SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 12, 2024

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati

Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na nusu

Hii ikiwa na ukubwa wa GB 128, yenye GB 256 bei yake inazidi hapo

samsung a55

Nini hasa cha kipekee na thamani vinavyopatikana kwenye Galaxy A55

Ubora wa hii simu umejikita hasa kwenye utendaji, ubora wa kamera na kioo kizuri

Utaelewa kiundani ukifuatilia vipengele vyote vilivyofafanuliwa hapa kwa kutazama pia sifa zake

Sifa za Samsung Galaxy A55

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 1480
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.75 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Xclipse 530
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6.1
Memori  256GB,128GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera TATU

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 1,150,000/=

Uwezo wa network

Samsung Galaxy A55 inasapoti laini za eSIM ambazo zinaruhusu kushika network ya mtandao bila kuwa na laini zile za plastiki

Pia hii ni samsung ya 5G ambayo inasapoti aina zote tatu za 5G

Kwa mkazi wa baadhi ya maeneo ya Dar na Dodoma, mtandao wa 5G unapatikana kwa laini za Airtel, Tigo na Vodacom

Chaguo ni lako

Upande wa 4G simu inasapoti 4G aina ya LTE Cat 18

LTE Cat 18 inaweza kupakua faili kwa kasi inayofika 5000Mbps

Hata hivyo hii spidi ni kubwa sana kwa mitandao ya hapa nchini upande wa 4G

Ubora wa Kioo cha Samsung Galaxy A55

Kioo cha Samsung Galaxy A55 ni cha aina ya Super Amoled

Hivi vioo vya amoled huwa vina utajiri wa rangi kitu kinachofanya kioo kuonyesha vitu kwa rangi zenye kuendana na uharisia kwa kiwango kikubwa

Kwa mfano rangi nyeusi kwenye vioo vya Amoled yaani vinaonekana ikiwa nyeusi kweli

Uzuri wa kioo cha hii unaongezewa na uwepo wa HDR10+ ambayo inaongeza kina cha rangi

HDR10+ huwa inafanya utofoutishaji mzuri sana wa rangi kwenye maeneo yanye mwanga mwingi na mwanga mdogo

Refresh rate ya kioo chake inafika 120Hz hivyo inakuwa “smooth” wakati ukiwa unatachi

Hata hivyo sio mara zote utahitaji refresh rate kubwa maana huwa inakula chaji nyingi

Nguvu ya processor Exynos 1480

Galaxy A55 inatumia chip ya Exynos 1480 katika kufanya kazi zake mbalimbali

Hii chip imegawanyika katika sehemu mbili ambapo sehemu yenye nguvu kuna core nne zinazotumia muundo wa Cortex A78

Cortex A78 inaweza fanya kazi nne kwa mzunguko wakati kuna mizunguko mingi kwa sekunde moja

Kwa maana hii processor nguvu yake ya kufanya nyingi na nzito ni kuridhisha

Ndio maana hata app geekbench inayopima uwezo wa processor inaipa hii chip alama 1168

Kwa mpenzi wa magemu atafurahia muonekano wa graphics za gemu

Uwezo wa betri na chaji

Ukiwa unacheza magemu muda wote betri ya hii simu itadumu kwa wastani wa masaa saba

Na ukiwa unaperuzi intaneti mara kwa mara bila kupumzika itakuchukua karibu masaa 12 mpaka chaji iishe

Kwa maana hiyo kwa mtumiaji mkubwa wa intaneti atalazimika kuchaji simu mara mbili kwa siku

Na kwa mchecha gemu atalazimika kuchaji simu zaidi ya mara tatu kwa siku

Uzuri ni kuwa chaji yake inasapoti wati 25 ambayo inachukua muda mfupi kujaa kwa asilimia mia

Kiwastani ukaaji wa chaji wa Samsung Galaxy A55 ni wa kuridhisha

Ukubwa na aina ya memori

Upande wa memori samsung zipo za matoleo mawili, ambazo kuna zenye GB 128 na GB 256

Na pia katika mgawanyo wa RAM zipo za aina tatu ambazo ni GB 8 na 12

Yenye RAM kubwa ndio inafaa zaidi kwani inakuwezesha kufungua app nyingi kwa wakati mmoja bila kukwama kwama

RAM ndogo huwahi kujaa hasa kama simu imefungua applikesheni nyingi kwa wakati mmoja kitu kinachosababisha simu kuwa nzito

Hii simu inatomia memori za aina UFS 3.1 ambazo huwa zina kasi kubwa ya kusafirisha data

Yaani kama unakopi video ya MB 500 kwenda kwenye simu utaona imemalizika fasta

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A55

Samsung Galaxy A55 ni simu yenye waterproof kwa maana ina IP67

IP67 ni viwango vinavyoashiria kuwa simu haiwezi kuingiza maji ikiwa imezama kwenye kina cha mita 1 kwa muda wa nusu saa

Hata kioo ambacho kimewekwa kwenye skrini ni imara na kigumu kupasuka

Kwa sababu kimewekewa kioo cha Gorilla Glass Victus+

Hata hivyo ni muhimu kuwa makini kwani Gorilla Glass Victus+ pia huchunika

Umakini ni muhimu kioo ni kioo, hupasuka

Ubora wa kamera

Hii simu ina jumla ya kamera tatu ambapo kamera kubwa ina megapixel na inaweza kurekodi video za 4K

Muonekano wa video za 4K huwa na kuvutia na angavu kutokana na kuwa na pixel nyingi

Utafurahi ukirekodi video ya 4K na kuitazama kwenye TV inavosapoti 4K

Kitu kingine ni kuwa hii kamera ina OIS ambayo huwa inatuliza mtikisiko wakati ukirekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa picha ni mzuri kwenye mazingira yote yaani ya mwanga hafifu na kwenye mwanga mwingi

Ubora wa Software

Samsung Galaxy A55 inakuja na toleo jipya la mfumo endeshi ambalo ni Android 14 na pia One UI 6.1

Kwenye One UI 6.1 kuna mifumo mingi ya akili bandia

Kwa mfano unaweza ukawasiliana na mtu anaeongea lugha nyingine ambayo wewe huwelewi

Lakini mfumo one ui 6.1 unaweza kutafsiri maongezi na kuyabadirisha kuwa kwenye lugha unayoielewa

Na kuna mambo mengine

One UI 6.1 ni moja mifumo ya Android ambayo ni mizuri ukilinganisha na mengine

Washindani wa Samsung Galaxy A55

Kwenye masoko ya nchi zinazoendelea kama hapa kwetu Tanzania kuna matoleo mengi ya simujanja kutoka China

Baadhi ya kampuni kama Oppo na Redmi zinatengeneza simu nyingi za daraja la kati na zenye bei nafuu kuliko Galaxy A55

Mfano mzuri tu simu ya Oppo Reno11 Pro ambayo na yenyewe bei yake ni shilingi milion 1.15

Oppo Reno11 Pro inaizidi Samsung Galaxy A55 katika maeneo mengi karibu yote ukitoa upande wa software

Hivyo kitu kama hicho kinaweza kumuhamisha mteja kununua Oppo

Hapo bado matoleo ya Redmi, Tecno na Infinix bila kusahau Realme na OnePlus

Ushindani ni mkubwa kwa samsung kutoka kwa matoleo ya simu za China

Neno la Mwisho

Kwa wapenzi wa Samsung ambao hawawezi kununua matoleo ya Samsung Galaxy S24 hawapaswi kuwaza sana

Kwani bei ya Samsung Galaxy A55 ni ndogo na pia inakupa baadhi ya vitu vinavyopatikana kwenye Samsung za madaraja ya juu

Kwa maana utakutana na toleo jipya la android na utakuwa unapata update za mara kwa mara kuipa simu yako uhai na kutunza thamani yake kwa muda mrefu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram