SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Oppo Reno7 na Sifa Muhimu 2023

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 27, 2023

Oppo Reno7 ni simu ya mwaka 2022 yenye mambo mengi ambayo yanaipa ubora unaendana na simu mpya za 2023

Kwa mfano simu ya Tecno Spark 10 Pro ya 2023 inaachwa nyuma na hii simu kwenye baadhi ya vitu.

oppo reno 7 showcase

Hivyo basi bei ya oppo reno7 bado ni kubwa na inazidi laki saba kwa hapa Tanzania

Fuatilia sifa zake zote muhimu utambue ubora wake ambao unaweza kukuvutia kuimiliki hii oppo ya 2022

Bei ya Oppo Reno7 ya GB 128

Reno7 yenye RAM ya GB 8 na ukubwa wa memori wa GB 128 inauzwa shilingi 850,000/=

Bei yake inaizidi simu ya iPhone 7 plus ikiwa used japo kiutendaji iphone ina nguvu kiasi

Hata Oppo inakuja ne teknolojia nyingi ambazo huwezi kuzikuta kwenye matoleo ya simu za zamani

Kuanzia kioo mpaka kamera na hata uimara wa simu kudumu kipindi kirefu, reno7 iko mbele

Kiwango cha bei kinaipelekea hii oppo kuwa mshindani wa Tecno Camon 19

Sifa za Simu ya Oppo Reno7

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 680 4G
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.4 GHz Kryo 265 Gold
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.9 GHz Kryo 265 Silver
  • GPU-Adreno 610
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 12
  • ColorOS 12.1
Memori UFS 2.2, 256GB,128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(MICROSCOPE)
  3. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 850,000/=

Upi ubora wa Oppo Reno8

Kama unajua kuzitafsiri vitu vilivyopo kwenye jedwari, tayari utakuwa ushaelewa maeneo ambayo yana ubora mkubwa kwenye hii simu

Moja wapo ni uwezo wa kupeleka chaji kwa kasi kubwa kitu kinachokupunguzia muda wa kuisubiria simu kujaa

Ina mfumo wa memori wenye kasi kubwa ya kusafirisha data

Kamera zake zinatoa picha zenye ubora

Pia kamera zake zinaweza kukipiga kitu kidogo na kuonekana kikubwa

Inatumia kioo chenye mgawanyiko mpana wa rangi hivyo rangi za vitu vingi vitaonekana kwa uhalisia wake

Uwezo wa Network

Simu inasapoti mpaka mtandao wa 4G

Haina teknolojia 5G japokuwa ni simu ambayo imetoka mwaka 2022

Kwa simu ambazo zilikuwa zinauzwa bei hiyo nyingi huwa zinasapoti mtandao wa 5G

Mfano wa simu hiyo ni Redmi Note 11 5G Pro+

Aina ya 4G ya hii oppo ni LTE Cat 13 ambayo kasi yake ya juu kabisa kwenye kupakua ni 390Mbps sawa na 48MBps

Hii ina maana kama mtandao wa simu unatoa kasi hii ya 4G basi simu inaweza kudownload app ya whatsapp kwa sekunde mbili tu.

Kasi hii kwa hapa Tanzania unaweza kuipata kwenye mtandao wa faiba na kwa gharama

Ila kwa mitandao ya simu za mikononi ni ngumu

Ubora wa kioo cha Oppo Reno7

Reno7 ina kioo cha AMOLED ambavyo huwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Kioo chake kina resolution kubwa ya 1080 x 2400 pixels

Yaani kama unatazama picha na video kwenye mitandao ya kijamii muonekano wa vitu unakuwa na ustadi mzuri

Kioo pia kina refresh rate inayofika 90Hz hivyo unapotachi kioo simu inakuwa nyepesi

oppo reno7 display

Reno7 inaruhusu kuzima refresh rate ya 90Hz maana ikiwa kubwa na matumizi ya chaji yanaongezeka pia

Kiwango cha juu cha unagavu wa hiki kioo ni 800 nits

Ina maana kuwa kioo kitaonyesha vitu kwa uwazi na vizuri ukiwa unaitumia simu kwenye jua

Unajua kuwa ukiwa juani skrini huwa hainekani vizuri kama uangavu wa kioo cha simu ni mdogo

Kitu utakachokikosa kwenye kioo cha reno7 ni HDR10 au Dolby Vision

Nguvu ya processor Snapdragon 680 4G

Chip ya Snapdragon 680 4G ni chip ya daraja la kati hivyo nguvu ya utendaji wa simu ni ya wastani

Simu haiwezi sumbua kuwa nzito hata kama mafaili yamejaa kwa sababu processor yake ina muundo wenye core kama Cortex A73(Kryo 265 Gold)

Uzuri wa hii chip ina ulaji mdogo wa chaji ambao unachangiwa kuwa na utendaji wa kiwango cha kati

Kwenye uchezaji wa magemu itakulazimu useti resolution ndogo ya graphics(picha za gemu) ili ucheze vizuri na kupunguza simu kupata moto mara kwa mara

Magemu makubwa mengi yanacheza vizuri kwenye hii simu kwa kiwango cha 58fps kwenye resolution ndogo

Tofauti na hapo ni ngumu kupata fremu nyingi

Hii processor ina sehemu(core) zingine zipatazo nne ambazo ni kwa ajili

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya oppo reno7 ina kasi ya wati 33

Ni kiwango kikubwa cha umeme na simu inajaa chini ya masaa mawili

Kwenye majaribio ya GSMArena, betri ya reno7 ilichuukua dakika 70 tu kujaa kutoka 0% mpaka 100%

Kwa mtu mwenye haraka hatosubiri muda mrefu

oppo reno7 chaji

Pamoja na kwamba kiwango cha betri sio kikubwa (4500mAh) ukilinganisha na simu ya redmi note 10;;;, reno7 inakaa na chaji masaa mengi zaidi

Ukiwa unatumia intaneti muda wote simu inachukua masaa 16 mpaka chaji kuisha

Na ukiwa unacheza magemu wakati wote, betri inachukua masaa 11 mpaka kuisha chaji

Ukubwa na aina ya memori

Upande wa memori kuna matoleo mawili ya Oppo Reno7 na yote yana GB 8

Kuna yenye ukubwa wa GB 128 na GB 256 ambazo zinatofautiana bei

Hata hivyo hiki ni kiwango kikubwa kwa watumiaji wengi ila kwa mtumiaji sana wa simu hiki ni kiwango kidogo

Kwa maana utalazimika kuongeza memori kadi kwani inayo sehemu ya memori kadi

Aina ya memori simu inayotumia ni UFS 2.2 ambayo ina njia mbili na kila njia inaweza kusafirisha data mpaka 1200MBps

Ni ngumu kukuta simu inakuwa nzito sababu ya kujaa mafaili

Uimara wa bodi ya Oppo Reno7

Uzuri wa simu nyingi za oppo ni kuwekea ulinzi wa kuzuia angalau vumbi na maji ya kiwango cha kunyunyiza

Kwani ina viwango vya IPX4, ila haifai kuizamisha kwenye maji haina uwezo wa kuzuia maji kupenya kama ikizama

Upande wa mbele simu imewekewa skrini protekta ya kioo cha Gorilla 5

Kioo cha gorilla 5 kinaweza kuzuia mpasuko kama simu ikianguka kwa kimo cha mita 1.5

oppo reno7 body

Hata hivyo unapaswa kuwa makini japo gorilla inakuhakikishia ulinzi

Hii simu ina fingerprint kwenye kioo sio upande wa nyuma

Fingerprint yake iko fasta pamoja na kuwa kwenye skrini kuna kioo kigumu

Ubora wa kamera

Oppo Reno7 ina kamera tatu aina ya wide, microscope na depth sensor

Ila kiuhalisia ni kamera mbili tu ndio zinapiga picha kamera ya depth sio kwa ajili ya kupiga picha

Kamera ya microscope yenye 2MP imeundwa kwa ajili ya kupiga picha vitu ambavyo ni vidogo sana kama sisimizi

Hii kamera inakikuza hiko kitu na kuonekana kikubwa

oppo reno7 kamera

Kamera kuu ina upigaji wa picha mzuri ila kuna kukolea kwa rangi usiondana na muonekano halisi

Kama mtu mwenye rangi nyeusi kama ilivyo kwa waafrika wengi kamera inamg’arisha

Kwa watu wa mitandao wanaopost picha instagram hii inaweza kuwafaa zaidi

Upande wa video simu inaweza kurekodi video za full hd pekee yake kwa fremu 30

Kamera ina gyro-EIS inayomaanisha utulivu wakati wa kurekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Oppo Reno7 inakuja na Android 12 pamoja na CorolOs 12.1

ColorOS 12.1 inakupa uwezo wa kubadirisha muonekano wa picha(icon) za app

Pia inakupa uwezo wa kubadirisha kiwango cha refresh rate kutoka 90Hz kwenda 60Hz na kinyume chake

oppo reno 7 software

Kingine ni kuwa simu inapokea updates za mfumo wa ColorOS mara kwa mara

Hii inakuhakikishia kuwa utaendelea kupata maboresho ya app mbalimbali kwa muda mrefu

Washindani wa Oppo Reno7

Bei ya Oppo Reno7 inaweza kuleta utata hasa unapokuja kufahamu matoleo mengine yanayouzwa kwa bei hiyo

Matoleo ambayo yanaweza kuipa hii simu changamoto ni Redmi Note 11 Pro+ 5G, Redmi Note 10, Realme 9 Pro+, Samsung Galaxy A53 5G

Ukianza na samsung kwanza ina 5G na ni simu yenye nguvu kubwa kiutendaji na haipitishi maji simu ikiiingia kwenye maji

Ukija kwa Redmi Note 11 Pro+ 5G ina kioo kikali cha amoled na HDR10 na refresh rate 120Hz pia kamera inayoweza kurekodi video mpaka za 4K

Mbaya zaidi redmi inapatikana kwa chini ya laki nane kwa mwaka 2023

Upande wa Realme 9 Pro+ inaendana kidogo na Reno7 ila Realme ni nzuri zaidi hasa upande wa kamera na utendaji na ina 5G vilevile

Realme 9 Pro+ na yenyewe inauzwa laki nane na nusu

Neno la Mwisho

Kama washindani wa hii simu hawakuvutii basi oppo reno7 bei yake itakuvuta kuimiliki

Ni simu inayokuhakikishia maisha marefu ya betri na ukaaji wa chaji wa muda kwa utendaji wa wastani

Kwa mtumiaji wa simu mwenye matumizi ya wastani oppo reno 7 ni chaguo zuri

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram