SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Simu Mpya

Sihaba Mikole

September 3, 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple

Tukio hili litarushwa moja kwa moja kupitia youtube

iphone 15 muonekano

Kwa wafuatiliaji watakuwa wanafahamu kuwa apple mpya mpaka sasa ni matoleo ya iPhone 14

iPhone 14 yalitoka mwaka 2023

Hivyo basi mwaka 2023 kutakuwa kuna uzinduzi toleo jipya kabisa la iphone

Bidhaa zitakazoingia sokoni

Kwenye uzunduzi, kampuni ya apple itatangaza matoleo ya manne ya iphone, saa janja na pia tetesi zinasema kutakuwa na uzinduzi wa ipods.

Kwa hapa tutaangazia simu tu zitakazoingia sokoni

iPhone 15

iPhone 15 ndio simu ambayo itakuwa na bei ya chini zaidi kati ya simu zingine nne

Bei tarajiwa ya iphone 15 ni zaidi ya milioni mbili

Ni simu ambayo kimo chake itakuwa na urefu inchi zisizozidi 6.1

Ukubwa wa memori wa iphone 15 unatarajiwa kuanza 128GB hadi kiwango cha 512GB

Kwenye ram simu hii itakuwa na ukubwa wa RAM ya GB 6

iPhone 15 itatumia chip iliyotumika kwenye iPhone 14 ambayo ni Apple A16 Bionic

Kwenye kamera ya mbele kuna dynamic island

iPhone 15 Plus

Urefu wa iPhone 15 Plus unatarajiwa kuwa ni inchi 6.7

Na yenyewe RAM itakuwa na ukubwa wa GB 6

Ukubwa wa memori unaanzia GB 128 hadi GB 512

Inakadiriwa kuwa bei ya iphone 15 plus ya GB 512 itakuwa ni shilingi milioni mbili na laki nne

Pia simu itatumia processor ya mwaka 2022 ya Apple A16 Bioni

Apple hawajaweka processor mpya kwenye simu za iphone 15 na iphone 15 plus

iPhone 15 Pro

iPhone 14 Pro bei yake inatarajiwa kuanza kwa kiasi cha shilingi 2,800,000 kwa bei ya dunia

Kwa hapa Tanzania bei inaweza kuwa kubwa zaidi ya hiyo

Kwenye memori simu inatarajiwa kuanza na ukubwa wa gb 128 hadi ukubwa wa 2TB

Zinatoa nafasi kubwa ya kuhifadhi vitu vingi bila kuwaza kuwa simu inaweza kujaa haraka

Ukubwa wa RAM pia unatarajiwa kuwa ni GB 6

iPhone 14 Pro itatumia processor mpya yenye nguvu zaidi ya Apple A17 Bionic

iPhone 15 Pro Max

Hili ndio litakuwa toleo la gharama zaidi na lenye betri kubwa

Kwa maana ndio itakuwa na uwezo wa kukaa na chaji muda mrefu kuliko matoleo mengine

Ukubwa wa memori wa iPhone 15 Pro Max unaanzia GB 128 hadi TB 2

Ram na yenyewe itakuwa ni GB 6

Simu itatumia processor yenye nguvu kubwa ya Apple A17 Bionic

Kwa wapenda simu zenye nguvu zisizo kwama kwama hata kwa mazingira gani iphone 15 pro max ndio inafaa

Kisanga kinaanza kwenye bei

Bei ya iphone 15 pro max inatarajiwa kuanzia shilingi milioni 3.3

Bei kubwa inatokana na sifa kubwa simu inatarajiwa kuwa nazo

Vitu Vipya vinavyotarajiwa

Kwa mara ya kwanza simu za iPhone zinatarajiwa kutumia waya wa kuchaji aina ya USB Type C

USB Type C ni zile waya zenye vichwa vipana

Apple kwa miaka mingi wamekuwa wakitumia aina tofauti kabisa ya chaji

Chaji zao iphone zinatambulika kama Lightning Port

Kutokana na sheria za Umoja wa ulaya kuzitaka kampuni za simu ziwe na muundo mmoja wa chaji, apple inaonekana watafuata mapendekezo ya hiyo sheria

iphone 15 chaji

Kitu kingine kipya ni kuwekwa kwa fremu za Titanium upande wa pembeni

Matoleo yaliyopita fremu ilikuwa ni stainless steel(chuma)

Titanium huwa ni ngumu hivyo uimara wa simu utakuwa mkubwa

Kitu kingine ni kuwa hizi simu zinatarajiwa kutumia kioo cha LIPO Display

Faida ya hii kioo ni kuwa inawezesha kioo kuchukua sehemu kubwa ya skrini na matumizi ya umeme ni madogo

Hitimisho

Kuna mabadiliko yapo ila sio makubwa ya kutofautisha na matoleo ya iPhone 14 Pro

Na pia apple inaungana na simu nyingi za android kwenye matumizi ya USB Type C

Unahitaji kuwa na bajeti ya kutosheleza kumiliki toleo lolote la iphone mpya

Maoni 2 kuhusu “Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

google pixel 8 appearance

Google Pixel 8, Simu ya Teknolojia ya Akili Bandia (AI)

Google Pixel 8 na Pro zinatarajiwa kuzinduliwa rasmi mwezi wa kumi tarehe nne Matoleo mapya ya pixel yatatumia toleo la android 14 Android 14 ilitangazwa tangu mwezi wa pili lakini […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram