SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu Mpya ya Samsung Galaxy S22+ 5G na sifa zake

Simu Mpya

Sihaba Mikole

May 10, 2022

Simu ya samsung galaxy s22+ 5g ni simu mpya ya samsung ya mwaka 2022

Galaxy s22+ ni moja ya simu bora iliyotengenezwa kwa ustadi mkubwa kwenye kila nyanja ikiwemo kamera

samsung galaxy s22+

Kitu kinachofanya bei ya samsung galaxy s22+ kuwa ni zaidi ya shilingi milioni mbili kwa sehemu kubwa ya Tanzania

Fuatilia bei yake, kisha fuatalia kila sifa ya S22+ uone ni namna gani ubora wake unavyoweza kuizidi simu ya iphone 13 pro max

Bei ya Samsung Galaxy S22+ Tanzania

Bei ya samsung galaxy s22+ 5g kwa baadhi ya maduka ya simu ya kinondoni ni shilingi 2,600,000/=

Hii ni bei itakayokupa galaxy ya GB 256 na RAM ya GB 8

Swali ambalo linaweza kuwa kichwani mwa mtu, ni kwa nini simu iuzwe kwa zaidi ya milioni mbili.

Bei kubwa ya hii simu hasa inasababishwa na ubora wake upande wa utendaji, kioo, uimara wa bodi, network nzuri na sifa zingine

Kama unataka kuifahamau Samsung S22+ kiundani basi zisome sifa zake zote ambazo zimeambatanishwa kwenye posti hii.

Sifa za simu ya Samsung Galaxy S22+ 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Exynos 2200
  • Core Kubwa Zaidi (1) – 1×2.8 GHz Cortex-X2
  • Core Zenye Nguvu (3) – 3×2.50 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Cortex-A510
  • GPU-Adreno 619
Display(Kioo) Dynamic AMOLED 2X, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • One UI 4.1
Memori UFS 3.1,256GB, 128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera nne

  1. 50MP, Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 12MP, (ultrawide)
  3. 10MP, PDAF(Telephoto)
Muundo Urefu-6.6inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 2,600,000/=

Upi ubora wa samsung galaxy s22+ 5g

Ubora mkubwa wa galaxy s22+ ni kuwa na chip yenye utendaji mkubwa

Ufanisi mkubwa wa chip unaifanya simu kuwa na uwezo wa juu kwenye kila sehemu

Lakini pia ina kioo kinachoonyesha vitu kwa uzuri sahahi

Ina uwezo wa kutumia aina zote za 5G na ina masafa ya 4G ya kutosha

samsung galaxy s22+ summary

Samsung s22 haipitihsi maji hata simu ikidumbukia kwenye kina cha maji ya mita moja

Ukitazama upande wa network mpaka kwenye software utaona ni simu ambayo imekamilika

Japokuwa ina changamoto zake chache kama utakavyoona baadae

Uwezo wa Network

Galaxy S22+ inaweza kutumia kila aina ya mtandao wa 4G na 5G

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 24

LTE Cat 24 ina spidi ya juu inayofikia 3000Mbps

samsung galaxy s22+ network

Ni spidi kubwa sana ambayo hakuna mtandao wa simu nchini Tanzania unaotoa kasi hiyo

Ila ina masafa ya LTE yanayotumika na mitandao yote ya simu hapa nchini

Hivyo kila la laini ya 4G itafanya kazi vizuri.

Pitia huu kurasa kujua, masafa ya mtandao wa LTE ya Tanzania

Ubora wa kioo cha samsung galaxy s22+ 5G

Simu mpya za samsung s-series za 2022 zinatumia kioo cha Dynamic AMOLED 2X

Dynamic AMOLED 2X ni super amoled iliyoboreshwa yenye ongezeko la rangi zaidi

Hivyo kuna uhalisia kiasi cha juu wa vitu kuonekana kwa jinsi vilivyo kwenye mazingira halisi

Ubora wa display yake unaongezewa na uwepo wa HDR10+

Na pia kioo kuwa na resolution ya kiwango kikubwa ya 1080 x 2340 pixels,

Kioo cha samsung galaxy s22+ 5g kina uangavu unaoweza kuonyesha vitu vizuri simu ikiwa inatumika juani

Kwani ina nits zinazofika 1700

Na kizuri zaidi kioo chake kina refresh rate inayoifanya simu kuwa nyepesi na nyororo wakati wa kuscroll

Kwa sababu refresh rate yake ni 120Hz

Nguvu ya processor ya Exynos 2200

Simu ya samsung galaxy s22+ 5G inatumia processor ya Exynos 2200 kufanya kazi zake zote

Kuhusu utendaji exynos 2200 ina nguvu kubwa

Inaweza kucheza gemu za kila aina kwa ubora wa ultra hd bila simu kupata joto

Kwenye app ya geekbench, hii processor ina alama 1161

samsung galaxy s22+ processor ya exynoss 2200

Na kwenye app ya antutu exynos ina alama 975,340

Ni chip chache sana ambazo zina alama kama hizo

Hii inasababishwa na processor ya simu kutumia muundo wa Cortex X2 kwenye core moja

Na cortex 710 kwenye core tatu

Na pia core ndogo zipo nne na zinatumia muundo wa Cortex-A510

Kwenye linki ifuatayo utatambua, jinsi ya kujua simu yenye processor bora 

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya samsung galaxy s22+ 5G ina ukubwa wa 4500 mAh aina ya Li-Po

Ukubwa unaosaidia simu kukaa na chaji takribani masaa 97 ikiwa haitumiki mara kwa mara

Ukaaji wa chaji wake si wa kiwango kikubwa kama simu ya oppo find x3 pro

Kwa mujibu wa gsmarena galaxy s22+ inajaa chaji kwa 100% baada ya dakika 62

Ujazaji wa haraka wa chaji kwa sababu simu inakuja na chaji inayopeleka umeme kwa kasi ya wati 25

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo mawili ya samsung galaxy s22+ upande wa memrori

Ipo ambayo ina ukubwa wa GB 128 na nyingine yenye ukubwa wa GB 256

Zote zinatumia RAM zenye ukubwa wa GB 8

Ufanisi wa simu huongezeka zaidi RAM ikiwa kubwa

Aina ya memori ambazo simu inatumia ni UFS 3.1

Hizi ni memori ambazo husafirisha data kwa kasi ianyofikia 2900 MB/s

Hivyo simu inawaka kwa haraka na app kufunga kwa urahisi ndani ya sekunde

Uimara wa bodi ya samsung galaxy s22+ 5g

Simu ina bodi ngumu ambayo haipitishi maji ikiwa imezama kwenye kina cha mita moja na nusu

Upande wa nyuma na kwenye kioo kunalindwa na kioo cha Gorilla Glass Victus+

samsung galaxy s22+ bodi

Na upande wa pembeni umewekwa aluminiamu

Pia simu urefu wake na uzito ni wa wastani unaoweza kukaa vizuri kwenye mkono

Ubora wa kamera

Galaxy S22+ ni samsung macho matatu

Ina kamera kwa ajili ya kupiga vitu ambavyo vipo mbali sana yaani Telephoto

Na kamera kwa ajili ya kupiga eneo pana kwa nyuzi ya 120 yaani Ultrawide

samsung galaxy s22+ kamera

Katika picha ambazo zimepigwa na gsmarena simu inatoa picha kwa rangi halisi za vitu

Vitu vinaonekana vitu kwa nyakati zote yaani usiku na mchana

Zitazame hapa, picha zilizopigwa na samsung s22+

Ubora wa Software

Simu inakuja na mfumo endeshi wa Android 12 na One UI 4,1

Kuna ongezeko la vitu ambavyo havipo kwenye android 11

samsung galaxy s22+ one ui 4.1

Kwa mfano toleo jipya la android inaweza kukuonyesha app ambazo zinatumia kamera

Hivyo inakuwa ni rahisi kujua app usiyoitambua ambayo inachota taarifa zako

Yapi Madhaifu ya samsung galaxy s22+ 5g

Changamoto kubwa ya galaxy s22+ ni uwezo wake mdogo wa kukaa na chaji

Ukitazama iphone 13 pro max ina betri dogo zaidi ya hii samsung

Lakini iphone inaweza kukaa na chaji masaa 18 simu ikiwa kwenye intaneti

Wakati galaxy s22+ ni masaa 14

Hii simu haiji na chaji

Mnunuaji atalazimika kununua pesa ya ziada kununua chaji yake

Neno la Mwisho

Kama una bajeti inayotosheleza na unapenda simu bora, galaxy hii itakufaa

Kama ukiagiza toka amazon bei ya samsung galaxy s22+ ni ya chini zaidi ya hapa Tanzania

 

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Simu Mpya ya Samsung Galaxy S22+ 5G na sifa zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

oppo find x6 pro thumbnail

Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Kuna matoleo mengi ya simu za oppo zenye ubora tofauti tofauti Zipo ambazo zina ubora wa kati, wa juu na wa chini Katika hizo, nyingi zinajitahidi kuwa na kamera zinazotoa […]

No Featured Image

Simu Mpya za Samsung na Bei Zake 2023

Kama unatafuta samsung mpya kwa mwaka 2023 basi upo sahihi Kwenye hii kuna simu zipatazo saba na maelezo mafupi kuhusu sifa zake Kwenye hii orodha ya simu mpya za samsung […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram