SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Hot 20i na Sifa Zake Muhimu

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 22, 2023

Kampuni ya infinix iliingiza sokoni simu ya Infinix hot 20i mnamo mwezi septemba 2023

Hivyo bado simu changa na ni bei ya infinix hot 20i ni ndogo kwa sababu ni ya daraja la mwisho

Sifa zake nyingi ni za kawaida ambazo kwa mtumiaji mwenye matumizi ya kawaida bado inafaa

Ila kwa mtu anaelenga kuitumia simu kwa mambo mengi sana itamlazimu kutafuta simu mbadala

Bei ya Infinix Hot 20i ya GB 64

Kwa hapa Tanzania Infinix Hot 20i yenye ukubwa uliotajwa inauzwa shilingi 285,000/=

Bei yake inatokana na kutumika kwa vitu vichache vyenye ubora mkubwa amabvyo huchangia gharama kuwa kubwa

Kuanzia processor, kioo, network, aina ya chaji vyote vina ubora wa kawaida

Hivyo ubora wa simu unaendana kwa kiasi kikubwa na kiwango cha pesa kinachohitajika kuipata hot 20i

Kwa mantiki hiyo kuna vitu vizuri na vingine vina ubora hafifu hivyo usitarajie makubwa sana kama ya simu ya Redmi Note 12

Sifa za Infinix Hot 20i

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G25
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.5 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 12
  •  XOS 10.6
Memori eMMC 5.1, 128GB,64GB na RAM 2GB,6GB,3GB,4GB
Kamera Kamera tatu

  1. 13MP,AF(wide)
  2. QVGA
  3. QVGA
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-10W
Bei ya simu(TSH) 285,000/=

Upi Ubora wa simu ya infinix hot 20i

Ubora mkubwa wa hii simu ni kukaa na chaji muda mrefu

Ikizingatiwa mfumo wake hauna vifaa vinavyotumia nguvu kubwa sana

Inakuja na memori kubwa inayokupa uwezo wa kuhifadhi mafaili mengi

Ni moja ya simu ya 4G inayouzwa kwa bei nafuu

Mengineyo ni ya kawaida

Uwezo wa Network

Hot 20i inasapoti mpaka mtandao wa 4G pekee

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 7 ambayo kasi yake ni 300Mbps sawa na 37.5MBps

Kwa maana kama unapakuwa app ya whatsapp kutoka playstore simu inaweza chukua sekunde mbili kumaliza

Ila 300Mbps sio kubwa ukilinganisha na 4G ya LTE Cat 24 ambayo kasi yake inafika 2000Mbps(kwenye samsung s23 ipo)

Hata hivyo kwa hapa nchini si rahisi kupata kasi hizo(300Mbps na 2000Mbps) kwa sasa japo kwa 5G inawezekana

Lakini hii sio ya 5G

Ina masafa matano tu ya 5G ila ni masafa yote yanayotumika na mitandao ya hapa nchini Tanzania

Kwa maana kila mtandao utafanya kazi pasipo na shida

Ubora wa kioo cha Infinix Hot 20i

Kioo cha infinix hot 20i ni cha ips lcd chenye resolution ya 720 x 1612 pixels

Kwa viwango vya sasa hii ni resolution ndogo ukizingatia kioo chenyewe ni cha ips lcd

Zingatia kuwa bei ya hii simu ni ndogo, haiwezi kuwa na kioo cha amoled

Amoled huwa na mkolezo mzuri wa rangi na resolution huwa kubwa

Muonekano wa vitu ni wa kuvutia ukilanginisha na kioo cha LCD

Uangavu wa kioo kwenye hii simu unafika nits 500

Simu itaweza kuonyesha vitu ukiwa juani japo si kwa mwanga mkubwa sana

Nguvu ya processor Mediatek Helio G25

Chip ya Helio G25 ina idadi ya core(sehemu) zipatazo nane zinazotumia muundo wa Cortex A53

Muundo wa Cortex A53 huwa una nguvu ndogo kiutendaji na mara nyingi zinatumika kwa kazi zisizohitaji nguvu kubwa

