SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy S10 Plus na Ubora Wake 2023

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 23, 2023

Simu ya Samsung Galaxy S10+ iliingia sokoni mwaka 2019 ikiwa kama simu ya daraja la kwanza

Kwa mwaka 2023 kuna matoleo ya daraja la kati yanaoizidi Galaxy S10 Plus kutoka makampuni mengine na hata samsung yenyewe

samsung galaxy s10+ thumbnail

Kitu kinachofanya bei ya samsung galaxy S10 Plus kuwa ndogo kwa sasa

Ila kwa sasa nyingi ni zile simu used kwa sababu ni miaka minne tayari imepita hivyo ni ngumu kupata ikiwa mpya kabisa

Bei ya Samsung Galaxy S10+ ya GB 128

Samsung yenye ukubwa ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 8 inauzwa shilingi 577,000 kwa hapa Tanzania

Bei ni ya simu iliyotumika na inaweza kukushangaza

Ukifuatilia sifa zake ambazo zimeorodheshwa na kisha ukaifananisha na simu ya Redmi Note 12   utaona galaxy ina vitu vingi vya ziada

samsung s10 plus summary

Vitu ambavyo vinapatikana kwenye simu za bei ghari na kubwa

Kwa hiyo hata Samsung s10 plus used bei yake haiwezi kushuka sana

Kwa mfano uimara wa bodi na ubora wa kioo sio rahisi kukuta kwenye simu za daraja la kati zilizotoka kipindi cha 2022 na 2023

Sifa za Samsung Galaxy S10 Plus

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 855
  • Core Zenye nguvu Kubwa(1) – 1×2.84 GHz Kryo 485
  • Core Zenye Nguvu(2)-3×2.42 GHz Kryo 485
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.78 GHz Kryo 485
  • GPU-Adreno 640
Display(Kioo) Dynamic AMOLED,
Softawre
  • Android 9
  • One UI 4.1
Memori UFS 2.1, 512GB,128GB,1TB na RAM 8GB,6GB,12GB
Kamera Kamera tatu

  1. 12MP,Dual pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(telephoto)
  3. 16MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.4inchi
Chaji na Betri
  • 4100mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 577,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy S10 Plus

Simu ina kamera nzuri inazoziacha mbali simu zilizotoka miaka ya karibuni

Ina bodi ngumu na imara ambayo haipitishi maji kirahisi

Inakuja na memori kubwa ya kutosheleza kuhifadhi mafaili

Utendaji wake ni wa kuridhisha unaoweza kufungua vitu kwa wakati mmoja pasipo kuwa na shida

Ina kioo chenye rangi nyingi na chenye kuonyesha vitu kwa uzuri

Inatumia mifumo mitatu ya GPS kitu kinachokupa uhakika wa kupata data sahihi za eneo fulani

Uwezo wa Network

Kikawaida simu za daraja la juu kwa hivi sasa husapoti mtandao wa 5G

Lakini Samsung Galaxy S10 Plus inasapoti mwisho mtandao 4G

Inatokana na uhalisia kuwa 5G mwaka 2019 ndio ilikuwa inaanza kwa nchi chache sana

Kwenye upande wa 4G inatumia LTE Cat 20 ambayo kasi yake inafika 5000Mbps kwa kudownload

samsung s10 plus network

Hii ni kasi kubwa hata Oppo A78 5G ya 2023 haifikii

Hata hivyo usisahau 4g ya Tanzania haina kasi inayofika huko

Kingine ni kuwa simu ina masafa yanayotumika maeneo mengi duniani

Utaweza kusafiri nayo popote na ikawa inafanya kazi

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy S10+

Kioo cha Samsung Galaxy S10+ ni aina AMOLED chenye HDR10+

Kikiwa kikiwa na HDR10+ inamaanisha kiasi cha rangi kinachozalishwa ni kikubwa

Kitu kinachoboresha muonekano wa vitu kwa uzuri

Ukizingatia vioo vya amoled huwa na muonekano sahihi wa rangi kama rangi nyeusi

samsung s10 plus display

Ukilinganisha rangi nyeusi kwenye kioo cha IPS LCD na AMOLED  utaona utofauti mkubwa

Uzuri pia resolution yake ni 1440 x 3040 pixels ambayo ni kubwa sana

Maana hata simu za siku hizi nyingi huishia 2400pixel

Ndio maana bei ya kioo cha samsung galaxy s10+ ni kubwa kama unataka kupata ubora uleule

Nguvu ya processor Snapdragon 855

Kwenye upande wa processor kuna galaxy s10 plus za aina mbili

Kwa marekani na china zinatumia snapdragon 855 wakati maeneo mengine zinakuja na Exynos 9820

Kwa hapa tunazungumzia Snapdragon kwani ndio nzuri zaidi kuliko exynoss

samsung s10 plus chip

Chip imegawanyika sehemu tatu, ambapo core yenye nguvu kubwa zaidi ipo moja na inatumia muundo wa Kryo 485 Gold (Cortex A76)

Utendaji wake ni mkubwa kwa kiasi fulani

Maana magemu mengi makubwa makubwa yanacheza kwa resolution kubwa kwa kiwango cha 60fps

Pamoja na processor kutumia nguvu ina ulaji mdogo wa chaji

Hivyo unapata utendaji mkubwa na kwa matumizi madogo ya umeme

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Samsung Galaxy S10 Plus sio kubwa ukilinganisha na viwango vya sasa vya simu za android

Betri yake ina ukubwa wa 4100mAh

Inaweza kukaa na chaji mpaka masaa 11 ikiwa kwenye intaneti muda wote ukiwa unaperuzi

Chaji yake inapeleka umeme kiodogo kwani ni wa wati 15

Umeme huu unasababisha simu kuchukua masaa zaidi ya manne mpaka kujaa

Inahitaji kuwa mvumulivu

Ukubwa na aina ya memori

Kuna galaxy s10+ za aina nne upande wa memori zikianzia GB 128 hadi 1TB

Unaweza ukapata yenye ram ya GB 6, 8 au GB 12

Zenye memori kubwa na bei yake inakuwa kubwa zaidi inayoweza karibia milioni

Aina ya memori inayotumia ni UFS 2.1 ambazo huwa na kasi kubwa inayofika 1200MBps

Ni mara mbili ya memori za eMMC 5.1 zinazotumiwa sana na simu za bei nafuu

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy S10 Plus

Samsung Galaxy S10 Plus bodi yake haipitishi maji kama ikizama kwenye kina cha mita 1.5 kwa muda wa nusu saa

Kwani ina viwango vya IP68

Kwenye kioo imewekewa glassi utoka kampuni ya Gorilla, na nyuma pia hivyo hivyo

Aina ya gorilla ni Gorilla Glass 6 hivi huwa ni vigumu kupasuka labda iwe imeanguka kwenye eneo baya sana

Kiujumla simu ina bodi ngumu na imara inayoweza kukaa muda mrefu

Ubora wa kamera

Simu ina jumla ya kamera tatu unaweza ita samsung macho matatu

Ina kamera ya telephoto maalumu kwa kupiga vitu vilivyopo mbali na ina megapixel 12

Ina kamera ya ultrawide kwa ajili ya kuchukua eneo kwa upana mkubwa na ina megapixel 16

Wakati kamera kuu ina megapixel 12 na kamera mbili zina OIS(Optical Image Stabilization)

samsung s10 plus camera photo

Ubora wa picha ni wa kiwango kikubwa kwenye mwanga hafifu na kwenye mwanga mwingi

Vitu vinaonekana kwa ustadi bila kuathiriwa na mwanga mwingi

Na kiwango cha noise nyakati za usiku si rahisi kukitambua kwani vitu vinaonekana vizuri

Kamera inajitahidi kuonyesha rangi halisi za kitu kinachopigwa picha

Upande wa video inaweza kurekodi mpaka video za 4K tena kwa kiwango cha 60fps

Ubora wa Software

Wakati simu inatoka ilikuwa inakuja na Android 9

Lakini inakubali kupokea toleo jipya mpaka la Android 12

Kwa sasa hivi simu mpya zinatumia Android 13 na hivi karibuni Google watatangaza la kumi na nne

Hata hivyo android 12 bado ni mfumo mzuri unaoweza kusapoti app nyingi kwa muda mrefu

Kwa sababu ni android za zamani sana ndio zinazokutana na utata wa kupokea maboresho ya baadhi ya app.

Washindani wa Samsung Galaxy S10 Plus

Mshindani wa nyakati za sasa ni Samsung Galaxy A14 5G ambayo ina kila kitu kilichopo kwenye s10 plus na pia unapata 5G

Na mshindani mwingine ni Oppo Reno8 5G bila kusahau Redmi Note 12 ambazo zina utendaji unaondana na galaxy s10 plus

Pia, kwa simu za zamani kuna Apple iPhone XS, Huawei Mate 20 Pro na hata Xiaomi Mi 9 bila kusahau

Hizo zote zina sifa zinazoendana kwa kiasi kiukubwa

Neno la mwisho

Samsung Galaxy S10 Plus ni simu yenye umri mkubwa ila ina ubora unaoendana na simu mpya nyingi

Ukiwa nayo utajikuta huoni tofauti na mmiliki wa simu za toleo la daraja la kati

Ila kuna tofauti mkubwa sana kati ya Samsung Galaxy S23 Plus na hii

Kwa miaka ya sasa s10 haiwezi kuwekwa kwenye kundi la simu za daraja la kwanza

 

Maoni 9 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy S10 Plus na Ubora Wake 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram