SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sababu na Jinsi ya Kudhibiti Simu Kupata Moto Sana

Miongozo

Sihaba Mikole

February 20, 2023

Umeshawahi kujikuta unatumia simu ila inakuwa ya moto hata kwa kazi ndogo

Unaweza ukajiuliza kwa nini

Kuna vitu vingi vinavyosababisha simu kupata moto ambavyo huna budi kuvifahamu

Kwani simu kuwa joto jingi muda mrefu kunaathiri utendaji wa simu na betri inaweza kufa

Hivyo hapa kuna maelezo yanayofafanua jinsi simu inavyopata moto na jinsi ya suluhisho zake

Hizi ni baadhi

Kutumia apps nyingi wakati mmoja

App zikiwa nyingi zinatumika wakati mmoja zinakuwa zinatumia moto mwingi wa betri

Na hivyo inailazimisha mfumo wa simu nzima kutumia nguvu kubwa

Kitu kinachopelekea kuongezeka kwa joto

Moja ya app ambayo inakamua sana betri ni kivinjari cha Google Chrome

Kudhibiti tatizo hili ni kufunga baadhi ya apps ambazo huzitumii wakati huo

Zifunge zote na utumie ile yenye umuhimu

Betri ya bovu

Mara nyingi betri  bovu hupata joto sana hata kwa app isiyohitaji nguvu kubwa

Kama una simu inayowahi kuisha chaji  kwa haraka na kupata joto haraka kuna uwezekano kuwa betri yake ni mbovu

Kupata uhakika kuna apps ambazo zinaonyesha afya ya betri

App nzuri kabisa ni AccuBattery

Hii app itakuonyesha afya betri yako na uwezo wake wa sasa

Kama unamiliki simu yenye betri 5000mAh app itakuonyesha kiwango kilichopungua

Iwapo upunguaji ni wa kiwango kikubwa basi betri ni bovu na ndio inasbabisha joto kwenye simu

Hivyo huna budi kutafuta betri jingine na ubadirishe

Mfumo wa simu kuji-update

Wakati mwingine mfumo endeshi mfano Android unaweza ukawa unafanya maboresho yaani upgrading

Upgrading huwa inakuja na vitu vingi

Vitu ambavyo vitakuwa vinawekwa kwenye simu

Uwekaji ambao utailazimisha simu kufanya kazi kubwa

Unaweza kwenda kwenye settings kisha kutafuta update na kuizima

Kama update ni ya muhimu basi vumilia kwa muda mfupi simu imalize huo mchakato

Uwepo wa Virusi(Malware)

Malware kwenye simu mara huwa inalenga kuchota data zako ama kuharibu simu

Ila siku hizi virusi huwa zinalenga kuchota data zako bila wewe kujua ama kuweka matangazo mengi kwenye simu

Unaweza kujikuta kila wakati “notification” za matangazo zinatokea mara kwa mara

Virusi huwa zinajaribu kutuma data kila wakati hata kama intaneti ikiwa imezimwa

Kitendo cha app aina ya aina hiyo inailazimisha simu kufanya kazi kubwa na kusababisha matumizi makubwa ya betri na hivyo simu kuanza kupata moto

Ili kudhibiti app ya namna hiyo, inakupasa uguse sehemu ya settings kisha utafute sehemu ya betri na ubonyeze

Ukibonyeza utaona kiwango cha matumizi ya betri na app zinazotumia na app zinazokula moto sana

Ukiona app ambayo huifahamu kuna uwezekano kuwa hiyo app ni kirusi

Baadhi ya kufunguka bila wewe  kujua

Baadhi ya app huwa zinajufungua pasipo wewe kuona hii inaitwa “opening in background”

Mfano wa app hizo ni whatsapp, instagram, chrome, tiktok na nyingine

Iwapo app nyingi zinajifungua kwa muundo huo basi simu inaweza pata moto

Hivyo huna budi kupunguza app ambazo zitakazokuwa zinajungua zenyewe

Ili kufanya hivyo unaenda kwenye settings kisha sehemu ya app halafu unachgua app unazotaka kuzifunga

Kutumia simu maeneo ya joto sana

Ukiwa unatumia simu kwenye eneo lenye joto sana mfano juani inafanya simu kuchemka

Joto jingi hufanya kila kitu kupata cha simu kupata moto

Na kadri unavyoitumia simu kwenye mazingira na ndivyo simu inavyozidi kuchemka

Ni si vizuri kuitumia simu kwenye jua kali

Suluhisho la tatizo hili ni kupunguza kuitumia simu kwenye mazingira hayo

Mwanga mwingi wa Screen

Moja ya kitu kinachokamua sana ni kioo cha simu hasa kikiwa kina resolution kubwa

Na pia kuweka mwanga wa kioo mpaka mwisho kunasababisha kutumika kiasi kikubwa cha betri

Hivyo inasababisha simu itumie nguvu kubwa kufanya kazi

Kiwango kikubwa cha mwanga kunaonheza joto

Joto linalosababisha simu nzima kuchemka

Hivyo unapopata tatizo la simu kuchemka jaribu kupunguza mwanga wa simu

Aina ya Processor ya Simu

Baadho ya simu kupata moto kunasabishwa na uwezo wa processor yenyewe

Watengenezaji wanaweza kuwa hawakiunda chip vizuri au uwezo wa chip si mkubwa

Hivyo simu inaweza kuwa inapata shida hata kwa kazi ndogo

Processor yenye nguvu ndogo hulazimika kufanya kazi kubwa kwa app ya aina yoyote hasa magemu

Huna budi kujua nguvu ya simu yako

Na hivyo uanze kupunguza matumizi ya simu hasa yale ambayo yanatumia nguvu kubwa

Kutumia chaji isiyo sahihi

Kila simu ina muundo wake saketi kwa ajili ya kupeleka

Baadhi ya simu zimeundwa kupokea chaji inayopeleka taratibu tu

Hivyo ukiweka chaji yenye kasi sana na mfumo wa simu ukawa hauna uwezo wa kupunguza kiwango cha umeme wa chaji basi itaenda kuharibu betri kwa kadri utakavyokuwa unachaji

Na betri ikiwa mbovu basi simu itaanza kuwa inapata moto

Ni vizuri ukazingitia matumizi ya chaji sahihi ili kuepuka uharibifu wa simu

 

Maoni 16 kuhusu “Sababu na Jinsi ya Kudhibiti Simu Kupata Moto Sana

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram