SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Mpya za Samsung 2024 (za bei rahisi na ghari)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

May 2, 2024

Kuna simu zaidi ya tisa zilizotengenezwa na kampuni ya Samsung kutoka

Hapa kuna orodha ya simu kumi mpya za samsung ambazo zimetoka mwishoni mwa mwaka 2023 hadi mwaka 2024

Ni listi yenye samsung za bei ndogo, bei ya kati na bei kubwa

Simu zote zinaanzia laki mbili na nusu kwenda na ubora unatofautiana hasa utendaji

Samsung Galaxy A15

Bei ya Samsung Galaxy A15: 420,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Simu ya Samsung Galaxy A15 iliingia rasmi mnamo mwishoni mwa mwaka 2023 yaani mwezi desemba

Utendaji wake ni wa wastani kutokana  na kutumia chip Mediatek Helio G99

Ina kioo kizuri kinachotumia teknolojia ya AMOLED kikiwa na refresh rate ya 120Hz

Yaani ukiwa unatachi kioo kinakuwa chepesi na maridhawa wakati wa kuperuzi kwa ku-scroll

Ubora wa kamera wake haufikii viwango vya simu vya bei kubwa ila ina ubora unaopiga picha za kuridhisha kiasi fulani

Kwa zaidi pitia: Ubora na bei ya Samsung Galaxy A15

Samsung Galaxy A15 5G

Bei ya Samsung Galaxy A15 5G: 500,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Hii ni samsung yenye sifa za ziada upande wa network ila kwa kiasi kikubwa inafanana na galaxy iliyotangulia

Na yenyewe ilitoka mwezi desemba kiutendaji haina tofauti na Galaxy A15 isiyo na 5G

Hii inaatokana na simu kutumia muundo mmoja wa Cortex A76

Ila faida ya hii simu unapata mtandao wenye kasi kwa wakazi wanaoishi maeneo yaliyo na mtandao wa 5G

Hii simu ukiwa unaperuzi intaneti betri yake inakaa mpaka masaa 11 (kama unaperuzi)

Ukiwa unacheza gemu muda unapungua zaidi

Samsung Galaxy A25

Bei ya Samsung Galaxy A25: 550,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Samsung Galaxy A25 ni toleo lingine la desemba ya mwaka 2023

Hii simu ina kioo kizuri cha Super AMOLED chenye resolution inayofika 120Hz

Ni kubwa sana ila pamoja na kuwa na betri kubwa ukaaji wa chaji ni wa kiwango cha kawaida

Kwani kwenye kuperuzi betri inadumu kwa masaa tisa

Masaa mawili pungufu ya Samsung Galaxy A25

Hii ni simu ya 5G na utendaji wake ni mkubwa kwani ina muundo wa Cortex A78

Samsung Galaxy S24

Bei ya Samsung Galaxy S24: 2,800,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Samsung Galaxy S24 ilitoka mwanzoni mwa mwaka 2024

Ni simu ya daraja la juu yenye ubora kwenye kila nyanja

Utendaji wake ni mkubwa unaoweza kufungua app za kila aina bila simu kukwama kwama

Ukaaji wa chaji pia unachukua mpaka masaa karibu kumi na moja kwenye matumizi tofauti tofauti

Kamera zake zipo tatu na zote zina ubora mkubwa kwenye upigaji wa picha na uchukuaji wa video

Samsung Galaxy S24+

Bei ya Samsung Galaxy S24+: 2,800,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Samsung Galaxy S24 Plus na lenyewe ni toleo la mwaka 2024

Hii ni simu ya kamera tatu huku kamera kubwa ikiwa na ukubwa wa megapixel 50

Galaxy S4+ inatoa picha yenye uhalisia mkubwa kwa nyakati zote za kwenye mwanga hafifu na mwanga mwingi

Ina kioo cha AMOLED chenye uwezo kubadilisha refresh rate kutokana na aina ya matumizi

Mfumo wa chaji unasapoti chaji ya wati 45

Hiyo ukiwa nayo utakuwa kwenye levo moja na iPhone 15 Pro

Samsung Galaxy S24 Ultra

Bei ya Samsung Galaxy S24: 3,330,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Samsung Galaxy S24 Ultra ndio simu yenye gharama zaidi katika hii orodha

Kwa mtumiaaji anayependa simu yenye kamera nzuri, nguvu kubwa ya kiutendaji, ukaaji wa chaji wa muda mrefu, simu yenye peni(stylus), simu yenye waterproof, kioo kikali, lazima uifikirie Samsung Galaxy S24 Ultra

Kwenye chaji Galaxy S24 Ultra inaweza kuchukua mpaka masaa 11 wakati wa kuperuzi

Na kucheza gemu inadumu kwa muda wa masaa 9

Haya ni masaa yanayofanya mcheza gemu kuchaji simu mara nyingi

Kuna vitu vingi vya msingi juu ya hii simu hasa upande wa matumizi ya Artificial Intelligence(AI)

Samsung Galaxy A55

Bei ya Samsung Galaxy A55: 1,150,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Kwa mpenzi wa Samsung Galaxy A55 mwenye uwezo mdogo wa kumudu matoleo ya S-series Samsung Galaxy A55 inakupa vitu vingi vya premium

Ndio maana hata bei yake imechangamka kidogo japo ni simu ya daraja la kati

Ina utendaji wenye nguvu kutokana na kutumia processor ya Exynos 1480

Na yenyewe ina betri kubwa hivyo chaji inakaa muda mrefu hata kwa kulinganisha na samsung nyingi zilizopo hapa

Kwa mfano kwenye kuperuzi simu inakaribia masaa 12 mpaka betri iishe

Samsung Galaxy A35 5G

Bei ya Samsung Galaxy A35: 950,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Hii ni simu nyingine ya toleo la kati japo bei kubwa lakini ni ya toleo la kati

Inatumia chip zinazoundwa na samsung yenyewe

Betri yake ni kubwa na ina ulinzi wa kuzuia maji kupenya yaani waterproof

Ina kamera tatu upigaji wake ni mzuri

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram