SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya simu ya Xiaomi 12 Pro na Sifa Zake [2022]

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 10, 2022

Simu ya xiaomi 12 pro ni simu ya android ambayo imetoka mwishoni mwa mwaka 2021

Xiaomi 12 Pro ina ubora ambao unachuana na simu ya samsung galaxy s22+ 5G

xiaomi 12 pro muonekano

Kitu kinachofanya bei ya xiaomi 12 pro kuzidi shilingi milioni moja na laki tano

Ukifahamu sifa itakusaidia kutambua kama ni simu nzuri inayostahili kununuliwa kwa bei iliyopo hapo chini

Bei Xiaomi 12 Pro Tanzania

Bei ya xiaomi 12 pro ya ukubwa wa GB 256 na RAM ya GB 8 ni shilingi 2,000,000/=

Hii ni bei ya Aliexpress.

Kama unainunua aliexpress mpaka ifike Tanzania itakugharimu shilingi 2,020,000/=

Ukubwa wa memori si kitu kinachosababisha simu hii ya xiaomi kuwa na bei kubwa

Bali ni processor, kioo, software, kamera na aina ya bodi ya simu

Fuatalia uzielewe sifa zake zote kama zilivyoainishwa humu

Sifa za simu ya Xiaomi 12 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 8 Gen 1
  • Core Kubwa Sana (1) – 1×3.00 GHz Cortex-X2
  • Core Zenye Nguvu (3) – 3×2.50 GHz Cortex-A710
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.80 GHz Cortex-A510
  • GPU-Adreno 730
Display(Kioo) LTPO AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • MIUI 13
Memori UFS 3.1, 256GB,128GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera nne

  1. 50MP, Dual Pixel PDAF(wide)
  2. 50MP(ultrawide)
  3. 50MP(Telephoto)
Muundo Urefu-6.73 inchi
Chaji na Betri
  • 4600mAh-Li-Po
  • Chaji-120W
Bei ya simu(TSH) 2,208,447.23/=

Upi ubora wa Xiaomi 12 Pro

Hii ni xiaomi ya daraja la kwanza hivyo tarajia ubora katika kila idara

Simu ina kioo ambacho kinaonyesha vitu bila kupoteza uhalisia wa rangi

xiaomi 12 pro

Inatumia chip yenye utendaji mkubwa kitu kinachoifanya simu kuwa na nguvu

Ni simu ambayo ina mfumo reverse charging kwa maana inaweza kuchaji kifaa kingine

Chaji yake inawahi kujaza betri chini ya dakika 25

Uwezo wa Network

Simu ina network zote ikiwemo 4G na 5G

Network yake ya 5G haisapoti 5G ya mmWave ambayo huwa na kasi kubwa zaidi

Aina ya 4G simu inayotumia ni LTE Cat 24

Spidi ya juu kabisa ya kudownload ya LTE Cat 24 ni 2500Mbps

Hii ni kasi ambayo huwezi kuipata kwenye mitandao karibu yote Tanzania

Ila simu ina masafa mengi yakiwemo yanayotumika na mitandao ya simu nchini

Ubora wa kioo cha Xiaomi 12 Pro

Kioo cha xiaomi 12 pro ni cha aina ya LTPO AMOLED

Hiki ni kioo ambacho kina rangi bilioni moja tofauti na IPS LCD ambazo huwa na rangi milioni 16

Hii inamaanisha vitu vingi vitaonekana kwa rangi zake halisi

Kioo pia kinaongezewa ubora wa Dolby Vision na HDR10+

Uangavu wa kioo unaweza kuonyesha vitu vizuri simu ikiwa inatumika juani

Kwa sababu kiwango chake cha nits (vipimo vya uangavu) unafika 1000

Na uzuri mwingine wa kioo chake unachagizwa na simu kuwa na resolution na refresh rate kubwa

Ina refresh rate ya 120 na resolution ya 1440 x 3200 pixels

Nguvu ya processor ya Snapdragon 8 gen 1

Processor ambayo xiaomi 12 pro inatumia ni snapdragon 8 gen 1

Ni processor ya simu inayoshika nafasi ya pili kiuwezo nyuma ya apple a15 bionic

Kwenye app ya geekbench, snapdragon 8 gen 1 ina alama 1216

xiaomi 12 pro processor

Wakati app ya antutu processor ina alama 1,037,000

Kiuhalisia hata exynos 2200 ya samsung galaxy s22+ inazidiwa na chip hii ya snapdragon

Hii inasababishwa na aina ya miundo ambayo chip imetumia

Kwenye core kubwa kuna Cortex X2

Na core zenye nguvu ndogo kumetumika muundo wa Cortex A710

Na pia core ambazo zinatumia nguvu ndogo zinatumia muundo wa Cortex A510

Uwezo wa betri na chaji

Ukubwa wa betri ya xiaomi 12 pro ni 4600 mAh aina ya Li-Po

Kiuwezo, simu inakaa na chaji masaa 74 kama ikiwa haitumiki mara kwa mara

Kwenye majaribio ya gsmarena, betri ya xiaomi inakaa na chaji masaa 10 na dakika 46 simu ikiwa inatumia intaneti muda wote

Kiujumla uwezo wa simu kukaa na chaji sio mkubwa

iPhone 13 Pro Max ambayo ina betri dogo inakaa na chaji masaa 18 simu ikiwa kwenye intaneti muda wote

Chaji ya xiaomi 12 pro inaijaza betri ya simu kwa dakika 21 tu

Hii inatokana na kasi ya chaji kupeleka umeme wa wati 120

Ukubwa na aina ya memori

Kwenye upande wa memori kuna xiaomi 12 pro ya GB 128 na RAM ya GB 8 na ya GB 256 na RAM ya GB 8 au 12

Hivyo kuna matoleo matatu

Aina ya memori simu inazotumia ni UFS 3.1 ambazo husafirisha data kwa kasi kubwa

Kitu kinachoifanya simu kuwaka kwa haraka

Na app kufunguka kwa sekunde chache

Uimara wa bodi ya Xiaomi 12 Pro

Kumbuka kuwa hii ni simu ya daraja la juu

Simu mpya za bei kubwa huwekewa bodi imara za kioo

Xiaomi 12 Pro ina kioo cha Gorilla Victus upande wa nyuma na mbele

Upande wa pembeni haijaainishwa aina ya bodi iliyopo

Simu ina urefu na upana wa inchi 6.73

Hivyo simu ni ndefu kiasi chake

Urefu ambao unaifanya simu kuwa na kauzito fulani wakati wa kuibeba

Kwani uzito wake ni gramu 204

Ubora wa kamera

Hii ni simu ya xiaomi macho matatu

Ina kamera ya Ultrawide inayopiga picha eneo pana sana kwa nyuzi 115

Pia ina kamera kwa ajili ya kupiga picha vitu ambavyo vipo mbali na kamera

Kamera ya aina hiyo huitwa Telephoto

xiaomi 12 pro kamera

Mfumo wake wa kamera una autofocus ya PDAF na dual pixel PDAF

Kitu kinachofanya picha kutokea kwa uzuri

Kwenye upande wa kurekodi video simu ipo vizuri zaidi

Inaweza kurekodi video kwa ubora mpaka wa 8K kwa kasi ya 24 fps na video za aina nyingine kwa kasi zaidi ya 60 fps

Ubora wa Software

Simu ya xiaomi 12 pro inakuja na mfumo endeshi wa android 12

Na inatumia pia software ya MIUI 13

Kwenye MIUI 13 kuna mfumo wa kuscreenshot unaoweza kupiga picha kwa urefu unaotaka wewe

Mfumo huo pia umeongezwa kwenye android 12

Kabla ya hapo mtu aliweza kupiga picha kipande cha screen pekee

Lakini pia toleo jipya la android lina kitu kinaitwa color extractor

Kwa maana rangi za vitu vingine vinanakili rangi ya theme (wallpaper)

Yapi Madhaifu ya Xiaomi 12 Pro

Udhaifu mkubwa wa simu hii ni uwezo mdogo wa kukaa na chaji

Mtumiaji wa simu atalazimika kuchaji zaidi ya mara moja kwa siku kama anatumia intaneti mara kwa mara

Kuchaji simu kwa chaji ya 120W mara kwa mara kunapunguza uwezo wa betri kukaa na chaji

Hivyo maisha ya betri yanakuwa mafupi

Kitu kingine ni simu kutokuwa na uwezo wa kuzuia maji kupenya

Fikiria simu ya daraja la kati ya samsung galaxy a73 haipistishi maji kwani ina IP67

Lakini simu hii haina

Neno la Mwisho

Bei ya xiaomi 12 pro ni ndogo ukilinganisha na ubora wa simu

Kwa muhitaji wa simu yenye uwezo mkubwa xiaomi hii itampa kila kitu kizuri kuhusu simu janja

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram