SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

July 25, 2023

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022

Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache

4-redmi 10a showcase

Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki tatu kwa hapa Tanzania

Kutokana na aina ya sifa ilizo nazo haifai kuuzwa kwa bei inayozidi laki tatu

Fuatilia kiundani kutambua jinsi sifa zake zinavyofanya bei yake kuwa ndogo na ujue kama inakufaa ama haikufahi

Bei ya Redmi 10A ya GB 64

Redmi 10A yenye ukubwa wa GB 64 inapatikana kwa shilingi 250,000

Hii ni bei ya mwaka 2023

Redmi 10A zenye ukubwa zaidi ya huo bei inakuwa zaidi ya hapo

Baadhi ya vitu vinavyofanya bei kuwa ndogo ni ubora mdogo kwenye kamera, utendaji na hata kioo

Hata hivyo, kwa mtumiaji wa kawaida simu inayoweza kukidhi mahitaji yake na anaweza asione shida yoyote

Tatizo tu linakuja kwa mtu anayetaka simu ya kupiga picha nzuri ndio atakutana na changamoto kwenye kamera

Sifa za Redmi 10A

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek helio G25
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.5 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
  • MIUI 12.5
Memori eMMC 5.1,128GB,64GB,32GB na RAM 3GB,6GB,4GB
Kamera Kamera moja

  1. 13MP,AF(wide)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-10W
Bei ya simu(TSH) 250,000/=

Upi ubora wa Redmi 10A

Inakuja na machaguo matatu moja ikiwa na memori kubwa yenye kutosheleza kuhifadhi vitu vingi

Uzuri ni kuwa bei yake inavumilika

Ina ukaaji wa chaji wa masaa mengi kwa sababu ya betri kubwa na utendaji unaotumia moto kidogo

Ni moja ya simu ya 4G yenye bei ndogo

Kama ilivyoelezwa mwanzoni, redmi 10a ni ya daraja la chini, vitu vingi vilivyopo havina ubora mkubwa

Yapo mambo yanayoweza kukidhi mahitaji yako kama ukiziangalia sifa zingine kiundani

Uwezo wa Network

Redmi 10A inasapoti mpaka mtandao wa 4G kama kiwango cha juu

4G ina kasi ya wastani inayofika 300Mbps ya kupakuwa vitu

Aina hii 4G huitwa LTE Cat 7

Kasi ya kawaida ila kwa Tanzania hakuna mtandao wenye kasi hii kwa upande wa 4G

Hii inamaanisha kwa mazingira ya nchini simu bado inafaa

Kwa maana kasi za mitandao ya simu huwa ni chini 100Mbps hata kama eneo lina watu wachache wanaotumia intaneti

Ubora wa kioo cha Redmi 10A

Ubora wa kioo cha redmi ni wa kawaida kutokana na kutumika kwa teknolojia ya IPS LCD

IPS LCD haina ubora mkubwa wa uwasilishwaji wa rangi ukilinganisha na vioo vya AMOLED

Kama ukitazama picha moja kwenye simu yenye kioo cha lcd na amoled, amoled, picha huonekana vizuri sana

Mbali na kuwa na kioo cha IPS LCD, na resolution sio kubwa ambayo ni 720 x 1600 pixels

Uangavu wake pia ni wa kiwango kidogo cha nits 400

Kwa maana kwenye jua kali sana mwanga kwenye kioo unakuwa sio wa kiwango cha kuonesha vitu vizuri

Nguvu ya processor Mediatek Helio G25

Nguvu ya processor mediatek helio g25 kwa ajili ya kufanya kazi kwenye vitu vinavyotumia nguvu ndogo

Linapokuja swala la vitu vinavyotumia nguvu kubwa hii simu haitokupa kitu kizuri

Nguvu ndogo ya processor yake ina sababishwa na kutumiwa kwa muundo aina ya Cortex A53 kwenye core zote nane

Cortex A53 ni muundo unaowekwa kwenye chip kwa ajili ya kutumia umeme kidogo kwa gharama ya utendaji wa chini

Ndio maana hii simu inakaa na chaji muda mrefu

Kwa mtu ambaye matumizi yake ni kupiga simu na intaneti kidogo haitaji sana processor yenye nguvu kubwa

Ila kumbuka processor ndio ubongo wa simu ikiwa duni vitu vingine vyote vinakuwa chini moja kwa moja

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Redmi 10A ina uwezo wa kupeleka chaji kwa kasi ya wati 10

Ni kiwango kinachozaja betri ya 5000mAh kwa masaa yanayozidi matatu

Betri yake ya 5000mAh ina ukaaji wa masaa mengi yanazidi 14 kama hutumii intaneti mara kwa mara

Pia soc yake inatumia umeme kidogo sana na vifaa vingine vina matumizi madogo

Hivyo kwa mtu anaeishi maeneo yenye changamoto ya umeme hii simu ni msaada mzuri

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo ya aina sita kwenye upande wa memori na ram

Kiwango kikubwa cha RAM ni GB 6 na memori ya kuhifadhi vitu ni GB 128

Kwa bahati mbaya bei inaongezeka kutokana na ukubwa wa memori

Kama utakuwa ni mtu wa kupakuwa sana mafaili, memori ya GB 128  inafaa zaidi

Iwapo kipato ni changamoto sana basi ya GB 32 inatosheleza kwa sababu bei yake ni 170,000

Uimara wa bodi ya Redmi 10A

Bodi ya redmi 10a ni ya plastiki

Haina uimara wa kuzuia maji kama simu ikiingia ndani ya maji

Kwani haina viwango IP vinavyoainisha uwezo wa kuzuia maji pindi simu ikizamishwa kwenye kina fulani

Kiujumla ni muhimu kuweka skrini protekta kwa sababu simu haina ulinzi wa aina yoyote ya kioo

Hivyo kuimarisha simu ikae muda mrefu huna budi kuwa na kava na protekta ya skrini

Ubora wa kamera

Hii simu haina mfumo mzuri wa kamera kiujumla

Ina kamera moja tu yenye megapixel 13 huku ikiwa na ulengaji wa kiwango duni ya AF

Hivyo ubora wa picha hasa kwenye mwanga hafifu sio mzuri

Upande wa video kamera yake inaweza kurekodi video za full hd pekee yake kwa kiwango cha 30fps

Hii inatokana na aina ya processor kutokuwa na nguvu ya kutosha kuchakata data za kutosha

Ubora wa Software

Redmi 10A inatumia android 11 na haina uwezo wa kupokea toleo jipya la android 13

Hata kwenye matoleo ya android ya miaka ya karibuni kumekuwa hakuna tofauti kubwa sana

Tena kwa redmi unaweza usione tofauti yoyote

Mbali na android 11 simu inakuja na mfumo wa android 12.5

MIUI ina vitu vingi kwa mfano app yake ku-screenshot inaweza kuchukua peji  kwa urefu unaotaka wewe

Kwa sababu yenyewe inaruhusu ku-scroll

Kitu utakachochukia kwenye MIUI ni matangazo japo sio yale ya kukela

Ila karibu app zote za MIUI huwa zina matangazo

Washindani wa Redmi 10A

Mshindani wa kwanza Redmi 10A ni infinix hot 20i

Infinix hot 20i imetumia vitu vyote vilivyotumika kwenye redmi 10a

Ila hot 20i inakuja na android 12 yaani toleo la mbele ya android

Na bei ya infinix ni sawa na ya redmi

Bingwa mwingine ni Samsung Galaxy A04

Japo yenyewe bei yake ipo juu kidogo ila inaruhusu kupokea android 13 ambalo ni jipya

Kwenye simu hakuna kitu cha muhimu kama kupata sapoti ya software

Neno la Mwisho

Redmi 10A ina bei ya kizarendo ila usitarajie makubwa sana

Kiukweli na kiuharisia simu nzuri kwenye kampuni yoyote huuzwa bei kubwa angalau laki tatu kwenda mbele

Ila kama hii simu unamnunulia mtu mfano mama au baba ambaye kijijini hili ni chaguo zuri kwake

 

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram