SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Sifa za simu

Sihaba Mikole

November 9, 2023

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series

Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni

Haina tofauti sana na infinix note 30 pro na tofauti yenyewe ipo katika sehemu moja tu upande wa network

infinix note 30 vip showcase

Ila bei ya infinix note 30 VIP ni kubwa kiasi na inazidi laki tisa kwa hapa Tanzania

Ni muhimu kuitazama vipengele vyote vya hii infinix kujua kama inakidhi mahitaji yako

Bei ya Infinix Note 30 VIP ya GB 256

Kwa hapa Tanzania infinix note 30 vip yenye RAM GB 8 inauzwa kwa shilingi laki tisa na elfu arobaini (940,000) ikiwa mpya

Bei yake inachagizwa na ubora katika maeneo matatu ambayo ni kioo, memori zenye kasi na kamera na pia uwepo wa wireless chaji ya kasi

Infinix wametumia vioo vyenye ustadi mkubwa wa uonyeshaji vitu

Aina hii ya vioo huchangia gharama kubwa katika uundaji wa simu

Ndio maana hata kioo kikipasuka mtumiaji hulazimika kutoa kiasi kikubwa cha bei kurekebisha kioo cha simu

Sifa za Infinix Note 30 VIP

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Dimensity 8050
  • Core yenye nguvu kubwa(1) – 1×3.0 GHz Cortex-A78
  • Core Zenye Nguvu(3)-3×2.6 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G77 MC9
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
  • XOS 13
Memori UFS 3.1, 256GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera nne

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 2MP
  3. 2MP
Muundo Kimo-6.67inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-68W
Bei ya simu(TSH) 940,000/=

Ubora wa infinix note 30 vip kiujumla

Infinix hii ina kioo kizuri chenye uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Chaji yake inajaza betri kwa haraka na pia inakaaa muda mrefu na chaji

Inakuja na memori kubwa inayotosheleza kuhifadhi mafaili mengi kwenye simu

Utendaji wake ni wa kuridhisha kutokana na kutumika kwa processor yenye nguvu

Ni simu inayokuja na mtandao wenye kasi

Uwezo wa network

Infinix Note 30 VIP ni simu ya 5G inayosapoti pia 4G yenye kasi

Network yake ina masafa yote yanayotumiwa na mitandao ya simu hapa nchini

Kama ilivyo kwa iPhone 15 Pro Max, note 30 vip inakubali 5G za SA(Stand Alone) na NSA(Non Stand Alone)

Kwa maana utaweza kuitumia simu unapotembelea maeneo mengi duniani

Pia simu inatumia 4G aina ya LTE Cat 21 inayoweza kupakua faili kwa kasi inayofika 4700Mbps

Yaani kama unadownload labda sizoni(filamu) ya MB 1,175, filamu itamalizika kudownload ndani ya sekunde mbili

Ila kumbuka kwa hapa Tanzania hakuna mtandao unaotoa kasi hii, na hata ikiwepo gharama yake lazima iwe kubwa

Ubora wa kioo

Kioo cha infinix note 30 vip ni cha aina ya amoled chenye refresh rate inayofika 120Hz

Vioo vya amoled huwa ni vizuri katika uonyeshaji mzuri wa vitu kwani kina uwanda mpana wa rangi

Hivyo vitu vingi huonekana kwa usahihi mkubwa

Kitu kingine kinachoongeza ubora wa skrini ya hii simu ni kuwa na resolution kubwa

infinix note 30 vip display

Kwa bahati mbaya infinix hawajeka teknlojia ya HDR kwenye kioo

HDR huboresha zaidi muonekano wa vitu kwani huongeza kina cha rangi

Hutopata tabu ya kuona vitu vizuri pindi ukiwa unatumia simu kwenye jua

Kwani uangavu wa kioo unafika nits 900

Nguvu ya processor ya Mediatek Dimensity 8050

Chochote unachokifanya kwenye simu yako basi kinafanyiwa kazi na processor (chip)

Simu ikiwa na chip dhaifu basi jua kuwa simu uliyonayo ni mbaya na yenye uwezo mdogo

Mediatek dimensity 8050 ina nguvu ya kuweza kufanya vitu bila tatizo

infinix note 30 vip processor

Ndio chip ambayo inatumiwa na infinix note 30 vip

Kwenye app ya geekbench inayopima nguvu ya utendaji wa processor, mdeiateek dimensity 8050 ina alama 1100

Kwa chip za kundi la kati hii ni alama nyingi

Japo inaachwa karibu mara mbili na processor iliyopo kwenye samsung galaxy s23 ultra, ila nguvu yake inaweza kucheza magemu bila kukwamakwama

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya infinix note 30 vip ina ukubwa 5000mAh, kwa maana simu inaweza kudumu kwa masaa zaidi ya kumi ukiwa unaperuzi intaneti muda wote

Infinix wameendelea kuimarika katika matumizi ya teknolojia

Ukiwa na hii simu utaweza kuichaji bila kutumia waya wa chaji

Kwani simu inasapoti wireless chaji yenye kasi inayofika 50W, na chaji yake ya waya kasi yake 68W

infinix note 30 vip chaji

Kiwango hiki kinaweza kujaza betri kwa 50% ndani ya dakika 30

Ndani ya dakika 70 simu inaweza kujaa kwa 100%

Uwezekano wa kuichaji simu mara moja au mara mbili kwa siku upo,inategemea na matumizi yako

Ukubwa na aina ya memori

Infinix note 30 VIP zipo za aina mbili zinatofautiana kwenye ukubwa RAM

Ukubwa wa memori ni GB 256 ila unaweza kupata yenye ram ya GB 8 au GB 12

Hii simu inatumia memori za UFS 3.1, UFS 3.1 inasafirisha data kwa kasi

Ukiwa unakopi kitu utaona kazi inamalizika ndani ya muda mfupi

Uimara wa bodi ya Infinix note 30 vip

Bodi ya Infinix note 30 vip ina ulinzi wa kuzuia maji ya kiwango cha kunyunyulizika

Haina uwezo wa kuzuia maji pindi ikizama kwenye kina kikubwa mfano ndoo ya lita 20

Ustahimilivu wake upo kwenye kiwango cha maji tiririka kama mvua

Hii inatokana na simu kuwa na viwango IP53

Hata hivyo infinix wameendelea kuboresha uimara wa simu zao

Ila kwa bei yake walipaswa waweke walau IP67

Ubora wa kamera

Infinix note 30 vip ina jumla ya kamera tatu

Kamera kuu ina ukubwa wa megapixel 108, kamera zingine hazijaainishwa ni za aina gani

Hii simu haina kamera ya telephoto wala ultrawide

3-infinix note 30 vip camera

Kwa kuzitazama vitu vinavyozingatiwa kwenye simu zenye kamera nzuri za bei kubwa, utaona kuwa kuna vitu infinix inavikosa

Ubora wa picha nyakati za mchana ni nzuri kwani kamera inakusanya data kwa kiwango kizuri na vitu vinaonekana kwa uzuri

Upande wa selfie kamera ubora si mzuri sana kwani mng’ao unaopoteza muonekano halisi wa mtu

Hii simu inaweza kurekodi video za 4k kwa kiwango cha 30fps

Ubora wa software

Hii simu inatumia android 13 na XOS 13

Kwa sasa android wameachia toleo jipya la Android 14

infinix note 30 vip software

Hakuna taarifa kama hii simu itapata toleo jipya

Hata hivyo hakuna tofauti kubwa kati ya android 13 na android 14

Washindani wa Infinix note 30 VIP

Bei ya infinix note 30 vip inaipeleka simu kwenye ushindani na baadhi ya simu za sasmung

Samsung hizo ni Samsung Galaxy A54 na Samsung Galaxy A34

Bei ya Galaxy A54 inaendana na hii infinix

Ila sasa Samsung A54 inaizidi infinix kwenye kila kitu isipokuwa upande wa chaji pekee

Infinix wanahitaji nguvu kubwa kupromoti hii simu kutokana na aina ya bei

Neno la mwisho

Katika orodha ya simu mpya na nzuri za infinix hii ni moja wapo

Kikubwa ni kwamba utahitajika kuwa na kiwango cha kutosha kuimiliki

Kama bajeti ni ndogo basi huna budi kutafuta matoleo mengine yenye unafuu

Maoni 2 kuhusu “Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix mpya thumbnail

Simu za Infinix zinazotamba na bei zake (2024)

Mwishoni mwa mwaka 2023 na mwanzoni mwa 2024 kuna matoleo mapya ya infinix yalitoka Matoleo hayo mengi ni ya daraja la kati na la chini yaani yamegusa kila mtu kulingana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya Infinix Hot 40 Pro na Ubora wake

Simu ya Infinix Hot 40 Pro ni simu janja ya daraja la kati ambayo imetoka pamoja na simu ya infinix hot 40 Hot 40 Pro ina ubora wa ziada kwenye […]

infinix hot 40

Bei ya Infinix Hot 40 na Sifa Zake Muhimu

Kuelekea mwishoni mwa mwaka 2023 infinix walitoa toleo jingine la simu aina ya Infinix Hot 40 Hili ni baada ya toleo la infinix hot 30 ambvalo limetoka mwaka 2023 pia […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram