SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy A34 5G na Ubora wake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 12, 2023

Kuna simu ya 5G ya Samsung Galaxy A14 5G utendaji wake unaweza usikushawishi.

Hapa ndipo Samsung Galaxy A34 5G inapokuja kuokoa jahazi

samsung galaxy 34 5g showcase

Kutokana na utendaji mkubwa bei ya Samsung Galaxy kwa Tanzania inaenda zaidi ya laki Tisa.

Toleo hili linatofatiana pakubwa na toleo kama la simu nyingine ya 5g ya Oppo A78 5G

Ukizisoma sifa za Galaxy A34 haitokustaajabisha kuona bei yake kuwa inakaribia milioni.

Bei ya Samsung Galaxy 34 5G ya Gb 128

Kwa Tanzania simu inauzwa kwa shilingi 930,000/-

Kwa nchi zingine kiwango hiki Cha pesa ni kidogo ila kwa hapa Tanzania ni Hela nyingi

Utendaji wa simu kwenye kamera, chaji na kioo bila uimara wa bodi ya simu ni moja ya sababu za simu kuuzwa kwa bei hiyo

Hivyo kama unazingtia simu yenye ubora mwingi huna budi kutafuta bajeti kubwa vinginevyo matoleo ya Spark 10 yanaweza kusadia kusukuma siku.

Sifa za Samsung Galaxy 34 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Dimensity 1080
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.6GHz Cortex A78
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0GHz Cortex A55
  • GPU-ARM Mali  G68 MP4
Display(Kioo) Super Amoled, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
  • One UI 5.1
Memori 256GB,128GB na RAM 8GB,6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 5MP(macro)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 930,000/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy A34 5G

Hiini simu ya daraja la kati la juu hivyo ubora upon kwenye nyanja

Mfano ni ukaaji wa chaji

Ni simu inayoweza kukaa na chaji karibu siku ukiwa kwenye intaneti

Ina utendaji mkubwa wa kufungua Kila aina ya app bila shida yoyote

Inakuja na mtandao wa 5G ambao ndipo wenye Kasi zaidi kwa Sasa

Kamera zake zinatoa picha zenye ubora hasta kwenye mwanga mwingi

Ina teknolojia ya utulizaji wa kamera wakati wa kurekodi video Hulu ukiwa unatembea

Kiufupi simu ina mapungufu machache Sana kama utakavyoona huko baadae

Uwezo wa Network

Simu inakuja na mtandao ya aina yote ikiwemo 4G na 5G kama ilivyonsimu zingine za 5g

Inasapoti aina zote tatu za 5G ikiwemo Ile ambavyo imetumia na mtandao wa Vodacom na Tigo

Aina ya 4G imu inayoumia ni LTE Cat 18 ambavyo Kasi yake inafika 2770Mbps saw na 346MB/s.

Yaani kama ukiwa unpakuwa gemu la Dream Soccer lenye MB 700 Kyle play store, simu italipkuwa kwa sekunde mbili

Ila Kasi ya intaneti itategemea na mtandao unaotumia Tena kwa hapa nchini so rahisi kuipata spidi kwenye 4G labda 5G

 Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A34 5G

Kioo inachotumia Galaxy A34 5G ni super Amoled

Ni kioo kinachoonyesha rangi nyeusi iliyokorea na halisi tofauti na vioo vya LCD

Kwenye rangi za vitu vinaonekana kwa kiwango sahihi na kwa rangi zilizokorea

Kwa mpenzi wa magemu ataridhika kuwa na simu hii kwani Ina refresh rate ya 120Hz

samsung galaxy a34 5g display

Refresh rate ya 120Hz itakufanya ufurahie kutumia kutokana na ulaini na uharaka pale unapokuwa unaperuzi

Muonekano wa vitu kwenye kioo cha hii simu unachangiwa na kiwango kikubwa cha resolution’

Resolution ya kioo cha galaxy a34 5g ni 1080×2340 pixels

Kama utakuwa unaangalia picha ya aina moja kwenye simu ya Tecno Spark 10 Pro, Oppo A78 na Samsung Galaxy A14 5G  na A34 utaona utofauti kwenye muonekano wa hio picha

Nguvu ya processor MediaTek Dimensity 1080

Galaxy A34 5G inatumia chip ya MediaTek Dimensity 1080

Ina sehemu mbili, sehemu ya kwanza ina core kubwa aina ya Cortex A78

Ukiona processor ina Cortex A78 jua kuwa simu itakuwa ina nguvu na pia utumiaji wake wa chaji

Kwenye samsung galaxy a34 5g hii chip inaweza kucheza gemu nyingi kwneye resolution na kwa idadi ya wastani upande wa fremu

Kwa mfano gemu ya PUBG inacheza kwa fremu 40 kwa wastani

Kwa jinsi chip ilivyo na utendaji, inafanya simu kuwahi kuwaka na kufungua apps kwa haraka

Na sehemu ya pili ya dimensity 1080 inaundwa na core maalumu kwa kazi zisizohitaji nguvu kubwa

Core hizi zipo sita na aina ya Cortex A55

Uwezo wa betri na chaji

Ukinunua hii simu utakutana na waya wa USB bila kichwa cha chaji

Hivyo basi itakulazimu utumie chaji ama ununue chaji za samsung

Hata hivyo mfumo wake chaji unaweza kupokea umeme mpaka wa wati 25

Betri ya hii simu ina ukubwa wa 5000mAh

Ukaaji wa chaji ni wa kiwango kikubwa kabisa na unaweza usichaji simu mara kwa mara

samsung galaxy a34 5g chaji

Kwa wastani ukiwa unaperuzi intaneti galaxy a34 5g inachukuwa masaa 19 kuisha

Ukiwa unatazama video muda wote mfululizo simu inachukua masaa 13 betri kusiha

Na kwa matumizi ya kawaida yasiyohusisha intaneti, magemu na video betri inaweza chukua zaidi ya siku nne kwa betri kuisha

Ni simu yenye utendaji mkubwa na wakati huo matumizi ya betri ni madogo

Ukubwa na aina ya memori

Samsung wanakupa machaguo matatu kwenye upande wa memori

Machaguo yenye memori ndogo ni GB 128, hapa unaweza ukapata RAM ya GB 6 au ya GB 8

Na chaguo la tatu lina GB 256 na RAM ya GB 8

RAM kubwa ni nzuri, na inakusaidia kufungua vitu vingi kwa ufanisi

Hii simu ina sehemu ya kuweka memori kadi

Aina ya memori haijainishwa ila chip ya hii simu inaweza kutumia memori mpaka za UFS 3.1

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A34 5G

Upande wa mbele simu imewekewa kioo kigumu cha Gorilla 5

Simu ikianguka kwa kimo cha mita 1.5 itavumilia kupasuka na kuchunika, ila inategemea na uso wa eneo hiyo simu ilipoanguka

Upande wa nyuma umewekewa plastiki

samsung galaxy a34 5g body

Simu haiwezi kupitisha maji kama ikizama kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu

Yaani unaweza ukaja maji kwenye ndoo ya lita 10 na ukaizamisha simu kamwe maji hayatoingia na ukiitoa, simu itaendelea kufanya kazi

Kiufupi, ukiona simu ina viwango vya IP67 basi jua hii inamaanisha si vumbi wala maji yataweza kupenya ndani ya simu

Ubora wa kamera

Simu ina kamera tatu na haina kamera ya depth sensor ambayo hainaga umuhimu kwa sasa

Kamera kubwa ina megapixel 48 na kamera nyingine ni maalumu kupiga eneo pana sana na ina megapixel 8 na nyingine 2MP

samsung galaxy a34 5g kamera

Kamera kuu inatumia ulengaji aina ya PDAF japo haiko vizuri kama dual pixel pdaf ila sio mbaya

Ubora wa picha ni mkubwa hata bila kutumia Auto HDR

Kamera yake inaweza kutofautisha rangi kwa usahihi mkubwa, hivyo muonekano wa vinavyopigwa picha unaendana na muonekano halisi

samsung galaxy a34 5g

Kitu kimoja ambacho kinakosekana ni kamera ya telephoto pamoja na kutokuwepo kwa optical zoom

Video pia inafanya vizuri unaweza kurekodi mpaka video za 4K kwa fremu 30 kwa sekunde

Pia ina OIS hivyo kutakuwa kuna utulivu wakati ukirekodi video huku ukitembea

Ubora wa kamera Ubora wa Software

Samsung Galaxy 34 5G inakuja na mfumo wa Android 13 na One UI 5.1

Kuhusu android 13, unaweza pitia: vitu vilivyomo kwenye android 13

Samsung watakuwa wanatoa matoleo mapya ya android kwenye hii simu kwa muda wa miaka minne

samsung galaxy a34 5g software

Na maboresho ya mifumo ya kiusalama kwa muda wa miaka mitano

Hii inamaanisha utapokea Android 14, 15, 16 na 17

One UI 5.1 ina mfumo mmoja wa akili bandia (AI) kwenye app yake kamera

Inakuruhusu kukitoa kitu chochote kwenye picha na kisha ukifadhi ama kuinga na picha nyingi

Kwa mfano, umepiga picha kwenye eneo la watu wengi na wewe ukawa huitaji wale watu watokee

Kamera iliyomo kwenye One UI 5.1 inakusaidia kutoa picha yako na ukaweka kwingine kwenye simu

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A34 5G

Kasoro chache zilizopo kwenye hii simu kwanza ni kutokuwepo tundu la earphone

Pia simu haina radio kwa hiyo ukitaka kusikiliza redio basi intaneti inakuhusu

Kingine ni simu kutokuja na chaji kunaongeza gharama kama hukuwahi miliki chaji ya samsung

Neno la Mwisho

Kwa mtu mwenye bajeti ya laki saba mpaka laki tisa lazima afikirie kuimiliki hii simu

Ni simu inayokuja na uwezo kuridhisha kwenye maeneo mengi na imara

Ukizingatia simu itakuwa inapokea matoleo mapya ya Android

Kitu kitakachokuwa kinatunza thamani ya simu kwa muda mrefu

Maoni 9 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy A34 5G na Ubora wake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram