SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Oppo A54 na Sifa Zake Muhimu (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

June 23, 2022

Tuingazie simu ya daraja la chini ya Oppo A54 kutoka kwenye kampuni namba tano kimauzo duniani

Simu  hii ilitoka mwaka 2021 mwanzoni kabisa

simu ya oppo a54 muonekano

Sifa zake zinafanya bei ya Oppo A54 kuwa chini ya laki tatu na nusu (inategemea na ukubwa wa memori)

Kwenye hii posti utafahamu bei yake kama inaendana na sifa zake kwa mwaka 2022

Bei ya OPPO A54 ya GB 64

Oppo A54 ambayo RAM yake ni 4GB na memori ikiwa na ukubwa wa 64 GB inauzwa shilingi 328,084.29/=

Kwa baadhi ya maduka kariakoo bei ya simu inaweza kuwa kubwa zaidi

Lakini haipaswi kuzidi laki tatu na nusu

simu ya oppo a54 summary

Bei ya hii simu ni kubwa ukifananisha na uwezo wake na sifa zake ambazo zimeorodheshwa chini

Kuna simu za Redmi na Vivo zenye bei sawa na A54 ya Oppo lakini kiubora A54 inazidiwa (utajua sababu)

Sifa za Simu ya OPPO A54

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio P35
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.35 GHz Cortex-A53
  • Core Za kawaida(4) –  4×1.8 GHz Cortex-A53
  • GPU-PowerVR GE8320
Display(Kioo) IPS LCD,
Softawre
  • Android 10
  • ColorOs 7.2
Memori eMMC,128GB,64GB na RAM 6GB,4GB
Kamera Kamera tatu (macho matatu)

  1. 13MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(macro)
  3. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.51inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 330,000/=

Ni upi ubora wa oppo a54?

Ubora mkubwa wa oppo a54 ni kuhifadhi chaji kwa muda mrefu

Simu ina betri kubwa linalosaidia moto kukaa masaa ya kutosha

Lakini pia ina memori kubwa inayoweza kuchukua app na mafaili mengi

Lakini kwenye nyanja zingine(kama utakavoona) simu ina vitu vyenye ubora wa chini

Uwezo wa Network

Oppo hi ya 2021 ina network ya 4G aina ya LTE Cat 7

Simu inayokuwa na LTE Cat 7 inakuwa na uwezo wa kudownload faili kwa spidi inayofika 300Mbps

Lakini spidi kubwa pia inatokana na nguvu ya mtandao wa simu unaotumia

Ikizingatiwa 4G ya Tanzania haina spidi kubwa kwa laini karibu zote

simu ya oppo a54 network

Kwa bahati mbaya hii simu ililenga soko la India

Hivyo kuna baadhi ya masafa ya LTE yanayotumiwa na laini za simu hapa nchini oppo a54 haina

Masafa iliyo nayo ni 1, 3, 5, 8, 38, 40, 41

Tazama kwenye linki kujua masafa ya mtandao wa 4G yaliyopo Tanzania

Ubora wa kioo cha oppo A54

Oppo A54 inatumia kioo cha IPS LCD chenye resolution ya 720 x 1600 pixels

Kwa kutazama tu ubora wake kwenye kioo ni wa chini

Amoled huwa na ufanisi mkubwa kwenye kuonyesha vitu zaidi

Pia na uangavu wake si mkubwa

Nguvu ya processor ya MediaTek Helio P35

Fahamu kuwa simu inayozungumziwa kwenye kurasa huu ipo kwenye daraja la chini

Inatokana na kitendo cha simu kutumia chip ya MediaTek Helio P35

Nguvu ya Helio P35 ni ndogo sana

simu ya oppo a54 processor

Kiasi cha kwamba ni ngumu kwa kamera ya A54 kurekodi video zanye ubora wa 4K

Kwenye app inayopima nguvu ya processor ya GeekBench, Helio P35 ina alama 171

Nguvu ndogo inasababishwa na processor kutumia muundo wa Cortex A53 kwenye core zote

Kama unacheza gemu kubwa kwa resolution ya juu simu inaweza ikawa inachemka sana

Ama kukwama kwama

Uwezo wa betri na chaji

Oppo A54 ni moja ya simu inayotunza chaji muda mrefu

Hii inasababishwa na simu kuwa na betri kubwa

Lakini pia kuwa na processor inayotumia umeme mdogo katika kufanya kazi zake

Uwezakano wa simu kukaa na chaji kwa masaa zaidi ya 14 ni mkubwa

Ila sasa simu hii lazima ichukue masaa mengi kujaa

Maana chaji inapeleka umeme wa wati 18

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo ya aina tatu upande wa memori na ram

Ukubwa wa memori unaanza GB 64 mpaka GB 128

Na RAM ya 4GB mpaka 6GB

Kwa bahati mbaya memori zake ni za aina ya eMMC 5.1

Inalazimika kutumia memori zinazofirisha data ndogo kwa sababu chip haina uwezo wa kuchakata data nyingi

Kwa hiyo OPPO A54 inaweza ikawa inachelewa kuwaka wakati wa kuwasha

Uimara wa bodi ya oppo A54

Karibu simu zote za daraja la chini huwa na bodi za plastiki

Pia hata hii oppo imeundwa kwa bodi za plastiki

Na ina sapoti laini mbili

imu ya oppo a54 bodi

Lakini pia inakubali memori kadi

Hivyo unapata uhuru wa kuitanua memori ya simu

Plastiki huwa ni rahisi kuchunika rangi

Kadri inavyotumika muda mrefu ndivyo  ubora unavyopungua

Ubora wa kamera

Kama unataka oppo macho matatu ya bei nafuu basi A54 ipo

Ila jua kuwa ubora wa kamera zake tatu sio mkubwa

Kwani zinarekodi video za ubora wa ful hd pekee

simu ya oppo a54 CAMERA

Kamera kubwa ina ulengaji wa PDAF

Processor ya hii simu inachangia sana kamera kutokuweza kurekodi video ya 4K na kwa fremu nyingi

Aperture yake inapitisha mwanga mdogo kwani kipimo chake ni f/2.2

Hivyo basi ubora wa picha kwenye mwanga mdogo utakuwa ni mbaya

Ubora wa Software

Mfumo endeshi uliopo kwenye simu hii ni Android 10

Hakuna taaraifa iwapo oppo a54 inaweza kupokea Android 12

Haiwezi kushangaza kutokana na chip za MediaTek za daraja la chini kuwa na sapoti ndogo ya software

simu ya oppo a54 colorOS 7

Lakini mtumiaji atanufaika na mfumo wa OPPO wa CorolOS 7.2

Oppo wanadai kuwa mfumo una kitu kinaitwa Super Power Saving Mode

super Power Saving Mode inaiongezea simu muda wa kutumika pale betri inapokuwa limebakiza chaji kidogo sana

Yapi Madhaifu ya oppo A54

Kutokana na simu kuwa kwenye kundi la chini inafanya kuwa mapungufu mengi

Kubwa zaidi ni nguvu ndogo ya utendaji

Inaondoa utamu wa kutumia applikesheni yoyote unayotaka kwa raha

Kioo cha ips lcd huwa na rangi chache

Kitu kinachofanya baadhi ya vitu kutoonekana kwa rangi halisi

Mfano rangi nyeusi

Neno la Mwisho

Kama bei ya oppo a54 ingekuwa ni chini ya laki tatu basi ingekuwa ni simu nzuri ya bei nafuu

Lakini bei yake kuzidi laki tatu kunaipeleka simu kwenye ushindani na simu ya Redmi 9

Redmi 9 ina utendaji wenye nguvu kiasi ukilinganisha na oppo iliyopo

Ila oppo wana mfumo mzuri unosaidia simu kukaa na chaji muda mrefu

Si simu mbaya kuimiliki kwa mwaka 2022

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

thumbnail oppo

Simu mpya 12 nzuri za Oppo na bei zake 2024

Tangu mwishoni mwa mwaka 2023 mpaka sasa 2024 tayari kampuni ya OPPO toka china wametoa simu zaidi ya 15 za madaraja mbalimbali Hapa utakutana na orodha ya simu mpya za […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya sasa ya Oppo A17K na Sifa Zake

Oppo  A17K ni simu iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2022 mnamo mwezi oktoba Ni simu ya daraja nafuu ambayo haihitaji bajeti kubwa kuimiliki Kwani bei ya oppo A17K haizidi laki tatu […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram