SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 7 plus na Nafasi Yake 2023

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 19, 2023

Apple iPhone 7  Plus ni simu janja ya mwaka 2016

Kwa sasa apple hawatengenezi hizi simu, nyingi zilizopo ni simu used

Kitendo kinachoifanya kuwa na bei nafuu ukilinganisha na simu zinazotengenezwa na kampuni ya apple

iphone 7 plus showcase

Kwa mwaka 2023, bei ya iphone 7 plus inatofautiana hata kama ni ya memori moja ila kwa kiwango kikubwa inazidi laki nne

Unahitaji kuitazama hii simu kiundani kuelewa kama inafaa kwa mwaka 2023 na miaka ijayo

Kwani ina miaka zaidi ya sita tangu ilipozinduliwa, huu muongozo utakupa picha kamili

Bei ya iPhone 7 Plus ya GB 128

Hapa Tanzania hasa Dar Es Salaam bei yake yenye ujazao wa GB 128 ni shilingi 500,000/=

Kama ilivyoilezwa awali, unaweza kuipata chini ya hapa inategemeana na eneo na uhitaji wa simu

Hii bei inaendana na matoleo mapya kama Samsung Galaxy A14 5G

Kuna nyanja hii simu inazikalisha simu zinazouzwa kati ya 400,000 mpaka 500,000

Kwa mfano utendaji wa redmi note 12 na Tecno Spark 10 Pro unaachwa na iPhone 7 Plus japo redmi ni ya 2022 na Tecno ni ya 2023

Hii iphone utendaji wake una nguvu unaoendana na nyakati za sasa

Kitu kinachofanya kuwa ni simu inayofaa kutumika 2023 na ukizingatia inapokea matoleo mapya ya mfumo endeshi

Zitazame sifa zake na utagundua hilo

Sifa za iPhone 7 Plus

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g 
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A10 Fusion
  • Core Zenye nguvu(4) – 2×2.0GHz kryo 460
  • Core Za kawaida(-) – Quad-core 2.34 GHz
  • GPU-PowerVR Series7XT Plus
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • iOS 10.0.1
  •  
Memori NVMe, 256GB,128GB,32GB na RAM 3GB
Kamera Kamera mbili
  1. 12MP,PDAF(wide)
  2. 12MP,(Telephoto)
Muundo Urefu-5.5inchi
Chaji na Betri
  • 2900mAh-Li-Po
  •  
Bei ya simu(TSH) 500,000/=

Upi Ubora wa iPhone 14 Plus

Simu inatumia chip yenye nguvu inayofanya simu kuwa nyepesi

Inapatikana kwa bei rafiki hata kwa matoleo yenye memori kubwa

Kamera zake zinatoa picha nzuri japo ni simu ya zamani

Inatumia mfumo wa memori unaosafirisha data kwa kasi kubwa

Ina mifumo karibu mitano ya gps kitu kinachofanya usahihi wa taarifa za eneo kuwa mkubwa

Inasapoti pia kasi kubwa ya mtandao wa 4G

Uwezo wa Network

Mtandao wa juu kabisa unaosapoti ni 4G

Mwaka 2016 hakukuwa na 5g hivyo kama 5g ni muhimu kwako basi simu haitokufaa

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 12 ambayo imetumika kwenye simu ya mwaka 2021 ya Redmi Note 10

Kasi ya LTE Cat 12 ni 600Mbps sawa na 75MB/s

Kama unapakuwa video ya MB 75 simu inachukua sekunde moja kumaliza kudownload

Sio spidi kubwa sana ukifananisha na uwezo wa simu za siku hizi

Hata hivyo bado kwa Tanzania sio rahisi kukuta mtandao wa simu za mkononi ukitoa kasi hiyo

Ubora wa kioo cha iPhone 7 Plus

Kioo cha iphone 7 plus ni cha aina ya IPS LCD

Miaka hii apple hawakuwa wanatumia vioo vya OLED

Kioo cha IPS LCD kikiwa na resolution kubwa muonekano wa vitu unakuwa wa kuvutia kiasi cha kwamba unaweza usione tofauti sana na vioo vya amoled

iphone 7 plus display

Ndio maana kioo cha hii simu kina resolution ya 1080 x 1920 pixels wakati baadhi ya  simu za 2023 zimeweka vioo vya resolution ya 720p 

Kwa nyanja hiyo ni kuwa ubora wake kwenye kioo unaridhisha na uendana na simu nyingi mpya zilizotoka hivi karibuni

Ambacho kinachokosekana hapa ni refresh rate kubwa ya kuanzia 90Hz

Refresh rate kubwa hufanya simu kuwa nyepesi(smooth) unapokuwa unatachi kwa kupeleka juu na chini

Nguvu ya processor Apple A10 Fusion

Kwa miaka mingi apple wamekuwa wakiunda processor za simu zenye nguvu zaidi ukilinganisha na kampuni za Snapdragon na Mediatek

Fikiria kuwa Apple A10 Fusion ina miaka sita ila inaizidi  chip ya Snapdragon 680 4G iliyopo kwenye simu ya Oppo A96

Kwenye app inayopima nguvu za chip ya Geekbench, apple a10 fusion ina alama zaidi ya 700 kwenye core moja

Hivyo inaifanya simu kuweza kufungua apps nyingi bila na kucheza magemu makubwa mengi japo si kwa kiwango kikubwa kiivyo

Ufanisi wa matumizi madogo ya umeme ni wa kiwango cha kati

Kwa maana chip pia ina matumizi makubwa betri hasa pale unapofanya kazi zinazotumia nguvu kubwa ya processor

Hii chip ina core nne tu tofauti na matoleo mengi ya siku hizi yanayoanzia na idadi ya core sita na kuendelea

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya iPhone 7 Plus ina ukubwa wa 2900mAh

Ni betri dogo kiuhalisia

Ukiwa unaongea na simu muda wote betri inakaa kwa masaa 21

Ni muda mdogo na kama ukiwa unaperuzi muda wote simu inakaa masaa 13

Hata hivyo ni muda unaoendana na simu nyingi zilizotoka hivi karibuni

Na pia kumbuka kiwango hicho cha muda ni pale simu ikiwa mpya kabisa

Kwa kuwa sasa hivi utapata iphone used usitegemee kupata muda huo kwani afya ya betri inaweza ikawa imeshuka

Simu haina fast chaji kwa maana upelekaji wake wa chaji ni wa taratibu

Ukubwa na aina ya memori

Kwenye upande wa memori kuna matoleo matatu yenye ukubwa wa 32GB, GB 128 na GB 256 na zote zina RAM ya GB 3

Bei ya GB 32 ni ndogo kwani unaweza kuipata kwa laki tatu na nusu

Aina ya memori simu inayotumia ni NVMe

NVMe huwa inasafirisha data kwa kasi, hii hufanya iPhone kuwa nyepesi

Ila ya GB 32 inaweza ikawa ndogo kwa sababu simu haina sehemu ya memori ya zaida

Hivyo kuhifadhi mafaili ya kutosha itakulazimu uchukue ya kuanzia GB 128

Uimara wa bodi ya iPhone 7 Plus

iPhone 7 Plus ina viwango vya IP67

IP67 inamaanisha simu haiwezi kuingia maji kama ikizama kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu saa

Ni ishara kuwa simu ina bodi ngumu na imara

iphone 7 plus body

Upande wa nyuma imewekewa vioo vya Glasi na upande wa mbele hivyohivyo

Vioo vyake vimeundwa na kampuni ya Corning wanaounda vioo vya gorilla

Simu pia sio ndefu ni fupi kwani ina inchi 5.5

Ni nyepesi kuibeba

Ubora wa kamera

Kwa kiwango cha picha ni cha kuridhisha na kinachuana na simu nyingi za madaraja ya kati

Kwenye mwanga picha zinatoka vizuri ila kuna cha noise (chengachenga) kinaonekana kwa mbali kama ukiikuza picha

Usahihi wa rangi na wa kuridhisha japo si mkubwa

Ila kumbuka simu nyingi bado haziwezi piga picha kwa ubora

Fuatilia: Picha zilizopigwa na simu ya iphone 7 plus

Kiujumla simu ina kamera mbili na zote zina megapixel 12 ambazo zinatosha kabisa kutoa picha nzuri

iphone 7 plus kamera

Kamera ya Telephoto(kwa ajili ya vitu vilivyopo mbali) inatumia optical zoom

Optical zoom huwa inakisogeza kitu cha mbali kwa kutumia lenzi ni sio app

Hii inafanya ubora wa picha kutokupotea tofauti ukizoom kwa kutumia kamera

Ubora wa Software

Wakati inatoka simu ilikuwa inakuja na iOS 10.0.1 ya zamani kwa sasa

Na kadri miaka inavyokwenda kuna iOS zinagoma kutumia baadhi ya apps kama sio zote

Ila iphone 7 plus inakubali kupokea toleo mpaka la iOS 15 inayopatikana kwenye iPhone 13 Pro Max

Hii inakupa uhakika wa kuitumia simu miaka mingi

Japo haipokei toleo jipya la iOS 16, toleo la 15 pia ni zuri na linaipa simu thamani ya muda mrefu

Washindani wa iPhone 7 Plus

Mshindani mkubwa wa iPhone 7 Plus kwanza kabisa ni simu zote za madaraja ya kati yenye 5G

Simu mfano wa Samsung Galaxy A14 5G au Redmi Note 12 Pro 5G zina teknolojia mpya na kamera kali kuliko iPhone 7 Plus

Samsung Galaxy S9 ni simu ya zamani yenye ubora sawa na hii iphone

Neno la Mwisho

Kuna watu wanapenda kumiliki simu za iphone ila bei huwa ni kikwazo

Ni ngumu kupata iphone mpya kabisa kwa shilingi laki tano

Mbadala ni kutumia simu ambazo zimetumika tena za zamani

iPhone 7 Plus inaweza ikawa ni huo mbadala tena kwa bei ya chini

Kumbuka Apple hawaundi tena hizi simu kwa sasa utakazokutana nazo zote kwa wakati huu ni used haijalishi ipo kwenye hali gani

Maoni 11 kuhusu “Bei ya iPhone 7 plus na Nafasi Yake 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram