SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

November 12, 2023

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba

Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki

Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu na nusu, ni moja ya oppo za bei nafuu

Kikawaida aina hii ya simu hufaa kwa matumizi ya kawaida kama kupiga simu, kuingia instagram nk

Hii inatokana na aina ya memori na chip inayotumiwa na hii simu kama utakavyoona kwenye maelezo yaliyomo

Bei ya Oppo A17K ya GB 64

Oppo A17K kwa sasa inauzwa shilingi laki tatu na elfu thelathini (330,000/=) ikiwa mpya

Kwa ambayo imeshatumika inapatikana chini ya laki tatu

Kwa kulinganisha na oppo zingine bei ya hii simu ipo kwenye kundi la oppo za bei nafuu

Japo kiutendaji haipo kwenye kundi moja kabisa na Oppo Reno8 ambazo ni simu za daraja la kati

Kwa maana usitarajie mambo makubwa sana kutoka kwenye hii kutokana na kuwa na sifa za kawaida

Sifa za Oppo A17K

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek  Helio G35
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.3 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 12
  • ColorOs 12.1
Memori eMMC 5.1, 64GB na RAM 3GB
Kamera Kamera moja

  1. 8MP,AF(wide)
Muundo Urefu-6.56inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 330,000/=

Upi ubora wa OPPO A17K

Simu ina betri kubwa inayoweza kukaa na chaji muda mrefu

Inatumia umeme kidogo sana kitu kinachoipa simu uwezo wa kukaa na chaji masaa mengi

Inasapoti mtandao wa 4G japo siku hizi karibu simu zote zina hii teknolojia

Ni simu pana na ndefu inayofanya vitu kuonekana kwa ukubwa

Vitu vingine ni vya kawaida ubora wake sio wa viwango vya juu.

Uwezo wa Network

Hii simu inasapoti mpaka mtandao wa 4G na haina uwezo wa 5G

Aina ya 4G inayosapoti ni LTE Cat 7 yenye kasi ya kupakuwa vitu inayofika 300Mbps

Na kasi ya kupakia(ku-upload) vitu ni 150Mbps

Hizi ni kasi kubwa ambapo kwa hapa Tanzania ni nadra sana kuipata

Na kama kuna mtandao unaotoa hii basi gharama yake ni kubwa na pia ni kasi ya 5G

Ina masafa yote yanayotumiwa na mitandao ya simu nchini hivyo intaneti itashika bila shida

Ubora wa kioo cha Oppo A17K

Hii oppo inatumia kioo cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1612 pixels

Hii resolution sio kubwa kwani muonekano wa vitu hautokuwa na ubora mkubwa kama ulivyo kwenye vioo vya amoled na oled

Uangavu wake unafika nits 600, ni kiasi cha kuridhisha cha kukupa mwangaza mzuri ili uweze kuona vitu ukiwa unatumia simu juani

Unajua simu ukiwa unatumia nje mahala pasipo kuwa na kivuli inakuwa ni shida kuona kwa ustadi

Ila simu yenye nits nyingi inaepusha hilo tatizo

Nguvu ya processor ya Mediatek Helio G35

OPPO A17K inatumia processor ya mediatek helio g35

Helio G35 imegawanyika katika sehemu 8, na sehemu zote zinatumia muundo unaojulikana kama Cortex A53

Cortex A53 ni muundo wenye nguvu ndogo na ni wa kitambo kwa sasa

Hii inamaanisha nguvu na uharaka wa simu katika utendaji ni mdogo kwa kazi zinazohitaji nguvu kubwa

Ndio maana gemu kama la PUBG linacheza kwa kiwango cha 25fps kwa kutumia mpangilio wa graphics za viwango vya chini

Yaani kama ukicheza kwa ultra hd simu inaweza kuanza kukwama kwama

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya Oppo A17K ni 5000mAh

Ni betri kubwa na ukaaji wa chaji unaweza ukamaliza masaa zaidi ya 10 ukiwa kwenye intaneti muda wote

Haina mfumo unaopeleka umeme kwa kasi kubwa

Kwa maana chaji yake inapeleka taratibu inayoweza chukua masaa mengi mpaka kuchaji kwa 100%

Ukubwa na aina ya memori

Memori ya oppo a17k ipo ya aina moja na yenye ukubwa wa GB 64

Na RAM yake ina ukubwa wa GB 3

Aina ya memori inayotumiwa ni eMMC, ambazo huwa zina kasi ndogo zinaposafirisha data

Hazina kasi kubwa kama ilivyo memori aina za UFS

Siku hizi simu nyingi hutumia memori za UFS, ukubwa wa memori unaweza kukulazimu kuweka memori kadi ya ziada

Kwa sababu apps huwa zinahifadhi data zinazochangia kula memori

Uimara wa bodi ya OPPO A17K

Kwenye upande wa skrini, simu imewekewa skrini protekta

Walau hii inaipa ulinzi simu lakini sio mbaya ukaongezea skrini protekta nyingine

Pia ina ulinzi wa kuzuia maji ya kiwango cha kutiririka kwa kasi ndogo

Kama ukizamisha simu kwenye maji ya kina kirefu, simu itaathirika ndani ya muda mrefu kwani haina IP67

Hivyo umakini unahitajika unapotumia

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera moja tu yenye resolution ndogo ya 8MP

Haina teknolojia ya ulengaji ya PDAF kama ilivyo kwa baadhi ya simu nyingi za bei nafuu

Na inaweza kurekodi video za full hd kwa kiwango cha 30fps

Kiujumla usitarajie ubora mkubwa wa kamera hasa unapopiga picha ukiwa kwenye mwanga hafifu.

Ubora wa Software

Oppo A17K inatumia mfumo endeshi wa Android 12

Kwa sasa kuna toleo jipya la android 14, hakuna uhakika kama itapokea toleo hili jipya au hata la Android 13

Lakini pia OPPO hii inaambatana na mfumo wa ColorOS

ColorOS 12.1 pia inakupa urahisi wa kuinganisha simu na laptop(kompyuta) bila kutumia app nyingine

Washindani wa oppo  A17K

Washindani wakubwa wa toleo hili ni simu kutoka Tecno, Infinix, Redmi na Realme

Tecno Spark 10 ina bei na sifa inayoendana na Oppo A17K

Spark 10 inakupa kioo kizuri chenye refresh rate inayofika 90Hz

Na pia ina kamera nzuri yenye resolution inayofika 50MP na yenye PDAF na pia inasapoti chaji yenye kasi inayofika 18W

Kwa mantiki hiyo inaweza ikamfanya mnunuaji kuchagua tecno badala ya hii oppo

Hitimisho

Kwa wapenzi wanaotaka kujaribu simu za OPPO huku wakiwa hawana bajeti kubwa wanaweza kuanza na hii

Lakini ikumbukwe OPPO A17K inalenga watumiaji wasiokuwa na matumizi mengi makubwa na simujanja

Kwa maana kama wewe ni mpenzi sana wa kupiga picha hili linaweza lisiwe chaguo sahihi

Ila kama unataka simu inayotunza moto hii inafaa.

Wazo moja kuhusu “Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

vivo y02t

Bei ya Vivo Y02t na Sifa Zake

Vivo Y02t ni simu ya bei nafuu ambayo imetoka katikati ya mwaka 2023 Bei ya vivo y02t haizidi laki tatu kwa hapa Tanzania kutokana na aina ya sifa ambazo simu […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram