SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Redmi 12C na Sifa Zake Muhimu

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

May 16, 2023

Mwishoni mwa 2022 Kampuni ya Xiaomi ilitoa toleo la simu ya Redmi 12C

Ni simu ya daraja la chini hivyo bei yake ni ndogo hata kwa ambazo memori zake ni kubwa

redmi 12c showcase

Hivyo basi tarajia bei ya redmi 12c kuanzia laki mbili na nusu na kuendelea mbele

Kwenye hii post zipo sifa zinazofafanua ubora na vitu vingine vinavyoihusu hii simu

Bei ya Redmi 12C ya GB 128

Redmi 12C yenye RAM GB 6 na memori ya GB 128 inapatakana kwa shilingi 350,000/= kwa Tanzania

Yenye GB bei yake ni ndogo zaidi ambayo ni shilingi 290,000/= ila inakuwa na ram ndogo

Bei ndogo inatokana na simu kuwa na vitu vichache vyenye ubora mkubwa

Hivyo vitu vichache vinaifanya bei kuendana na ubora wa simu

Inachuana na simu ya tecno spark 10 pro kiutendaji

Sifa za Simu ya Redmi 12C

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G85
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 12
  • MIUI 13
Memori eMMC 5.1, 128GB,64GB,32GB na RAM 3GB,6GB,4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 0.8MP(depth)
Muundo Urefu-6.71inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-10W
Bei ya simu(TSH) 350,000/=

Upi Ubora wa Redmi 12C

Simu inakuja na machaguo mengi ya memori na inakupa nafasi ya kuipata kwa pesa kidogo

Mbali na hivyo pia utunzaji wa chaji ni wa kiwango cha kulidhsisha

Ukizingatia kuwa inatumia chip ambayo ina matumizi madogo ya chaji

Kamera yake pia ni nzuri kiasi fulani japo si sana

Baadhi ya matoleo yana ram kubwa muhimu kwa kufungua app nyingi kwa wakati mmoja

Yote ya yote ni kuwa usitarajie makubwa sana ukizingatia bei yake ni ya chini

Ila ina vitu ambavyo kwa simu zingine hufanya bei kuwa ya juu zaidi

Uwezo wa Network

Simu inasapoti mtandao mpaka wa 4G si zaidi ya hapo.

Ina jumla ya masafa ya 4G yapatayo tisa ikiwemo yanayotumika na mitandao ya simu nchini

Aina ya 4G simu inayosapoti ni LTE Cat 7 ambayo kasi ya kupakua ni 300Mbps sawa na 37.5MBps na kupakia(upload) ni 100Mbps sawa na 12.5Mbps

Kwa bahati mbaya ni ngumu kwa maeneo mengi Tanzania kupata 4G inayofika 300Mbps mara nyingi utachezea kwenye 75Mbps kama kiwango cha juu

Hata kwa kulinganisha na Redmi Note 12 utaona kuwa kasi ya hii simu sio kwenye uwezo wa Network

Ubora wa kioo cha Redmi 12C

Kioo cha Redmi 12C ni aina ya IPS LCD ambacho resolution yake ni ndogo (720 x 1650 pixels)

Simu ina uangavu unaofikia nits 500

Sio kiwango kikubwa sana cha kuonesha vitu vizrui ukiwa unaitumia simu juani

Kiwango cha refresh rate ni cha kawaida hakifiki 90Hz

Kiujumla ubora wa kioo sio mkubwa ukizingatia kuwa ips lcd huzidiwa pakubwa na vioo vya Amoled

Hasa kwenye uonyeshaji wa rangi nyeusi

Amoled huonyesha rangi nyeusi iliyokolea, yaani inakuwa halisi.

Nguvu ya processor Mediatek Helio G85

Redmi 12C inatumia processor ya Helio G85 ambayo ina core mbili zenye nguvu na core sita zenye nguvu ndogo

Utendaji wake sio mkubwa hasa kama ukiwa ni mpenzi wa magemu makubwa

Itacheza ila unaweza kushuhudia kukwama kwa baadhi ya magemu

Hivyo itakulazimu kucheza kwa kuweka settings ndogo za muonekano wa picha za gemu

Kwenye app ya kupima nguvu za processor ya Geekbench, Helio G85 ina alama 360

Kwangu mimi, chip ikiwa na alama chini ya 500 naiona kuwa ni dhaifu

Hata hivyo ulaji wa chaji sio mkubwa, utaitumia simu kwa muda mrefu

Uwezo wa betri na chaji

Simu inakuja na betri ya ukubwa wa 5000mAh na chaji ya kasi ya 10W

Na kichwa chake cha chaji ni Micro USB (zile ndogo) wakati kwa sasa simu nyingi huja na USB Type C(zile pana)

Kama ilivyotanguliwa kuelezwa kuwa, bei ya simu hii ndogo hivyo usitarajie makubwa

Betri yake inaweza kukaa masaa zaidi ya 14(kwenye intaneti) ikitegemea namna ambavyo unatumia simu husika

Ila wati 10 kwenye chaji itajaza betri kwa masaa zaidi ya matatu

Kwani ina kasi ndogo japo wenyewe xiaomi wanaita kuwa ni fast chaji

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo matano ya Redmi 12C upande wa memori

Yenye memori ndogo bei yake ndio inakuwa ndogo zaidi

Aina ya memori ya Redmi 12C ni eMMC 5.1

eMMC 5.1 inasafirisha data kwa kasi ndogo ukilinganisha na memori za UFS 2.1

Hivyo kuna kauzito utakumbana nacho wakati utakopokuwa unafungua vitu vingi kwa wakati mmoja

Japo simu ina mfumo huo wa memori ila processor ya simu inasapoti ufs 2.1 ila redmi hawakuweka

Kwenye Ram utakutana na yenye 3GB, 4GB na 6GB

Ni vizrui ukachukua yenye RAM na memori kubwa kuhifadhi vitu vingi kwenye simu na kuepuka kukwama kwama

Uimara wa bodi ya Redmi 12C

Simu imeundwa kwa bodi za plastiki kama ilivyo kawaida ya simu za daraja la chini

Pia kwenye skrini hakujaainishwa uwepo wa protekta

redmi 12c bodi

Inambidi mtumiaji kununua skrini protekta na pia kutumia kava mara kwa mara ili ubora wa simu uwendelee kudumu

Na haina viwango vya IP kitu kinachoashiria kuwa Redmi 12C haina uwezo wa kuzuia maji kupenya ndani

Kiujumla umakini unahitajika pindi utumiapo hii simu kwenye mkusanyiko wa maji au kwenye mvua

Ubora wa kamera

Redmi 12C haina mfumo mzuri wa kamera kama utafananisha na simu zenye kamera nzuri

Fuatilia, orodha ya baadhi za simu zenye kamera bora 2023 uone ubora wa picha na vitu vilivyopo kwenye hizo simu.

Redmi 12C ina kamera mbili ila kiuhalisia ni kamera moja tu ndio inayofanya kazi

redmi 12c kamera

Teknoloji ya ulengaji iliyotumika ni PDAF kwenye kamera ya megapixel 50

Inaweza kurekodi video za full hd pekee kwa kiwango cha 30fps ambapo simu za daraja la kati zinakupa zaidi ya hiyo

Ila kwa kulinganisha na bei inayouzwa na simu zilizopo kundi moja, hii ina kamera nzuri vilevile

Utakachokosa kwenye kamera zake ni kukosekana kwa kamera za ultrawide na telephoto

Ubora wa Software

Hii simu inakuja na MIUI 13 ikiwa inatumia mfumo wa Android 12 ambapo kwa sasa tupo kwenye Android 13

MIUI 13 ina vitu vizuri vingi kwa mfano uwezo wa kuscreenshot peji kwa kiwango unachotaka wewe

Kalkuleta yake inatoa chaguo la kutazama mabadilishano ya fedha za kigeni

Ila MIUI inakera kwenye swala la matangazo

Ukifungua app ya file manager unakutana na matangazo

Na pia MIUI ni nzito kiasi fulani, ila bado ni mfumo mzuri

Washindani wa Redmi 12C

Mshindani wa kwanza wa hii simu ni Pixel 3a ambayo kwa sasa unaweza kuipata kwa bei ya chini ya laki tatu

Pixel 3a ni simu inayotoa picha nzuri upande wa kamera na ina kioo kizuri chenye resolution kubwa

Mshindani mwingine ni simu ya Samsung Glaxy A04 na yenyewe ina bei ndogo kuliko Redmi

Na chaguo linigne linalotoa ushinda kwa simujanja hii Tecno Spark 10 Pro

Spark 10 pro ina utendaji unaoendana japokuwa tecno ina bei ya juu kidogo

Lakini ukiwa na tecno unaenda kupata kioo chenye refresh rate inayofika 90Hz

Neno la Mwisho

Kwa wanaotamani simu ya ubora wa kati huku wakiwa na kiwango kidogo Redmi 12C ni chaguo bora kwa sasa

Sio rahisi kupata simu ya GB 128 na RAM ya GB 6 kwa kiwango cha chini ya laki nne

Na pia ni ngumu kupata kupata simu yenye kamera ya wastani kwa bei hii

Na kama bajeti inabana zaidi hii simu inakupa simu mpaka ya memori ya GB 32 japo kwa sasa ni kiwango kidogo

Maoni 6 kuhusu “Bei ya Redmi 12C na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram