SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Tecno Camon 19 Pro na Sifa Muhimu

Simu Mpya

Sihaba Mikole

July 23, 2022

Tecno mpya za Camon 2022 zinaweza kuwa ni simu za Tekno zinazoweza kushindana na matoleo mengi ya Android daraja la kati

Mfano simu ya Tecno Camon 19 Pro ina sifa nzuri upande wa kamera na utendaji kama ilivyo Tecno Camon 19 Pro 5G

Kitu kinachofanya bei ya Camon 19 Pro  kuwa zaidi ya laki sita

tecno camon 19 pro showcase

Japokuwa kuna vitu vya msingi vinavyoweza kuifanya simu isiwe shindani

Hii inatokana na bei na sifa zake kupatikana kwa baadhi ya simu ambazo zinauzwa bei sawa na Camon 19 Pro

Bei ya Tecno Camon 19 Pro ya GB 256

Simu inauzwa kwa bei ya shilingi laki sita na nusu (650,000/=) kwa maduka ya Kariakoo

Uwezekano wa kuipata chini ya hapo pia upo

Ila sifa za hii simu kwenye display (kioo) ina ukakasi kwa kuzingatia bei

tecno camon 19 pro summary

Baadhi ya simu zinazoendana bei hututmia vioo vya amoled

Ukitizama sifa zake kwenye jedwari utagunduoa jinsi camon 19 inavyoachwa nyuma na simu ya Realme 9 Pro

Japo Realme 9 Pro ina memori NDOGO ila bei hazitofautiani sana

Sifa za Tecno Camon 19 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G96
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.05 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • HIOS 8.6
Memori  256GB,128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera TATU

  1. 64MP,PDAF, Laser AF(wide)
  2. 2MP(depth)
  3. 50MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 650,000/=

Ni upi ubora wa simu ya Tecno Camon 19 Pro

Tecno Camon 19 Pro ina mfumo mzuri wa kamera ambao unaifanya simu kurekodi na kupiga picha vizuri

Inakuja na memori kubwa inayoweza kuhifadhi vitu vya kutosha

Ina chaji inayojaza simu kwa dakika chache

Betri yake inaweza kukaa na chaji masaa mengi

Ina kioo kizuri kwa kucheza gemu kwa sababu ya kuwa na refresh rate kubwa

Hata RAM pia ni kubwa kitu kinachohitajika kwenye simu nyingi za android

Kwenye vipengele vya Network mpaka Software kuna ubora na kasoro kadhaa pia

Fuatilia uvifahamu kiundani.

Uwezo wa Network

Camon 19 Pro ni simu ya 4G

Na 4G inayotumia ni LTE Cat 13

LTE Cat 13 ina spidi ya kudownload inayofikia 390Mbps

tecno camon 19 pro network

Kwa maana kama simu inadownload kitu cha ukubwa wa 960MB basi simu itadownload kwa sekunde ishirini

Spidi hii ingewezekana kama unatumia mtandao wa USA kama AT& T

Spidi ya AT&T kwa USA inafika 280Mbps

at&t speed test 4g

Lakini kwa Tanzania bado mitandao ya simu ina spidi ndogo

Camon 19 Pro haina mtandao wa 5G

Japokuwa kwa 5G bado haijatua nchini ila serikali imeshaanza taritibu za kuweka mtandao huo

Unaweza pitia hii habari: Vibali vya 5G

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 19 Pro

Kwa kuangilia resolution, kioo cha Tecno Camon 19 Pro kinaoonyesha vitu vizuri

Hii inachangiwa na simu kuwa resolution kubwa ya 1080 x 2460 pixels

Uwepo wa refresh rate inayofikia 120Hz kunaoongeza ulaini(smoothness) wa kioo kuonyesha vitu kwa ustadi

Kwa maana kama unaperuzi sehemu inayooleza picha zilizopo kwenye simu basi ukiwa unatachi kwa kupekeleka kidole juu picha zinakuwa zinabadirika haraka na wepesi

tecno camon 19 pro kioo

Refresh rate kubwa huwa inatumia umeme mwingi wa betri

Lakini hii simu ina betri kubwa hivyo inaweza isiwe tatizo

Kwa bahati mbaya Tecno Camon 19 Pro ina kioo cha IPS LCD na sio LTPO Amoled

LTPO Amoled inajua ni mazingira yapi ya kutumia refresh rate ya 120Hz

Na mazingira yapi ya kutumia refresh rate ya kawaida yaani 60Hz

Nguvu ya processor Mediatek Helio G96

Camon 19 Pro inatumia chip ya mediaatek helio g96 katika kufanya kazi zote za simu inazofanya

Ni processor ya simu daraja la kati hivyo utendaji wake ni wa kuridhisha

Hii ni processor inayoweza kucheza gemu kubwa kama Genshin Impact kwa spidi ya 23fps kwenye resolution ndogo

App ya geekbench inayopima nguvu za processor inaipa Helio G96  alama 540

tecno camon 19 pro performance

Hivyo uwezo wa Camon 19 Pro kiutendaji unaendana na Redmi Note 10 kwa kiasi kikubwa

Nguvu kubwa ya processor inatokana na chip kutumia muundo wa Cortex A76 kwenye core kubwa

Cortex A76 huwa inaweza kufanya kazi nne kwa kila mzunguko kwa sekunde moja

Kumbuka Spidi ya core kubwa ni 2.05GHz(mizunguko bilioni 2.05)

Uwezo wa betri na chaji

Simu ina betri aina ya Li-Po yenye ukubwa wa 5000mAh

Kuifahamu li-po pitia: ufafanuzi wa betri aina ya lipo kwa sisi hapa sio wanakemia hatuwezi kuielezea kiundani tofauti ya Li-Ion na Li-Po

Simu nyingi zenye betri za 5000mAh zinakaa na chaji masaa yanayozidi 14 simu ikiwa kwenye intaneti

Chaji ya simu ikiwa inapeleka umeme mdogo betri lazima ichelewe kujaa ikizangatiwa ni kubwa

Lakini Tecno Camon 19 Pro chaji yake inapeleka umeme wa wati 33.

Huu ni umeme unaoweza jaza simu ndani ya dakika 65

Kama ukiwa una haraka inakuhitaji dakika chache tu simu kujaa

Waya wake wa chaji ni ule wenye kichwa kipana hujulikana kama USB Type-C 2.0 na sio ule mdogo (micro usb)

Ukubwa na aina ya memori

Camon ina matoleo ya aina mbili upande wa memori

Kuna ya ukubwa GB 128 na GB 256

Haifahamiki kama ni memori za UFS au eMMC

Ila kama ni UFS itakuwa nzuri zaid kwani zina kasi kubwa ya kusafirisha data

Kwneye RAM zipo za aina moja pekee ambazo ni GB 8

RAM ikiwa kubwa inaipa simu nafasi ya kuweza kufanya mambo mengi kwa wakati mmoja

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 19 Pro

Simu ina bodi ya plastiki na haijatumia vioo vya gorilla

Uzito wa simu ni gramu 204 (Na kazito kidogo)

tecno camon 19 pro bodi

Camon hii haina viwango vinavyoonyesha uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi

Hivyo ni muhimu kununua kava ya simu na screen protekta

Itasaidia simu kutoka kwenye mikwaruzo na kupasuka pindi inapodondoka

Ubora wa kamera

Tecno Camon 19 Pro ni tecno macho matatu

Kwa maana ina kamera kubwa (wide) yenye resolution ya 64MP

Kuna kamera kwa ajili ya kupiga vitu vilivyopo mbali , hii huitwa telephoto na ina megapixel 50MP

tecno camon 19 pro kamera

Na kamera nyingine ni depth yenye 2MP ambayo hutumika kupiga mahesabu kujua kitu kinachostahili kutokeo kwa sehemu kubwa kwenye picha

Ndio kamera inayotumika kutengeneza ukungu kwa nyuma ya kitu kinachopigwa picha (hufahamika kama bokeh effect)

Kamera zake zimeboreshwa na uwepo wa OIS, PDAF na Laser AF bila kusahau HDR

Pitia: Jinsi ya kujua kamera nzuri ya simu ili ufahamu umuhimu wa hivyo viyu vilvyotaja

Tecno Camon ya 19 Pro inaweza kurekodi video za full hd pekee

Ubora wa Software

Tecno Camon 19 Pro inakuja na Android toleo la 12 na mfumo wa HIOS 8.1

HIOS 8.1 ina mpangalio muziri wa setting ambao unamrahishia mtu kufikia kile anachokitafuta

tecno camon 19 pro software

Na pia kwenye mpangilio wa phonebook una muonekano unaovutia macho

HIOS 8.1 ina applikesheni unayoweza kuitumia kuficha baadhi ya app ambazo hutaki watu wengine wazitumie

Yapi Madhaifu ya Tecno Camon 19 Pro

Udhaifu wa kwanza ni simu kutumia kioo cha IPS LCD na sio AMOLED

AMOLED ni vioo vinavyoweza kuonyesha rangi nyingi

Kitu kinachofanya vitu kuonekana kwa rangi zake halisi kwa asilimia kubwa ukilinganisha na LCD

Kamera yake haiwezi kurekodi video za 4k ambazo huwa zina resolution kubwa

Utendaji wa processor ni wa wastani na unazidiwa na processor ya Snapdragon 695 5G

Ikizingatiwa simu zenye Snapdragon 695 5G zina bei sawa na Camon 19 Pro

Kioo chake hakina HDR10 wala Doldy Vision ambazo huboresha muonekano wa vitu

Neno la Mwisho

Tecno kwa miaka ya karibuni wamekuwa wakitoa simu nzuri ikiwemo hii inayozungumziwa hapa

Kitu kinachoweza kufanya mtu kusita kununua simu hii ni bei

Mfano, bei ya tecno camon 19 pro na pro 5g zinaweza nunua simu za Realme 9 Pro au Redmi Note 11 Pro 5G

Realme 9 Pro na Redmi Note 11 Pro 5G zinatumia chip ya Snapdragon 695 5g

Snapdragon 695 5g inaiacha pakubwa kiutendaji chip Helio G96 iliyomo kwenye camon 19 pro

Ila kiujumla, Tecno Camon 19 Pro ni moja ya simu bora ya daraja la kati kwa mwaka 2022

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu ya Tecno Camon 19 Pro na Sifa Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram