SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Spark 10 Pro na Ubora Wake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 27, 2023

Iwapo bajeti ya kununua simu aina za iphone au matoleo ya samsung s23 ni ndogo basi kuna Tecno Spark 10 Pro

Tecno Spark 10 Pro ni tecno mpya ya mwaka 2023 inayokuja na kamera tatu

tecno spark 10 pro showcase

Ni simu ya daraja la kati hivyo bei ya tecno spark 10 pro haiwezi kuzidi laki nne na nusu

Simu ina sifa nzuri kwenye baadhi lakini pia ina kasoro kadhaa kama ilivyofafanuliwa kwenye hii post

Fuatilia mwanzo mwisho

Bei ya Tecno Spark 10 Pro ya GB 128

Kwa Tanzania, tecno spark 10 pro ya GB 128 inauzwa shilingi 415,000/=

Bei inaonekana ni kubwa kwa anayetarajia simu za laki mbili, ila kumbuka hii ni simu ya daraja la kati’

Ina sifa nyingi zinazojitofautisha na simu za bei ndogo sana

tecno spark 10 pro summary

Kuanzia kamera na display(kioo) cha hii simu ni vya kuridhisha

Kuna vitu vya msingi unapaswa kuvielewa ili ujue iwapo tecno spark 10 pro inastahili kuuzwa bei iliyotajwa ama la

Na utaweza kuelewa kwa kuangalia sifa zote spark 10 pro

Sifa za Tecno Spark 10 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G88
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 13
  • HIOS 12.6
Memori eMMC 5.1, 256GB,128GB na RAM 8GB,
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 415,000/=

Upi ubora wa Tecno Spark 10 Pro

Simu inakuja na kioo chenye refresh rate kubwa ambavyo huwa ni vizuri kwa ajili ya magemu

Betri yake ina ukubwa unaoweza kukaa na chaji masaa mengi

Ni simu ndefu hivyo vitu vinaonekana kwa ukubwa

Inakuja na sehemu kuweka earphone tofauti na matoleo ya sasa ambayo huondoa kipengele hiko

Pamoja na simu kuwa na memori kubwa ila ina sehemu ya kuongeza memori kadi

Ina utendaji wa kuridhisha kutokana na aina ya processor iliyotumika kuwa na nguvu

Kuna nyanja pia simu imepungukiwa ubora ila haishangazi kutokana na aina ya wateja inayowalenga

Uwezo wa Network

Spark 10 Pro inakuja na network ya 4G bila kuwa na 5G

Kwa Tanzania 4G imesambaa maeneo mengi kuliko teknolojia ya 5G

Ni hivi karibuni Tigo na Vodacom wameleta kizazi hiki kipya cha network

Aina ya 4G iliyopo kwenye simu ni LTE Cat 7

tecno spark 10 pro network

Kasi ya kupakua faili ya LTE Cat 7 inafika 300Mbps

Yaani kama unadownload app ya TikTok yenye MB 86 basi app itamalizika kuwekwa kwenye simu ndani ya sekunde tatu tu.

Japo kwa nchini si rahisi kupata kiwango hiki ila kama intanet ya starlink ingekuwepo hiyo spidi ingeweza kupatikana

Kwa 5G ya Tigo na Voda hiyo ni spidi ya kawaida kuipata

Ubora wa kioo cha Tecno Spark 10 Pro

Kioo cha Tecno spark 10 pro ni aina ya IPS LCD chenye resolution ya 1080 x 2460 pixels

Resolution yenye pixels kama hizo huitwa FHD+ (full hd plus)

Kwa sifa za kioo ni kizuri na picha zinaokana zikiwa safi japokuwa hakina HDR10 ama Dolb Vision

HDR10 na Dolb Vision huboresha muonekano wa vitu na kufanya rangi zake zionekane kama zilivyo kwenye mazingira halisi kwa kiasi kikubwa

tecno spark 10 display

Changamoto kubwa ya vioo vya LCD  na kutokuonyesha rangi nyeusi halisi

Na ukoleaji wake wa rangi unazidiwa sana na vioo vya AMOLED

Unaweza kuliona kama ukilinganisha muonekano kwenye kioo cha Samsung Galaxy A54 5g

Ila isikushangaze sana kwani Spark 10 pro ina bei ndogo hivyo baadhi vitu lazima viwe vya kawaida

Nguvu ya processor MediaTek Helio G88

MediaTek Helio G88 ni chip yenye uwezo wa kati katika utendaji

Ndiyo iliyopo kwenye tecno spark 10 pro

Imegawanyika katika sehemu mbili ambapo sehemu yenye nguvu sana ina core mbili inayoweza fanya mizunguko bilioni mbili kwa sekunde

tecno spark 10 pro processor

Na inatumia core aina ya Cortex A75 na ile sehemu yenye nguvu ndogo zinatumia Cortex A55

Hii inacheza gemu nyingi bila shida ila kuna baadhi ya magemu simu inahitaji kupunguza resolution

Mfano wa gemu hizo ni Genish Impact yenye GB 20 kwa processor ya Helio G88 inacheza kwa settings za chini

Yote kwa yote ni kuwa Mediatek helio g88 inaifanya simu kuweza kufungua app yoyote bila shida

Uwezo wa betri na chaji

Kutokana na simu kutumia chip yenye nguvu ya wastani na betri kuwa kubwa ya 5000mAh ukaaji wake wa chaji ni wa kuridhisha pia

Kikawaida simu za 5000mAh zina uwezo wa kudumu na chaji kwa kipindi cha masaa yanazidi 13

Chaji ya Tecno Spark 10 Pro ina kasi ya wati 18

tecno spark 10 pro charge

Ni kasi ya wastani hivyo betri yenye ukubwa wa 5000mAh inaweza chukua muda kidogo kujaa

Kuna simu zenye chaji ya wati 30 na huwa zinajaza betri ya kiwango hiko kwa lisaa

Kwa viwango vya chaji za siku hizi wati 18 ni kiwango cha wastani na si fast chaji

Ukubwa na aina ya memori

Tecno spark 10 pro ina matoleo mawili kwenye upande wa memori na zote zinakuja na GB 8 ya RAM

Aina ya memori simu inayotumia ni eMMC 5.1

Hizi ni memori za zamani na kasi ya usafirishaji wa data si mkubwa kama memori za UFS

Simu hii inakuja na sehemu ya kuongeza memori card kama simu ikiwa imejaa na haitoshi

Uimara wa bodi ya Tecno Spark 10 Pro

Bodi ya Tecno Spark 10 Pro ina glassi upande wa nyuma ila sio vioo vya gorilla

Na kwenye screen imewekwa protekta ya plastiki

Hii simu haina uwezo wa kuzuia maji kama ikidumbukia kwenye kina kikubwa

tecno spark 10 pro

Ni tofauti na simu za samsung galaxy s23

Kikawaida simu zisizopitisha maji huwa zina bei kubwa inayozidi milioni

Hii simu inaweza pia kukaa muda mrefu bila kuharibika sababu ya kuwa na kioo upande wa nyuma

Hata hivyo ni muhimu kuweka kava kuepuka uharibifu unaweza tokea ghafla

Ubora wa kamera

Kamera za Tecno Spark 10 Pro zipo tatu ambapo mbili hazijaainishwa ni za aina gani

Kwa maana haijaelezwa kama ni kamera za kupiga eneo pana au ni vitu ambavyo vipo mbali sana

Kwa baadhi ya video za youtube kuhusu hii simu ni kuwa haina kamera za ultrawide wala telephoto

Kamera yake kuu yenye 50MP inapiga picha zenye wa kawaida sana na ubora hafifu kwenye mwanga mdogo

tecno spark 10 pro kamera

Nyakati za usiku noises (chengachenga) zinaweza kuonekana kwa uwazi

Kamera inapiga video za full hd pekee kwani haipigi video za resolution kubwa zaidi za 4K

Hii inachangiwa na ufinyu wa utendaji wa processor yake kutokuwa na uwezo wa kuchakata video za aina hiyo

Wakati wa kurekodi video huku ukitembea itakulazimu kuwa makini

Kwani simu haina OIS ya kutuliza mitikisiko

Ubora wa Software ya HiOS 12.5

Tecno Spark 10 Pro inakuja na mfumo endeshi wa Android 13 na HiOS 12.5

HiOS 12.5 inakupa chagua la kuonheza ukubwa wa ram

Android ni mfumo endeshi unaotumia sana RAM na kuna app huwa zinatumia ram nyingi

tecno spark 10 pro virtual ram

Kulitambua simu za siku hizi zinatoa uwezakaono wa kutumia sehemu ya memori ya simu kama ram

HiOS 12.5 inaweza kupokea simu moja kwa moja pindi unapoweka sikioni

Sio lazima kubofya kitufe cha kupokelea simu

Yapi Madhaifu ya Tecno Spark 10 Pro

Chaji yake haina kasi kubwa

Mfumo wake wa kamera si wa kuvutia na haina aina zingine muhimu za kamera

Inatumia mfumo wa memori wenye kasi ndogo ya kusoma na kuandika data

Kioo chake hakina HDR

Neno la Mwisho

Tecno Spark 10 Pro ina bei shindani ila hii bei inaenda moja kwa moja kwenye ushindani na simu aina ya Redmi Note 10

Ukikaa na kuringanisha hizi simu utagundua kuwa Spark 10 pro inaachwa mbali sana

Ila redmi note 10 ni toleo la mwaka 2021, kwa mpenzi wa matoleo mapya anaweza kuchagua hii tecno mpya ya 2023

Maoni 32 kuhusu “Bei ya Tecno Spark 10 Pro na Ubora Wake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

tecno camon premier 30

Ubora wa simu za Tecno Camon 30 na bei zake(Pro, Premier)

Tangu mwezi wa nne kampuni ya walitoa matoleo ya Tecno Camon 30 Matoleo ya Camon 30 yapo matatu ambayo ni ya daraja la kati yaani mid range Ubora wa kiujumla […]

tecno camon 30 thumb

Bei ya Tecno Camon 30 Pro na Sifa Muhimu

Simu ya Tecno Camon 30 Pro ilitangazwa mwezi februari ila imetoka rasmi mwezi wa nne 2024 Ni simu ya daraja la kati(midrange) hivyo bei yake sio sawa na Tecno matoleo […]

tecno camon 30 premier thumbnail

Bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G na Sifa zake muhimu

Kwenye matoleo bora ya simu kutoka Tecno, matoleo ya Tecno Camon huja na ubora katika vipengele vingi Hata bei za matoleo ya Camon huzizidi bei za Tecno Spark na Tecno […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company