SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Oppo A78 5G na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 11, 2023

Oppo A78 5G ni simu nyingine ya 5G inayouzwa kwa bei nafuu ukilinganisha na simu zinazotumia mtandao

Ni simu ya mwaka 2023 na inakuja na baadhi ya vitu vipya ambavyo havikuwepo kwenye oppo A77

Bei ya Oppo A78 5G kwa Tanzania inazidi laki sita pia inategemea na mkoa uliopo

oppo a78 5g showcase

Bei inaonekana kuwa ni kubwa ila ukilinganisha na simu nyingi za 5G, bei hii nafuu

Ina sifa zinazochuana na simu ya Redmi Note 10 5G ila redmi inauzwa chini ya laki nne

Kuna sababu za msingi zinasobabisha bei ya oppo kuwa kubwa hasa ukitazama sifa za hii simu

Bei ya OPPO A78 5G ya GB 128

Kwa Tanzania unaweza kuimiliki simu kwa bei ya shilingi 610,000/=

Si bei rafiki kwa mtu anaetaka simu ya laki mbili

oppo a78 5g summary

Uwepo wa 5G na mfumo mzuri wa kamera ndio unaosababisha bei ya hii simu kufika huko

Kama isingekuwa na vifaa vya kawaida kwa kiwango kikubwa ungeweza kuinunua simu kwa bei chini ya laki nne

Vinginevyo huna budi kujichanga kumili simujanja yenye 5G

Sifa za Oppo A78 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 700
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2GHz Cortex A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8GHz Cortex A55
  • GPU-Arm Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 13
  • ColorOs
Memori UFS 2.2,128GB na RAM 8GB na 4gb
Kamera Kamera MBILI

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 610,000/=

Upi ubora wa Oppo A78 5G

A78 inakaa na chaji muda mrefu sabau ya uwepo wa betri kubwa

Inakuja na chaji yenye kasi inayojaza betri kwa muda mfupi

Inasapoti mtandao wa 5G na inadownload mafaili kwa kasi kubwa

Ina ulinzi wa kuzuia manyunyu ta maji

Kamera zake zinatoa picha nzuri hasa nyakati za mchana

Inakuja na mfumo endeshi mpya wa android

Uwezo wa Network

Kama jina la simu linavyooleza ni kuwa utaweza kutumia 5G bila shida

5g ya OPPO A78 spidi yake inafika zaidi ya 1000Mbps hasa ukiwa nje

Ukiwa ndani ya jengo spidi inashuka mpaka mpaka 500Mbps

oppo a78 5g network

Mawimbi ya 5G huwa yanapata changamoto pale inapokutana na kigingi kama ukuta

Ila hata hivyo spidi ya 500Mbps ni kubwa kwa sababu ukipakua gemu la GB 1.2 kule playstore inachukua sekunde 30 tu kumaliza

Hiki kitu ni kigumu kukipata kwenye 4G ya mitandao ya hapa Tanzania

Bahati mbaya kuwa 5G Tanzania ndio kwanza ipo hatua za mwanzoni bado haijasambaa sehemu kubwa hata kwa mji kama Dar Es Salaam

Ubora wa kioo cha Oppo A78 5G

Kioo cha hii simu ni cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1080 pixels

Na kinasapoti refresh rate ya 90Hz ni kama tu ilivyo kwa simu Tecno Spark 10 Pro

Refresh rate 90Hz husaidia simu kuwa “smooth” na nyepesi wakati ukiwa unatachi kioo mfano kuangalia picha za instagram picha zinakuwa zinadirika kwa mwendo mzuri na wa haraka

Ila kuna kasoro kwenye hii simu upande wa kioo

oppo a78 display

Resolution ni ndogo ukilinganisha na bei lakini pia kutumia kioo cha IPS LCD ni kama simu imeshushwa hadhi

Kwa bei iliyoanishwa simu ilipaswa kuwa na kioo cha amoled na resolution kubwa

Resolution ndogo husababisha muonekano usiovutia kwa baadhi ya vitu

Yaani kuna vitu vinakuwa vinaonekana vikubwa kwenye simu sababu ya mkusanyiko mdogo wa pixel kwa kila inchi

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 700

Oppo A78 5G inatumia processor ya MediaTek Dimensity 700 kufanya kazi zake

Ina nguvu ya wastani kutokana na muundo wake wenye nguvu kutumia Cortex A76 yenye kasi inayofika 2.2GHz

Kwa viwango vya sasa chip zenye nguvu huanza kutumia Cortex A78 na matoleo mengine mapya

oppo a78 5g processor

Kwa mpenzi wa magemu makubwa, atalazimika kucheza kwa resolution za chini kuepuka kugandaganda na simu kupata moto

Ukicheza kwa resolution za juu simu itapata shida hata kufika kwa frem 30 na hali ya kuganda ganda itakuwa inatokea

Dimensity 700 ina ufanisi mkubwa kwenye matumizi ya betri

Nguvu yake ni ya wastani na ndio maana betri inachelewa kuisha

Uwezo wa betri na chaji

Oppo A78 5G ina betri kubwa ya 5000mAh na inakuja na chaji ya 33W wanaita supervooc

Chaji yake inajaza betri kwa asilimia 100 kwa karibu masaaa mawili

Hii kasi inakaribiana na simu na simu ya Samsung Galaxy A14 5G

oppo a78 5g charge

Ukiwa unaangalia video muda wote na ukaseti mwanga kwa kiwango cha juu kabisa simu inachukua masaa 12 kuisha chaji

Na ukiwa unaitumia matumizi madogo inaweza mpaka siku mbili chaji kuisha

Kwa kifupi uwezo wa Oppo A78 5G kutunza chaji ni wa kuridhisha isipokuwa kasi ya chaji ni tofauti na kiwango cha wati chaji inayopeleka

Ukubwa na aina ya memori

OPPO hii mpya inatumia  memori aina ya UFS 2.2 ambazo huweza kusoma na kuandika data kwa kasi ya 1200MBps

Kasi hii inafanya mafaili kuhifadhiwa kwa haraka wakati unatumia 5G

Na pia ukiwa unakopi faili kwenda kwenye simu basi kitendo hiki kitachukua muda mfupi sana

A78 5G ipo ya aina moja upande wa memori na yenyewe ina GB 128 na RAM GB 8 au GB 4

Ni ukubwa sahihi kuhifadhi vitu vingi ndani ya simu

Uzuri mwingine ni kuwa simu ina sehemu ya kuweka memori card

Hivyo ikijaa utaongeza nafasi kwa kununua memori kadi

Uimara wa bodi ya OPPO A78 5G

Bodi ya oppo a78 5g ina uwezo wa kuzuia maji tiririka kama yale ya mvua

Kwani ina viwango vya IP54

oppo a78 5g body

Ila haiwezi zuia maji kama simu ikizama kwenye kina cha maji mengi

Upande wa nyuma simu ina plastiki wala haina kioo

Ni muhimu kuwa na kava ili rangi isichunike kirahisi

Ubora wa kamera

Simu inakuja na kamera mbili pekee moja ikiwa na megapixel 50 na nyingine ina megapixel 2

Kiuhalisia simu ina kamera moja tu kwa sababu kamera ya depth haipigi picha

Huwa inatumia kukotoa umbali kati ya kamera na kinachopigwa picha

oppo a78 5g kamera 1

Depth sensor haina umuhimu kwa miaka na sijui kwa nini kampuni bado wanaendelea kuziweka

Ubora wa picha ni wa kiwango kizuri kiasi fulani kwa nyakati zote za usiku na mchana

Kiwango cha chengachenga(noises) ni ngumu kuziona ila zipo

oppo a78 5g photo quality

Na usahihi wa rangi na utofautishaji kati ya rangi nyeusi na nyeupe ni wa kuridhisha

Ukitumia AI muonekano wa picha unakuwa hauwendani na picha halisi

Upande wa video simu inaweza kurekodi video za full hd pekee

Ubora wa Software

Oppo A78 5G inatumia mfumo wa Android 13 na mfumo wa ColorOS 13

oppo a78 5g software

Mfumo wa coloros ni mzuri na unakuja na apps zingine za ziada

Changamoto utakayokutana nayo ni matangazo kwa njia ya notification

Yapi Madhaifu ya A78 5G

Mfumo wa kamera wa hii simu unakosa kamera ya Ultrawide

Kamera ya ultrawide huwa inapiga picha eneo pana sana mfano uwanja wa mpira

Matangazo kwenye mfumo wa software ni kitu kinachokera

Ukizingatia bei ya simu ni kubwa hakukuwa na haja ya kuwa na matangazo mengi

Chaji yake inachukua muda mrefu ukilinganisha na wati za chaji

Chip yake si nzuri kucheza gemu nzito kwenye resolution kubwa

Neno la Mwisho

Matoleo ya 5g ya bei ya kati yanazidi kuachiwa ikiwemo OPPO A78 5G

Sio mbaya ukajiandaa wakati ukisubiria 5G kuenea maeneo mengi

Mpenzi wa kamera na utendaji, hii simu inakidhi hitaji lako kwa kiasi kikubwa

Ila ukiona huielewi kuna mbdadala kama Mi 11 , Realme 10 na hata OPPO Reno8 5G

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram