SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora wa Simu Mpya za iPhone 14 (Plus, Pro na Pro Max)

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 11, 2022

Kampuni ya apple imetoa matole manne ya simu mpya za iphone kwa mwaka 2022

Simu hizo ni iPhone 14, iPhone 14 Plus, iPhone 14 Pro na iPhone 14 Pro Max

Kwa kutazama muundo, hizi simu zinafanana kwa kiwango na matoleo ya iPhone 13

Ila kuna maboresho mapya ambayo hayakuwepo kwenye matoleo yaliyopita

Vitu vipya vilivyopo kwenye iphone 14 zote

Matoleo mapya ya apple yameweka maboresho kwenye chip (processor), kamera, kioo (display) na software kwa maana mfumo endeshi

Kamera

Kwa mara ya kwanza apple wamekuja na kamera yenye megapixel kubwa

Kamera hii ipo kwenye iPhone 14 Pro Max na iPhone 14 Pro na kamera ina 48MP

Kikawaida simu za apple huwa zinatumia kamera zenye megapixel 12

kubwa huo ni kawaida sana kwenye simu za Android ambazo kwa miaka mbili zimekuwa zinakuja na megapixel za kutosha

Kwa mfano camera ya Samsung Galaxy S22 Ultra ina kamera ya 108MP inayoweza kurekodi video za 8K kwa frem 30fps

iPhone zingine zimeendelea kutumia kamera za 12MP

Kumbuka wingi wa megapixel si kitu pekee kinachotambulisha ubora wa kamera ya simu

Ndio maana hata simu zenye megapixel kubwa huwa zinapiga picha za 12MP

Ni mpaka ubadirishe settings ndio zinapiga picha za megapixel 48 (au kubwa yoyote)

Mfumo Endeshi

iPhone mpya za 2022 zinakuja na mfumo endeshi wa iOS 16

Huu ni mfumo unaoruhusu always on display kwa mara ya kwanza kwenye iPhone

Hivyo mtumiaji ataweza kuangalia muda simu ikiwa imejilock

Kwa mtumiaji wa simu za Android sio kitu kigeni kwani kimekuwepo kwenye simu nyingi kwa muda sasa

Ila upande wa iOS zilizopita hazikuwa zinatoa hiko kitu

Display (Kioo)

Mara hii apple wametumia kioo kilichowezeshwa LTPO

Samsung pia wamekuwa wakitumia vioo vya aina hii kwa miaka mingi

Kitu kingine ni kwamba kamera ya selfie ipo ndani ya kioo na sio kwa juu kama zamani

Hivyo display imekava urefu wa simu yote

Kwenye kamera kuna kitu kimeongezwa kinaitwa dynamic island

dynamic island inaonyesha icon za app pindi unapoifunga

Ukiboonyeza upana wa dynamic island uongezeka na unaweza kuifungua app

Hii kitu inafanya animation nzuri

Processor

Maboresho makubwa yamefanyika kwenye utendaji kwa kuweka chip yenye nguvu kubwa

Kwa mujibu wa kampuni ya apple, Apple A16 Bionic ina nguvu zaidi ya 40%  ya washindani

Kwa maana Snapdragon 8+ Gen 1 inaachwa nyuma na Apple A16 Bionic

Snapdragon 8+ Gen 1 ni processor ya inayotumika kwenye simu a daraja za juu za android

Ndio chip yenye nguvu kwa sasa lakini bado imeshindwa kuifikia Apple A15 Bion achilia mbali Apple A16

Kwa mujibu wa data za geekbench zilizovuja hivi karibuni zimeonyesha processor apple ina alama 1800 kwenye core moja

Ila iPhone 14 na iPhone 14 Plus zinakuja na Apple A15 Bionic

Hazina tofauti na simu za iPhone 13

Sifa za simu za iphone mpya

iPhone 14

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g na 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.23 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.82 GHz Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core graphics)
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB na RAM 6GB
Kamera Kamera mbili

  1. 12MP, dual pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • mAh-Li-Ion
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 2,400,000/=

iPhone 14 Plus

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g na 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.23 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.82 GHz Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core graphics)
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB na RAM 6GB
Kamera Kamera mbili

  1. 12MP, dual pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • mAh-Li-Ion
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 2,681,800.00/=

iPhone 14 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A16 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.46 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(6) – 4×1.8 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core graphics)
Display(Kioo) LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB,1020GB na RAM 6GB
Kamera Kamera tatu

  1. 48MP,Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(telephoto)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • mAh-Li-ion
  • Chaji-15W Wireless Charge
Bei ya simu(TSH) 2,915,000.00/=

iPhone 14 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g na 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A16 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.46 GHz Avalanche
  • Core Za kawaida(6) – 4×1.8 GHz  Blizzard
  • GPU-Apple GPU (5-core graphics)
Display(Kioo) LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 16
Memori NVMe, 256GB,128GB,512GB,1020GB na RAM 6GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP(telephoto)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • mAh-Li-ion
  • Chaji-4323W Wireless Charge
Bei ya simu(TSH) 3,381,400.00/=

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram