SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Simu 10 Nzuri za Huawei na Bei Zake (2022)

Brand

Sihaba Mikole

June 20, 2022

Hii ni orodha ya simu kumi za Huawei ambazo zimetoka kati ya mwaka 2017 mpaka 2022

Simu nyingi za Huawei zilizopo kwenye orodha ni zile za daraja la kati na la juu

Hivyo bei zake ni kubwa ambazo zinazidi laki tatu

Utaziona simu bora za huawei ambazo zinatumia mfumo endeshi wa Android na HarmonyOS

Tuchambue simu moja baada ya nyingine kuufahamu ubora wa simu za Huawei kiufasaha

Huawei P50 Pro

Simu ya Huawei P50 Pro ni simu ya mwaka 2021 inayotumia mfumo endeshi wa HarmonyOS 2.0

HarmonyOS 2.0 ni mfumo uliotengenezwa na Huawei kama mbadala wa Android

Kumbuka serikali ya USA iliiwekea vikwazo huawei vinavyoizuia kutumia teknolojia za kampuni za marekani ikiwemo Google

Kitu kinachoilazimisha huawei kutotumia huduma zinazomilikiwa na google kama youtube na Android yenyewe

Mbali na hiyo, P50 ni simu yenye utendaji mkubwa sababu inatumia processor ya Snapdragon 888 4G

huawei p50 pro

Kwa bahati mbaya simu haina 5G

Hii inatokana na kampuni inayounda chip ya TSMC ya Taiwan kusitisha kuitengenezea Huawei chip mpya zenye 5G

Sababu kubwa ni vikwazo vya Marekani

Kiujumla simu ni nzuri kwani haipitishi maji, inatumia kioo cha oled, ni moja ya simu yenye kamera nzuri betri yake inawahi kujaa chaji haraka kwa sabau chaji yake ina kasi ya Wati 66

Iwapo Huawei isingekuwa na vikwazo basi Huawei P50 Pro ingewekwa kundi moja na matoleo ya Samsung S21

Bei ya Huawei P50 Pro Tanzania

Kwenye masoko ya duniani hasa china na ulaya bei ya Huawei P50 Pro ni shilingi 2,097,900.00/=

Hii simu janja ina ubora karibu kwenye kila nyanja

Hivyo kwa Tanzania bei yake inaweza kukaribia milioni tatu

Huawei Nova 9 SE

Simu ya Huawei Nova 9 SE ni simu mpya ya Huawei ambayo ipo kundi la kati

Imetoka mwezi machi mwaka 2022

Na inatumia mfumo endeshi wa Android 11 ambao hauna apps za google kama gmail, youtube na google search

Utendaji wa simu ni wa wastani kwa sababu simu inatumia processor yenye uwezo wa kawaida

Processor hiyo ni Snapdragon 680 4G hivyo simu haina 5G

huawei nova 9 se

Kioo chake ni aina ya IPS LCD chenye resolution ya 1080 x 2388 pixels na refresh rate ya 90Hz

Hivyo uonyeshaji wavitu ni mkubwa lakini ubora wa LCD si mkubwa sana kama amoled au oled

Betri ya Nova 9 SE ina ukubwa wa 4000mAh na chaji yenye kupeleka umeme wa kiwango cha Wati 66

Kiwango hiko cha umeme kinajaza betri kwa 75% ndani ya dakika 25

Pia upande wa kamera upo vizuri kiasi chake japo si sana

Kuna jumla ya kamera nne ambazo hazitumii teknolojia dual pixel pdaf kwenye ulengaji

Bei ya Huawei Nova 9 SE

Bei ya Huawei nova 9 se yenye ukubwa wa GB 128 na RAM ya GB 8 ni shilingi 1,247,085.00/=

Sifa za huawei nova 9 se zinaifanya simu kuwa na bei kuwa kubwa kuliko uhalisia

Simu zinazotumia processor ya Snapdragon 680 huuzwa chini ya laki tano

Kiuhalisia simu kama Infinix Note 12 VIP inaiacha mbali Nova 9 SE

Huawei P30 Lite

Huawei P30 Lite ni simu ya mwaka 2019 ambayo inakuja na Android 9

Lakini inaweza kupokea toleo la Android 10

Hizi ni simu ambayo haikukutana na vikwazo vya USA

Hivyo applikesheni za google zinaweza kutumika

huawei p30

Simu inatumia chip ya yenye utendaji wa wastani hivyo utendaji wake sio mkubwa

Kioo chake ni cha IPS LCD chenye resolution kubwa 1080 x 2312 pixels

Betri yake ina ukubwa wa 3340mAh kitu kinachofanya ukaaji wa chaji kuwa mdogo

Simu ina jumla ya kamera nne huku kamera kubwa ikiwa na resolution ya 48MP

Bei ya Huawei P30 Lite

Bei ya Huawei P30 Lite inafika shilingi 1,031,417.15/=  za Tanzania

Hii ni bei kubwa ambayo inaweza kununua simu bora zaidi ya OPPO A96 5G na chenji ikabaki

Bei haina uhalisia na ubora wa simu

Kwani washindani wana simu nzuri za bei nafuu kuliko hii

Huawei Nova 9

Simu ya Huawei Nova 9 imetoka mwaka 2021

Inatumia mfumo endeshi wa HarmonyOS kwa simu za china

Ila kwa Nova 9 zinazopatikana ulaya hutumia android yenye EMUI 12

Lakini EMUI 12 haina youtube, gmail, google search, google play store na app zingine za google

huawei nova 9

Kioo cha nova 9 ni kizuri kutokana na kuwa na OLED ambacho kina rangi nyingi zinazofikia bilioni moja

Betri yake ina ukubwa wa 4300mAh

Ukubwa huu unaifanya simu kukaa na chaji masaa chini ya 100 kama ikiwa haitumiki mara kwa mara

Kamera zake nne zinaweza kurekodi video mpaka za 4K kwa spidi ya kawaida.

Ila video za HD kamera hurekodi kwa fremu nyingi zipatazo 960fps

Bei ya Huawei Nova 9

Bei ya Huawei nova 9 yenye ukubwa wa GB 128 ni shilingi 932,400.00/=

Bei ni kubwa kuliko ubora wa simu

Huawei Mate Xs 2

Huawei Mate Xs 2 ni simu ya kujikunja (Foldable) iliyotoka mwaka 2022

Unaweza ukiafanya simu kuwa pana kwa kuikunjua (inakuwa kama Tablet)

Ama unaweza kuifanya simu kuwa na upana mdogo kwa kuikunja(inakuwa simu ya kawaida)

Utendaji wa simu ni mkubwa kwa sababu simu inatumia chip ya Snapdragon 888 4G

huawei mate xs 2

Hivyo simu haina mtandao wa 5G

Ina kioo bora kinachoweza kuonyesha rangi nyingi

Kioo hiko ni OLED chenye resolution kubwa ya 2200 x 2480 pixels

Ukaaji wa chaji ni wa kuridhisha kwa sabau simu ina betri yenye ujazo wa 4600mAh

Na pia chaji yake inapeleka umeme mwingi wa wati 66 unaojaza betri chini ya dakika 60

Pia Mate Xs 2 inakuja na memori inayofika mpaka GB 512

Inatumia mfumo endeshi wa Harmony pekee

Bei ya Huawei Mate Xs 2

Bei ya Huawei Mate Xs 2 ni shilingi 4,911,510.24/=

Kama hujaona vizuri bei yake ni zaidi ya shilingi milioni nne na laki tisa

Kama ikija Tanzania bei yake lazima izidi shilingi milioni tano

Huawei Y9 Prime

Mwaka 2019 huawei walizindua toleo la simu ya daraja la kati ambayo ni Huawei y9 Prime

Hii simu inatumia mfumo endeshi wa Android 9 (Pie)

Lakini inaweza kupokea mfumo endeshi uliofuata yaani Android 10

Utendaji wa simu sio mkubwa kwa sababu chip ya huawei ya Kirin 710F ndio imetumika

Kioo cha Huawei Y9 Prime ni cha IPS LCD chenye resolution kubwa ya 1080 x 2340 pixels

Hivyo ubora wa kuonyesha vitu ni mzuri japo si kama kioo cha OLED

Chaji yake sio kubwa kama ya Huawei Mate, kwani ukubwa wake ni 4000mAh

Kwa hiyo simu haitokaa na chaji masaa mengi sana

Bei ya Huawei Y9 Prime

Bei ya Huawei Y9 Prime ni kubwa inayofika 540,266.13/=

Ni kubwa kwa sababu ni bei ambayo inaweza kununua simu ya Redmi Note 10

Ambapo Redmi Note 10 ina vitu vizuri vingi kuliko hii simu ya Huawei

Huawei P50 Pocket

Huawei wanatengeneza simu nzuri nyingi lakini changamoto ya vikwazo inawafanya kutumia chip zisizoendana na ubora wa simu

Mfano mzuri ni hii simu ya mwaka 2021 Huawei P50 Pocket

Ina kamera kali yenye kutumia teknolojia ya Laser Af kwenye ulengaji

Haitoshi inatumia kioo kinachoweza kujikunja cha OLED

huawei p50 pocket

Ambacho kina resolution kubwa ya 1188 x 2790 pixels

Hii simu unaweza ukaikunja na ikawa kama pocket (kipochi)

Japo betri si kubwa ila chaji yake ina kasi ya kuijaza betri kwa haraka

Kwani umeme unaoenda kwenye betri ni wati 40

Na inaweza kuchaji kifaa kingine kwa wati 5

Lakini pamoja na mazuri yote simu inatumia chip ambayo haina 5G  japo utendaji ni mkubwa

Chip hiyo Snapdragon 888 4G

Pitia hapa uelewe, aina ya processor za simu na kazi zake

Bei ya Huawei P50 Pocket

Hii ni simu nyingine ya Huawei yenye gharama kubwa kwani bei yake shilingi 2,797,200.00/=

Simu za kujikunja(Folding Phone) zimekuwa zikiuzwa bei kubwa

Kwa bahati mbaya hii huawei ubora wake si mkubwa sana ukilinganisha na bei

Bei hii inanunua simu ya iPhone 13 Pro Max

Huawei P50

Huawei P50 inaweza ikawa simu ya daraja la juu ya bei nafuu kutoka kwa kampuni ya Huawei

Kwani za hii simu pia inapiga picha nzuri

Kioo chake kinaonyesha picha vizuri na kwa uangavu

Kwani ni cha oled ambacho kina resolution ya 1224 x 2700 pixels

huawei p50

Pia simu inatumia mfumo endeshi wa HarmonyOS 2.0

Huawei P50 ni simu ambayo haipitishi maji kama ikidumbukia kwenye kina cha mita moja kwa muda wa nusu saa

Kwani ina viwango vya IP68

Utendaji wake ni mkubwa lakini simu inatumia mtandao wa 4G kwani haina 5G

Betri yake ina ukubwa wa 4100mAh na chaji yake inapeleka umeme wa wati 66

Bei ya Huawei P50

Bei ya Huawei P50 ni shilingi 1,678,320.00/=

Bado bei ni kubwa kwa nyakati za sasa zenye ushindani mkubwa

Zitazame, simu za sony na bei zake halafu linganisha na hizi za huawei

Utaona kuwa simu za sony bei zake ni nafuu.

Huawei P Smart

Hii ni simu ya kitambo kidogo kwani imetoka mwaka 2017

Ni simu ya daraja la chini kutokana na kutumika kwa chip ya Kirin 659

Utendaji wa Kirin 659 ni wa kiwango kidogo

Kutokana na simu kuwa kwenye kundi la mwisho tegemea vitu vingi kuwa kwenye ubora wa kawaida au wa chini

huawei p smart

Kwa mfano, kioo chake ni cha IPS LCD chenye resolution ya 1080 x 2160 pixels

Na memori zake ni aina ya eMMC 5.1

eMMC 5.1 huwa na kasi ndogo ya kusafirisha data ukilingansha na memori za UFS

Kamera zake haziwezi kutoa picha nzuri hasa kutokana na kutmua ulengaji wa kawaida yaani AF

Simu ina betri dogo ambalo linafanya simu kukaa na chaji masaa machache

Bei ya Huawei P Smart

Wakati simu imetoka bei yake ilikuwa ni shilingi 417,478.37/=

Lakini kwa sasa bei yake inaweza ikawa ni chini ya shilingi laki mbili

Hii ni simu ambayo ipo kundi moja na simu za itel

Huawei Nova 9 Pro

Simu ya Huawei Nova 9 Pro ni simu ya mwaka 2021 inayotumia mfumo endeshi wa HarmonyOS 2.0

Ni Huawei yenye kamera nne ambapo kamera moja ina ulengaji wa PDAF

Utendaji wa simu ni wa kuridhisha kwa sababu inatumia chip yenye nguvu ya Snapdragon 778G 4G

Kwa bahati mbaya hii chip haina 5G

Tembelea ukarasa huu unaofafanua, maana ya 5G na aina zake na umuhimu wake

huawei nova 9

Kioo chake kina uangavu na uonyeshaji wa rangi zipatazo bilioni moja

Kwa sababu simu inatumia kioo cha OLED

Betri yake ya ukubwa wa 4000mAh inawahi kujaa kwa 100% ndani ya dakika 20

Hii inatokana na chaji ya Huawei Nova Pro kuweza kupeleka umeme wa wati 100

Bei ya Huawei Nova 9 Pro

Bei ya Huawei Nova 9 pro ni shilingi 1,129,647.36/= za Tanzania

Ukilinganisha na huawei nyingi ambazo zimeorodheshwa hapa hii ni nafuu

Lakini bei hii inakupa simu kali ya Samsung kama Samsung s21 FE 5G

Maoni 5 kuhusu “Simu 10 Nzuri za Huawei na Bei Zake (2022)

  • Kiukwel sim zenu n nzur sn na hilo swala lenu la kutokuwa na google kwa baadhi ya sim munafikiriaje ili kuepukna na huwo mgogoro wenu kuhusiana na google ila jaribun kutengeneza na sim za bei rahisi zenye uwezo mnzur zaid ili muweze kupata wateja waaina zote wenye vipato vikubwa na wenye vipato vidogo

  • Nina simu ya Huawei nova 7i nahitaji kujua kama kwa bahati mbaya ikiibiwa munaweza kunisaidia kuipata kwani naipenda sana????

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

huawei mate60 pro

Huawei Mate 60 Pro Pigo kwa Marekani?

Kama ni mfuatiliaji wa habari za teknolojia utakuwa unafahamu vikwazo vya Marekani dhidi ya huawei Huawei kutoka china imekuwa na wakati mgumu wa kutumia teknolojia mbalimbali zenye mafungamano na marekani […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

oppo find x6 pro thumbnail

Oppo Yenye Kamera Nzuri na Ubora wa Picha

Kuna matoleo mengi ya simu za oppo zenye ubora tofauti tofauti Zipo ambazo zina ubora wa kati, wa juu na wa chini Katika hizo, nyingi zinajitahidi kuwa na kamera zinazotoa […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram