SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Redmi 10C na Sifa Muhimu (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

June 26, 2022

Moja ya simu ambayo Xiaomi wameachia mwaka 2022 ni Redmi 10C

Ni simu inayoingia kwenye kundi la kati la chini kutokana na sifa zake

Bei ya Redmi 10C kwa maeneo mengi ya Tanzania inazidi laki tatu na nusu

redmi 10c muonekano

Lakini ni simu ya bei ndogo inayoendana na ubora wa simu ila sio kama iPhone 11 Pro Max

Unaweza ukatembelea linki iliyopo inayoonyesha ubora na bei ya iPhone 11 Pro Max

Katika uchambuzi uliopo utafahamu bei halisi ya Xiaomi Redmi 10C katika masoko ya dunia na sifa zake kiundani

Bei ya Redmi 10C ya GB 64 na GB 128

Redmi 10C yenye ukubwa wa GB 64 bei yake ni shilingi 330,000/=

Na ile ambayo memori yake ni GB 128 inaenda mpaka shilingi 415,000/=

Hizi ni bei za aliexpress ya China, na inajumuisha gharama zote mpaka usafirishaji

Lakini gharama zinaweza kubadilika kutokana na mabadiliko ya shilingi ya Tanzania na dola

6redmi 10c summary

Hii simu haina sifa kubwa sana lakini inaizidi simu ya oppo a54 ambayo bei yake ni kubwa kiasi

Pitia hapa: Sifa muhimu na bei ya OPPO A54

Kisha linganisha kwa kutazama sifa za redmi kwenye jedwari

Sifa za Simu ya Redmi 10C

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Snapdragon 680 4G
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.4 GHz Kryo 265 Gold
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.9 GHz Kryo 265 Silver
  • GPU-Adreno 610
Display(Kioo) IPS LCD
Softawre
  • Android 11
  • MIUI 13
Memori UFS 2.2,128GB,64GB na RAM 3GB,4GB
Kamera Kamera mbili

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 330,000/=

Ni upi ubora wa Redmi 10C?

Ubora mkubwa wa hii simu ni kutumia memori ambazo zinasafirisha data kwa kasi kubwa

Ni moja ya simu inayokaa na chaji muda mrefu

Pia kamera zake zinatoa picha za kuvutia

Inakuja na memori zinazoweza kuhifadhi appilkesheni nyingi

Ina bei inayovumilika

Ila simu za kundi la kati huwa zina mazuri mengi na mapungufu mengi pia

Fuatilia vitu vyote vya redmi iliyopo kuanzia network mpaka ubora wa software hapa

Uwezo wa Network

Redmi 10C ni simu ya 4G yenye masafa yapatayo 12

Hivyo kila laini ya simu inayosapoti 4G itakubali Tanzania

Aina ya 4G inayotumia ni LTE Cat 13

edmi 10c network

Fahamu kiundani : maana ya 4G na aina zake

Smartphone yenye LTE Cat 13 inaweza kudownload kwa kasi inayofikia 300Mbps

Ukiwa nchini marekani na ukawa unatumia mtandao wa AT&T utaweza kuifikia hii spidi lakini sio Tanzania

Kasi 300Mbps inaweza kupakua faili la 1500MB kwa sekunde 40

Ubora wa kioo cha Redmi 10C

Simu haina kioo kizuri kutokana na kuwa na resolution ndogo ya 720 x 1650 pixels

Japokuwa vitu vitaonekana vizuri lakini si kwa ubora wa kama vioo vya amoled

Kwa bahati mbaya kioo cha redmi 10c ni ips lcd

Kirefu cha ips lcd ni in-plane switching liquid crystal display

redmi 10c display

Hivi vioo huwa vina contrast ndogo

Kwa maana vina uwezo wa kuonyesha rangi chache

Na huwa vinapata shida kuonyesha rangi nyeusi sahihi

Gharama na bei ya kioo cha lcd huwa ni ndogo

Ndio maana na simu imekuwa na bei nafuu kiujumla

Nguvu ya processor Snapdragon 680 4G

Redmi 10C inatumia chip ya Snapdragon 680 4G katika kufanya kazi zake

Kila kitu unachokifanya kwenye simu kinachakatwa na processor

Chip ikiwa na nguvu kubwa itaweza kufanya kazi nyingi kwa haraka na kwa ufanisi

Snapdragon 680 ina core nane ila utendaji wake ni wastani kama sio wa chini

processor ya simu ya redmi note 10 pro

Hii inazidiwa na chip ya mwaka 2017 iliyopo kwenye Samsung Galaxy Note8

Katika applikesheni inayopima nguvu ya processor ya GeekBench Snapdragon 680 ina alama 376 kwenye core moja

Kiasi cha magemu mengi kucheza kwa resolution ndogo

Hii inatokana na core nne zenye nguvu kutumia muundo wa Kryo 265 Gold

Kryo 265 Gold huwa una mizunguko michache na kufanya kazi chache kwa sekunde

Kama utaitumia simu kucheza gemu sana basi tegemea simu kuwa inachemka mara kwa mara

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya Redmi 10c ni kubwa

Hivyo simu inaweza kukaa na chaji kwa masaa yanayozidi 14 ukiwa unatumia intaneti muda wote

Hii inatokana na ujazo wa betri kuwa 5000mAh

Chaji yake inapeleka umeme wa wati 18

Hivyo simu inaweza ikachukua masaa takribani matatu kujaa

Inatokana na betri kuwa kubwa sana kitu kinachosababisha betri kujaa taratibu

Ukubwa na aina ya memori

Hii simu ina matoleo ya aina tatu

Bei ya redmi 10c zinaoongezeka kadri ukubwa wa RAM na ROM unayoongezeka

Simu ipo ya GB 64 inayotumia RAM ya GB 3 au GB 4

Pia ipo ya GB 128 na RAM ya GB 6

Cha kuvutia ni kuwa aina memori simu iliyonayo ni UFS 2.2

Kasi ya kusafirisha data ni 1200MBps

Hii huwa inafanya simu kufungua applikesheni kwa sekunde chache ukilinganisha simu zenye memori za eMMC 5.1

Uimara wa bodi ya Redmi 10C

Mara nyingi simu za bei nafuu huwa inaundwa kwa bodi za plastiki upande wa nyuma

Hii simu haina kioo cha Gorilla kwenye screen

Na pia haina uwezo wa kuzuia maji kupenya

redmi 10c bodi

Hivyo ni muhimu kuweka kava ya simu na screen protector

Bila hivyo rangi ya simu upande wa nyuma inaweza ikawa inachunika mara kwa mara

Ama simu kupasuka kirahisi

Ubora wa kamera

Ubowa wa kamera ya Redmi 10C sio mkubwa sana

Kwani aina ya ulengaji inayotumia ni PDAF

PDAF inaweza kukitambua kitu kinachopigwa picha kama haraka ila sio kama dual pixel pdaf

Simu janja hii ina kamera mbili ambazo ni wide(kamera kuu) yenye 50MP na depth yenye 2MP

redmi 10c muonekano camera

Hii kamera ya depth huwa haina maana kwa sababu haipigi picha na simu yenye camera PDAF

Kazi kubwa ni kupima kiasi cha eneo kinachostahili kuonekana kwenye picha

Na pia kutengeneza ukungu ukungu(brul) nyuma ya kitu kinachopigwa picha

Kamera zake zinaweza kurekodi video za full hd pekee

Ubora wa Software

Mfumo endeshi ambao simu inatumia ni Android 11

Xiaomi bado hawajaainisha kama redmi 10c inaweza kupokea android 12

Xiaomi ni tofauti kidogo na simu za google pixel upande wa kupokea matoleo mapya ya android mara kwa mara

Mbali na hilo redmi inakuja na mfumo wa MIUI 13

redmi 10c SOFTWARE

MIUI 13 ina mfumo mzuri wa ku-screenshot

Kwani inakupa chaguo la ku-screenshot kitu kwa urefu unaotaka

Na pia kamera yake ina scanner inayoweza kuscani dokumenti mbalimbali

Yapi Madhaifu ya Redmi 10C

Simu hii ni nzuri kiasi chake ila ukilinganisha na simu za huawei utagundua simu ina madhaifu mengi

Kioo chake cha IPS LCD kina resolution ndogo na uangavu mdogo

Utendaji wake ni wa kiwango cha chini hasa kwenye uchezaji gemu

Chaji inapeleka umeme kidogo unaojaza betri masaa mengi

Redmi 10c haina kamera ya ultrawide wala telephoto

Simu haiji na toleo jipya la android 12 ambalo limeboreshwa kiusalama

Neno la Mwisho

Madhaifu unayoyaona yanafanya bei ya simu ya Redmi 10C kuwa ndogo

Simu za daraja la juu huwa zina kasoro chache sana

Na aina ya simu hizo bei yake huwa ni kubwa

Yote ya yote Redmi 10C ni simu nzuri ya daraja la kati yenye bei inayovumilika na inayoendana na ubora wake

Maoni 4 kuhusu “Bei ya Simu ya Redmi 10C na Sifa Muhimu (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

xiaomi 14 ultra

Simu 13 mpya na kali za Redmi na Xiaomi 2024

Kampuni ya Xiaomi sio ngeni kwa wengi Ni kampuni ya china inayotengeneza simu za madaraja yote kwa brandi za Xiaomi, Redmi na Poco Hapa kuna orodha ya simu mpya za […]

No Featured Image

Bei ya Redmi Note 13 na Sifa Zake Muhimu

Redmi Note 13 5G ni simu kutoka Xiaomi ya China ambayo bei yake kwa sasa ni shilingi laki nane Hii ni bei ya toleo lenye ukubwa wa GB 256 na […]

redmi 10a thumbnail

Bei ya Sasa ya Redmi 10A na Sifa Muhimu

Simu ya Redmi 10A iliiingia sokoni mwaka 2022 Ni aina ya simu inayolenga watu wenye matumizi ya kawaida kama sio machache Hivyo bei ya Redmi 10A ni chini ya laki […]

Jinsi ya Kutumia GPS kwenye Simu (Hatua kwa Hatua)

GPS kirefu chake ni Global Positioning System, ni mfumo wa utambuzi wa maeneo ambao unasimamiwa na Marekani Simujanja karibu zote zina huu mfumo Una faida kubwa sana hasa kama unajua […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram