SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 14 Pro Max na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

September 25, 2022

Kampuni ya Apple imeachia simu za aina nne kwa mwaka 2022

Moja ya simu iliyoingia sokoni ni iPhone 14 Pro Max

Ina muonekano unaofanana na iPhone 13 Pro Max kwa sehemu kubwa

phone 14 pro max showcase

Utofauti kati ya simu iphone toleo jipya na la zamani upo sana kwenye kioo (display), kamera na processor

Vitu vipya vinafanya bei ya iPhone 14 Pro Max kuwa kubwa kuliko 13 pro max pindi ilipotoka

Utafahamu sifa zake za muhimu miundani

Bei ya iPhone 14 Pro Max ya GB 128

Bei ya iPhone 14 Pro Max yenye ukubwa wa GB 128 ni shilingi 2,581,387.60/=

Uwezekano wa bei kuwa kubwa zaidi ya hiyo kwa hapa Tanzania ni mkubwa

Na iwapo GB 128 ni ndogo basi huna budi kuwa na zaidi ya shilingi milioni tatu

iPhone 14 Pro Max Summary

Kwani ya GB 1020 inaenda 3,754,745.60/=

Kwa hapa Tanzania bei yake ni lazima ifike milioni nne

Ila, bei inaendana na sifa za simu husika?

Jibu la hili swali utalipata kwa kupitia ufafanuzi wote uliopo hapa

Sifa za iPhone 14 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g na 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A16 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.46 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core graphics)
Display(Kioo) LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB,1020GB na RAM 6GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4323mAh-Li-Ion
  • Chaji-15W Wireless Charge
Bei ya simu(TSH) 3,754,745.60/=

Ni Upi Ubora wa iPhone 14 Pro Max

iPhone 14 Pro Max ni moja ya simu za apple zinazokaa na chaji masaa mengi hata ukiwa unaitumia muda mrefu kwenye intaneti

Ni simu ngumu kupasuka kutokana na ugumu wa bodi

Inatumia aina zote za mitandao ukiwemo ule wenye kasi

Ina mfumo endeshi mpya kabisa wenye vitu ambavyo havikuwepo kwenye mifumo endeshi iliyopita ya apple

Chaji yake inapeleka umeme unaojaza betri kwa haraka

Kamera zake tatu zinatoa picha nzuri hata nyakati za usiku

Ina nguvu kubwa ya utendaji kwani ina processor inayoizidi nguvu processor za simu karibu zote duniani

Tuitazame kiundani zaidi katika nyanja tofauti

Uwezo wa Network

Simu ya iPhone 14 Pro Max ni simu ya 5G kama ilivyo Samsung Galaxy S22+ 5G

5G yake inasapoti masafa yote kwa maana ya kati, chini na yale makubwa

Kwa sasa nchini inaingia akilini kumiliki simu ya 5G

Vodacom Tanzania wamefanya uzinduzi wa mtandao huu wenye kasi zaidi duniani kwa sasa

Kuelewa mtandao wa 5th Generation (kizazi cha tano) pitia, maana ya 5G na aina zake

iphone 14 pro max network

Hata mtandao wa 4G simu inakubali karibu masafa yote ya nchi mbalimbali

Zingatia kwamba iPhone za mwaka 2022 kwa Marekani hazina sehemu ya kuweka laini ya simu

Bali zinakuja na eSIM(embeded SIM) ila kwa nchi zingine simu inakuwa na sehemu kwa ajili ya laini

eSIM inatumia software(dijitali) ambayo ipo kwenye chip inayofahamika kama eUICC kuweka laini kwenye simu bila kadi

Kitu kingine kipya kabisa ni uwezo wa simu kuwasiliana na satiiphone 13 pro max displaylaiti kwa ajili ya dharura

Hii inafaa kama simu ikiwa ipo kwenye maeneo yanayokosa mtandao wa simu za mkononi

Kuhusu eSIM, hapa Tanzania hakuna mtandao wenye huduma hii kwa sasa

Kenya mtandao wa Safaricom inayo hiyo huduma

Ubora wa kioo cha iPhone 14 Pro Max

Hii simu janja inatumia kioo cha OLED ambacho apple wanaita Super Retina XDR OLED

Moja kwa moja ubora wa kuonyesha vitu lazima uwe mkubwa

Kwa sababu vioo vya OLED (na AMOLED) huonyesha rangi nyingi na vina kiwango kikubwa cha utofautishaji wa rangi za vitu

Kioo chake ni angavu sana kwani kina kiwango cha unagavu (nits) zinazofika 2000

-iphone 14 pro max display

Kioo kikiwa na nits nyingi kinakuwa kinaweza kuonyesha vitu vizuri ukiwa unatumia simu nje kwenye jua

Mbali na wingi wa nits, ni kioo chenye  HDR10, Dolby Vision, refresh rate ya 120Hz na resolution ya 1290 x 2796 pixels

Mpaka sasa unapata picha kwa nini bei ya iPhone 14 Pro Max inaanzia milioni mbili na nusu

HDR10 na Dolby Vision hizi ni teknolojia kwa ajili ya kurekebisha muonekano wa vitu uendane na jinsi kitu kinavyoonekana kwenye mazingira halisi.

Pitia, Jinsi HDR inavyofanya kazi na ufafanuzi wake kiundani

Refresh rate ya 120Hz huwa inafanya screen kuwa laini na nyepesi wakati unaperuzi

Nguvu ya processor Apple A16 Bionic

Linapokuja swala la processor za simu, apple huwa wako mbele kuliko washindani wake

Apple wanadai chip ya Apple A16 Bionic iliyopo kwenye iPhone 14 Pro Max ina nguvu kwa 40% kuliko washindani wake

Hali ndio ipo hivyo hasa kama utatumia app ya Geekbench na Antutu kupima nguvu ya processor

Kwenye Geekbench Apple A16 Bionic ina alama 1800 kwenye core moja

iPhone 14 Pro Max Processor benchmark

Antutu inaipa alama 978147

Wakati mshindani mkubwa wa chip za bionic ni Qualcomm kwa kutumia SoC ya Snapdragon 8+ Gen 1 ambayo imetumika kwenye baadhi ya simu mpya za Xiaomi

Geekbench inaipa Snapdragon 8+ Gen 1 alama 1321 kwenye core moja

Na majaribio ya Antutu inapata alama 1032660

Ukiitazama alama za Geekbench, snapdragon inazidiwa kwa 26%

Hii inamaanisha simu ina utendaji mkubwa na wa haraka unapotumia kwenye kazi zozote hasa kucheza magemu

Uwezo wa betri na chaji

Toleo jipya la iphone 2022 linakuja na betri lenye ukubwa wa 4323mAh aina ya Li-Ion

Hii betri ni kubwa inayoweza kukaa na chaji masaa mengi

Kwenye majaribio ya Tomhardware kwenye kutumia intaneti masaa mengi mfululizo simu inatunza chaji masaa 13 na dakika 39

Ni karibu masaa 14

Kwa kiwango hiki inamaanisha iPhone 14 Pro Max inaweza kukaa na chaji masaa mengi zaidi kwenye kazi za kawaida

Muda huo unaendana na simu ya Redmi Note 10 yenye betri la 5000mAh aina ya Li-Po

Kwa bahati mbaya simu haiji na chaji hivyo utalazimika kununua chaji

Chaji za iPhone za wati 25 zinaweza kujaza simu kwa 50% ndani ya nusu saa

Sio kitu cha ajabu hiki kwani simu ya Tecno Camon 19 5G VIP inajaa 100% kwa dakika 17 tu

Ukubwa na aina ya memori

Kwenye upande wa memori kuna matoleo manne ya iPhone 14 Pro Max

Kuna ya GB 128, 256, 512 na TB 1 zote zinatumia RAM ya 6

Memori zake ni za aina ya NVMe ambazo husafirisha data kwa kasi kubwa kuliko hata UFS

Uimara wa bodi ya iPhone 14 Pro Max

Simu imeundwa kwa bodi yenye glasi za Gorilla upande wa nyuma na mbele

Upande wa pembeni simi imewekewa chuma (stainless steel)

Kama iliyo ada, ni simu ngumu kupasuka

Lakini pia haipitishi maji iwapo simu ikidumbukia maji ya kina cha mita sita kwa muda wa nusu saa

Uimara wake unaendana na iPhone 13 Pro Max na hata iPhone 12 Pro Max

Ubora wa kamera

iPhone 14 Pro Max ni iphone macho matatu yenye kamera aina za wide, ultrawide na telephoto

Kwa mara ya kwanza Apple wametumia  kamera yenye megapixel kubwa ya 48MP

iphone 14 pro max kamera 2

Kwa picha chache zilizopigwa na hii simu, kamera yake inatoa picha nzuri

Lakini uchakataji wa picha umekuwa ni wa kupitiliza hata kwa kamera yenye 48

Uchakataji unalenga kupunguza Noise(vitu visivyohitajika) lakini unasababisha picha kupungua kwa uhalisia

iphone 14 pro max kamera

Ukipiga picha kwa kamera ya 48MP itapiga picha ya 12MP kama haujaseti kutumia kamera ya 48MP

Kwenye video ukirekodi na kamera kubwa kwa kutumia ProRaw faili linakuwa kubwa  mno

Kamera za Apple zinaishia kurekodi video za 4k tu pamoja na lenzi yake kuwa na uwezo wa kurekodi 8K

Ubora wa Software (iOS 16)

Simu ya iPhone 14 Pro Max inakuja na mfumo endeshi wa iOS 16

Huu ni mfumo unakuja na kitu kinaitwa Always On Display

-iphone 13 pro max always on display

Kwa maana ukilocki simu, saa na vitu vingine vinaonekana kwa sekunde kadhaa

Ni kitu ambacho kiliwepo kwa miaka mingi kwenye simu za Android hivyo Apple wamechelewa

Kitu kingine cha kuvutia ni Dynamic Island ambayo imeambatanishwa kwenye kamera ya mbele

iphone 13 pro max dynamic island

Ukipiga simu au ukisikiliza mziki icon zake zinahamia kwenye hiyo sehemu

Pia ni sehemu unayoweza kuitumia kufungua baadhi ya app

iphone 13 pro max dynamic island 2

Ifahamu zaid: Vitu vipya vilivyopo kwemye  matoleo iphone 14

Yapi Madhaifu ya iPhone 14 Pro Max

Simu za iPhone 14 Pro Max zinalazimisha kununua chaji kwani haziji na chaji yake

Hazina sehemu ya kuwekea memori hii inaweza kuwa changamoto kwa simu yenye GB 128 na ikiwa inarekodi video za ProRaw nyingi

Huduma ya kutumia setilaiti inapatikana marekani pekee

iPhone 14 Pro Max iliyonunuliwa USA haitakuwa na uwezo wa kutumika kwenye nchi ambazo hazina huduma ya eSIM

Bei ya iPhone 14 Pro Max ni kubwa na si ndogo ukilinganisha na uwezo wa watanzania japo simu ina uwezo mkubwa

Neno la Mwisho

iPhone 14 Pro Max ni simu ya kuwa nayo kwa mwaka 2022

Lakini inafaa kama una hela ya kutosha

Kwa kiasi kikubwa bei yake inaendana na ubora wa simu

Na ni muhimu kujua kwa nini unahitaji simu ya zaidi ya milioni tatu

Wazo moja kuhusu “Bei ya iPhone 14 Pro Max na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail

[VIDEO]:Simu zote za iPhone za bei ndogo na zinazofaa

Kabla ya kununua iphone za bei rahisi ambazo mara nyingi huwa ni used, kitu cha kwanza cha kuangalia ni kama itakuwa inapata sapoti ya kupokea mfumo endeshi wa iOS Tofauti […]

iphone thumbnail

iPhone za bei rahisi za kumiliki kwa sasa(2024-2027)

Katika pitapita zangu na kuchunguza simu bora za bei ndogo na ya chini nimekuja kugundua kitu cha kustahajabisha kidogo Wapenzi wa iPhone wenye bajeti ndogo wananunua iphone used hazipokei maboresho […]

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company