Hivyo kiutendaji chip ya mediatek helio g25 ina uwezo mdogo kiutendaji

Kwa maana kama unacheza sana magemu utakumbana na changamoto ya simu kukwama kwenye gemu kubwa

Kwa mfano gemu kama PUBG Mobile inaweza isicheze ukiweka resolution kubwa(Ultra high settings)

Ila kwa mambo mengine ya kawaida itaendelea kudunda

Ndio maana app ya kupima ubora ya geekbench inaipa alama 135 ambayo ni ndogo ukilinganisha na chip ya Helio G85 inayofika alama 300

Kwa sababu processor inatumia nguvu kidogo hivyo inakula umeme kidogo kitu kinachorefusha maisha ya betri

Uwezo wa betri na chaji

Simu inakuja na betri ya ukubwa wa 5000mAh aina ya Li-Po

Kama unatumia mara kwa mara kwa kazi za kawaida betri inaweza chukua hata siku kuisha

Chaji yake inapeleka umeme wa wati 10

Ni kiwango kidogo na betri itachukua muda mpaka kujaa

Ukubwa na aina ya memori

Infinix Hot 20i imegawanyika katika matoleo matano upande wa RAM na memori

Ila kwenye memori kuna toleo la 64GB na 128GB na RAM inaanzia 2GB mpaka GB 6

Kiushauri ram ya GB 4 ndio inafaa zaidi na memori kubwa kwa ajili ya kuweza kuhifadhi na kufungua mafaili mengi

Aina ya memori inayotumiwa na hii simu ni eMMC 5.1 ambazo spidi sio kubwa kama memori za UFS

Uimara wa bodi ya infinix hot 20i

Bodi ya hii simu ni ya plastiki upande wa nyuma

Haina viwango vya aina yoyote vya IP vinavyoashilia uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi

Hivyo simu ikiingia kwenye maji inaweza kuharibika tofauti na simu ya iphone 14 pro max

Ni vizuri ukawa makini na kuweka skrini protekta kama njia ya kuilinda simu

Na pia kutumia kava kuepusha kupungua kwa ubora wa rangi ya plastiki

Ubora wa kamera

Hot 20i ina jumla ya kamera zipatazo tatu

Kamera kubwa ina kubwa ina megapixel 13 wakati kamera zingine zina resolution ndogo sana na za kizamani

Bila kuzama kiundani ni kuwa kwenye nyanja ya kamera simu haina kamera nzuri kiujumla

Si kwa sababu ya kuwa na 13MP bali ni kukosekana kwa vitu vingine muhimu kama ulengaji wa PDAF na kutokuwepo kwa HDR

Upande wa video kamera zinarekodi video za full hd pekee kwa kiwango cha 30fps

Kwa kuwa hina OIS ni lazima urekodi kwa kutuliza mkono ili video itokee vizuri kama ukirekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Simu inakuja na toleo la Android 12 na mfumo wa XOS 10.6

XOS 10.6 inakuja na app nyingi za simu baadhi unaweza usizutumie

Moja ya kitu utakachokutana nacho ni matangazo

Na Android 12 ina maboresho ya kuisalama ambapo kama app inatumia kamera kuna icon ya kijani inatokea

Kwa hiyo inakuwa rahisi kujua kama kuna app inatumia baadhi ya vitu pasipo ridhaa yako

Hitimisho

Kwa muhitaji wa simujanja na mwenye bajeti ndogo infinix hot 12i ni moja ya chaguo zuri

Ila inapaswa kuwekwa akilini kuwa kuna vitu vinakosekana na hata hivyo haishangazi kutokana na bei yake

Kama kamera na utendaji ni muhimu sana basi huna budi kutazamia kuongeza bajeti yako ya kununua simu

Zingatia kuwa simu nzuri iliyo kamiri kila idara haiwezi kuuzwa kwa bei ya chini sana

 

Maoni 3 kuhusu “Bei ya Infinix Hot 20i na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

Bei ya Tecno Spark 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Spark 20 ni toleo la Tecno lilotoka mwishoni mwa mwaka 2023 hivyo ni simu inayofaa hata kwa mwaka 2024 Bei ya Tecno Spark 20 yenye ukubwa wa memori ya […]

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram