SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy Z Fold 4 na Ubora wake kiundani

Sifa za simu

Sihaba Mikole

March 7, 2023

Kwa miaka ya karibuni baadhi ya makampuni ya simu yamekuwa yakiachia simu za kujikunja yaani Fold

Simu hizi ukikunjua upana wa screen unaongezeka na ukikunja upana unakuwa wa simu ya kawaida

Na inakuwa na screen mbili, mbele na ndani

samsung fold 4 thumbnail

Moja ya simu hiyo ni Samsung Galaxy Z Fold 4 ya mwaka 2022

Simu za kujikunj(Fold) a huwa zinakuwa na gharama kubwa bila kujali kampuni

Mfano bei ya samsung galaxy z fold 4 inazidi milioni tatu kutegemeana na ukubwa wa memori

Bei ya samsung galaxy z fold 4 ya gb 512

Galaxy Z Fold ya Gb 512 na RAM GB inaenda shilingi 3,500,000/=

Kwa baadhi ya wauzaji wa Tanzania bei inaweza kuwa kubwa zaidi

Muundo wasimu unachangia bei kuwa kubwa Sana

samsung fold 4 summary

Kwa mfano, upande wa vioo kuna display mbili amabapo vioo vyote ni vya AMOLED

Vioo vya AMOLED vinatengezwa kwa gharama za juu.

Sasa ukijumlisha na sifa zingine zote utagundua kuwa sio rahisi kuipata hii kwa bei ndogo.

Sifa za Samsung Galaxy Z Fold 4

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8+ Gen 1
  • Core Zenye nguvu sana(1) – 1×3.19 GHz Cortex-X2
  • Core Zenye Nguvu(3)-3×2.75 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.80 GHz Cortex-A510
  • GPU-Adreno 730
Display(Kioo) Foldable Dynamic Amoled 2x, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12L
  • One UI 5.1
Memori UFS 3.1, 256GB,512GB,1TB na RAM 12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 10MP(Telephoto)
Muundo Urefu-7.6inchi
Chaji na Betri
  • 4400mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 3,500,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy Z Fold 4

Hii ni simu yenye utendaji wenye nguvu kutokana nakutmia processor yenye nguvu

Simu Ina kupa uhuru kutokana na kuwa na screen kubwa inayoweza kufanya kazi nyingi yaani multtask

Kwa maana unaweza kutumia apps nyingi kwa wakati mmoja

Ina vioo viwili kimoja Cha kujikunja na chingine Cha kawaida

Ni simu nzuri kwa wanaopenda kusoma vitabu kutokana na upana wake

Uwezo wa Network

Samsung Galaxy Z Fold 4 Ina uwezo wa kutumia mtandao wa 5G

Hii inamaanisha 3g na 4g pia inaweza kufanya kazi

Inakubali masafa yote ya 5G ikiwemo Yale yenye mask Sana aina ya mmWave

samsung fold 4 network

Kwenye eneo lenye minara ya mmWave simu inaweza kupakua mafaili kwa Kasi inayozidi 1gbps

Kwa bahati mbaya kwa Tanzania kuna mtandao mmoja tu wenye 5g kwa maeneo machache.

Na 5G iliyopo ni ya Masafa ya kati, inawezekana mbeleni mambo yakabadilika

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy Z Fold 4

Galaxy Z Fold 4 inatumia kioo Cha dynamic Amoled chenye resolution ya 1812 x 2176 pixels

Na pia kina refresh rate inayofika 120Hz kitu kinachofanya kioo kuwa na unyororo flani wakati wa kutachi bass ukiwa unaperuzi vitu mfano meseji

Ubora mwingine ni kioo kuwa na HDR10+ hii ni teknolojia inayotengeneza utofauti sahihi kati ya sehemu yenye mwanga mkubwa na sehemu zenye kiza

samsung fold 4 display

Hii inahakikisha muonekano wa vitu unaendana na jinsi vinavyoonekana kwenye mazingira halisi

Refresh rate ikiwa kubwa kunakuwa na matumzi makubwa ya betri

Lakini kioo Cha hii simu hakitumii refresh kubwa muda wote

samsung galaxy fold 4 display

Maana kuna kazi zingine zinaitaji kiwango kidogo Cha refresh rate

Hivyo ni kioo chenye urahisi katika matumzi ya chaji

Nguvu ya processor Snapdragon 8+ Gen 1

Snapdragon 8+ Gen 1 ndio processor inayoiwezesha Samsung Galaxy Z Fold 4 kufanya kazi zake

Hii ni processor yenye core ambazo zimegawanyika sehemu tatu

Kuna sehemu moja yenye nguvu sana ambalo hufanya kazi pale simu inapofungua vitu vingi Sana au ukiwa unacheza gemu

Magemu hutumika nguvu kubwa ndio maana huhitaji core yenye nguvu sana

snapdragon-8+-gen-1-infographics

Core hiyo yenye nguvu kubwa zaidi kwenye hii simu huitwa Cortex X2 na Kasi yake inafima 3.19GHz yaani mizunguko bilioni tatu na zaidi kwa sekunde

Ndio maana gemu la Call of Duty Mobile inacheza kwa 60fps kwa graphics zenye resolution kubwa Sana yaani ultra

Hii inamaanisha simu haiwezi kuganda Ganda unapocheza magemu mazito

Uwezo wa betri na chaji

Kutokana na ukubwa wa simu unaweza ukazani betri yake itakuwa kubwa lakini la hasha.

Betri yake Ina ukubwa wa wastani wa 4400mAh

Lakini itakushangaza kuwa hii ni moja ya simu yenye utendaji wenye nguvu unaokaa na chaji muda mrefu

Hii simu inaweza kukaa na chaji takribani masaa 15 ikiwa kwenye intaneti muda wote mfululizo.

samsung fold 4 chaji

Chaji yake Ina Kasi ya wastani ila inaweza kujaza betri kwa haraka kwa sababu betri lenyewe sio kubwa sana

Kwa mujibu wa data za GSMArena, Samsung Galaxy Z Fold 4 inajaa kwa asilimia 50 kwa muda wa nusu saw

Hii inamaanisha kuwa simu  inaweza kujaza kwa 100% ndani ya dakika 120

Kumbuka kuwa chaji yake ni ya watu 25 tu

Ukubwa na aina ya memori

Unapotaka kujua simu yenye utendaji mkubwa basi aina ya memori ni mambo la muhimu kulijua.

Fold 4 inatumia memori za UFS 3.1 ambazo huwa Zina Kasi Sana japo si kama UFS 4

Kwa memori hii, simu itakuwa inafungua app kwa haraka, inawahi kuwaka na mafaili yanakopika kwa muda mfupi

Kuna matoleo matatu ya hii simu upande wa memori na zote Zina RAM ya GB 12

Kuna Z Fold 4 ya GB 256, 512 hadi 1TB

Na Haina sehemu ya ziada ya kuweka memori

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy Z Fold 4

Pamoja na kuwa hii ni simu ya kujikunja ila simujanja isiyopitisha maji

Kwani Ina viwango vya IPX8 inayomaanisha kuwa maji hayawezi kuingia kama itaingia kwenye maji ya kina Cha MITA 1.5 kwa muda wa nusu saa

samsung fold 4 body

Pia simu imewekewa kioo Cha gorilla victus+ ni vioo ambavyo vimetengenezwa kuhimili mipasuka na michubuko

Kiujumla Galaxy z fold 4 ni simu ngumu na inaweza kudumu miaka mingi hats ukaja kuiuza kwa bei rafiki ikiwa imeshatumika

Ubora wa kamera

Hii ni simu yenye kamera zipatazo tatu

Kamera zake zinakuwezesha kupiga picha eneo Pana Sana na kukiliga picha kitu ambacho kitu kilicho mbali Sana

Ubora wa picha ni mkubwa kwa nyakati zote

samsung fold 4 camera

Na uhalisia wa rangi ni WA kiwango sahihi, sehemu yenye kivuli inaokana vizuri bila kuathiriwa na mwanga mwingi wa just

Kamera zake zinaoa picha bila chengachenga ikiwa unachukua picha nyakati za usiku

samsung fold 4 photo quality

Vitu vinatokea kwa ustadi na hata kurekodi video simu inatumia kutokana na uwezo wa OIS

OIS hutuliza kamera kama ukiwa unarekodi video Hulu ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Samsung Galaxy Z Fold 4 inatumia android 12l na mfumo wa One UI 5.1

Vitu vingi vinapatikana kwenye hii simu ila Cha kuvutia ni jinsi mfumo unavyoweza kutumia vizuri upana wa kioo.

Mfumo wa simu unaruhusu kutumia app zaidi ya moja tofauti na tablet nyingi

samsung fold 4 software

Kwa maana unaweza kuweka YouTube upande wa kushoto na upande wa kulia unachati

Kitendo hiki kinaitwa multitasking

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy

Hii simu Ina mapungufu machache kama vile kutokuwa na sehemu ya memori, redio na sehemu ya earphone

Hata matoleo ya simu hizi ya bei ya juu hayaji na hivyo vitu

Ikiwa unahitaji kuwa navyo gharama ya ziada lazima ilipwe

Neno la Mwisho

Samsung Galaxy Z Fold 4 ni simu ya mwaka 2022 ila ni toleo Kali hata kwa mwaka 2023

Changamoto kubwa ni bei ila kwa anaependa kitu kizuri hii ni moja ya simu ya kuwa navyo kwa mwaka huu.

Wazo moja kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy Z Fold 4 na Ubora wake kiundani

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram