SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Kampuni 10 Bora za Simu Kimauzo Duniani (2022)

Brand

Sihaba Mikole

June 13, 2022

Hii ni orodha ya kampuni bora za simu ambazo zimefanya vizuri kimauzo toka mwezi wa kwanza mpaka wa tano 2022.

Katika orodha kuna kampuni za simu kutoka Marekani, Korea Kusini na China pia Japani

Hapa kuna takwimu za idadi ya simu janja zilizouzwa tangu mwaka uanze

Na utaelewa maneneo na aina za simu ambazo zimeongoza kuuza sana

Tuziangazie takwimu za mauzo kwa undani wake

Samsung

Samsung ni kampuni kubwa zaidi nchini korea ambayo ndio imeuza simu nying mpaka sasa

Simu za samsung zimenunuliwa kwa 28.5% kati ya simu zote duniani kote

Kampuni hii ya korea inatengeneza simu za aina tatu aina ya galaxy

Na simu zake zinazofanya vizuri ni zile zinazotumia mfumo wa Android

kampuni bora za simu

Zipo samsung za bei rahisi, bei ya kati na bei kubwa

Galaxy ambazo zinauza sana ni matoleo ya Samsung A-Series

Ambapo katika simu milioni 74.5 zilizouzwa na samsung, Samsung Galaxy A12 na Galaxy A32 ndio zinaongoza kwa mauzo

samsung

Hii ni tofauti na apple wanauouza sana simu za daraja la juu

Pamoja na mauzo mengi, samsung inaachwa nyuma kimapato na apple

Kwani mapato ya samsung upande wa simu ni dola bilioni 21

Zifuatalie hapa, samsung za bei rahisi zenye soko kubwa

Apple

Apple ni kampuni ambayo inashika nafasi ya pili kimauzo ya simu duniani

Kabla ya mwezi machi simu za iphones zilikuwa zinaongoza kwa kununuliwa zaidi

Kwani apple iliuza simu kwa zaidi ya 29% mpaka mwezi januari

apple logo

Lakini baaada ya Samsung kuja na matoleo mengi mapya, apple ikawa inashika nafasi ya pili kwa mauzo ya 27.83%

Simu ambazo ziliifanya apple kushika usukani ni matoleo ya iPhone 13

Kumbuka kuwa apple hutengeneza simu janja za daraja juu pekee

Hizi simu hupatika kwa bei kubwa

Hivyo inaifanya iphones kuipatia mapato kampuni ya Apple Inc yanayofiki dola bilioni 97 kwa miezi minne ya mwanzo 2022

Apple inaweza kurudi nafasi ya kwanza kama watazindua smartphone mpya

Masoko makubwa ya iphones ni nchi zilizoendelea

Unaweza kutizama mlinganisho hapa kati ya samsung s22 ultra vs iphone 13 pro max

Xiaomi

Xiaomi ni kampuni ya china inayotengeneza simu za xiaomi, redmi na pocco

Hii ni kampuni inayofanya vizuri sana katika mauzo ya simu za kundi la kati

Kwa mwaka 2022, watengenezaji wa simu za redmi wanashikilia soko kwa mauzo ya 12%

xiaomi logo

Kwa kutazama, xiaomi bado ina safari ndefu kufikia nafasi za samsung na apple

Hata hivyo xiaomi wanajitahidi

Kwani kabla, huawei ilikuwa inaipita xiaomi kimauzo

Lakini tangu vikwazo vya Marekani iikumbe huawei imefanya kampuni zingine toka china kupanda juu

simu ya redmi note 10

Kwa mwaka 2022 Xiaomi wameachia simu za gharama aina ya matoleo Xiaomi 12

Lakini soko la China linatawaliwa sana huawei na oppo huku xiaomi yenyewe ikishika nafasi ya tano

Pitia hapa kufuatalia simu za xiaomi na bei zake

Huawei

Kabla ya mwaka 2020, Huawei ilikuwa imeshaipiku Apple kimauzo

Na hivyo kushika nafasi ya pili huku ikiwa inatawala kwa kiasi kikubwa nchini China kwa mauzo yanayozidi 39%

Aliyekuwa raisi wa USA bwana Trump aliishitumu Huawei kuhusu ukusanyaji wa taarifa za watu

huawei logo

Basi huawei ikapitia vikwazo vya USA vilivyoizuia simu zao kutokutumia huduma za google na Android

Taratibu huawei ikaanza kuanguka mpaka kushika nafasi ya nne

Huku kampuni tanzu ya huawei ikifahamika Hornor ikiwa ndio muokozi wa Huawei kwa sasa

huawei p50 pro

Kwa sasa huawei soko lake lina 6% pekee

Huku simu za hornor zikiwa zinaongoza kwa mauzo nchini China

Kumbuka huawei ni simu zinazotoa picha kali

Angalia hapa kuona picha ambazo zimepigwa na simu ya huawei

Oppo

Oppo ni kampuni ya smartphone iliyo chini ya kampuni ya BBK Electronic

Katika robo muhula wa kwanza oppo imeuza nakala za simu zipatazo milioni 30

Ambayo ni sawa na 5%

oppo logo

Mauzo ya oppo ni makubwa kwa sababu inatengeneza sana simu za daraja la kati na la chini

Japokuwa oppo pia huuza simu za gharama kama matoleo ya Oppo Find x

Lakini soko lake linapata shida kufikia simu za iphone na samsung

Oppo ina soko kubwa huko kwao china kuliko sehemu zingine

Na pia oppo hupatikana kwa wingi india

Vivo

Kampuni ya BBK Electronic ya China pia inaimiliki kampuni ya Vivo Communication Technology Co. Ltd.

Vivo Communication Technology ndio watengenezaji simu zote za vivo

Kwenye soko la mauzo ya simu duniani vivo ina 4%

vivo

Xiaomi inaizidi vivo kwa zaidi ya mara tatu wakati Samsung na Apple zinaizidi vivo karibu mara saba

Simu za vivo hazijaenea sana duniani

Japokuwa na wenyewe huwa wanatengeneza simu za madaraja yote

Kwa mfano Africa vivo inaachwa kimauzo na simu za infinix

vivo

Ila kiubora, smartphone nyingi za vivo ni nzuri kuliko za Infinix na tecno

Moja ya simu za vivo zinazofanya ni Vivo X70 Pro+ ambayo ina kamera kali

Realme

Simu za realme zinashika nafasi ya nane kimauzo kwa 3%

Hii inatengenezwa na kampuni toka china ambayo ipo chini ya oppo

realme

Mauzo mengi ya realme yapo china na india

Na yenyewe haijasambaa sana duniani kama ilivyo kwa simu za redmi

Baadhi ya simu ya realme Realme 9 5G na Realme C21

Hii kampuni hutngeneza kwa asilimia kubwa simu za madaraja ya chini na ya kati

Motorola

Motorola Mobility ni kampuni ya Marekani ambayo kwa sasa ipo chini ya Lenovo

Motorola ni moja ya kampuni inayotengeneza simu nyingi

Mwaka huu tu kwa mfano imeshazindua simu karibu nne mpya

motorola logo

Lakini ukubwa wa motorola sio kama zamani

Kwani mauzo yao kidunia ni 2.4%

Baadhi ya simu ambazo motorola inatengeneza ni Morola Moto G62 5G

motorola. phone

Pia motorola ni tofauti na apple

Kwani inatengeneza vile vile simu za matoleo ya daraja ya chini mpaka ya juu

LG

LG hufahamika zaidi kwenye uundaji wa tv na vitu vya majumbani kama mafriji

Lakini pia kuna smartphone nyingi tu ambazo LG wanatengeneza

lg

Kwa bahati mbaya hii kampuni imeshindwa kuhimili usindani mkubwa

Hivyo wameamua kusitisha kutengeneza simu

Pamoja na hayo, LG inashika nafasi ya tisa na kuziacha simu za Nokia na Sony kimauzo

lg wing

Kampuni hii ya korea kusini bado inashikilia soko kwa mauzo ya 1%

Moja ya LG ambazo zilifanya vizuri ni simu ya LG G8 ThinQ

Kampuni nyingine

Kampuni zingine za simu ambazo hazikutokea kwenye orodha zinauza chini ya 1%

Mfanno mzuri ni kampuni ya sony

sony

Wakati huo kampuni zingine za simu zimejikita kwenye soko la maeneo machache

Kwa mfano infinix, tecno na itel wamejikita kwenye baadhi ya nchi za Afrika na Asia

Hivyo inakuwa na ngumu kutokea kwenye list

 

Maoni 12 kuhusu “Kampuni 10 Bora za Simu Kimauzo Duniani (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

oppo find x6 pro thumbnail

Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Kuna matoleo mengi ya simu za oppo zenye ubora tofauti tofauti Zipo ambazo zina ubora wa kati, wa juu na wa chini Katika hizo, nyingi zinajitahidi kuwa na kamera zinazotoa […]

No Featured Image

Simu Mpya za Samsung na Bei Zake 2023

Kama unatafuta samsung mpya kwa mwaka 2023 basi upo sahihi Kwenye hii kuna simu zipatazo saba na maelezo mafupi kuhusu sifa zake Kwenye hii orodha ya simu mpya za samsung […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram