SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Android ni nini na Ifahamu Android 13

Android/iOS

Sihaba Mikole

March 13, 2023

Android ni mfumo endeshi(yaani operating system) wa simu ambao uko chini ya usimamizi wa kampuni ya Google

Mfumo endeshi (Operating System) ni software(mfano applikesheni) unaosimamia vifaa vifaa vya simu au kompyuta kiingereza hutambulika kama hardware na appliksheni.

Appliksheni inapotaka kufanya kazi inapita kwenye mfumo endeshi kisha mfumo endeshi unaipa appliksheni huduma inayohitaji

Kwa mfano ukifungua app ya kamera ni mfumo endeshi (OS) ndio utakaounganisha applikesheni  na kamera

Mfumo endeshi wa android una matoleo mengi yanayofahamika kama Android Versions ambayo yamefika 13

Na toleo jipya kabisa ni Android 14 inayotazimiwa kuachiwa rasmi muda wowote mwaka huu 2023

Kwa hapa tunaenda kuitazama vitu vilivyopo kwenye android 13

Ijue Android 13

Android 13 ni operating system iliyotoka mwezi wa nane mwaka 2022

Simu za mwanzo kupokea android 13 zilikuwa ni simu za pixel ambazo hutengenezwa na google

Mfumo huu una vitu vya ziada na mabadiliko yanayofika 15

Mabadiliko haya yamegawanyika kwenye usalama, maboresho ya kimuonekano na matumizi rahisi ya simu

Hakuna mabadiliko makubwa sana ila mabadiliko machache yana upekee na kuongeza uhuru wa matumizi ya simu

Baadhi ya simu ambazo zina Android 13 ni samsung galaxy s23 Ultra na Google Pixel 7 Pro

Baadi ya vitu vilivyoongezwa ni kama ifuatavyo.

Notification lazima ziombe ruhusa ya mtumiaji

Kwenye matoleo ya zamani appliksheni za simu zilikuwa zinatoa notification bila ruhusa yako

Iwapo appliksheni nyingi zinafanya hivi inakuwa kero kwa kiasi kikubwa

Na kwa baadhi ya simu unakuwa unashangaa notification ni nyingi na hujui zimekujajew

Google kwenye Android 13 kila app inayotaka kutuma ujumbe kwa njia ya notification lazima ipate ridhaa ya mtumiaji

Maana yake utaweza kuzuia app ambazo hutaki zitume notification na zile unazotaka

Hii inapunguza usumbufu

Ruhusa ya kuruhusu app kutuma nofication inakuja pindi unapoipakuwa app kutoka play store

Ukiifungua tu ujumbe wenye machaguo mawili utakuja na kukutaka kuchagua “Allow” au “Don’t Allow”

Kuchagua Lugha Yoyote kwenye app Husika

Matoleo ya Android kabla ya Android 13 yalikuwa yanatumia lugha uliyoichagua kabla kwenye kila app

Yaani kwenye settings kuna sehemu ya kuchagua lugha kama ukichagua English basi english inatumika kwenye kila app

Mabadiliko yamefanywa kwenye toleo la 13 ambapo utaweza lugha mbalimbali kwa kila app

Kwa mfano kama unataka app ya Chrome iwe na settings za kiswahili pekee basi hivi sasa unaweza kufanya hivyo bila kuathiri mpabngilio wa lugha kwenye app zingine

Ili kubadirisha lugha ya app husika unachatakiwa kufanya ni kwenda kwenye settings na kisha chagua apps

Itakuja orodha ya app zote zinazopatikana kwenye simu

Utabonyeza app unaoitaka kisha unaenda sehemu ya “Language” na kuchagua lugha unayopendelea itumiwe na app hiyo

Kukufahamisha app zinazofanya kazi bila mtumiaji kuziona (Background apps)

Kuna apps huwa zinafunguka pasipo wewe kujua kuwa app imefunguka

App ikifunguka kwa mtindo huu inaitwa background app mfano mzuri ni app za mijandao ya kijamii instagram

Hizi huwa zinafunguka mara nyingi hata kama huitumii na ndio maana huwa zinatuma notification mara kwa mara

Background huchangia matumizi makubwa ya betri

Pitia: Simu kupata moto sana na jinis ya kuzuia

Android 13 itakujulisha apps ambazo zipo “active”

Na hivyo utaweza kuifunga, hii ni njia moja wapo ya kudhibiti appiksheni zinazotrack mawasiliano na data zako pasipo wewe kujua

Ulinzi wa data zinazokopiwa umeongezwa

Unapokopi maandishi kwenye simu za android taarifa huwa zinaifadhiwa kwanza kwenye kitu kinaitwa Clipboard

Clipboard inasaidia kuhamisha taarifa kutoka app moja kwenda nyingine

Kitendo hiki kinaipa nafasi app mbalimbali kupata hizo data

Hivyo kuna changamoto ya kiusalama inaibuka

Inakuwaje app zenye ambazo zinazamilia kuiba password yako zikifanya hivyo?

Android 13 imeboresha Clipboard kwa kuipa uwezo wa kuondoa taarifa “automatically” baada ya muda fulani baada ya kuwa umeshatumia

Hii inaepusha app zinazotumia mwanya huo kuchukua taarifa pasipo ridhaa yako

Muonekano mpya wa app ya audio

App ya kusikiliza mziki na vitu vingine una muonekano unaokujulisha kwa haraka urefu wa windo ambao tayari ushasikiliza

Kwenye mstari unaonyesha muda (urefu wa audio) husika kuna muonekano wa mawimbi kwenye kipande ambacho umeshasikiliza

Itakusaidia kujua kwa haraka kujua urefu uliobaki

Lakini ni muonekano unaovutia na kukufanya kutazama simu muda wote

Kitufe cha settings kimeamishwa upande wa chini

Kikawaida ukitaka kwenda settings njia ya haraka ni kubonyeza kitufe cha settings ambacho huwa kipo juu

Kwa sehemu ndefu kama Tecno Phantom X2 Pro inaweza ikawa kero kiasi fulani

Android 13 imerahisisha kufikia kitufe cha settings

Uki-swipe simu kutoka juu kitufe hiki kinaenda chini kabisa

Unakuwa unakifikia kwa haraka na urahisi

Kwa simu zenye inchi nyingi huu ni msaada mkubwa

Simu yako inaweza pata Android 13?

Sio simu zote zinazopata matoleo mapya ya Android

Simu za madaraja ya juu huwa yanapokea maboresho ya Android kila yanapotoka

Kwa simu za bei ndogo huwa zinakumbana na changamoto ya kupata mfumo endeshi mpya

Kikawaida watengeneza simu hawazitilii maanani sana simu za daraja la chini

Zipo njia mbadala ambazo zinaweza saidia mtumiaji kupata toleo lolote la android

Njia hizo zinahusisha kuweka ROM (hapa panahitajika utaalamu) vinginevyo utalazimika kununua simu mpya

Hitimisho

Pamoja na android 13 kuja baada ya Android 12 ila hakuna tofauti kubwa sana kati ya mifumo miwili

Tofauti ambazo zimekuwa zinakuja ni zile zinazohusisha maboresho ya kiusalama zaidi

Kadri muda unavyokwenda android inazidi kuwa na ulinzi madhubuti dhidi ya app ambazo si salama

 

 

Maoni 2 kuhusu “Android ni nini na Ifahamu Android 13

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram