SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

eSIM ni nini? Fahamu kama simu yako inayo

Miongozo

Sihaba Mikole

April 4, 2023

eSIM ni aina ya laini ambayo inakuwa ndani ya simu huku ikifanya kazi bila kuwa na laini zilizozoeleka za muundo wa plastiki (PVC)

Kifaa cha mwanzo kuwa na eSIM ni saa ya Samsung Gear S2 Classic 3G mwaka 2016 kabla ya makampuni mengine kuanza kutumia

Umaarufu wa huu muundo umekuwa mkubwa hasa baada ya kampuni ya Apple kuzindua iphone 14 ambazo hazina sehemu ya kuweka laini nchini Marekani.

Umuhimu wake mkubwa hutohutaji kutembea ni kibati cha laini ama kuwa na wasi wa sim card yako kupotea

eSIM inaweza kuhifadhi namba mpaka nane ila zinazotumika huwa ni mbili

Kuna simu nyingi zenye teknolojia hii hivyo jifunze jinsi ya kutazama kama simu yako inasapoti eSIM

eSIM nchini Tanzania

Teknoljia hii inategemea kama mtandao wa simu una mfumo unaokubali kutumia eSIM

Kwa Tanzania kuna kampuni moja mpaka kufika leo april 2023 inayosopati embeded SIM(eSIM)

Kampuni hiyo ni Airtel

Kama ni mteja wa Airtel unaweza kutembelea ofisi zao na kisha wakakupa utaratibu wa kupata huduma hii

Ila usiende kabla ya kuangalia iwapo simu unayotumia inasapoti eSIM

Jinsi ya kutazama eSIM kwenye simu

Kuna njia chache ya kujua kama simu inaweza kutumia aina hii ya laini

Njia ya kwanza ni kwa kupiga namba *#06# 

Baada ya kupiga utaona namba nyingi zenye lebo za IMEI, ICCID na EID

EID ni kitambulisho kuwa simu inayo eSIM

Kirefu chake eSIM ID, kama kifaa chako haina hii basi jua kuwa huwezi tumia muundo huu wa laini

Njia ya pili ni kwenda kwenye settings kisha kwenye sehemu ya search andika “IMEI”

Bonyeza sehemu ya imei itakuja sehemu inayoonyesha taarifa za imei zilizopo kwenye simu yako

Moja ya taarifa ya imei inayotakiwa kuwepo ni ya eSIM tofauti na hapo kifaa chako hakina muundo huu

Jinsi ya kuwezesha eSIM

Iwapo umegundua kuwa simu yako inayo, hizi ni hatua unazopaswa kufuata

Kitu cha kwanza lazima upate code kutoka kwenye kampuni ya simu unayotumia

Mara nyingi hizi huwa zipo kwenye muundo wa QR Code

Kisha washa simu yako (kwa upande wa android samsung)

Ingia kwenye Settings na chagua Connection halafu chagua SIM Card Manager

Itatokea orodha ya laini zilizopo kwenye simu ikiwamo eSIM

Kwa chini utaona pameandikwa Add mobile plan bonyeza hiyo sehemu

Simu ita-load ikicheki kama kuna simu kadi baada ya muda itakuja kitufe kinachosema “scan carrier qr code

Inabidi uichague hiyo sehemu na kisha uanze ku-scan qr code ambayo umepewa na mtandao husika

Kisha kitakuja kitufe kikisema “add and use it now” chagua na hapo utakuwa umeiwezesha simu yako na eSIM

Kwa upande wa iPhone kuna hatua chache.

Nenda kwenye settings halafu data plan kisha chagua add data plan

Baada ya hapo itakuja screen ya kuscan qr code halafu utaendelea na hatua zingine

Simu zenye uwezo wa eSIM

Iwapo umeshafamu kuwa simu yako haina kabisa eSIM hizi ni baadhi ya simu janya unazoweza kuwa nazo

  1. Google Pixel 3
  2. iPhone XR
  3. Samsung Galaxy S20 Ultra
  4. iPhone 13 Pro Max
  5. Google Pixel 4
  6. iPhone 14
  7. iPhone 14 Pro
  8. iPhone 14 Pro Max
  9. Samsung Galaxy S21 Ultra
  10. Samsung Galaxy S21
  11. Samsung Galaxy S23 Ultra
  12. Samsung Galaxy S23 Plus
  13. Google Pixel 3a
  14. Google Pixel 4 XL
  15. Xiaomi 12T Pro
  16. Google Pixel 6
  17. Samsung S20 Plus

Yapo matoleo mengi kikubwa ni kuicheki kwa kufuata hatua zilizoelezewa hapa

Jinsi eSIM inavyofanya kazi

Embed Subscriber Identity Module yaani eSIM inakuwa ndani ya simu kama “chip”

Jina la hiyo chip huitwa eUICC inakuwepo ndani ya simu milele na haiwezi kutolewa

Chip ya eUICC inawekewa programu kiwandani programu itakoyoweza kusoma taarifa zinazohitajika na mtandao wa simu

Taarifa hiyo ikiwemo namba yako ya simu

Hivyo simu ikishascan qr code eUICC itazisoma taarifa na kuzihifadhi na kisha kukuanganisha na mtandao husika

Na itaanza kufanya kama laini za kawaida plastiki

Taarifa za laini hii inaweza kuondolewa ama kuongezwa nyingine kikawaida eSIM inaweza kuhifadhi mpaka laini nane

Hitimisho

Natumai maelezo haya mafupi yameweza kukupa mwangaza wa maana ya eSIM

Hutokuwa na haja ya kujiuliza eSIM ni nini isipokuwa kazi kubwa ni kukagua kama kifaa unachotumia kinayo hiyo teknolojia

Maoni 38 kuhusu “eSIM ni nini? Fahamu kama simu yako inayo

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

nokia thumbnail

Simu mpya za Nokia zilizotoka 2023-2024 na bei zake

Kwa mwaka 2024, kampuni ya HMD Global inayotengeneza simu za Nokia hawajatoa toleo jipya mpaka sasa machi 2024 Taarifa kutoka vyanzo mbalimbali zinasema HMD inatarajia kutoa matoleo 17 mwaka 2024 […]

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram