SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu 10 Zenye Kamera Nzuri na Bora 2023-2024

Ulinganishi

Sihaba Mikole

May 15, 2023

Mwaka 2023 yapo mateo ya simu yaliyoingia sokoni yakiwa na kamera nzuri na bora kwa kupigia picha na kurekodi video

Kuna simu zenye kamera kali zaidi na mfumo mzuri kwenye nyanja zote

Haziwezi fananishwa na simu zenye kamera nzuri zenye bei ndogo kabisa

Na ndio maana kwenye hii orodha utakuta bei zake karibu zote ni kubwa

Kwenye hii posti utaona ubora wa picha wa kila simu iliyoorodheshwa na upekee wa kamera za simu husika unaojitofautisha na simu zingine

Oppo Find X6 Pro

Oppo Find X6 Pro ni simu mpya ya mwaka 2023 iliyotoka mwezi machi

Ina jumla ya kamera zipatazo tatu

Mfumo mzima wa kamera unaonyesha wazi kuwa ubora wa picha na kurekodi video ni wa kiwango kikubwa

Kwani kamera zake tatu zina teknolojia ya ulengaji ya  multi-directional PDAF inayoweza kukitambua kinachopigwa kitu kwa haraka

Hiyo haitoshi, kamera zake zote zina OIS(Optical Image Stabilization) ambayo kazi yake ni kutuliza kamera wakati unarekodi huku ukiwa unatembea

Teknolojia za ulengaji wakati mwingine zinapata shida kulenga kitu kwenye mwanga hafifu ila find x6 pro inatumia teknolojia ya Laser Af

Kamera zake zote zina ukubwa wa megapixel 50

Ubora wa picha wa Oppo Find X6 Pro

Iwe mchana ama usiku kwenye mwanga mdogo, uwezo wa hii ni simu ni kiwango cha juu.

Kamera inajitahidi sana kutoa picha zinazoendana na uhalisia wa muonekano wa kitu

Pia zinabalansi kwa usahihi rangi nyeupe sana na rangi  nyeusi

Kwa maana kama eneo lina vivuri basi huonekana bali kuathiriwa na mwangaza mwingi

picha ya oppo find x6 pro

Hii ni picha moja wapo iliyopigwa kwa kutumia simu ya oppo find x6 pro

Rangi za jengo na nyasi pia muonekano wa rangi anga hazina mkolezo uliopitiliza

Na wala noise(chenga chenga) hakuna na ukizoom vitu ambavyo vipo vinaweza onekana kwa usahihi

Mfano mzuri ni upande wa kuria juu ambao una ngazi

oppo find x6 pro 2nd image

Hii ni ishara kuwa kamera inakusanya data za kutosha ya eneo lote linalostahili kutokea kwenye picha

Samsung Galaxy S23 Ultra

Simu ya Samsung Galaxy S23 Ultra ni toleo la samsung mpya kwa mwaka 2023

Samsung Galaxy S23 Ultra ina jumla ya kamera nne huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 200

Kamera ya kubwa inatumia teknolojia ya ulengaji ya multi-directional PDAF na Laser AF kwa ajili ya kwenye mwanga hafifu

Huku kamera zilizozabaki zikiwa zinatumia ulengaji wa dual pixel pdaf

Pia kamera zote zina zina mfumo wa kutuliza kamera wakati wa kurekodi huku ukiwa unatembea yaani OIS

Uzuri mkubwa wa kamera za Samsung ni uwezo mkubwa wa kuchukua kitu ambacho kipo mbali sana

Maana inakuja na kamera ya Telephoto yenye optical zoom yenye uwezo wa kukuza kitu mara 10 bila kupoteza ubora wa pixel

Ubora wa picha

Kwa baadhi,Galaxy S23 Ultra ni simu yenye kamera bora zaidi

Ukitazama picha nyingi zilizopigwa na simu utaona usahihi wa rangi wenye utofautishaji mkubwa

Pia samsung haina swala la “noise”, na muonekano wa vitu usiku unaonekana kwa usahihi

samsung galaxy s23 ultra kamera mchana

Ukitazama hiyo picha ya paka ambayo imepigwa na Galaxy S23 hasa kwenye jicho la paka

Ni kuwa kiini cha macho hakiaathiriwa na sehemu nyingine ya jicho

Rangi ya kiini ni nyeusi na ndio muonekano unavyoonekana kwenye picha husika

Xiaomi 13 Ultra

Xiaomi 13 Ultra ni simu nyingine ya kamera nne

Kamera zote nne zina megapixel 50 huku kamera kubwa ikitumia teknolojia ya ulengaji ya multi-directional PDAF

Na kamera zilizobaki zinatumia dual pixel pdaf

Uzuri ni kuwa kamera zake zote zina OIS hivyo hutowaza wakati ukirekodi video ukiwa unatembea

Kamera zake zinaweza kurekodi video mpaka za 8k

Ubora wa picha wa Xiomi 13 Ultra

Xiaomi kama ilivyo simu zingine kwenye orodha inatoa picha nzuri na usahihi mkubwa wa rangi

Rangi mbalimbali zinaonekana kama vinavyoonekana kwenye mazingira halisi kwa kiwango kikubwa

xiaomi 13 ultra kamera

Na pia kwenye mwanga hafifu utaweza kuviona vitu kwa uzuri

iPhone 14 Pro Max

iPhone 14 Pro Max ilitoka kwenye robo ya mwisho ya mwaka 2022, kwa sasa hakuna toleo jingine zaidi ya hili

Ina jumla ya kamera tatu huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 50

Kwneye swala la ulengaji iphone inatumia dual pixel pdaf ambapo kwa sasa simu nyingi za bei kubwa wameanza kuachana nayo.

Kamera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa kiwango  kinachofikia 60fps

Pia zina OIS kama ilivyo kwa simu nyingi

Ubora wa picha wa iPhone 14 Pro Max

Moja ya kitu unachoweza kukiona kwenye iPhone ni picha kali ila kuna kukolea kwa rangi kulikopitiliza

iphone 14 pro max

Rangi ya anga imekuwa ya bluu sana na hata jengo rangi zimezidi kiasi fulani

Hata hivyo usahihi wake kwenye rangi ni wa kiwango kikubwa

Vivo X90 Pro+

Kama hujui basi ni kuwa vivo ni moja ya simu zenye kamera hasa haya matoleo ya Vivo X

Kwenye orodha ya simu kali zenye kamera nzuri vivo lazima utaikuta

Basi  jua kuwa Vivo X90 Pro+ ni vivo yenye kamera nzuri zaidi kwa sasa

Idadi ya kamera kwenye Vivo X90 Pro+ zipo nne huku kamera ya Telephoto ikiwa na 60 megapixel na zingine ni megapixel 50

Na yenyewe kamera yake inaeza kurekodi mpaka video za 8K kwa kiwango cha 30fps

Ubora wa kamera yake ya kupiga vitu vya mbali haufikii samsung galaxy s23 ultra kwani yenyewe inaweza kukuza mara tatu tu

Aina ya ulengaji ambayo simu inatumia ni Dual Pixel PDAF, na yenyewe inatambua umbali wa kitu kinachopigwa kwa haraka pia

Ubora wa picha

Kwenye mwanga mwingi inatoa muonekano mzuri wa kinachopigwa picha

Kiasi cha kwamba unaweza usione kasoro yoyote

Japo kuna kiwango cha noise kwa mbali hasa kwa kitu kinachopigwa kikiwa kinatembea

vivo x90 pro+

Honor Magic5 Pro

Honor ilikuwa ni tawi ya kampuni ya Huawei ila kwa sasa imeuzwa kama njia ya kuepuka vikwazo vya USA

Honor Magi5 Pro ina jumla ya kamera zenye ukubwa wa megapixel 50 huku kamera kuu ikiwa inatumia ulengaji wa multi-directional PDAF

Kanera zake zinaweza kurekodi mpaka video za 4K na pia kamera mbili zina OIS, kamera ya tatu(ultrawide) haina.

Kwenye orodha hii, honor ndio yenye mfumo wa kamera za kawaida (pixel 7 pro ilifaa iwekwe?)

Hata hivyo ni simu inayotoa picha safi kabisa hata ukizoom mara nyingi vitu vinaonekana kwa kiwango kidogo cha noise

Uhalisia wa rangi hasa kwenye mwanga mwingi ni wa kiwango cha kuridhisha ila si kiwango kikubwa sana

honor magic5 pro

Motorola Edge 40 Pro

Motorola Edge 40 Pro ni simu ya macho matatu ambayo imetoka mwezi wa nne 2023

Kamera mbili zina megapixel 50 na moja ikiwa na megapixel 12

Kamera kuu ina multi-directional PDAF na OIS zingine hazina

Hivyo ukiwa unarekodi video kwa kutumia kamera za ultrawide, video itatokea ikiwa inatikisika kama hutulizi mkono

Ubora wa picha

Ukilinganisha na simu ya Horo Magic5 Pro, usahihi wa rangi Motorola Edge 40 Pro ni mkubwa

Vitu vinaonekana vizuri nyakati za mchana na kwenye mwanga hafifu

huawei p60 pro
Ukichukua picha za hili eneo na ukalinganisha na zilizopigwa na kamera zingine kwenye eneo hilo hilo utaona huawei inatoa picha halisi kwa kiwango kikubwa zaidi

Huawei P60 Pro

Huawei P60 inaweza kuwa nido simu yenye kamera nzuri zaidi kwenye hii orodha

Mfumo wake wa kamera ni wa kawaida ila ubora wa picha ni mkubwa

huawei p60 pro
Ukichukua picha za hili eneo na ukalinganisha na zilizopigwa na kamera zingine kwenye eneo hilo hilo utaona huawei inatoa picha halisi kwa kiwango kikubwa zaidi

Rangi ya anga, majani na jengo vinaendana na uhalisia

Hata picha ukiikuza mara nyingi vitu vinaonekana na unaweza usigundue kuwa kuna chengachenga

Kamera za hii simu zinaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa kiwango cha 60fps

Na ulengaji wa kamera uliotumika kwenye simu ni dual pixel pdaf

Samsung Galaxy S23 Plus

Ubora wa picha upande wa samsung Galaxy S23 Plus unaendana na mkubwa wake yaani samsung ultra

Simu ina jumla ya kamera tatu huku kamera kubwa zaidi ina megapixel 50

Na kamera mbili zimewekewa mfumo wa OIS

Pia hizi kamera zinaweza kurekodi video za 8K kwa kiwango cha juu cha 30fps

iPhone 14 Pro

Apple iPhone Pro ina kamera tatu na kamera kubwa zaidi ina megapixel 48

Ubora wa kamera unaendana sana na iPhone 14 Pro Max

Kamera mbili zinatumia teknolojia ya ulengaji ya dual pixel pdaf nyingine inatumia PDAF

Na zina uwezo wa kurekodi video mpaka za 4K

Simu Zingine

Matoleo yapo mengi yanayopiga picha nzuri

Moja ya simu ambayo imeachwa kwenye orodha ni Google Pixel 7 Pro

Haikuwekwa kwa sababu simu za google pixel kiujumla huwa wanatoa simu zenye kamera nzuri

 

Maoni 10 kuhusu “Simu 10 Zenye Kamera Nzuri na Bora 2023-2024

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

tecno camon premier 30

Ubora wa simu za Tecno Camon 30 na bei zake(Pro, Premier)

Tangu mwezi wa nne kampuni ya walitoa matoleo ya Tecno Camon 30 Matoleo ya Camon 30 yapo matatu ambayo ni ya daraja la kati yaani mid range Ubora wa kiujumla […]

[VIDEO]: Simu bora duniani na bei zake 2024

Huu ni muendelezo mwingine wa simu tano ambazo hazitumikii sana na watanzania. Lakini kiulimwengu ni kati ya simu bora duniani kwa mwaka 2024. Hizi ni simu zenye utendaji mkubwa kwenye […]

Simu bora duniani na bei zake 2024

Leo tuzungumzie kuhusu simu bora duniani na bei zake kwa mwaka 2024 Kuna matoleo mapya ya simu kali yenye ubora wa kiutendaji na wenye nguvu madhubuti katika maeneo mengi Ubora […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company