SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Camon 19 Pro 5G na Sifa Zake (Tecno Mpya)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

July 18, 2022

Kampuni ya Tecno imeingia katika ushindani wa simu za 5G kwa kuzindua simu mpya ya Tecno Camon 19 Pro 5G

Bei ya Tecno Camon 19 Pro 5G inazidi laki saba kwa Tanzania kutokana na simu kuja na teknolojia imara zenye utendaji mkubwa

tecno camon 19 pro 5g showcase

Hii ni simu ambayo imezinduliwa mwezi wa saba mwaka 2022

Ukizifuatilia sifa zake zitakuonyesha jinsi Tecno inavyoimalika katika kutengeneza simu

Baadhi ya sifa za CAMON 19 Pro 5G zinashindana na simu za Redmi na Oppo ambazo zinashika hatamu siku baada ya siku

Bei ya Tecno Camon 19 Pro 5G Tanzania

Tecno Camon 19 Pro 5G yenye GB 256 na RAM ya GB 8 inauzwa shilingi 760,000/= kwa maduka ya Dar Es Salaam

Bei inaweza ikawa isiwe moja na ikatofautiana kutoka duka moja hadi lingine

Lakini kiasi kilichotajwa ndicho sahihi

tecno camon 19 pro 5g summary

Kwa kuziangazia sifa za hii simu kuna maeneo inafanya vizuri

Kuna nyanja simu haijatendewa haki kiasi kinachofanya bei yake kutoendana na ushindani

Zitazame sifa za camon hii mpya kwenye jedwari.

Sifa za Simu ya Tecno Camon 19 Pro 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 810 
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.4 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • HIOS 8.6
Memori 256GB,128GB, na  RAM 8GB
Kamera Kamera tatu

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 760,000/=

Ni upi wa simu aina ya Tecno Camon 19 Pro 5G?

Ubora mkubwa wa Camon 19 Pro 5G ni kuwa na utendaji mkubwa

Utendaji ambao umeifanya simu kuwa na sapoti ya mtandao wa 5G

Pia kioo chake ni kizuri kwa kucheza gemu

Kwa sababu kina refresh rate kubwa inayofanya simu kuwa nyepesi

Ina uwezo wa kupeleka chaji kwa haraka na betri kujaa kwa dakika chache

Na ukaaji wa chaji ni mkubwa kwani betri ya simu ni kubwa kiujumla.

Uwezo wa Network

Upande wa network simu inakubali kutumia mtandao wa 5G

Aina ya mtandao wa 5G simu inayotumia ni SA na NSA

SA kirefu chake ni Stand Alone na NSA inamaanisha Non Stand Alone

Unaweza kupitia: maana ya 5G kujua aina mbalimbali za 5G

65-8tecno camon 19 pro 5g network

Upande wa 4G haijainishwa aina ya masafa simu iliyonayo

Kutokana na aina ya processor simu inayotumia, kasi yake ya 4G inaweza kufika 1200Mbps

Kwa sababu chip yake huwa ina lte aina ya LTE Cat 18

Na simu pia ina GPS ya aina moja aina ya A-GPS (GPS ya Marekani)

Pitia: Kazi ya GPS kwenye simu na ufanyaji kazi wake

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 19 Pro 5G

Kioo cha Tecno Camon 19 Pro 5G ni cha IPS LCD chenye resolution ya 1080 x 2460 pixels

Kioo chenye resolution kubwa huonyesha picha na video kwa ustadi mzuri

Ila vioo vya IPS LCD huwa vina rangi chache ukilinganisha na amoled

Hivyo basi baadhi ya vitu havitoonekana kwa rangi zake halisi

Hasa rangi nyeusi

Kuna uzuri kwenye screen ya camon kwani kuna refresh rate inayofika 120Hz

Tazama video hii inavoonyesha utofauti wa 120Hz(kushoto) na 60Hz(kulia)

Refresh rate ikiwa kubwa inasaidia screen ya simu kuwa nyepesi

Chukulia umefungua app ya meseji na ukakuta kuna meseji nyingi

Kisha ukaanza kutafuta meseji unayotaka kuisoma kwa ku-scroll (kutachi simu kwa kwenda juu au chini)

Kioo cha 120Hz kitakuwa kinascroll kwa haraka na kuifikia meseji ndani ya muda mfupi

Changamoto yake ni utimiaji wa moto mwingi

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 810

Kumbuka ukiwa na simu yenye processor dhaifu basi jua simu itakuwa dhaifu kwenye kila sehemu.

Ila sio MediaTek Dimensity 810 ambayo inaipa nguvu Tecno Camon 19 Pro 5G

Hii ni chip ya simu yenye utendaji mkubwa kutokana na muundo mzima wa core kubwa na core ndogo.

tecno camon 19 pro 5g processor mediatek

Ina jumla ya core zipatazo nane, core kubwa zipo mbili na core ndogo zipo sita

Uwezo wa Core Kubwa

Dimensity 810 ina core mbili ambazo hutumika pindi simu ikiwa inafanya kazi nyingi na kubwa kwa wakati mmoja

Mfano ukiwa unarekodi video za 4K au kucheza gemu basi core hizi mbili ndizo zitakazokuwa zinachakata kazi zote

Utendaji wake mkubwa unatokana na core kutmia muundo wa Cortex A76

Cortex A76 inaweza kufanya kazi 4 kwa mzunguko mmoja ndani ya sekunde

Izingatiwe clock spidi ya dimensity 810 ni 2.4GHz (mizunguko bilioni mbili nukta nne kwa sekunde)

Kutokana na nguvu hii, vipimo vya app geekbench inaipa chip alama zaidi ya 600

Na pia inafanya simu kuweza kucheza gemu ya Call of Duty: Mobile kwa resolution kubwa na kwa kasi ya 42fps

Hivyo picha za gemu zinaoonekana vizuri na bila simu kupata joto jingi

Uwezo wa Core Ndogo

Core ndogo zipo sita ambazo hufanya kazi pindi simu ikiwa inafanya kazi ndogo kama kupiga simu

Hizi ubora wake hupimwa kwa matumizi madogo ya umeme

Na huwa na utendaji mdogo kwa sababu zinatumia muundo wa Cortex A55

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Tecno Camon 19 Pro 5G ina ukubwa wa 5000mAh

Hivyo ukaaji wa chaji lazima uchukue masaa mengi hata ukiwa umewasha intaneti muda wote

Simu inakuja na chaji inayopeleka umeme wa wati 33

tecno camon 19 pro 5g chaji

Ni kiasi kinachoweza kujaza betri ya simu ndani ya dakika 75

Hutokuwa na wasi pindi simu inapoisha chaji na ukiwa na haraka ya kuchaji

Ukubwa na aina ya memori

Upande wa memori kuna aina mbili za camon iliyopo kwenye posti hii.

Kuna camon ya GB 128 na Camon ya GB 256

Zote zinakuja na RAM ya GB 8

Kitu kichoisadia simu kufungua vitu vingi kwa wakati mmoja bila kukwama

Tecno hawajasema aina ya memori ambazo simu inatumia

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 19 Pro 5G

Simu ina kimo cha inchi 6.8

Ni kimo kikubwa japo kuna baadhi ya watu wanapendelea simu ndogo

Hakuna pia taarifa kuhusu aina ya bodi simu inayotumia

tecno camon 19 pro 5g bodi

Lakini kiujumla haina vioo vya gorilla ambavyo huwa ni vigumu kupasuka

Mfano ni kioo cha Gorilla Victus kilichopo kwenye simu mpya ya Xiaomi 12S Ultra

Ubora wa kamera

Hii simu unaweza kuita Tecno Macho Matatu

Kwani ina kamera za wide, macro na depth

Lakini ni kamera moja tu ndio yenye ubora unaotakiwa

Kamera za macro na depth zina resolution ndogo ya 2MP

Hivyo utoaji wa picha utakuwa wa kiwango cha chini na kibaya hazina aufocus wala OIS

tecno camon 19 pro 5g camera

Kumbuka macro ni aina ya kamera kwa ajili ya kupiga vitu ambavyo ni vya karibu sana na kamera

Kamera ya depth hutumika kutambua kitu au eneo linalotakiwa kuonekana kwa kiasi kikubwa

Hivyo kitu au eneo ambalo halitakiwi hutokea ukungu kwa nyuma

Ila ni simu ambayo haizwezi kurekodi video za 4k japokuwa simu ina processor yenye nguvu

Ubora wa Software

Tecno Camon 19 Pro 5G inakuja na Android 12 na mfumo wa HiOS 8.1

Ukiwa na HiOS 8.1 utaweza kutengeneza video yenye mkusanyiko wa picha zako

Pia ni mfumo ambao una app inayoitwa Phone Cloner

Phone Cloner inasaidia kuamisha vitu kutoka simu moja kwenda nyingine kwa haraka

Na pia tecno wameboresha mfumo wa kuscreenshot dokumenti

Yapi Madhaifu ya Tecno Camon 19 Pro 5G

Tecno Camon 19 Pro 5G haina mfumo wa kamera nzuri

Ukizingatia bei yake ni kubwa simu ilikuwa inastahili kuweka kamera inayoweza kurekodi video za 4k

Kwani kuna simu za laki nne ambazo zina kamera zinazorekodi video za 4K kwa kasi ya 60fps

Simu haina ulinzi wa vioo vya gorilla na pia bado inatumia kioo cha IPS LCD

Kamera zake zinatumia HDR ya kawaida badala ya angalau HDR10

Neno la Mwisho

Tecno Camon 19 Pro 5G inawafaa zaidi watu wanaotegemea simu kufanya vitu vingi kwa wakati mmoja

Kama kamera na kioo sio kigezo kwako hii simu inafaa kuimiliki

Ila bei ya tecno camon 19 pro 5G ni kubwa

Kwa sababu simu ya Redmi Note 11 Pro 5G inapatikana chini ya laki saba

Kiubora Redmi inaicha Camon pakubwa

Maoni 8 kuhusu “Bei ya Tecno Camon 19 Pro 5G na Sifa Zake (Tecno Mpya)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Spark 4 na Spark 3 Pro na sifa muhimu 2023

Simu za Tecno Spark 4 na Spark ni simu za daraja la chini za mwaka 2019 Spark 3 ilitangulia kabla ya spark 4 Kiteknolojia, hazina vitu vizuri na hivyo basi […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram