SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu Nzuri za Google Pixel na Bei Zake (2022)

Brand

Sihaba Mikole

June 23, 2022

Kwenye ukurasa huu kuna orodha ya simu kumi za google pixel na bei zake

Google Pixel ni simu nzuri za android ambazo huwa zinapiga picha safi na bora

Na kiuhalisia simu za zamani kama iPhone 6 Plus hazifiki simu za zamani za pixel kama 3a

Katika hii orodha kuna pixel za kuanzia mwaka 2019 hadi 2021

Mpaka mwezi juni 2022 google ilitangaza toleo jipya moja

Google Pixel 6

Google Pixel 6 ni toleo jipya kabisa la pixel ambalo lilitoka 2021 mwezi wa kumi

Matoleo ya Pixel 6 yanatumia processor ambazo google wamezibuni wenyewe

Chip hizo ni Google Tensor

Google Tensor utendaji wake una nguvu kwa sababu core zenye nguvu zinatumia Cortex X1 na Cortex A76

Ubora wa kioo pia ni wa kuvutia kutokana na kutumika kwa Amoled

simu ya google pixel 6

Kioo cha pixel 6 kina HDR10+

HDR10+ huboresha muonekano wa vitu ili viendane na jinsi vinavyoonekana kwenye mazingira halisi

Simu inatumia kamera  ambazo zinapiga picha kali

Pamoja na simu hii ya google kuwa na betri yenye 4614mAh, ukaaji wake wa chaji sio mkubwa sana

Kwani simu ikiwa inaperuzi intaneti inachukua masaa 12 kuisha chaji

Bei ya Google Pixel 6 Tanzania

Katika masoko ya dunia google pixel 6 yenye GB 128 na RAM GB 8 inauzwa shilingi 1,235,430.00/=

Ukiitazama simu hii kiundani, ina vitu vingi ambavyo wake ni mkubwa

Vitu ambavyo si rahisi kuvikuta katika simu zinazouzwa chini ya laki nne

Google Pixel 6 Pro

Simu ya Google Pixel 6 Pro ni simu ya android ya daraja la juu.

Katika orodha ya simu zenye camera nzuri Google Pixel 6 Pro ipo

Na yenyewe uwezo wake wa kufungua app na kucheza gemu ni wa kuridhisha sana

Hii inatokana na simu kutumia chip ya Google Tensor

Kioo cha Google Pixel 6 Pro ni cha LTPO AMOLED chenye refresh rate 120Hz na resolution ya 1440 x 3120 pixels

simu ya google pixel 6 pro

Hii inamaanisha ustadi wa kioo kuonyesha rangi halisi ina usahihi mkubwa

Ni moja ya simu za 5G zinazotumia toleo jipya la Android 12

Google Pixel 6 Pro ina betri kubwa lenye ujazo wa 5003mAh

Ila ukaaji wa chaji unazidiwa na simu ya iPhone 13 Pro Max

Pixel 6 Pro inadumu na chaji masaa 12 tu simu ikiwa kwenye intaneti masaa yote

Bei ya Google Pixel 6 Pro Tanzania

Pixel yenye memori ya GB 128 na RAM ya GB 8 ni 1,864,800.00/=

Kwa Tanzania tarajia pesa kuwa zaidi ya milioni mbili

Bei yake kiuhalisia ni kubwa

Kiasi hiki cha bei kinaepeleka simu kwenye ushindani na Samsung Galaxy S22+ 5g

Samsung Galaxy S22+ 5g inaicha pixel 6 pro kwa sehemu kubwa

Google Pixel 6a

Simu ya Google Pixel 6a ni simu mpya ya pixel ambayo imetangazwa hivi karibuni mwezi mei

Inatarajiwa kuingia sokoni ifikapo mwezi julai

Hivyo hakuna taarifa za bei yake kwa wakati huu

simu ya google pixel 6a

Lakini inatarajiwa kutumia chip ya Google Tensor, kioo cha amoled, memori aina ya UFS

Pia uwezo wa kuzuia maji kupenya ndani simu

Kwa Taarifa zaidi kuhusu pixel 6a, pitia sifa za simu ya pixel 6a kwenye tovuti ya GSMArena

Google Pixel 5

Moja ya simu ambayo Google waliizindua 2020 ni simu ya Google Pixel 5

Hii ni smartphone yenye viwango vya IP68

Kwa maana maji ya kina cha mita moja hayawezi ingia ndani ya simu

Kioo chake ni kizuri linapokuja uangavu na uonyeshaji wa vitu kwa rangi zake halisi

Ubora wa rangi unachagizwa na kioo cha oled, refresh rate ya 90Hz na HDR10+

simu ya google pixel 5

Pitia hapa kuelewa, maana ya hdr na jinsi inavyofanya kazi

Ina idadi ya kamera zipatazo mbili ambapo kamera kubwa inatumia dual pixel pdaf

Lakini ukaaji wa chaji sio wa kuridhisha

Inatunza moto kwa muda wa masaa 12 wakati wa kuperuzi

Ila chaji ianpeleka umeme wa wastani wa wati 18

Hivyo betri ya 4000mAh inaweza chukua modo kujaa

Bei ya Google Pixel 5

Kwa sasa simu inapatikana kwa bei ya 1,1655,00.00/=

Bei hii ni kubwa hasa kama utailanginisha na simu za xiaomi

Lakini pixel 5 ni simu inayopokea toleo jipya la Android 12

Google Pixel 5a 5G

Google Pixel 5a 5G ni simu ya 5g ambayo inatumia chip ya snapdragon 765G 5G

Hii chip ina nguvu inayoifanya simu kuwa na utendaji mkubwa na wa haraka

Simu inakuja na Android 11 lakini inaweza kupokea toleo la Android 12

Kioo cha google pixel 5a 5G ni cha oled chenye resolution ya 1080 x 2400 pixels

simu ya google pixel 5 5g thumbnai

Hii ni simu nyingine isiyopitisha maji kutokana na kuwa na IP67

Betri ya google pixel 5a 5G ina ukubwa wa 4680 mAh

Ila ukaaji wa chaji ni kiwango kikubwa ukilinganisha na pixels  nyingi

Ukiwa unaperuzi intaneti simu inachukua masaa 18 mpaka chaji kuisha

Huu ndio muda ambao iPhone 13 Pro Max inatumia kwenye intaneti mpaka kuisha chaji

Bei ya Google Pixel 5a 5G

Pixel 5a 5G yenye ukubwa wa GB 128 na GB 6 ni shilingi 933,200.00/=

Maamuzi ya kununua simu hii yanaweza kukwama kama utakutana na sifa za xiaomi 12 pro

Ilinganishe hapa bei ya hii simu na ubora wa simu ya xiaomi 12 pro

Google Pixel 3a

Google Pixel 3a ni simu ya mwaka 2019 hivyo inakuja na Android 9.0

Na inaweza kupokea toleo la Android 12

Ni moja ya simu ya bei nafuu ya pixel inayoweza kununuliwa na Watanzania wengi

Uzuri ni kuwa unafuu huo wa bei unakupa pixel yenye kioo cha oled, memori ya GB 64 kamera inayoweza kurekodi video za 4K

simu ya google pixel 3a

Angalizo,

Usitarajie makubwa sana kwenye Google Pixel 3a

Kwani ina kamera moja, inatumia memori za eMMC, betri yake ni dogo

Na hata kasi yake ya kuchaji simu ni ndogo pia kwani ni wati 18

Bei ya Google Pixel 3a

Bei halisi ya pixel 3a ni shilingi 320,000/=

Kwenye mtandao wa aliexpress unaweza kuipata chini ya laki tatu

Ila kwa Tanzania bei yake inafika laki tatu na nusu

Google Pixel 4 XL

Kwa sasa Google Pixel 4 XL ni moja pixel ambazo unaweza kuipata kwa bei nafuu

Wakati ilipotoka mwaka 2019 ilikuwa ni simu ya kundi la juu

Hii ni kwa sababu simu inatumia processor yenye nguvu katika kufanya kazi

Chip inayotumi pixel 4 xl ni Snapdragon 855

simu ya google pixel 4 xl

Na pia ina kioo cha oled chenye refresh rate 90HZ

Refresh rate kubwa huwa inafanya simu kuwa nyepesi wakati wa kutachi na kuperuzi

Ila sasa betri yake lina ukubwa 3700mAh hivyo usitarajie ukaaji wa chaji wa kiwango kikubwa

Simu ina kamera aina ya wide na Telephoto

Kamera ya wide ina OIS na dual pixel pdaf

Kitu kinachoongeza ufanisi wakati wa kurekodi video na kupiga picha

Bei ya Google Pixel 4 XL

Kuna google pixel 4 xl ya GB 64 ambayo bei yake kwa sasa ni 839,880.00/=

Kwa Tanzania bei inaweza ikawa kubwa

Ila kama ni used bei inaweza kuwa chini

Google Pixel 4

Simu ya Google ina vitu vingi vinavyofanana na pixel 4 xl

Ikiwemo processor, kioo, aina za kamera

Ila pixel 4 ina betri dogo sana la ukubwa wa 2800mAh

simu ya google pixel 4 xl

Hii inafanya simu kukaa na chaji masaa machache kama ukiwa unatumia intaneti

Japokuwa inakuja na android 10 aimu inaweza kupokea toleo la 12

Bei ya Google Pixel 4

Bei ya Google Pixel 4 ya GB 64 ni shilingi 613,579.00/=

Kwenye mtandao wa aliexpress simu inapatikana kwa bei ya chini zaidi

Google Pixel 4a

Pixel 4a ni simu nyingine nzuri yenye kamera moja yenye kupiga picha kwa usahihi

Google Pixel 4a iliingia sokoni mwaka 2019

Imepita miaka mitatu ila ni simu inayochuana na simu nyingi za mwaka 2021 na 2022

Hilo linasababishwa na simu kutumia kioo cha oled chenye resolution ya 1080 x 2340 pixels

simu ya google pixel 4a

Pia simu kuwa na protector ya Gorilla 3 ambapo simu kama infinix note 12 vip haina

Lakini pia kamera yake kuwa na Dual Pixel Pdaf na OIS

Kuna simu za oppo mpya ambazo hazina OIS

Betri yake pia sio kubwa hivyo ukaaji wa chaji ni wa masaa machache

Bei ya Google Pixel 4a

Kwenye mtandao wa Aliexpress bei ya hii simu ni shilingi 676,570.00/=

Hii ni bei ya pixel 4a ya GB 64

Kwa wauzaji wa Tanzania bei inaweza kuzidi laki saba

Google Pixel 3

Simu ya Google Pixel 3 ni simu ya Android 9 iliyotoka mwaka 2018

Kisifa inafanana na pixel 3a

Ila hii na yenyewe ina betri dogo

Ni simu ambayo haina sehemu ya kuweka earphone

simu ya google pixel 3

Utendaji wake ni wa wastani kwa nyakati za sasa

Japokuwa inatumia chip ya Snapdragon 845 ambayo ilikuwa ni moja ya chip yenye nguvu nyakati hizo

Chaji yake ina kasi ndogo ya wati 18

Bei ya Google Pixel 3

Kutokana na simu kuwa na ubora katika sehemu chache inafanya kuwa na bei ndogo

Kwani bei yake ya GB 64 ni shilingi 373,280.00/=

Inaweza ikawa ni bei kubwa kwa baadhi ya watu ila hii ni bei ndogo ukizitazama pixel nyingi zilizomo

Maoni 37 kuhusu “Simu Nzuri za Google Pixel na Bei Zake (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 pro thumbnail

Bei ya Google Pixel 8 Pro na Sifa zake Muhimu

Simu ya Google Pixel 8 Pro imezinduliwa mwezi wa kumi (oktoba) 2023 Ni simu ya daraja la juu kama ilivyo kwa iphone na samsung matoleo ya S-series Kwa maana hiyo […]

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

google pixel fold thumbnail

Ubora na bei ya simu mpya ya Google Pixel Fold

Fold ni aina ya simu za kujikunja. Kwa muda mrefu makampuni ya Samsung, Huawei na Oppo wamekuwa wakitengneza simu za aina hii Hivi karibuni tecno na pixel pia zimeingia katika […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram