SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 27, 2024

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023

Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya GB 128

Ila kama unaweza kuagiza kutoka nje bei yake ni chini ya hapa

samsung galaxy a25 showcase

Sifa zake nyingi ni za kiwango cha wastani ila upande wa kamera na skrini kuna ubora wenye viwango vya “premium”

Kabla ya kujiuliza sana kuhusu bei yake ni vizuri kuzitazama sifa za samsung galaxy a25 kinaga ubaga kufahamu iwapo sifa zake zinaendana na mahitaji yako

Sifa za Samsung Galaxy A25

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 1280
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.4 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G68
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6
Memori  256GB,128GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-25W
Bei ya simu(TSH) 700,000/=

Uwezo wa network

Samsung Galaxy A25 inatumia laini za kawaida na haisapoti eSIM

Kama unataka eSIM ya samsung yapo machaguo mengine kama Samsung Galaxy A55

Ni galaxy ya 5G na inasapoti aina zote za 5G ikiwemo ya masafa ya kati inayotumiwa na mitandao ya simu mingi nchini

Pia si tu 5G hata 4G inakama vizuri kwa masafa ya hapa nchini

Aina ya 4G ni LTE Cat 18 yenye kasi ya kupakuwa faili ya 2550Mbps

Kiuhalisia hakuna mtandao wa simu kwa hapa nchini kwa sasa unatoa spidi hii

Labda mbeleni hasa upande wa 5G

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A25

Kioo cha Galaxy A25 kinatumia teknolojia ya Amoled na resolution yake ni 1080 x 2340 pixels

Kitu cha kufurahisha kwenye kioo ni uangavu wenye nits zinazofika 1000 na refresh rate inayosogea hadi 120Hz

Kiwango hiki cha nits kinasaidia sana kutumia simu hata ukiwa juani na kioo kikawa kinaonyesha picha vizuri

Refresh rate kubwa inafanya kioo kuwa fasta ukiwa unaperuzi ama muonekano mzuri ukiwa unacheza gemu

Ila kioo cha hii simu sio kama cha Galaxy A55 kwani hakina HDR10+

HDR10+ huongeza kina cha rangi kitu kinachofanya vitu vingi kuonekana kwa rangi zenye kuondana na uhalisia

Nguvu ya processor Exynos 1280

Galaxy A25 inapewa nguvu na processor ya Exynos 1280

Kiuwezo Exynos 1280 ina nguvu ya kufanya kazi nyingi hata zile zinazotumia nguvu kubwa kubwa

Hii inatokana na simu kutumia muundo wa Cortex A78

5-samsung galaxy a25 chip

Kitu kinachoifanya exynos 1280 kuwa na alama zaidi ya 800 kwenye app ya kutesti nguvu za processor

Kwa mfano kwa sekunde moja exynos inaweza kufungua kurasa zaidi ya 50

Hii ni tofauti na chip ya mediatek helio g35 inayofungua kurasa 25 kwa sekunde

mediatek helio g35 imetumika kwenye simu za daraja la chini kama Nokia G20 na Redmi 9C

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Galaxy A25 ukubwa wake ni 5000mAh

Changamoto ukaaji wake wa betri uko chini ya standard ukilinganisha na simu nyingi zenye betri ya 5000mAh

Ukiwa unaperuzi intaneti simu inachukua mpaka masaa 9 na dakika 30 kuisha chaji

Simu nyingi huweza kumudu hadi masaa 12

samsung galaxy a25 betri

Kwa samsung zinazotumia chip ya exynos huwa hazina ufanisi mkubwa wa matumizi ya betri ukilinganisha na snapdragon

Chaji yake ina wati 25 ambao ni umeme mwingi wa kuchaji simu kwa dakika chache

Inaichukua simu dakika 84 tu kujaa kutoka 0 hadi 100%

Ukubwa na aina ya memori

Aina ya memori simu inayotumia ni UFS 2.2 kama ilivyo kwa simu nyingi za daraja la kati

UFS husafirisha data kwa kasi kwa maana ukiwa unakopi faili kwenda kwenye simu linawahi kumalizika

Simu imegawanyika katika makundi mawili zipo za GB 128 na GB 256 na mgawanyo wa RAM ni GB 6 na GB 8

Ni vizuri kununua yenye RAM kubwa kama ili uweze kutumia vitu vingi bila kwa wakati mmoja

Ukiwa unacheza gemu RAM hujaa kitu kinachoweza kusababisha kuganda ganda

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A25

Bodi ya Samsung Galaxy A25 ni ya plastiki upande wa nyuma na mbele

Na haina viwango vyovyote vya IP, kwa hiyo sio simu imara kuzuia maji kwani hakuna waterproof

Hivyo unapotumia kwenye mazingira yenye maji au kwenye mvua unapaswa uwe makini ili isikutane na maji

Kwa sababu kama ikizama kwenye kina kirefu haitochukua muda mrefu simu kuanza kuharibika

Kama unajari juu ya muonekano mzuri wa simu kwa muda mrefu huna budi kutumia kava

Ubora wa kamera

Hii ni samsung ya macho matatu kwa maana ina kamera ya wide, ultrawide na macro

Kamera kubwa ina megapixel 50 na ikiwa na OIS na ulengaji wa PDAF

Ubora wa picha hasa kwenye mwingi ni mzuri kwani kamera inapiga picha zenye vitu kwa ustadi

samsung galaxy a25 camera

Kama ukizoom picha iliyopigwa na kamera kubwa utaona kiwango kidogo cha noise

Ila ukiacha tu hivi kawaida kwa jicho la kawaida utakuwa na wakati mgumu kutofautisha ubora wa kamera kwenye simu zingine za bei kubwa

Hii kamera inaweza kurekodi mpaka video za 4K

Mara nyingi kamera zinazoweza kurekodi 4K hupiga picha nzuri kwa kiasi kikubwa

Ubora wa software

Samsung Galaxy A25 inakuja na Android 14 na One UI 6

One UI 6 inaambatana na app zingine kama facebook, tiktok, Temu nk

Hizi zote unaweza kuziondoa kama huzihitaji tofauti na simu zingine za daraja la chini

One UI 6 imeepuka kuweka matangazo(ads) ambazo baadhi ya watumiaji hawafurahishwi nayo

Pia one ui 6 ina autoblocker ambayo inazuia app zinazotaka kuingia kwenye simu bila ridhaa yako

Kuna hali kama hiyo kwenye simu za android

Washindani wa Samsung Galaxy A25

Kwa hapa Tanzania bei ya Samsung Galaxy A25 ni kubwa tofauti ne bei halisi inayouzwa huko duniani

Kwani bei yake ni dola 200 ambayo ni kama laki tano na thelathini

Kwa maana hiyo washindani wa samsung galaxy a25 ni matoleo ya zamani ya Samsung S-series mfano Samsung Galaxy S10

Japo kwa sasa Samsung Galaxy S10 utapata used ila ina baadhi ya vitu vinavyokosekana kwenye galaxy a25 kama HDR10+ na waterproof

Washindani wengine ni kutoka kwa kampuni za China kama poco x6 neo, poco m6 pro na motorola edge 40

Poco x6 neo inakuja na waterproof ya kuzuia maji yenye kasi ndogo na pia ina screen protekta ya kioo cha Gorilla Glass 5

Kwa bahati mbaya au nzuri Poco X6 Neo inauzwa chini ya laki tano

Neno la mwisho

Kwa mpenda kamera asiye na uwezo wa kununua Samsung Galaxy S24 Ultra, Galaxy A25 ni mbadala mzuri

Inakupa baadhi ya vitu vichache vinavyopatikana kwenye matoleo ya daraja la juu

Japo haiwezi ikakupa utendaji wa juu kama simu za bei ghari, ila chaguo madhubuti kwa bajeti ndogo

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Simu Mpya za Samsung 2024 (za bei rahisi na ghari)

Kuna simu zaidi ya tisa zilizotengenezwa na kampuni ya Samsung kutoka Hapa kuna orodha ya simu kumi mpya za samsung ambazo zimetoka mwishoni mwa mwaka 2023 hadi mwaka 2024 Ni […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram