SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A54 5G na Upekee Wake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 17, 2023

Samsung wameendelea kuachia matoleo mapya kwa mwaka 2023 kwenye upande wa matoleo ya A-Series

Toleo mojawapo ni Samsung Galaxy A54 5G yenye Android 13

Hii ni simu ya daraja la kati kitu kitakochasababisha simu kuwa na bei iliyochangamka kiasi

Kwa masoko ya ulaya ya ulaya bei ya Samsung Galaxy A54 5G inazidi shilingi milioni moja kutegemeana na ukubwa wa memori

Ubora wake unashawishi kwa kiwango kikubwa kuinunua kwa bei tajwa

Bei ya Samsung Galaxy A54 ya GB 128

Tangu kuzinduliwa mwezi machi bei yake ya GB 128 inaanzia shilingi 1,300,000/=

Kwa Tanzania kuna uwezekano bei ikaongezeka kidogo

Ukiangalia aina ya screen, memori, chip, bluetooth na vifaa vingine utagundua kuwa ni simu tofauti sana na Samsung Galaxy A04

Ila kuna sifa zinazoendana kwa kiasi fulani na simu ya Samsung Galaxy Z Fold 4 hivyo bei yake haiwezi kuwa nafuu

Pitia sifa zote zilizoainishwa humu kufahamu ubora wake kiufasaha

Sifa za Samsung Galaxy A54 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 1380
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.4 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G68 MP5
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
  • One UI 5.1
Memori 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
Muundo Urefu-6.4inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 1,300,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy A54

Galaxy A54 ina kioo kizuri kwenye uoneshaji wa vitu kwa usahihi

Ina utendaji unaoweza kufungua applikesheni yoyote bila kukwama

Inakuja na chaji yenye kujaza simu kwa haraka

Ina toleo la jipya la android na inaweza kupokea toleo jipya

Maji hayawezi kupenya kwenye hii simu kwa urahisi

Betri yake ni kubwa hivyo kuna uhakika wa simu kustahimili muda mrefu kwenye ukaaji wa chaji

Uwezo wa Network

Samsung Galaxy A54 ni simu ya daraja la kati yenye 5G

Inakubali aina zote za 5G ikiwemo mmWave ambayo hutumika sana kwa USA

Kitendo cha simu kuwa na uwezo wa kupokea mmWave inamaanisha kasi yake ni kubwa kwenye mtandao

Kwa sasa hutakiwi kuwanza kuhusu mtandao, 5G ya Tigo inaweza kufika mpaka 1Gbps ni tofauti na ile ya Vodacom

Na upande wa 4G  simu inasapoti LTE Cat 18 kwa maana kama kuna mtandao wenye kasi ya 3790Mbps basi inaweza kuchakata kiwango hiko cha data

Ila kiuhalisia hii ni kasi ya 5G

Kama hupendelei kuwa na laini za simu, Galaxy A54 inaweza kufanya bila kuwa na laini

Hii inatokana na kuwezeshwa kwa eSIM(embedid SIM) ambayo haihitaji laini zile za plastiki kabisa

Airtel wameanzisha huu mfumo hapa Tanzania

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A54

Galaxy A54 ina kioo cha Super Amoled

Vioo  vya amoled huwa havitegemei mwanga wa taa bali ni vioo vinavyozalisha mwanga wenyewe

Kitendo hiki hufanya amoled kuzalisha rangi nyeusi halisi tofauti na vioo vya IPS LCD

Faida ya vioo hivi ni kuwa na uwezo wa kuzalisha rangi nyingi zinaweza fika bilioni

Kitendo cha kuwa na rangi nyingi huchangia rangi za vitu kuonekana kwa rangi halisi na kukolea vizuri

Ndio maana huwa ni vioo vyenye bei

Na pia resolution yake ni full hd+ na kikiwa na refresh rate ya 120Hz

Hivyo simu inakuwa nyepesi wakati wa kutachi

Nguvu ya processor Exynos 1380

Kitu chochote ambacho simu inakifanya huwa kinachakatwa na processor

Processor ikiwa na nguvu ndio utendaji wa simu unakuwa mkubwa

Samsung inatumia chip ya Exynos 1380 ambayo imegawanyika katika sehemu

Kila sehemu ina idadi ya core(sehemu za processor) nne

Kuna core zenye nguvu sana kwa ajili ya kufanya kazi kubwa na zile zenye nguvu ndogo

Core zenye nguvu kubwa zinatumia muundo wa Cortex A78 na zile ndogo ni Cortex A55

Cortex A78 inaweza kufanya mizunguko zaidi ya bilioni tatu na kila mzunguko ukwa unachakata kazi 4 kwa sekunde

Huu utendaji unaifanya simu kuweza kucheza kia aina ya gemu ama kutumia applikesheni nyingi kwa wakati mmoja pasipokuwa na tatizo

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya galaxy a54 5g ni 5000mAh

Huu ni ujazo unaofanya simu kukaa muda mrefu na chaji

Chaji yake inakuja na kasi ya wati 25 hivyo betri hii kubwa itajazwa kwa haraka bila tatizo

Lakini ukaaji wa chaji unategemea sana  na aina ya matumizi

Ila kwenye simu zingine za samsung zenye 25W, ujazaji wa chaji ni wa kiwango kidogo ukilinganisha na simu zenye wati 33 au wati 120

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili ya Samsung Galaxy A54 5G linapokuja swala la memori

Kuna zenye GB 128 na pia zile zenye GB 256

Simu za bei ya juu siku hizi huwa haziji na sehemu ya kuweka memori ya ziada

Ila simu hii inakuja nayo

Hivyo memori kama ikijaa utaweza kuongeza memori kadi kuhifadhi mafaili zaidi

GB 128 sio memori kubwa sana kama unapakuwa na kurekodi sana video

Simu inaweza kujaa ndani ya muda mfupi

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A54

Bodi yake haiwezi kupitisha maji kama simu ikidumbukia kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu saa

Simu ina viwango vya IP67 vinavyooshiria kuwa maji na vumbi haviwezi kupenya ndani

Kuwa na bodi ngumu ya namna inasaidia simu kukaa muda mrefu

Na ni msaada mkubwa kwa ambaye ana shughuli zinazomfanya ashinde sana kwenye mvua

Ubora wa kamera

Simu ina kamera tatu zinawezoweza kupiga picha kwenye eneo pana sana na kitu cha karibu

Kamera kuu ina ukubwa wa 50MP ambayo ina OIS na ulengaji wa PDAF

OIS husaidia utulivu wakati wa kurekodi video huku ukiwa unatembea

Inafanya video kutokutikisika tikisika

PDAF hufanya kamera kukitambua kitu kinachopigwa kwa haraka japo inazidiwa na dual pixel pdaf

Hii simu inaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa kiwango cha 30fps

Ubora wa Software

Ukiinunua ikiwa mpya kabisa utakutana na Android 13 na mfumo wa One UI 5.1

One UI 5.1 ni mfumo mwepesi na hauji na matangazo kama  baadhi ya mifumo mingine

One UI 5.1 ina kitu kinaitwa image clipper

Image Clipper inakuwezesha kukikopi kitu chochote kutoka kwenye picha na kukitengenezea picha nyingine

Kwa mfano umepiga picha nyuma ya gari na gari ikatokea

Kama unataka picha ya gari kutoka kwenye picha uliyoipiga basi hapo utatumia hiyo image clipper

Kuna mengi unawe yapata, pitia hapa

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A54

Mfumo wake wa kamera si wa kuvutia sana ukilinganisha na simu za samsung galaxy s23

Simu haina sehemu ya kuweka earphone kama ilivyo kawaida ya simu za siku hizi

Hivyo mbadala ni kutumia earphone za bluetooth

Na kwa wapenzi wa redio pia hii simu inaweza isiwafae kwa sababu haina redio

Neno la Mwisho

Wale ambao wana mfuko ulionona hii ni moja ya simu ya kuwa nayo

Japokuwa bei yake inaingia kwenye ushindani na simu za xiaomi 13 pro na OPPO Reno 5G

Ila bei yake inaendana na ubora wake kwa kiasi kikubwa

 

Maoni 6 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy A54 5G na Upekee Wake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram