SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu zenye Kamera Nzuri za Bei Rahisi (2023)

Miongozo

Sihaba Mikole

February 11, 2023

Hakuna kitu kigumu kama kupata simu yenye kamera kali kwa bei ndogo

Ukifuatilia simu zenye kamera nzuri utagundua kuwa zinauzwa kwa bei kubwa

Kiasi cha kwamba ni watu wachache wanaweza kumudu kuwa nazo kwa hapa Tanzania

Hapa imeorodheshwa orodha ya simu zenye nzuri na zinazouzwa kwa bei rahisi

Ubora wa picha wa hizi simu zilizopo si mkubwa ila ni ubora unaotoa picha ama video za kuweleweka.

Samsung Galaxy A23 5G

Samsung Galaxy A23 5G ni simu yenye kamera nne aina ya lenzi za wide, ultrawide, macro na depth

Hii ina maana kuwa Galaxy A23 inaweza kupiga picha eneo pana sana

Kamera kubwa ina ukubwa wa megapixel 50 huku ikiwa imewekewa OIS na ulengaji wa PDAF

OIS inaifanya simu kutulia wakati wa kurekodi video na ulengaji PDAF inaifanya kamera kulenga kitu kwa ustadi na picha kuwa “sharp”

Ila kamera zilizobaki zina megapixel ndogo na hazijaekewa teknolojia za ziada

Kamera zake pia hazina HDR ambazo husaidia kurekebisha muonekano wa vitu hasa maeneo yanapaswa kuonekana kiza na mwanga

Ubora wa picha wa wakati wa mchana ni wa kuridhisha sana

Na kwenye mwanga mdogo kamera inajitahidi kuonesha vitu na kwa kasoro ndogo sana

Bei ya Samsung Galaxy A23 5G ya GB 128 ni shilingi 640,000/=

Samsung Galaxy A14 5G

Hii ni simu yenye kamera tatu ambazo ni wide ina 50MP, Macro yenye 2MP na Depth pia ina 2MP

Macro na Depth huwa hazina umuhimu kihivyo

Hii simu inatumia ulengaji wa PDAF hivyo ina utambuaji wa haraka wa vitu vinaavyostahili kupigwa picha kinapotokea mbele ya kamera

Uwezo wa simu kurekodi video ni wa Full HD na haiwezi rekodi video za 4K

Wakati wa kurekodi utalazimika kutuliza mkono kwa sababu simu haina OIS

Pia kamera zake zina uwezo wa kukusanya mwanga wa kutosha

Hivyo kwenye mwanga hafifu kamera inapiga picha vizuri

Bei ya Samsung Galaxy A14 5G kwa sasa ni 470,000/=

Google Pixel 4

Google Pixel 4 ni simu ya mwaka 2019 yenye kamera mbili tu

Kamera hizo ni wide (kamera kuu) na kamera kwa ajili ya kupiga vitu vya mbali yaani Telephoto

Kamera zote zina resolution ya megapixel 12

Kamera zake zote ni nzuri kwani zinaweza kurekodi video za 4K na zina HDR (High Dynamic Range)

Kwa hiyo kamera za hii simu zina uwezo wa kutofautisha kiza(rangi nyeusi) na mwanga(nyeupe)

Kwenye ulengaji inatumia teknolojia ya juu zaidi aina ya dual pixel PDAF ambayo iko na kasi kubwa kukilenga kitu

Tembele hapa, kuangalia ubora wa picha wa kamera ya google pixel 4

Kwenye mazingira ya mwanga hafifu na mwanga mwingi muonekano wa vitu unaonekana kama yalivyo kwenye mazingira halisi

Bei ya pixel 4 kwa sasa ni 450,000/= na nyingi utakayopata ni used kwani ni miaka minne sasa tangu imetoka

Redmi Note 10

Simu ya Redmi Note 10 ni simu ya mwaka 2021 yenye kamera zipatazo nne

Kamera hizo ni ultrawide, wide, macro na depth huku wide ikiwa na lenzi ya 50MP

Hii simu ina ulengaji PDAF na pia ina HDR kitu kinachotoa uhakika wa kupata picha nzuri

Kwa bahati mbaya kamera zake hazina OIS

Ubora wa kamera ya hii simu ni kuwa inaweza kurekodi video kwa 30fps

Pia ina uwezo wa kukusanya mwanga mwingi kitu inachoiboresha simu kupiga vizuri kwenye mwanga mdogo

Bei ya Redmi Note 10 kwa sasa haizidi 400,000/= bei yake imeshuka sana

Realme 10

Realme 10 ina kamera mbili ila kiuhalisia ni kamera mbili kwa sababu depth huwa haipigi picha

Kamera kubwa ina ukubwa wa megapixel 50 na ina PDAF hivyo swala la ulengaji hakuna shida

Pia ina ukusanyaji wa mwanga wa kiwango kikubwa na lenzi yake ni kubwa.

Kwenye ubora wa picha, Realme 10 iko vizuri

Inapiga picha bila chengachenga wakati wa mchana ila nyakati za usiku ni changamoto

Chengachenga zinaonekana kwa uwazi kama ukiikuza picha

Haina uwezo wa kurekodi video za 4K na haina OIS kwa ajili kuchukua video kwa utulivu

Bei ya Realme 10 ni shilingi 480,000 za Tanzania

Infinix Note 12i

Infinix Note 12i ni simu ya kamera tatu ila ni kamera moja tu ndio inayopiga picha vizuri

Kamera mbili zingine zina resolution ndogo sana

Kamera yenye ubora unaotakiwa imewekewa PDAF lakini inakosa OIS

Uwezo wa kurekodi video ni wa aina moja pekee ambao Full HD PLus

FHD+ inaonyesha picha nzuri

Na pia kamera za hii simu ina HDR, hivyo uboreshaji wa muonekano wa vitu upo

Bei ya Infinix Note 12i ni shilingi 430,000/=

Japokuwa inaachwa mbali sana na infinix yenye kamera nzuri, ila infinix yenye kamera kali gharama

OnePlus 6t

Simu ya OnePlus 6t ni simu ya daraja la juu ya mwaka 2018 ambayo ina kamera mbili

Kamera za oneplus 6t ni za kiwango kikubwa

Kwa mfano kamera aina ya WIDE(kamera kubwa) ina megapixel 16 na ina OIS na PDAF

Tundu la kupitisha mwanga lina upana wa f/1.7 kwa maana kamera inaweza kukusanya mwanga wa kutosha

Inaweza kurekodi video za 4K na ina HDR bila kusahahu teknolojia ya kuongeza utulivu kwa ajili ya kurekodi video aina gyro-EIS

Simu inatoa kamera iliyokolea rangi kiasi fulani wakati wa mchana

Bei ya OnePlus 6t kwa sasa ni shilingi 480,000/=

Uzuri ni kuwa simu hii inaweza kupokea toleo la Android 11

Redmi Note 11

Unaweza ukadhani simu ya Redmi Note 11 ina kamera nzuri zaidi ya Redmi Note 11 ila sivyo ndivyo

Redmi Note 11 kamera yake inaachwa na mtangulizi wake

Hii simu ina jumla ya kamera nne ila kamera mbili tu ndio za msingi

Redmi Note 11 inaweza kurekodi video za full hd na haina OIS

Kwenye ulengaji simu inatumia teknolojia ya PDAF kama zilivyo simu nyingi zilizopo

Wakati wa mchana kamera inapiga vizuri na rangi za vitu vinaendana na uhalisia

Nyakati za usiku kamera haitoi picha za kuvutia kwani chengachenga zinaweza kuonekana iwapo ukiikuza picha

Bei ya Redmi Note 11 kwa mwaka 2023 ni shilingi 380,000/=

Pia pitia: Ubora wa simu ya Redmi Note 11 Pro+ 5G

Vivo Y22

Vivo Y22 inaweza ikawa ndio simu yenye kamera ya kawaida sana kwenye hii orodha

Ni simu ya mwaka 2022 yenye idadi ya kamera tatu ila moja ndio yenye ubora sahihi

Kwani ina megapixel 50 na ulengaji wa PDAF

Ila ni simu yenye kamera inayokosa teknolojia ya HDR

Hii inamaanisha kwenye giza simu inaweza kupata shida kutoa picha nzuri

Ila kwenye mwanga mwingi ubora wa picha ni wa kuridhisha

Bei ya Vivo Y22 ni shilingi 400,000/=

Google Pixel 3 XL

Linapokuja idara ya camera, simu za google Pixel lazima uzifikirie hata kama imetoka miaka mingi ya nyuma

Google Pixel 3 XL ni simu ya mwaka 2018 yenye kamera moja tu ambayo ni matata sana

Kamera ya hii simu ina teknolojia ya juu ya ulengaji aina ya dual pixel pdaf

Huwa iko fasta kuliko PDAF

Ina uwezo wa kurekodi wa video za 4K na pia ina OIS

Kwa hiyo kunakuwa na utulivu wakati wa kuchukua video

Bei ya sasa ya Google Pixel 3 XL ni shilingi 330,000/=

Lakini kwa wakati huu utapata simu used hivyo umakini unahitajika

Maoni 5 kuhusu “Simu zenye Kamera Nzuri za Bei Rahisi (2023)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram