleo jipya zaidi kwa sasa

Upande wa memori kuna matoleo mawili ya GB 64 na 128 na RAM ya GB 6

Simu ina kamera mbili na zinaweza kurekodi video za 4K

Hivi ni vitu vichache ambavyo baadhi ya simu mpya za samsung hazina

Kwa sasa bei ya Google Pixel 4 used yenye GB 64 ni shilingi 400,000

Hitimisho

Kununua simu mpya kuna changamoto zake na unapaswa uzitilie maanani

Ubora wa simu used zozote bila kujali bei sio sawa na simu ikiwa mpya

Hivyo kuna uwezekano ukanunua bidhaa itakayokuja kukusumbua kama hufahamu namna ya kuchunguza

Ni vizuri ukauliza au kama huwezi matoleo mengi ya daraja la kati yanaweza kukupa vitu ambavyo vipo kwenye hizi simu za zamani za tabaka la juu

 

Maoni 3 kuhusu “Simu used za bei rahisi za madaraja ya kati na juu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram