SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 13, 2024

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa

Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa

Ndio maana bei ya Samsung Galaxy A15 ya GB 128 ni shilingi laki nne na nusu kama kima cha juu kabisa

samsung a15 showcase

Kwenye eneo lenye ubora mkubwa zaidiĀ  ni upande wa kioo

Japo sifa zingine zipo zenye ila skrini yake ni nzuri zaidi kama utakavyoona

Sifa za Samsung Galaxy A15

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G99
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6
Memori 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB,4GB
Kamera Kamera TATU

  1. 50MP,AF(wide)
  2. 5MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 450,000/=

Uwezo wa Network

Hii ni simu ya 4G haiji na uwezo wa mtandao wa 5G na haisapoti eSIM

Kuna Galaxy A15 yenye laini moja na nyingine zinakubali laini mbili

4G yake inakubali mitandao yote ya simu hapa Tanzania

Aina ya 4G yake ni LTE Cat 13 ambayo kasi yake ya kupakua faili mtandaoni inaweza fika 650 iwapo mtandao wa simu unasapoti kasi hii ya 4G

Kasi hii inaweza kudownload vitu kwa sekunde chache hata mafaili makubwa hayachukui muda kumalizika

Hata hivyo sio rahisi kupata kasi ya 4G ya kiwango kikubwa hiki kwa sehemu kubwa hapa Tanzania

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A15

Samsung Galaxy A15 inatumia kioo cha Super Amoled chenye resolution ya 1080 x 2340 pixels

Resolution kubwa kwenye kioo cha super amoled kinaongeza uwezo wa kioo kuonyesha vitu kwa ufanisi

Kioo cha hii simu kama kioo cha Samsung Galaxy A55

samsung a15 display

Kwani chenyewe kinakosa HDR10+ ambayo huboresha muonekano wa vitu

Ila utapata refresh rate inayofika 90Hz ambayo ni kubwa

Hii inafanya kioo kuwa fasta unapokuwa unatachi

Nguvu ya processor Mediatek Helio G99

Mediatek helio G99 ndio chip inayotumika katika kufanya kazi mbalimbali kwenye hii simu

Ina core mbili zenye muundo wa Cortex A76 yenye mizunguko 2.2GHz

Hii speed 2.2GHz inaweza kufikiwa iwapo simu inafanya kanzi nzito sana kama kucheza gemu

samsung a15 processor

Ila mara nyingi ni nadra app za simu za kawaida kufika kiwango hiko

Kiujumla utendaji wa Mediatek helio G99 ni wa kuridhisha

Yaani hata gemu zinazotumia nguvu kubwa zinacheza kwa graphics zenye resolution kubwa

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya hii simu ina ukubwa wa 5000mAh

Ukaaaji wa chaji wa Galaxy A15 ni mkubwa kwani kwa mchangachiko wa matumizi inaweza chukua masaa karibu 15

Kwenye kuperuzi intaneti ukaaji wa chaji unatumia karibu masaa 12

Ila magemu yanakula chaji kwa kiwango kikubwa kwani smu inachukua masaa 7 tu mpaka kuisha

samsung a15 charge

Hii simu inasapoti chaji yenye kupeleka umeme wa wati 25

Na unapoichaji hii simu na chaji ya wati 25, simu inajaa ndani ya dakika 81

Huu ni muda mdogo kwa kiasi fulani, japo siku hizi kuna chaji zinajaza betri kwa dakika 17 tu

Ukubwa na aina ya memori

Siku hizi simu nyingi za daraja la kati huja na memori za ukubwa wa GB 128 kwenda mbele

Hivyo hata Samsung Galaxy A15 zipo za GB 128 na GB 256

Mgawanyo wa RAM ni GB 4, 6 na 8

Kiushauri RAM ndogo haifai kwa mtumiaji anayefanya vitu kwenye simu kwa wakati mmoja

Kwa mfano ukiwa unacheza gemu kama ya Dream Soccer ram inajaa nyingi kwa haraka

Hivyo inapelekea simu kuganda ganda

Hivyo basi chukua yenye RAM kubwa kama bajeti yako inaruhusu

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A15

Bodi ya Samsung Galaxy A15 imeundwa kwa plastiki haina kioo nyuma wala mbele

Hii simu haina waterproof, kwani hakuna kiwango chochote cha IP kilichoainishwa

samsung galaxy a15 bodi

Ikizama kwenye maji uwezekano wa simu kuathirika ni mkubwa kama hujaiwahi

Kwa hiyo ni lazima kuwa makini unapokuwa na simu kwenye mazingira ya mvua au maeneo yanye maji

Na pia ni muhimu kuweka

Ubora wa kamera

Ubora wa kamera wa Galaxy A15 ni wa kawaida sio mkubwa kama Galaxy A55

Kwa mfano ubora wa picha nyakati za usiku yaani kwenye mwanga mdogo unaathiriwa na kiwango kikubwa cha chengachenga(noise)

Ila kwenye mwanga mwingi muonekano niĀ  mzuri japo sio kiivyo

samsung a15 camera

Kamera ya hii simu haiwezi kurekodi video za 4K bali inarekodi video za full hd pekee kwa kiwango cha 30fps

Pia inakosa teknolojia ya OIS, inabidi kutuliza mkono sana wakati ukirekodi huku ukiwa unatembea

Tembelea hapa kuona picha zilizopigwa na Samsung Galaxy A15

Ubora wa Software

Samsung Galaxy A15 inakuja na toleo la Android 14 na One UI 6

Hii ina uhakika wa kupata matoleo mapya ya android kwa kipidi cha miaka mitatu

Kwa maana hiyo Galaxy A15 itapata hadi Android 17

samsung a15 software

Simu inapopata maboresho ya namna hii kwa inaongeza maisha ya simu kutumika muda mrefu

Na pia inaimarisha usalama na pia kupata vitu vipya ambavyo havipo kwenye matoleo ya nyuma

Washindani wa Samsung Galaxy A15

Kama ilivyo ada washindani wakubwa wa Samsung ni simu za kampuni kutika china

Siku hizi kampuni za china pia zinatengeneza simu nzuri za madaraja ya kati

Simu ya kwanza ni Redmi Note 13 ambayo inapatikana kwa laki nne aliexpress

Kioo cha Redmi Note 13 ni kizuri na chaji yake ina kasi kubwa

Pia kuna simu za iQOO na zenyewe zipo za bei ndogo ya hii zenye kuendana kisifa

Kwa bei ya Samsung Galaxy A15 inatoa fursa kwa muhitaji wa simu kuona machaguo mengi mbadala

Neno la Mwisho

Simu ya Samsung Galaxy A15 ni ya bei nafuu yenye ubora wa ziada unaokosekana kwenye matoleo ya Samsung A05

Angalau hii simu ina baadhi ya vitu vya S24 kwa bei nafuu

Kwa wahitaji wa simu wanaotaka kujaribu simu mpya yenye kutoa matoleo mapya ya Android kwa muda mrefu basi hili ni moja ya Chaguo sahihi

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram