SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

September 23, 2023

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023

Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji

Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana na matoleo ya mwaka uliopita

-iphone 15 pro showcase modified

Na pia hakuna mabadiliko makubwa sana ya kuweza kuruka kutoka iphone 14 pro mpaka kwenye hii iphone mpya

Ndio maana hata bei ya iphone 15 pro ina ufanano na matoleo yaliyopita

Iangazie kwenye kila nyanja ujue vitu vipya ambavyo vimekuja na hii simu.

Bei ya iPhone 15 Pro ya GB 256 Tanzania

Bei halisi ya iPhone 15 Pro yenye ukubwa wa GB 256 ni shilingi 2,800,000(milioni mbili na laki nane)

Kwa Tanzania bei yake inaweza kufika milioni tatu kutokana na gharama zingine

Maboresho makubwa yaliyopo kwenye iphone mpya ni kwenye uchezaji wa gemu na utendaji kiujumla

Pia kwa mara ya kwanza apple wamelazimika kuweka muundo wa chaji wa USB Type C ambazo hutumika sana kwenye simu za android

Hii ilitokana na mapendekezo yaliyotolewa na umoja wa ulaya kuzitaka kampuni za utengenezaji wa simu kuwa na muundo mmoja wa chaji usiolazimisha watumiaji kununua chaji za aina tofauti.

Sifa za iPhone 15 Pro

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A17 Pro
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×3.78GHz
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.1GHz
  • GPU-Apple GPU (6-core graphics)
Display(Kioo)  LTPO Super Retina XDR OLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • iOS 17
Memori NMVe,, 256GB,128GB, 1TB na RAM 8GB
Kamera Kamera TATU

  1. 48MP,PDAF(wide)
  2. 12MP(telephoto)
  3. 12MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.1inchi
Chaji na Betri
  • 3274mAh-Li-Ion
  • Chaji-
Bei ya simu(TSH) 2,800,000/=

Upi ubora wa iPhone 15 Pro

Simu inakuja na processor mpya na yenye nguvu ukilinganisha processor zilizotumika kwenye simu zilizopo sokoni kwa sasa

Chaji zinazotumika kwenye simu za android zinaweza kuichaji hii simu bila shida na kwa spidi kubwa

Kioo chake kina refresh rate kubwa na uwezo wa kuonyesha vitu kwa muonekano mzuri

Hii ni simu ngumu ambayo haitumii vioo kama ilivyo matoelo ya awali

iPhone za mwaka 2023 zinatumia RAM kubwa tofauti na miaka iliyopita ambapo RAM ya simu zimekuwa ni ndogo yaani GB 6.

Ni simu ngumu hata ikiingia kwenye maji

Ni simu inayosapoti eSIM ambapo kwa Tanzania mitandao ya Vodacom na Airtel wanayo hii huduma

Kufahamu eSIM, ufafanuzi huu hapa: Maana ya eSIM kwa lugha nyepesi

Kuna mengi kwenye hii simu kama utakavyoona mbeleni

Uwezo wa Network

iPhone 15 Pro ni simu ya 5G na inasapoti aina zingine za network

Inaweza kutumia aina zote za 5G ikiwemo ya mmWave

5G ya mmWave ndio yenye kasi kubwa zaidi kwanza ambayo inapatikana sana marekani

Kwa bahati mbaya yenyewe inahitaji minara mingi ili imfikie mtumiaji

Kwa sababu masafa yake hayaendi umbali mfreu kama ilivyo 5G nyingine

Kwa hapa Tanzania mitandao yenye b5G ni Airtel, Vodacom na Tigo

Na zote zinatumia masafa ya kati na mafupi

Ubora wa kioo cha iPhone 15 Pro

Kioo cha iPhone 15 Pro ni cha aina ya LTPO OLED, apple wenyewe wanakiita LTPO Super Retina XDR OLED

LTPO kirefu chake ni Low Temperature Crystalline Oxide kazi yake kubwa ni kudhibiti kiwango cha refresh rate

Kioo cha iphone 15 pro kina refresh rate ya 120Hz

Kama kioo kikiwa kinaonyesha vitu muda wote kwa kiwango cha refresh rate kubwa hata kwenye hali ambayo haihitaji refresh rate kubwa basi betri itawahi kuisha

Uwepo wa LTPO unasaidia kutumika kwa refreshbrate kubwa kwenye nyakati inapohitajika

Pia kioo chake kina kiwango kikubwa cha reslution ambayo ni 1179 x 2556 pixels

Uzuri ni kuwa simu ina teknolojia ya dolby vision na hdr10, vitu vinavyoongeza kina cha rangi kwenye kioo

Hivyo vitu vingi vinaweza kuonekana kwa rangi zake halisi bila kupoteza ubora wake

Nguvu ya processor Apple A17 Pro

Simu inatumia processormpya ya Apple A17 Pro ambayo imegawanyika katika sehemu sita

Sehemu mbili za mwanzo inahusisha core zenye utendaji mkubwa

Mara hufanya kazi pale simu inapokuwa inatumia app zinazohitaji nguvu kubwa mfano magemu

Na sehemu ya pili inahusisha core zenye nguvu ndogo ama wastani ambazo zipo nne

Hizi hutumika wakati simu inafungua apps zinazohitaji nguvu ndogo ama ya kawaida mfano kutuma meseji ama kupiga simu au kuangalia video za instagram

Mtindo huu unaongeza ufanisi wa matumizi mazuri ya betri

App ya kupima nguvu za processor inayoitwa Geekbench inaonyesha kuwa Apple A17 Pro ina alama zipatazo 2500

Hii inaashiria apple a17 pro ndio chip ya simu yenye nguvu zaidi kuliko zingine kwa sasa

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya iPhone 15 Pro kwenye makaratsi ni ndogo

Ila kwa jinsi apple wanavyounda simu zao ukaaji wa chaji huwa ni wa masaa mengi

Hata  hivyo iPhone 15 Pro ukaaji wa chaji sio mkubwa ukilinganisha na toleo la iPhone 15 Plus

Tuchukulie data kutoka kwenye tovuti ya tomsguide, ambapo iphone 15 pro imeweza kukaa na chaji kwa masaa 11 kwenye majaribio mbalimbali ikiwemo intaneti

iphone 15 pro chaji

Sio kiwango kikubwa kama ilivyo kwa iPhone 15 Pro Max ambayo chaji yake inaenda mpaka masaa 13

Simu pia inasapoti wireless chaji, kasi yake sio kubwa kama simu ya Infinix Note 30 Premier inayopeleka umeme wa wati 50W

Wakati iphone 15 pro inapeleka umeme wa chaji wa wati 15 kama kiwango cha juu.

Ukubwa na aina ya memori

Simu inakuja na aina NNE za upande wa kubwa wa memori huku zote zikiwa na RAM ya GB 8

Kuna iPhone 15 Pro ya GB 128, 256, 512 na 1TB

Aina ya memori simu inayotumia ni NVMe ambayo usafirishaji wake wa data ni mkubwa

Yaani kama unakopi kitu kutoka kwenye kompyuta ya mac kwenda kwenye simu utaona faili linamalizika kukopi kwa haraka

Uimara wa bodi ya iPhone 15 Pro

Kitu kikubwa ambacho apple wamekinadi sana ni madini mapya yaliyotumika kuundia bodi

Madini hayo hutwa titanium, inasemwa kuwa madini haya huwa ni magumu

Tukipata undani wa uimara kwenye hii simu tutakutaarifu

iphone 15 pro body

Kama ilivyo kwa matoleo ya iphone ya zamani, hii pia haipitishi maji kwani ina viwango vya IP68

Kama simu ikizama kwenye cha mita 6 kwa muda wa nusu saa simu haitoathiriwa na maji

Ubora wa kamera

Hii simu ina kamera zipatazo tatu yaani macho matatu

Kuna kamera moja kwa ajili ya kupiga eneo pana hufahamika kama Ultrawide

Na nyingine kwa ajili ya kupiga kitu ambacho kipo mbali kamera hii huitwa telephoto

Kuna maboresho upande wa kamera ya telephoto, apple wameongeza kiwango cha kuweza kuzoom

Simu hii inaweza kuzoom mpaka mara tano bila kupoteza ubora wa picha

iphone 15 pro kamera

Bado ni kiwango cha chini ukifananisha na simu ya Samsung Galaxy S23 Ultra

Ubora wa picha hauna tofauti na iPhone 14 Pro japokuwa kuna mifumo imeboreshwa ya kuchakata ubora wa picha

Tutajadili ubora wa picha wa hii simu kiundani katika makala zingine

Ubora wa Software

Unaijua NameDrop, muundo wa kushea namba kati ya simu mbili kwa kugusisha sehemu ya juu

Huu ni muundo ambao umekuja kwenye iOS 17

Sio kitu kigeni kwenye simu za Android japo Google waliachana na hiki kitu

Sina uhakika kama itakuwa na mafanikio kwenye iphone

Kiujumla iPhone 15 Pro inatumia mfumo endeshi wa iOS 17

iOS 17 umeweka kwa kiasi kikubwa teknolojia ya Artificial Intelligence(AI) kwa maana isiyo rasmi Akili bandia

Washindani wa iPhone 15 Pro

Washindani wakubwa wa iphone 15 Pro kwanza ni iPhone 14 Pro

Kama ilivyoelezwa awali kuna tofauti ndogo sana kiasi cha kwamba mtumiaji wa kawaida anaweza asione kipya

Kwa sasa iPhone 14 Pro inaenda kuuzwa kwa bei ya chini ya toleo jipya

Mshindani mwingine ni Samsung Galaxy S23+

Japokuwa iphone ina nguvu zaidi kiutendaji lakini kwenye uhalisia hakuna tofauti ya wazi kiutendaji kati ya hizi simu mbili

Samsung inakuja na betri kubwa na kamera nzuri zaidi naweza kusema

Neno la Mwisho

Kwa mtu mwenye simu ya iPhone 14 Plus akinunua iPhone 15 Pro ataona utofauti kubwa

Ila kwa mtu ambaye ana iPhone 14 Pro Max anaweza asione tofauti kubwa

Mwitikio wa matoleo ya iPhone 15 haujawa mkubwa kama miaka iliyopita

Hata hivyo hii ni simu kali na nzuri kwa mwenye bajeti inayotosheleza

Wazo moja kuhusu “Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A25 na Sifa zake

Simu ya Samsung Galaxy A25 ilitoka rasmi mnamo mwezi desemba 2023 Ni simu ya daraja ambayo bei yake kwa Tanzania ni shilingi laki saba (700,000/=), hii ikiwa ni bei ya […]

samsung galaxy a15 thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

samsung a55 showcase

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram