SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ni nini Maana ya 5G na aina zake

Miongozo

Sihaba Mikole

May 12, 2022

Kama umekuwa ukijiuliza 5G ni nini na maana yake ni ipi

Basi jibu lake ni hili hapa chini

5G ni teknolojia ya kizazi cha tano cha network za simu za mkononi ambayo kasi yake ni kubwa kuliko aina za network za simu za mkononi zilizowahi kutangulia

Utendaji wa 5G umejikita kwenye kasi kubwa sana na kutumia muda mchache kwenye mwitikio wa data (Low Latency) kati ya vifaa mbalimbali

Kikawaida kiwango cha chini cha spidi ya mtandao huu inaanzia 50Mbps

Kuna aina tatu za 5G ambazo zinatofautiana kasi

Kwenye posti hii utafahamu mambo ya msingi yote yanayohusiana na 5G ikiwemo mwanzilishi wake

Nani mwanzilishi wa 5G?

Hakuna taasisi, wala mtu au kampuni moja ambayo imetengeneza 5G

Bali 5G imeundwa kwa ushirikiano wa makampuni ya mabara yote duniani

Umoja ambao umekutanisha hayo makampuni ni 3GPP

Kirefu cha 3GPP ni Third Generation Patnership Project

Kwenye 3GPP kuna kampuni kama Qualcomm, Nokia, Huawei, Samsung, Cisco, Ericson, AT&T, TTC na mengineyo mengi

Kiufupi 3GPP ina wanachama wanaofikia 700 kwa mwaka 2022

Hii ndio jumuiya inayoseti vigezo (standards) vya network kuwa 5G

Aina za 5G

Kuna aina tatu za mtandao wa 5G

Si kila 5G ina kasi kubwa, bali kuna aina nyingine haina tofauti na 4G linapokuja swala la kasi

Kwani kasi za 5G zinatofautiana kulingana na aina ya masafa

Hizi ndizo aina zake

  • Masafa mafupi (Low Band)
  • Masafa ya kati (Mid Band)
  • Masafa marefu (High Band au mmWave)

5G ya Low Band masafa yake yanaanzia 600 MHz mpaka 900 MHz

Spidi yake haitofautiani sana na mtandao wa 4G

Kwani inaweza kusafirisha kwa kasi inayoanzia 30Mbps mpaka 250Mbps

Nchi nyingi duniani zinatumia 5G ya Masafa ya Kati (Mid Band 5g) pia inafahamika kama sub-6

Masafa ya mid band yanaanzia 1.7GHz mpaka 4.7 GHz na spidi ipo kati ya 100Mbps mpaka 900Mbps

Na masafa marefu yanaanzia 24 GHz mpaka 40 GHz

Haya ni masafa yanayoweza kusafirisha data kwa kasi kubwa inayofika 1Gbps

Pia hufahamika kama mmWave (milimetre Wave)

Changamoto za 5G

Mawimbi ya High Band (Masafa marefu) huwa yanapata shida kupenya kwenye ukuta na wakati wa mvua

Hivyo ukiwa unatumia intaneti ndani ya nyumba spidi inapungua

Mawimbi yake pia hupatikana eneo dogo

Hivyo inalazimisha kampuni za simu kuweka minara mingi ili network ipatikane

Minara mingi inaongeza gharama kitu kinachofanya intaneti yake kuwa sio rafiki kutokna na bei kubwa

Ndio maana nchi nyingi za Afrika hazijaweka huu mtandao

Gharama kubwa zinalazimisha wauzaji wa huduma za intaneti kujikita mijini kuliko vijijini

Vifaa vingi vya 4G hasa smartphone vinauzwa kwa bei ya juu

Utofauti wa 5G na 4G

Utofauti wa 4G na 5G ni spidi tu

Japokuwa 5G inaweza ikatumia miundo mbinu ya 4G kusafirisha data

Aina hii ya muundo hufahamika kama NSA (Non Stand Alone)

Kikubwa ni kuwa 5G inaanzia 50Mbps wakati 4G inaanzia 18Mbps

Lakini kuna ufanano kwa sababu 4G pia inatumia masafa ya mafupi na ya kati

Simu za 5G

Baadhi ya simu za daraja la kati huwekewa uwezo wa kutumia 5G ya low band na mid band

Mfano wa simu hizo ni Vivo T1, Infinix Zero 5G, Redmi Note 10 5G, Samsung Galaxy A73 5G, Oppo A96 5G nk

Lakini bei ya hizi simu ni zaidi ya laki tatu na nusu

Pia simu zote za daraja juu lazima iwe na uwezo wa network ya 5G

Mfano wa hizo simu ni Samsung Galaxy S21 Ultra 5G, iPhone 13 Pro Max, Xiaomi 12 Pro, Oppo Find x3 Pro, Sony Xperia Pro-I, Vivo X70 Pro na nyingenezo nyingi

Ili utumie 5G unahitaji simu yenye uwezo huo ikiwemo na laini ya 5G

Kama sehemu haina mtandao huo basi hautoweza kupata kasi yake kubwa

Mitandao yenye 5G Tanzania

Mwaka 2020 Vodacom Tanzania ilianza mipango ya kuweka 5G wakati wa maazimisho ya miaka 20 tangu wameanza biashara Tanzania

Lakini hakuna taarifa zozote mpya

Kiufupi, hakuna mtandao wa simu ambao umewekeza kwenye hii teknolojia mpya ya mawasiliano

Lakini matumaoni yapo

Kwani mkutano uliandaliwa na ubalozi wa marekani chini ya udhamini wa United States Telecommunications Training Institute (USTTI) na Wizara ya Teknolojia ya habari na mawasiliano waligusia suala hilo

Hii ni kwa mujibu wa taarifa ya ubalozi wa Marekani ambayo imechapishwa Mei 9, 2022

Ipitia hapa kuisoma yote, Mkutano wa ubalozi wa USA na Wizara ya tehama Tanzania

Update septemba 2022

Vodacom imekuwa kampuni ya kwanza Taznania kuzindua mtandao wa 5G

Aina ya 5G ambayo vodacom inatumia ni Non Stand Alone

Kwa maana 5G yake itakuwa inatumia miundo mbinu ya 4G

Jifunze zaidi hapa: Vodacom na uzinduzi wa 5G Tanzania

Kwa nini simu za 5G zina bei kubwa

5G inahusisha mtandao ambao una kasi kubwa ya kusafirisha data

Kitu kinachoifanya simu iwe na processor yenye utendaji mkubwa

Chip zenye nguvu kubwa huwa na teknolojia bora ambayo inatumia pesa nyingi

Mwisho wa siku gharama za simu zinakuwa juu

5G na Ugonjwa wa Uviko (Covid)

Mtandao wa 5G ulikutana na changamoto ya kuhusishwa na kusambaa kwa kirusi cha corona

Corona ni kirusi ambacho kinasababisha uviko

Haya madai yaliegemea kwenye dhana za kufikirika zaidi kuliko taifiti za kisayansi

Kiuhalisia ni mawazo ambayo hayana mantiki

5G ya masafa ya chini na ya kati yanatumia miundo mbinu ya 4G

4G pia inatumia baadhi masafa yanayotumika na 5G

Sasa kwan nini covid haikusambazwa na 4G ije isambae leo hii

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram