SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya Infinix Note 12 VIP na Sifa Zake Muhimu

Brand

Sihaba Mikole

June 11, 2022

Simu ya infinix note 12 vip ni simu ya android ambayo imetoka mwezi juni mwaka 2022

Ni ifinix ambayo inakuja na sifa nzuri hasa upande wa chaji, kioo na betri

Kitu kinachochangia bei ya infinix note 12 kuzidi laki nane kwenye maduka ya infinix

simu ya infinix note 12 vip

Fuatilia, vitu vinavyofanya simu kuwa bora na bei ya gharama

Simu hii ina ufanano wa kisifa na note 12

Fuatalia mgawanyiko wa bei upande wa memori na sifa zake zote ili ujue kama simu inastahili bei hiyo

Bei ya Infinix Note 12 VIP ya GB 256

Kwenye maduka ya infinix yaliyopo Dar Es Salaam simu inauzwa kwa shilingi 820,000/=

Bei inaweza kuwa kubwa lakini simu ina sifa zinazoweza wavutia wengi

Kikawaida simu nyingi za infinix huuzwa kwa bei rahisi

Lakini note 12 vip ni tofauti na bei yake itapata wakati mgumu kushindana na simu za redmi na oppo zinazopatikana kwa bei ya laki nane

Kwa sababu kuna baadhi ya sifa za VIP haziendani na bei

Sifa za Infinix Note 12 VIP

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Helio G96
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.05 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 12
  • XOS 10.5
Memori UFS 2.2, 256GB,128GB, na RAM 8GB, 4GB
Kamera Kamera tatu

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 13MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
Muundo Urefu-6.7inchi
Chaji na Betri
  • 4500mAh-Li-Po
  • Chaji-120W
Bei ya simu(TSH) 830,000/=

Upi ubora wa simu ya Infinix Note 12 VIP

Ubora mkubwa wa infinix note 12 vip ni uwezo wake wa kujaza betri kwa dakika CHACHE

Kwani simu inachukua chini ya dakika 20 betri kujaa kwa 100%

Lakini pia ni moja ya simu yenye display yenye uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Infinix Note 12 VIP summary

Note 12 VIP inakaa na chaji masaa mengi kwa sababu ya kuwa na betri kubwa

Utendaji wa simu pia ni wa kuridhisha japo si sana

Na pia ina kamera inayotoa picha vizuri

Uwezo wa Network

Infinix Note 12 VIP inasapoti mtandao wa 4G aina ya LTE Cat 13

Simu yenye LTE Cat 13 inaweza kudownload kwa spidi inayofika 390 Mbps

Ila hakuna laini ya simu yenye kasi kubwa ya namna hii hapa Tanzania

INFINIX NOTE 12 VIP network

Mtandao wenye 4G yenye kasi zaidi ni Halotel

Kwa maeneo ambayo nimewahi jaribu spidi yake inaenda mpaka 75Mbps

Uzuri Note 12 VIP ina masafa ya 4G yapatayo 13 yakiwemo yanayotumika hapa Tanzania

Ubora wa kioo cha infinix note 12 vip

Kioo cha infinix note 12 vip ni aina ya AMOLED

Kioo chake kina utajiri wa rangi zinazofikia bilioni moja

Hivyo simu inaweza kuonyesha vitu vingi kwa rangi zake halisi

Ubora wa kioo chake kuonyeza vitu vizuri unachangiwa pia na kuwa na resolution ya 1080 x 2400 pixels

Kioo chake ni chepesi wakati wa kutachi na kuscroll

Kwani kina refresh rate kubwa inayofikia 120 Hz

Hivyo ukiwa unaperuzi majina au sms simu itaonyesha orodha majina kwa haraka kila unapotachi

Nguvu ya processor MediaTek Helio G96

Infinix note 12 VIP inapewa nguvu ya kiutendaji na MediaTek Helio G96

Helio G96 ni processor ya simu yenye uwezo wa wastani.

Uwezo wake wa wastani unaifanya simu kuweza kucheza magemu mengi ya simu

Japokuwa gemu zinazohitaji nguvu kubwa kama Call of duty Mobile zinacheza kwa resolution za chini

INFINIX NOTE 12 VIP PROCESSOR

Nguvu yake ya wastani inasababishwa na Core kubwa kutumia muundo wa Cortex A76

Cortex A76 inazidiwa kiutendaji na Cortex A78 kwa asilimia kubwa

Ndio maana app ya GeekBench inaipa alama 542 wakati chip ya Dimensity 900 yenye muundo wa Cortex A78 ina alama 710

Kiuhalisia infinix wangeifanya simu kuwa nzuri zaidi kama wangetumia chip ya dimensity 900

INFINIX NOTE 12 VIP PROCESSOR

Core sita zina nguvu ndogo na zimetumia muundo wa Cortex A55

Huu ni muundo ambao huwa unatumia umeme kidogo

Mara nyingi hutmika pale ambapo simu ikiwa inafanya kazi nyepesi kama kupiga simu

Uwezo wa betri na chaji

Katika simu ambazo zinazowahi kujaa cha kwa haraka sana Infinix Note 12 VIP ipo

Ukiwa unachaji hii infinix basi simu inajaa ndani ya dakika 17 tu tena kwa 100%

Hii inatokana na chaji yake kupeleka umeme wa wati 120

Infinix Note 12 VIP thumbnail betri

Umeme huu unafanya betri ya simu yenye ukubwa wa 5000 mAh kujaa ndani ya dakika chache

Kutokana na betri kuwa kubwa, ukaaji wa chaji unachukua masaa yanayozidi 14 simu ikiwa kwenye intaneti masaa yote mfululizo

Ukubwa na aina ya memori

Kuna matoleo ya aina mbili ya hii simu

Kuna infinix note 12 vip ya GB 128 na ya GB 256

Huu ni ukubwa unaoweza kuhifadhi applikesheni na mafaili mengi

Lakini pia simu inatumia memori aina ya UFS 2.2

Memori za UFS husafirisha data kwa kasi kubwa kitu kinachoongezea simu utendaji

Tofauti na memori za eMMC ambazo husafirisha data kwa kasi ndogo

Simu ikiwa na ufs hufungua applikesheni kwa haraka bila kuchelewa

Uimara wa bodi ya infinix note 12 vip

Bodi ya infinix note 12 vip imetengenezwa kwa glassi upande wa nyuma

Na kwenye screen kumewekewa glassi ila sio za gorilla

Glassi hasa upande wa nyuma huepusha simu kuchunika rangi pindi inapotumika miaka mingi

INFINIX NOTE 12 VIP BODI

Ila sio kila aina ya glassi ni imara hasa kama sio gorill 5 kwenda mbele

Hivyo kuna haja ya kuongeza protector na kava ili kuipa simu ulinzi zaidi

Ubora wa kamera

Simu ina jumla ya kamera tatu

Hivyo ni infinix nyingine ya macho mamatu ya mwaka huu 2022 ikiwemo pia Infinix Hot 12

Simu ina kamera aina ya ultrawide ambayo hupiga eneo pana tu.

Na pia kamera kubwa ina megapixel 108 na ina ulengaji aina ya PDAF na Laser AF

INFINIX NOTE 12 VIP CAMERA

PDAF inasaidia kamera kulenga kitu kwa usahihi na kwa haraka hivyo picha inatokea ikiwa vizuri

Japokuwa hailngi kwa ustadi mkubwa kama teknolojia ya dual pixel pdaf

Na Laser AF hutumika kulenga vitu nyakati za usiku au kwenye mwanga hafifu

Upande wa video kamera zinarekodi za full hd na full hd plus pekee

Na kwa spidi ya 30fps na 60fps

Kwa bahati mbaya simu haina teknolojia ya OIS ambayo hutuliza kamera wakati wa kurekodi huku ukiwa unatembea

Ubora wa Software

Infinix note 12 Vip inakuja na toleo la android 12

Android 12 ina vitu vipya vingi ikiwemo kuonyesha app zinazotumia kamera kila ikufunguka

Hivyo inakuongezea usalama wa kuzitambua app zinazotumia kamera bila ruksa yako

INFINIX NOTE 12 VIP xos

Pia VIP inaambatana na software ya XOS 10.5

Baadhi ya mazuri ya XOS 10.5 ni kukupa uwezo wa kuongeza ukubwa wa RAM

RAM kubwa inaifanya simu kuweza kufungua apps nyingi kwa wakati mmoja bila kukwama kwama

Kitu kingine kilichopo kwenye mfumo XOS 10.5 ni uwezo wa kurudisha picha ambazo umezifuta

INFINIX NOTE 12 VIP xos 2

Kama ukifuta picha kwa kipindi cha siku 30 basi mfumo wa AI Gallery utaweza kuzirudisha hizo picha

Kwa mengi kuhusu XOS 10.5 tembele, vitu vinavyopatikana kwenye xos

Yapi Madhaifu ya infinix note 12 vip

Simu haina mtandao wa 5G

Japokuwa Tanzania haina 5G lakini waziri wa habari na mawasiliano alisema wameshaanza kupokea maombi ya kuweka 5G

Kwa hiyo kuna uwezekano 5G ikaanza kutumika miaka ya karibuni nchini

Pitia hapa kufahamu Uwanzishwaji wa mtandao wa 5G Tanzania

Si sawa kwa simu mpya ya laki nane kutokuwa na teknlojia mpya ya mawasiliano kwa mwaka 2022

Pia kamera zake hazina ois

Na simu inakosa ulinzi wa kuzuia maji kupenya

Aina hii ya ulinzi hujulikana kama IP

Neno la Mwisho

Bei ya infinix note 12 VIP inaipeleka simu kuingia kwenye ushindani mkali na simu za oppo a96 na Redmi Note 11 Pro 5G

Wakati ubora wa hizo simu mbili kwenye kila idara unaiacha kwa kiasi kikubwa ubora wa note 12 vip

Ila kwa mtu anayehitaji simu inayojaa haraka na inayokaa na chaji muda mrefu, note 12 vip inafaa sana

Wazo moja kuhusu “Bei ya Simu ya Infinix Note 12 VIP na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone feki 2

Simu Origino ni Zipi na Unazitambuaje? (Hatua za kufuata)

Matoleo ya simu yamekuwa yakitoka mara kwa mara yakiwemo yenye bei kubwa na zinazotamaniwa na watu wengi Aina hizi ya simu huvutia watu wasio waaminifu kutengeneza simu feki zenye ufanano […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram