SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Redmi Note 12 na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 9, 2023

Kampuni ya Xiaomi toka China ilitangaza ujio wa Redmi Note 12 mnamo mwezi januari mwaka 2023

Ni toleo baada ya simu ya daraja la kati Redmi Note 11 hivyo kuna maboresho kiasi fulani

Maborsho yanayoifanya bei ya Redmi Note 12 kutokuzidi shilingi laki tano kutegemeana na ukubwa wa memori

Kwenye posti hii utazifahamu sifa zake zote muhimu na simu kutoka kwenye kampuni zingine zinazoendana kisifa na hii redmi

Bei ya Redmi Note 12 ya GB 128

Kwa Tanzania Redmi yenye ukubwa wa memori ya GB 128 inapatikana kwa kiasi cha shilingi 490,000/=

Ukizitazama sifa za simu hii na kulinganisha na simu zingine utagundua bei yeke ni nafuu

Ni mara chache kama sio ngumu kupata toleo la simu yenye kioo cha amoled, 5g, chaji yenye kasi na mfumo memori wenye nguvu kwa bei ya chini ya laki tano

Unaweza kuliona hili kwenye mfano wa simu ya Samsung Galaxy A34, ina bei kubwa.

Sifa za Redmi Note 12

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 4 Gen 1
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • MIUI 14
Memori UFS 2.2, 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB,4GB
Kamera Kamera TATU

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-33W
Bei ya simu(TSH) 490,000/=

Upi ubora wa Redmi Note 12

Simu ina kioo chenye refresh rate inayozidi 100Hz

Inakuja na chaji yenye kasi kubwa ya kupereka chaji

Betri yake inakaa na chaji masaa mengi kwani ni kubwa

Kamera zake zinatoa picha nzuri bila kuharibu uhalisia wa rangi halisi za vitu vilivyopigwa picha

Ina utendaji mkubwa wa kuweza kila aina ya appliksheni bila shida

Kioo chake kina uwezo wa kuonyesha rangi nyingi kiasi cha kwamba vitu vingi vitaonekana kwa uhalisia wake

Ni simu ndefu na inakuja na kioo cha kinachoweza kuzuia michubuko

Japo simu ina kamera nzuri kwa kiasi kikubwa ila kuna kasoro kiasi ambayo utaiona baadae

Uwezo wa Network

Redmi note 12 inasapoti mtandao mpaka wa 5G

Inasapoti masafa ya 5g yapatayo matano ila yote ni masafa ya chini yaani low bands 5G

Ambapo inakuwa na tofauti ndogo na 4G kwenye spidi na uharaka wa muitikio(latency)

Faida ya masafa ya chini upande wa 5G ni kupenya kwenye kuta bila shida

5G yenye kasi kubwa (masafa ya juu) hukumbana na ugumu wa mawimbi kupenya kirahisi

Hivyo kasi hupungua ukiwa ndani ya nyumba

Kwa mitandao ya Vodacom na Tigo wana Masafa ya Kati

Upande wa 4G inakubali 4G aina ya LTE Cat 18 yenye kasi inayofika 2500Mbps

Ubora wa kioo cha Redmi Note 12

Kioo cha Redmi Note 12 ni aina ya AMOLED ambacho kina refresh rate ya 120Hz

Kiwango cha refresh rate ya 120Hz kinaifanya simu kuwa na mwitikio wa haraka wakati unagusa

Na hivyo hufanya kuscroll(kugusa simu kwa kupeleka juu na chini) kuwa mzuri hasa ukiwa unaperuzi vitu

Ubora wake wa kioo unaongezewa na uwepo wa kiwango kikubwa cha resolution ya 1080 x 2400 pixels

Ujazo mkubwa unasaidia simu kuwa na mkorezo mzuri wa rangi zilizokorea vizrui bila kuwa na muonekano wa kupauka

Kioo kina uangavu unaosaidia vitu kuonekana vizuri ukiwa unaitumia kwenye jua

Kwani kiwango chake cha uangavu kwa kipimo cha nits kinafika 1200

Kwenye kuchunika simu inaweza kustahimili kwa sababu ina skrini protekta ya toleo la Gorilla 3

Nguvu ya processor Snapdragon 4 Gen 1

Kiutendaji simu ina nguvu ya kufungua applikesheni za aina nyingi kutokana na kutumia processor ya Snapdragon 4 Gen 1

Snapdragon 4 Gen 1 imegawanyika katika sehemu mbili ambapo sehemu yenye nguvu ina core mbili zenye kasi inayofika 2.0GHz

Muundo wa hizi unaotumia ni Cortex A78 ambayo nguvu yake ni kubwa na pia ulaji wa chaji ni wa kiwango kidogo

Hata hivyo utendaji wa snapdragon 4 gen 1 ni wa wastani ukilinganisha na simu za Samsung Galaxy S23 au iPhone 14 Pro Max

Ila ni utendaji endapo utaieka kwenye kundi moja na Tecno Spark 10 pro

Upande wa kucheza magemu simu ina utendaji wa wastani

Kutokana na gemu kubwa nyingi kama PUBG kucheza kwa 30fps kwenye resolution kubwa

Ila iwapo utaseti resolution ndogo za graphics kiwango cha fremu kitapanda kwa gharama ya kupungua ubora wa picha

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Redmi Note 12 ina ujazo wa 5000mAh na aina ya Li-Po

Ukiwa unaperuzi intaneti masaa yote simu itadumu kwa kipindi cha muda wa masaa 13

Inakuja na chaji yenye kasi ya wati 33 ambayo inachukua dakika 68 tu kujaza simu kutoka 0% mpaka 100%

Kiwastani utunzaji wa chaji ni kiwango cha kawaida hasa ukiilinganisha hii simu na Samsung Galaxy 34 ambayo inakaa zaidi ya masaa hayo.

Uwezekano ni kwamba mfumo wake wa software ukawa unachangia matumizi ya ziada ya chaji

Hata hivyo masaa kumi na tatu ukiwa kwenye intaneti ni mengi

Na ukizingaitia simu inawahi kujaa chaji kwa dakika chache

Ukubwa na aina ya memori

Simu ipo na matoleo mawili upande wa memori

Aina ya memori iliyotumika ni UFS 2.2 ambayo kasi ya kusafirisha data inafika 1200MBps

Hivyo ukiwasha simu itawahi kuwaka na app kufunguka kwa haraka

Unaweza kupata redmi ya GB 128 kwa RAM ya 4GB au 6GB

Na pia yenye GB 256 mabayo RAM yake ni 8GB

Yenye memori kubwa bei yake ni kubwa vile vile kwa mtumiaji ambaye GB 128 ni ndogo atalazimika kuongeza pesa ya ziada kupata ya GB 256

Uimara wa bodi ya Redmi Note 12

Upande wa nyuma simu ina plastiki na mbele kuna kioo cha gorilla 3

Gorilla 3 ni kioo imara kuzuia michubuko ila sio kupasuka, ukiangusha simu kwenye eneo baya simu inapasuka

Ila kama umeweka funduo na simu kwenye mfuko mmoja kukwaruzika hakutotokea

N i tofauti na vioo vya Gorilla 5 au Victus

Maji ya kiwango cha kuchuruzika hayawezi kupenya ndani ya simu kwa sababu ina viwango vya IP53

Hivyo ukiizamisha ndani ya kina cha mita moja maji yatapenya ndani ya simu kwa muda mfupi

Kiujumla, umakini unahitajika kwani uimara wake sio sawa na simu kama Xiaomi 13 Pro

Ubora wa kamera

Idadi ya kamera kwenye redmi note 12 zipo tatu huku kamera kubwa ikiwa na megapixel 48

Kamera nyingine ni kwa ajili ya kupiga eneo pana inafahamika kama ultrawide na ina megapixel 8

Na kamera ya mwisho kwa ajili ya kupiga kitu kilicho karibu sana na kamera ina megapixel 2 na hufahamika kama macro

Nyakati za mchana ambapo mwanga ni wa kutosha picha zinatokea vizuri

Kuna kiwango kidogo cha noise kinaonekana kama ukiikuza simu kidogo

Ila uhalisia wa rangi za vitu vilivyopigwa picha ni wa kiwango cha kuridhisha

Kamera yake inaweza kurekodi video za full hd pekee kutokana na processor yake kutokuwa na uwezo wa kuchakata video za 4K

Ubora wa Software

Redmi Note 12 inakuja na Android 12 na mfumo wa MIUI 14

Ukiwa na MIUI utakutana na mfumo wa kuscan app pindi ukimaliza kuidownload kutoka play store

Mfumo huo unalenga kutambua uwepo wa virusi kwenye app inayowekwa

Kitu kimoja ambacho kitakukela kwenye MIUI ni swala la matangazo

Kuna matangazo japo si ya kukera kama yale yanayokuja kwa mtindo wa notification

Calculator ya MIUI ina sehemu ya kutazama thamani za sarafu mbalimbali duniani

Washindani wa Redmi Note 12

Jambo ngumu ni kupata simu yenye sifa sawa na redmi note 12 kwa bei ya chini ya laki tano

Ila wapo washindani wenye sifa za ziada zinazokosekana kwenye Redmi Note 12 kwa bei zinazokaribiana kwa kiasi

Kuna Samsung Galaxy A33 5G.

Samsung Galaxy A33 5G ni samsung isiyopitisha maji ukiizamisha kwenye maji ya kina cha mita moja kwa muda wa nusu saa

Na pia ina kioo kigumu kupasuka cha Gorilla 5, na bei yake ni shilingi laki sita na  sabini

Mshindani mwingine ni Xiaomi Pocco X5

Pocco X5 inakaribiana vitu vingi na redmi note 12 japo redmi inaizidi kidogo kwenye utendaji

Poco bei yake ni ndogo zaidi na inapatikana chini ya laki tano na bado pia ni simu ya 5G

Neno la Mwisho

Yote ya Yote ni kuwa sifa za redmi note 12 inaifanya kuwa ni simu ya 5g yenye bei ndogo

Mtumiaji anayependa simujanja yenye nguvu ya kuridhisha hawezi kusita kuimiliki hii

Iwapo unahitaji vitu vingine vya ziada zaidi basi kuna washindani wake wenye bei zinazokaribiana kiasi fulani

Maoni 4 kuhusu “Bei ya Redmi Note 12 na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

huawei mate60 pro

Huawei Mate 60 Pro Pigo kwa Marekani?

Kama ni mfuatiliaji wa habari za teknolojia utakuwa unafahamu vikwazo vya Marekani dhidi ya huawei Huawei kutoka china imekuwa na wakati mgumu wa kutumia teknolojia mbalimbali zenye mafungamano na marekani […]

google pixel fold thumbnail

Ubora na bei ya simu mpya ya Google Pixel Fold

Fold ni aina ya simu za kujikunja. Kwa muda mrefu makampuni ya Samsung, Huawei na Oppo wamekuwa wakitengneza simu za aina hii Hivi karibuni tecno na pixel pia zimeingia katika […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram