SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Simu Mpya

Sihaba Mikole

February 22, 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11

Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la juu

Hivyo basi bei zake sio ndogo kwa maana inahusisha simujanja zinazouzwa kwa zaidi ya laki sita

Ipo pia orodha ya mwaka 2023 ya simu za bei rahisi zenye kamera nzuri

TWENDE KAZI

1. Sony Xperia 5 V

Bei inayouzwa: 2,100,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 8

Sony Xperia 5 V kwa mara ya kwanza iliwekwa wazi mwezi septemba 2023

Bado ni simu mpya upande wa Sony japo inatumia processor ya Snapdragon 8 Gen 2

sony v experia

Ina kamera mbili za ultrawide na wide ambazo zote zinapuga picha kwa ufanisi mzuri

Betri yake ujazo wake ni 5000mAh na chaji ina kasi ya 30W

2. Samsung Galaxy S24 Ultra

Bei inayouzwa: 3,500,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Utendaji wa Samsung Galaxy S24 Ultra ni mkubwa sana kwani inatumia processor yenye nguvu ya Snapdragon 8 Gen 3

samsung s24 ultra thumbnail

Hii simu imetoka mnamo mwezi januari 2024

Inatarajiwa kuwa ndio simu bora kwa mwaka huu kutokana na uwepo wa mambo mengi ya  akili bandia(Artificial Intelligence)

Tembele hapa, uwezo na ubora wa Samsung Galaxy S24 Ultra

3. Samsung Galaxy S24+

Bei inayouzwa: 2,500,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Ina jumla ya kamera zipatazo tatu na zote zinapiga picha nzuri

samsung s24 plus showcase

Utendaji wake na wenyewe ni mkubwa kwani inatumia chip yenye nguvu kwa kila kazi

Betri inakaa na chaji muda mrefu tu kwani ina ukubwa wa 4900mAh

Chaji inapeleka kasi ya wati 45

4. Redmi Note 13 Pro+

Bei inayouzwa: 930,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Redmi Note 13 Pro+ ina utendaji wa kuridhisha kwa sababu chip iliyotumika ya MediaTek Dimensity 7200 zina core zenye muundo wenye kusukuma kazi tano kwa mzunguko mmoja kati ya mizunguko bilioni mbili kwa sekunde

redmi note 13 pro+

Japokuwa utendaji wake unaachwa kwa mbali na Snapdragon 8 gen 3 ila ni chip nzuri pia kwenye utendaji

Hii simu pia imetoka septemba mwaka 2023, lakini bado ni toleo jipya upande wa simu za note

5. Xiaomi 14 Pro

Bei inayouzwa: 1,800,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Xiaomi 14 Pro inaweza ikawa ni mbadara mzuri wa Samsung Galaxy 24 Ultra

Maana sifa kwenye utendaji, kioo, na betri zinafanana

xiaomi 14 pro

Moja ya kitu utakachofulia kwenye Xiaomi 14 Pro ni kasi yake ya kuchaji inayofika wati 120

Hii inaweza jaza betri ndani ya dakika thelathini kwa 100% toka zero

6. iQOO 12

Bei inayouzwa: 1,600,000/-, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Jina la hii simu linaweza kuwa gani masikioni mwa wa Tanzania wengi

Ila simu za iQOO huwa ni nzuri na kampuni ambayo ni tawi la vivo

iqoo 12

Utendaji wa iQOO hautofautiani na Xiaomi 14 Pro kwani na yenyewe inafanya kazi kwa kutumia processor ya Snapdragon 8 Gen 3

Kioo chake na chenyewe ni cha LTPO AMOLED kama ilivyo kwa simu zingine za matoleo ghari

7. iQOO 12 Pro

Bei inayouzwa: 1,800,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

iQOO 12 Pro ni kaka mkubwa wa iQOO 12

iqoo 12 pro

Hii simu inapeleka chaji kwa umeme mkubwa wa wati 120

Hivyo ndani ya nusu saa betri linaweza kujaa kikamilifu

Pia Snapdragon 8 Gen 3 ndio imetumika kama processor kwenye simu ya iQOO 12 Pro

8. Asus Rog Phone 8 Pro

Bei inayouzwa: 3,400,000/=, ukubwa ni : GB 512, RAM GB 16

Katika hii ordha hii ndio simu yenye bei kubwa zaidi

Kisifa, inafanana na simu zingine zilizotangulia kwani inatumia processor ya Snapdragon 8 Gen 3

asus rog 8 pro

Utofauti ambao Asus Rog Phone 8 Pro imejiwekea ni ukubwa wa RAM ambayo ni GB 16.

Ina betri yenye ukubwa wa 5500mAh na Chaji yenye kasi ya wati 65

Kamera zake zipo tatu na nzuri kiasi chake

9. Asus Rog Phone 8

Bei inayouzwa: 2,500,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 16

Hii simu na yenyewe utendaji wake ni mkubwa kwani inatumia Snapdragon 8 Gen 3

Kioo chake ni cha LTPO Amoled kama ilivyo kwa simu nyingi za bei kubwa

asus rog 8

Kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 8K ambayo ni resolution kubwa inayohitaji simu yenye uwezo mzuri kurekodi

Betri yake ukubwa ni 5500mAh na kiwango cha kasi ya kuchaji ni wati 65

10. Tecno Spark 20 Pro+

Bei inayouzwa: -, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 8

Hii ni simu nyingine ya daraja la kati ambayo imetoka desemba 2023

Hivyo ni simu ambayo ipo kwenye trendi kwa mwaka 2024

tecno spark 20 pro+

Kioo chake ni cha aina ya amoled chenye refresh rate ya 120Hz

Utendaji wake ni wa wastani unaoweza kidhi vitu kwa ustadi

11. Tecno Phantom V Flip

Bei inayouzwa: 1,500,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 8

Simu ya Tecno Phantom V Flip ni simujanja kukunja na kukunjua

Ubora wake umejikita kwenye kwenye utendaji , kioo cha amoled na kasi kubwa ya kuchaji simu

tecno phantom flip

Ina jumla ya kamera mbili tu zenye lenzi za ultrawide na wide

Betri yake si kubwa kutokana na udogo wa simu kwani ina 4000mAh

12. Infinix Hot 40 Pro

Bei inayouzwa: 450,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 8

Infinix Hot 40 Pro ndio simu ya bei nafuu zaidi kwenye hii orodha

infinix hot 40 chaji

Ni simu ya daraja la kati na utendaji wake ni wastani kwani inatumia chip ya Mediatek Helio G99

Kamera zake ni za kawaida japo zinaendana na bei ya simu kiujumla

Unaweza ifuatilia kiundani hapa: Ubora na bei ya infinix hot 40 pro

13. Oppo Find X7 Ultra

Bei inayouzwa: 2,300,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Oppo Find X7 Ultra ni moja ya simu bora kwa mwaka 2024 inachuana na simu za iPhone na matoleo ya Samsung S24

Idara yake ya kamera iko kamili sana kwenye kamera zake zote nne

oppo find x7 ultra

Kioo chake ni cha LTPO AMOLED ambacho kimetumiwa na matoleo mengi ya daraja la juu

Betri ni kubwa kwa ujazo wa 5000mAh

14. Oppo Find X7

Bei inayouzwa: 2,300,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 12

Oppo Find X7 ni moja ya simu yenye kamera kali na nzuri kwa mwaka 2024

Inatumia processor yenye nguvu kubwa ya kiutendaji ambayo ni Mediatek Dimensity 9300

oppo find x7

Kioo chake kina vikorombwezo vyote vinavyoboresha muonekano wa vitu, ikizingatiwa ni cha aina ya LTPO AMOLED

Kama ilivyo kwa simu nyingi kuwa na betri ya 5000mAh, na hii pia ina ukubwa huo

15. Vivo V30 Lite

Bei inayouzwa: 1,300,000/=, ukubwa ni : GB 256, RAM GB 8

Vivo V30 Lite ni simu aina ya daraja la kati iliyotoka desemba 2023 yaani ina miezi miwili tangu iingie sokoni

Utendaji wake sio mkubwa ni wa wastani kwani inatumia chip ya Snapdragon 695 5G

vivo v30 lite

Kamera zake zipo tatu ikiwemo ya Ultrawide

Kioo chake ni kizuri pia ambacho ni amoled chenye refresh rate kubwa

Betri yake ni kubwa ila haifiki 5000mAh bali ni 4800mAh

16. Vivo Y100

Bei inayouzwa: 800,000/=, ukubwa ni : GB 128, RAM GB 8

Vivo Y100 ilingia rasmi sokoni februari ya mwaka 2024

Hii simu inatumia processor ya Snapdragon 4 Gen 2 ambayo ina core zenye kubwa za wastani zipatazo mbili

vivo y100

Simu ina idadi ya kamera mbili aina za wide na ultrawide

Betri yake na yenyewe ni kubwa kama ilivyo kwa simu zingine, ukubwa wake ni 5000mAh

17. Huawei Nova 12 Ultra

Bei inayouzwa: 1,800,000/=, ukubwa ni : GB 512, RAM GB 12

Huawei Nova 12 Ultra imetoka mwezi wa kwanza 2024

huawei nova

Utendaji wake unategemea processor iliyoundwa na Huawei wenyewe ya Kirin 9000S ambayo imewafanya USA kubaki midomo wazi

Pitia hapa kujua kwa nini: Hatua kubwa imepigwa na Huawei

Betri yake ni 4600mAh na idadi ya kamera ni mbili

18. Huawei Nova Y72

Bei inayouzwa: 1,600,000/=, ukubwa ni : GB 128, RAM GB 8

Hii ni simu inayotumia mfumo wa HarmonyOS 4.0

huawei nova 72

Soko kubwa la hii simu ni china kwa maana kuna baadhi ya apps za google hazifanyi kazi kwenye hii simu

Utendaji wake wa wastani kwani inatumia chip ya Kirin 710A yenye Cortex ya kitambo kutokana na vikwazo

Betri yake ina ukubwa wa 6000mAh na kamera zake zipo mbili tu

19. Google Pixel 8 Pro

Bei inayouzwa: 1,600,000/=, ukubwa ni : GB 128, RAM GB 12

Google Pixel 8 Pro ni simu ya kwanza kuja na Android 14 Oktoba 2023

Bado ni simu nzuri sana na shindani kwa mwaka 2024

Utendaji wake wa kuridhisha unachagizwa na kutumia chip ya Google Tensor G3

Betri ina ujazo wa mAh 5050 ambayo ni kubwa tu

Pia kioo aina ya LTPO OLED chenye refresh rate ya 120, kioo kizuri kiujumla

20. OnePlus 12

Bei inayouzwa: 2,400,000/=, ukubwa ni : GB 512, RAM GB 16

OnePlus 12 iliingia rasmi mwishoni mwa mwaka 2023

-one plus

Utendaji wa hii simu ni mkubwa na unaendana na kwa kiasi fulani na Samsung Galaxy S24

Ukubwa wa betri ni 5400mAh ambayo inaweza kukaa na chaji masaa zaidi ya kumi hata ukiwa unacheza gemu

Kioo chake ni cha ltpo amoled na kamera zake zipo tatu

Maoni 10 kuhusu “Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram