SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Simu Mpya

Sihaba Mikole

March 2, 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi

Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco

Hapa kuna orodha ya simu mpya za xiaomi na redmi kwa mwaka 2024 na bei zake

Listi imekusanya xiaomi za bei ndogo, ya kati na bei kubwa

Hivyo kuna uwanda mpana wa kuchagua simu kulingana na kiasi cha pesa ulicho nacho

Xiaomi Pad 6S Pro 12.4

Bei ya Xiaomi Pad 6S Pro: 2,000,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Xiaomi Pad PS Pro 12,4 ni kishikwambi kilichotoka mwaka 2024 mwezi februari

Ina mfumo wa chaji unaopekea umeme wa wati 120

redmi pad 12

Hivyo betri yake yake kubwa ya 10000mAh inajaa ndani ya lisaa moja

Utendaji wak ni kutokana na kutumia chip ya Snapdragon 8 Gen 2

Xiaomi Redmi A3

Bei ya Xiaomi Redmi A3: 250,000/= ,Ukubwa wa Memori: 64GB, RAM:  3GB

Redmi A3 ni xioami ya bei nafuu iliyotoka mwezi februari 2024

Haina kamera nzuri ila ina kioo kikubwa chenye refresh rate ya 90Hz

redmi a3

Betri yake ina ukubwa wa 5000mAh ila kasi ya chaji yake sio kubwa

Inafaa kwa mtumiaji mwenye matumizi ya kawaida kwani inakaa na chaji muda mrefu

Redmi Note 13 Pro 4G

Bei ya Redmi Note 13 Pro 4G: 600,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  8GB

Simu ya Redmi Note 13 Pro 4G inatumia kioo chenye uonteshaji mzuri wa vitu

Kioo hicho kinatumia teknolojia ya AMOLED

redmi note 13 pro 4g

Chaji yake ina uwezo wa kupeleka chaji kwa kiwango cha wati 67

Kwa maana hiyo betri yake ya mAh 5000 haiwezi chukua muda mrefu kujaa

Ila hili ni toleo ambalo halina 5G ni kwamba ina 4G kama mtandao wenye kasi zaidi

Redmi Note 13 4G

Bei ya Redmi Note 13 4G: 500,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  6GB

Hii ni simu nyingine ya daraja la kati yenye sifa nzuri upande wa kioo, kamera, na utendaji wa wastani

Processor yake ina nguvu ya wastani, chip hiyo ni Snapdragon 685

Ina betri yenye ukubwa wa 5000mAh kama ilivyo kwa simu nyingi

redmi note 13 4g

Kamera yake kubwa ina megapixel 108 na inaweza kurekodi mpaka video za FULL HD

Hii sio kama Redmi Note 10 ambayo kamera yake inarekodi mpaka video za 4K

Redmi Note 13

Bei ya Redmi Note 13: 700,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Hii ni Redmi Note 13 yenye 5G na inatumia processor tofauti na ile yenye utendaji

Redmi Note 13 inatumia chip ya Mediatek Dimensity 6050

redmi note 13 snapdragon

Ukiondoa uwepo wa 5G sifa zingine zote zinaendana na redmi note 4G

Hakuna tofauti kwenye vipengere vingine

Xiaomi Poco X6 Pro

Bei ya Poco X6 Pro: 890,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Kioo cha Poco X6 Pro kina HDR10+ kitu kinachosaidia kuwa na utajiri wa rangi na kuonyesha vitu vingi kwa rangi zake halisi

Hii simu inatumia mfumo mpya wa Xiaomi unaitwa HyperOS badala MIUI

Ina kamera tatu huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 64

redmi poco x6 pro

Chaji yake inapeleka umeme kwa kiwango cha wati 67

Ina betri kubwa pia na ukaaji wa chaji ni wa kuridhisha

Xiaomi Poco X6

Bei ya Poco X6: 750,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Hii simu ina kamera zipatazo tatu ambapo kamera kubwa inaweza kurekodi video za 4K kwa kiwango cha 30fps

Ina processor ya Snapdragon 7s Gen 2 ambayo nguvu yake kiutendaji ni kubwa pia

poco x6 plain

Betri ina ukubwa wa 5100mAh, ongezeko la 100mAh ukilinganisha na simu nyingi za siku hizi

Chaji yake ya wati 67 inaweza kujaza betri hili kwa dakika 44

Xiaomi Poco M6 Pro

Bei ya Poco M6 Pro: 610,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  8GB

Simu ya Poco M6 Pro iliingia sokoni mnamo mwezi januari 2024

Hii ni poco yenye 4G kwani kuna Poco M6 Pro 5G ya mwaka 2023 mwezi august

poco m6 pro

Hii ina kioo kizuri cha AMOLED chenye uangavu unaofika nits 1000

Inatumia chip ya daraja la kati Mediatek Helio G99

Na yenyewe chaji yake ina wati 67 hivyo betri itajaa kwa haraka

Xiaomi Poco M6

Bei ya Poco M6: 300,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Xiaomi Poco M6 ni simu ya bei nafuu ambayo ina vitu vilivyopunguzwa ukilinganisha na Poco M6 Pro

Kwa mfano, skrini ya POCO M6 sio ya amoled bali ni IPS LCD japo refresh rate yake ni kubwa

poco m6

Siku hizi app nyingi zinachukua nafasi kubwa ya simu kitu kinachochangia RAM kujaa

Hivyo kuwa na simu yenye RAM ya GB 4 inaweza kuwa changamoto

Hata hivyo, utendaji wa Poco M6 ni wa wastani unaoweza fanya vitu bila tatizo

Ila itafaa zaidi kwa matumizi ya wastani pia

Redmi 13R

Bei ya Redmi 13R: 370,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Hii ni simu yenye utendaji wa wastani na simu ya daraja la kati

Inatumia processor yenye nguvu ya wasatani ambayo ni Dimensity 6100+

redmi 13r

Kioo chake ni vile vyenye resolution 720 na ni cha aina ya IPS LCD

Kasi ya chaji yake ni 18W, hii inachukua muda kidogo kujaza simu

Ina kamera moja yenye megawati 50 na ulengaji wa PDAF

Redmi 13C 5G

Bei ya Redmi 13C 5G: 370,000/= ,Ukubwa wa Memori: 128GB, RAM:  4GB

Simu ya Redmi 13C 5G ni toleo lingine la simu ya 5G ya bei nafuu

Sifa zote za Redmi 13C 5G zinalingana na Redmi 13R

redmi 13C 5g

Kinachotofautisha ni hiyo teknolojia ya mtandao wenye kasi zaidi kwa sasa

Kwa hiyo mnunuaji ana uwanda wa kuchagua simu aitakayo kati ya hizi mbili

Redmi K70

Bei ya Redmi K70: 970,000/= ,Ukubwa wa Memori: 256GB, RAM:  12GB

Simu ya redmi k70 ni moja ya simu kali amabayo imetoka novemba 2023

Ila inatazimiwa kuwa ni toleo litakaloendana kiushandani na matoleo mapya ya 2024 yanayotarajiwa kutoka mbeleni

Redmi K70 inapewa nguvu na chip kutoka kwa kampuni Qualcomm ambayo ni Snapdragon 8 Gen 2

redmi k70

Ina kamera tatu na kamera moja inapiga picha hadi za 8K

Kitu kingine kitakachokufurahisha ni aina ya chaji iliyo nayo

Chaji yake inaweza kupeleka umeme kwa spidi mpaka ya 120w

Hii inajaza simu kwa muda wa dakika 28

Xiaomi 14 Ultra

Bei ya Xiaomi 14 Ultra: 4,200,000/= ,Ukubwa wa Memori: 512GB, RAM:  16GB

Xiaomi 14 Ultra ni simu mpya kabisa na imeingia rasmi sokoni mwezi februari 2024

Katika hii orodha, hii ndio simu mbayo imekamilika kila idara na ubora mwingi

xiaomi 14 ultra

Kamera zake tatu za wide, ultrawide na telephoto zote zina mfumo mzuri wa upigaji picha

Simu inatumia processor yenye nguvu kubwa kiutendaji aina ya Snapdragon 8 Gen 3

Hii ina maanisha Xiaomi 14 Ultra ipo kundi moja na Samsung Galaxy S24 Ultra na iPhone 15 Pro Max

Kwa bahati mbaya bei yake ni kubwa na ni maalumu kwa wenye uwezo wa kununua simu kwa bei ya milioni nne

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

redmi 12c thumbnail

Bei ya Redmi 12C na Sifa Zake Muhimu

Mwishoni mwa 2022 Kampuni ya Xiaomi ilitoa toleo la simu ya Redmi 12C Ni simu ya daraja la chini hivyo bei yake ni ndogo hata kwa ambazo memori zake ni […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram