SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Maana ya 4G na aina zake

Miongozo

Sihaba Mikole

May 12, 2022

4G ni aina ya mtandao wa simu za mkononi wenye spidi inayoanzia 10Mbps na inayoweza kufika mpaka 100Mbps

Lakini inapendekezwa zaidi spidi inayoanzia 18Mbps

Kirefu cha 4G ni fourth generation

Kwa maana ni kizazi cha nne cha mtandao wa simu

Kwenye posti hii utafahamu masafa ya 4G ya Tanzania na Maeneo yote ambayo 4G inapatikana hapa nchini

Tuchimbe kiundani.

Aina ya 4G

Kuna aina mbili za mtandao wa 4G

Aina zake zinatofautiana na taasisi ambayo imeweka vigezo vya mtandao kuitwa 4G

Aina hizo ni

  1. LTE (Long Term Evolution)
  2. WiMax ( Worldwide Interoperability for Microwave Accesses)

Lakini LTE ndio inayotumika kwa sehemu kubwa duniani ikiwemo hapa Tanzania

Hivyo tutaangazia zaidi LTE

Ndio maana baadhi ya simu zikiwa zinatumia 4G zinaandika LTE, ni kitu kimoja

Long Term Evolution zinatofautiana spidi

Kuna LTE ya kawaida ambayo spidi yale ya juu kabisa ya kusafirisha data inafika 100Mbps

Halafu kuna LTE Advance ambayo spidi yake ya kusafirisha data inafika 1Gbps kwenye kudownload

Kwa maana kama kuna miundombinu ya minara yenye kasi kubwa basi faili la ukubwa 1GB litamalizika kudownload baada ya sekunde nane tu

Sifa za mtandao wa 4G

Mtandao wa 4G huwa na masafa mengi yanayotofautiana kutoka nchi moja na nyingi

Hivyo kifaa chenye aina hii mtandao kinaweza kikatumika nchi moja lakini ikashindikana kutumika kwenye nchi nyingine

Kasi ya 4G huzidi 42Mbps na inaweza kufika mpaka 1Gbps

Kama unatest kasi ya mtandao unaotumia na ukapata chini ya 18Mbps maana yake wewe upo kwenye 3G aina ya HSPA

Tofauti ya 4G na GPRS, EDGE, H na H+

Kabla ya 4G kuna watangulizi wake ambao 3G na 2G

3G (third Generation) imegawanyika kati sehemu nyingi zinazotofautiana kasi

Aina za 3G ni kama zifuatazo

  1. WCDMA ambayo spidi yake ya kudownload inafika
  2. UMTS yenye spidi inayoweza kufika 2Mbps
  3. HSDPA ambayo spidi yake inafika 14.4Mbps
  4. HSPA (H) yenye kasi ya 14.4Mbps
  5. HSPA+ (H+) ambayo kasi yake ya juu inafika 28Mbps

Wakati mtandao wa Edge (E) spidi yake ya juu kupakua vitu inafika 473Kbps

Na upande wa mtandao wa GPRS (G) spidi yake ni ndogo zaidi ya edge

Hivyo utofauti mkubwa wa 4G na watangulizi wake ni kasi

Ukiwa na edge na gprs simu inashindwa kufungua hata picha za Whatsapp

Masafa ya 4G Tanzania

Kwa sasa mitandao yote ya Tanzania inakubali network ya 4G

Masafa yanatofautiana kutoka mtandao mmoja kwenda mwingine

Ni vizuri ukayafahamu masafa yote ili uweze kujua kama kifaa unachotumia kinaweza kukubali intaneti ya 4G nchini

Vodacom – 1800 MHz (B3 au 3)

Tigo – 800 MHz (B20 au 20) na 1800 MHz (B3 au 3)

Airtel – 700 (B28 au 28) MHz na 2100 MHz (B1 au 1)

Halotel – 2600 MHz (B7 au 7)

TTCL – 1800 MHz (B3 au 3) na 2300 MHz (B40 au 40)

Smile – 800 MHz (B20 au 20)

Zantel – 1800 MHz (B3 au 3)

Maeneo ya 4G Tanzania

Maeneo mengi ya mijini yana network ya 4G hapa Tanzania

Ila sehemu kubwa ya nchi hasa vijijini 4G haijafika

Kwa bahati mbaya maeneo mengine yanakosa mpaka 3G

Kama una simu ya ya 4G lakini eneo unaloishi halina, basi hutoweza kutumia network hiyo ya kasi zaidi hapa nchini kwetu

Baadhi ya Simu za 4G

Siku hizi kila simu inawezeshwa aina hii ya network

Ni simu chache ambazo hazina 4G

Mara nyingi ni simu chache za daraja la chini ndizo unaweza kutokuta lte

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram