SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Samsung Galaxy S24 Ultra na Sifa zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

February 17, 2024

Hivi karibuni simu mpya ya Samsung Galaxy S23 Ultra imeingia sokoni huku bei yake ikiwa haitofautiani sana na Apple iPhone 15 Pro Max

Kwenye soko la dunia bei ya samsung galaxy s24 ultra inaanzia shilingi milion tatu na laki mbili

Na kwa hapa Tanzania bei yake ya GB 256 inafika mpaka milioni tatu na laki tano kutegemea na duka

samsung s24 showcase

Simu za milioni tatu huja na vitu vingi sana vyenye ubora mkubwa kwenye nyanja nyingi

Kikubwa ambacho Samsung wamekipromoti sana na matumizi ya AI(Artificial Intelligence) kama ilivyo kwa Google Pixel 8 Pro

Tuitazamie kila kipengele cha hii simu kwa kuzingatia sifa zake zilizoambatana nazo

Sifa za Samsung Galaxy S24 Ultra

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8 Gen 3
  • Core Kubwa zaidi(1) – 1×3.39GHz Cortex-X4
  • Core Zenye nguvu(3) – 3×3.1GHz Cortex-A720
  • Core Zenye Nguvu kiasi(2)-2×2.9GHz Cortex A720
  • Core zenye nguvu ndogo(2)-2×2.2GHz Cortex-A520
  • GPU-Adreno 750
Display(Kioo) Dynamic LTPO AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • One UI 6.1
Memori UFS 4.1, 256GB,512GB,1TB na RAM 12GB
Kamera Kamera nne

  1. 200MP,multi-directional PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 10MP(telephoto)
  4. 50(Periscope Telephoto)
Muundo Urefu-6.8inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 3,300,000/=

Ubora wa kamera

Kama una muda zitazame picha ambazo ambazo zimepigwa na samsung galaxy s24 ultra kupitia hapa

Utaona picha iliyopigwa kwenye mwanga hafifu(kiza kingi)

Kamera ya hii simu ina ubora mkubwa katika kuonyesha vitu

Pamoja na kwamba mwanga ni mdogo maandishi ya jengo, rangi za majani na rangi ya jengo zinaoonekana na hajiathiriwa na kiza kingi kilichopo kwenye eneo husika

samsung s24 ultra kamera

Usahihi wa rangi ni mkubwa hata nyakati za mchana, vitu vingi vinaonekana kwa muonekano wake wa asili

Hakuna muangaza uliopitiliza

Kamera za hii simu zinaweza kurekodi mpaka video za 8K kwa kasi ya 30fps

Na tena kamera yake inaweza kurekodi kwa HDR10+ ambayo inaongeza kina cha rangi

Hivyo kuipa kamera uwezo wa kuzalisha rangi nyingi zaidi

Uwezo wa network

Samsung Galaxy S24 Ultra inasapoti network zote ikiwemo 5G

Inasapoti 5G za aina zote tatu hata ile yenye masafa marefu ambayo yana kasi kubwa ya kupakua na kupakia mafaili

Kwa maana hiyo simu inaweza kutumika popote duniani

Ni jambo zuri kuwa na simu ya 5G kwa sababu 5G imeshaanza kupatikana kwa baadhi ya maeneo

4G yake ni aina ya LTE Cat 24 ambayo kasi yake inafika 10000Mbps ambayo ni kubwa sana kwa 4G

Kama miundombinu ya mtandao husika inasapti kasi hii ya intaneti basi simu itakuwa inadownload vitu kwa sekunde

Ubora wa kioo

Samsung Galaxy S24 Ultra inatumiaa kioo cha Dynamic LTPO AMOLED 2X

Vioo vya LTPO huongeza ama kupunguza kasi ya refresh rate kutokana na aina ya matumizi

Kwa sababu refresh rate kubwa hutumia sana moto mwingi

Na kiwango kikubwa cha refresh rate hufanya simu kuwa nyororo unapotachi

samsung galaxy s24 ultra display

Ila si mara zote utahitaji refresh rate ya 120Hz, apo ndipo umuhimu wa LTPO unapokuja

Uangavu wa kioo cha samsung s24 ultra unafika mpaka nits 2400 kwa kiwango cha juu za zaidi

Hii inafanya kioo kuonyesha kwa uangavu kwenye mazingira yoyote, iwe juani ama ndani

Nguvu ya processor Snapdragon 8 gen 3

Samsung Galaxy S24 Ultra inatumia prosesa ya snapdragon 8 gen 3 kufanya kazi zake

Hii ni chip yenye na ufanisi mkubwa wa matumizi ya umeme

Kwa baadhi ya app za kupima nguvu za prosesa snapdragon 8 gen 3 inaizidi hata Apple 17 Pro ambazo zinatumiwa na simu za iPhone 15 Pro

Snapdragon 8 gen 3 imegawanyika katika sehemu nne, sehemu mbili inahusisha core zenye nguvu ambazo huwa ni mahususi katika kufanya kazi zinazohitaji nguvu kubwa

samsung galaxy s24 ultra summary

Na pia core zilizobaki ni kwa ajili ya ufanyaji kazi zinazotumia nguvu ndogo

Moja ya vitu utakavyonufaika navyo kuwa na simu yenye snapdragon 8 gen 3 ni utendaji wake kwenye mambo ya akili bandia yaani Artificial inteligence(AI)

Snapdragon 8 Gen 3 inakuja na kitu kinaitwa Stable diffusion ambacho kinakupa uwezo wa kutengeneza picha kwa kuipa simu maneno ya jinsi picha unavyotaka iwe

Ndio maana samsung wameweka mifumo mingi ya AI kwenye hii simu

Uwezo wa betri na chaji

Kama ilivyo kwa simu nyingi siku hizi, betri ya galaxy s24 ultra ina ukubwa wa 5000mAh

Hivyo ukaaji wa chaji ni wa kiwango kikubwa

Ukiwa unacheza gemu muda wote, betri inaweza kudumu kwa muda wa masaa tisa

Wakati wa kucheza gemu simu hutumia nguvu kubwa na kioo cha simu kutumika muda mwingi pia kunawahi kumaliza betri ya simu

Ndio maana simu inaweza kudumu kwa muda wa masaa tisa

samsung galaxy s24 ultra chaji

Ukiwa unaperuzi intaneti simu inaweza kukaa na chaji mpaka masaa 11

Kiwasatani samsung hii inazidiwa na Apple 15 Pro Max kwa takribani masaa matatu katika ufanisi wa betri

Simu haiji na chaji ila inasapoti kasi ya wati 45

Mpaka simu ijae kwa 100% kutoka 0% inachukua takribani dakika 65 (muda mfupi huu)

Ukubwa na aina ya memori

Samsung Galaxy S24 Ultra ina matoleo matatu upande wa memori

Kuna ya GB 256, 512 na 1TB na zote ukubwa wa RAM ya GB 12

Memori ni kubwa zinazoweza kutosheleza kujaza mafaili na RAM ni kubwa inayosaidia kufungua mafaili mengi kwa wakati mmoja

Mfumo wa memori wa hii simu  ni ule mpya wa UFS 4.0 yenye uwezo wa kusafilisha data zaidi ya mara mbili ya mifumo iliyotangulia

Hii inaongezea simu utandaji mkubwa katika maeneo mengine pia.

Uimara wa bodi ya simu

Samsung Galaxy S24 Ultra ni simu yenye waterproof kwani ina viwango vya IP68

Hii ina maanisha kuwa simu haiwezi pitisha maji kama ikizama kwenye kina cha mita 1,5 kwa muda wa nusu saa

Yaani hata simu ikizama kwenye diaba maji hayaingii kwa huo muda

Pia upande wa skrini kumewekewa kioo cha gorilla armor, kampuni ya gorilla wanadai hiki kioo ni kigumu mara nne ya toleo lilopita

Kwa maana ni kigumu kuvunjika na kuchunika, uthibitisho zaidi unahitajika

Hata hivyo vioo vya gorilla huwa ni vigumu hasa gorilla 6 na kuendelea mbele

Ubora wa Software

Ni zama za Akili bandia yaani AI ndio hype iliyopo kwa sasa

Kabla ya yote, Samsung Galaxy S24 Ultra inakuja na android 14 na One UI 6.1

Mfumo wa hii simu unaweza kutafsiri simu unayopigiwa na mtu mwingine ambaye anatumia lugha nyingine

Yaani inafanya Live Translation ya maongezi kati yako na mtu mwingine

galaxy s24 software

Hii ni inaondoa ugumu wa mawasiliano kati ya watu wawili

Yaani kama hujui kiingereza unaweza kuwasiliana na mtu huyo ukiwa na hii samsung

Kitu kingine cha kufurahisha kinaitwa circle to search

Circle to search inakupa uwezo wa kugoogle kitu kwa kutumia picha kwa kuchora duara kwenye kitu unachotaka kutafuta

Washindani wa Samsung Galaxy S24 Ultra

Ni ngumu kuiona simu inayoweza kushindana na samsung hii kwa sasa

Ila Google Pixel 8 Pro, iPhone 15 Pro Max na Sony Xperia 5 V na simu zingine toka China

Washindani wengine ni Oppo Find X7 Ultra na Realme GT5 Pro ambazo zina utendaji unaochuana

Hitimisho

Kwa wapenzi wa Samsung na simu za daraja juu basi jua kuwa ubora wa hii samsung umeweza kugusa nyanja nyingi

Hii inaweza ikawa moja ya simu bora kwa mwaka huu 2024

Bei yake haishtui kwa mtu anaelewa ubora wa kina uliopo kwenye simu

Ila unahitaji bajeti ya kutosha kumiliki Samsung Galaxy S24 Ultra

Maoni 5 kuhusu “Bei ya Samsung Galaxy S24 Ultra na Sifa zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram