SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

September 28, 2023

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao

Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G

Hii ni simu kali kwenye idara nyingi

infinix zero 30 5g showcase

Kwa jicho haraka unaweza ukahisi haina tofauti na iPhone 15 Pro (natania)

Vitu vingi vya maana inafanya bei ya infinix zero 30 5g kuwa zaidi ya milioni moja kwa Tanzania

Baadhi ya watu wataanza kujiuliza kwa nini ununue infinix kwa zaidi ya milioni

Ukitazama sifa zake utaacha kujiuliza swali la aina hii.

Bei ya Infinix Zero 30 5G ya GB 256

Bei ya infinix zero 30 inatarajiwa kuwa ni shilingi 1,060,000/=(milioni moja na themanini)

Hii ni bei ya pre order kwa hapa Tanzania

Kwa nchi za nje hasa india bei ya hii simu inaenda shilingi 800,000 kwenye mtandao wa amazon india

Ukijumlisha na gharama zingine bei yake inaweza isifike milioni ukiagiza kutoka India

Ila kuna changamoto zake kuagiza simu kutoka nje

Hii bei kwa kiasi kikubwa inashabiana na ubora na sifa zake kiujumla

Sifa za Infinix Zero 30 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Dimensity 8020
  • Core Zenye nguvu(4) – 4×2.6GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G77 MC9
Display(Kioo) AMOLED, Refresh rate:144Hz
Softawre
  • Android 13
  • XOS 13
Memori UFS 3.1, 256GB na RAM 8GB,12GB
Kamera Kamera Tatu

  1. 108MP,PDAF(wide)
  2. 13MP(ultrawide)
  3. 2MP
Muundo Urefu-6.78inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-68W
Bei ya simu(TSH) 1,060,000/=

Upi ubora wa Infinix Zero 30 5G

Kuna maeneo mengi ambayo yenye ubora mkubwa katika hii infinix

Ila upande wa utendaji, kamera, chaji, na kioo yana uimara mkubwa wa kushindana na matoleo ya simu toka kwenye kampuni nyingine

Kioo cha infinix zero 30 kimeundwa kuwa na uwezo wa kuonyesha rangi nyingi

Uwezo wa kuonyesha rangi nyingi inasaidia kioo kuonyesha kitu kwa ranfi zake halisi kwa kiwango kikubwa

Infinix hii ina nguvu ya utendaji kubwa sababu ya kutumia processor yenye nguvu

Chaji yake inawahi kujaza betri kwa dakika chache

Na ukaaji wake wa chaji ni wa kiwango cha kuridhisha

Utafahamu mengine kadri utakavyofuatilia taarifa zote zilizopo kwenye hii post

Uwezo wa Network

Infinix Zero 30 5G inaweza kutumia aina zote za network pamoja na 5G

Inaonekana ni simu inayolenga kutumika maeneo mengi duniani

Hii inatokana na aina ya 5G inayosapoti

Inasapoti karibu aina zote za 5G ikiwemo SA(yaani Standalone)

SA ni aina ya 5G inayotumia miundo mbinu mipya iliyouniwa kwa ajili ya 5G bila kutegemea miundombinu ya zamani

5G ya NSA(Non Stand Alone) inasafirisha mawimbi yake kutumia mifumo ya 4G

NSA imesambaa na inatumika kwenye nchi nyingi ikiwemo hapa Tanzania kwenye mitandao ya Vodacom, Tigo na Airtel

Hata hivyo 5G bado inapatikana maeneo machache hapa nchini hasa jijini Dar Es Salaam

Ubora wa kioo cha Infinix Zero 30 5G

Simu inatumia kioo cha AMOLED kinachosapoti refresh rate 144Hz

Hii refresh rate kwa mpenda magemu inafanya gemu kuonekana vizuri na kwa ustadi hasa gemu kama za magari

Pia kiwango hiki hufanya simu kuwa nyororo unapoperuzi kitu kama kusoma vitabu, kutafuta meseji, kuangalia majina nk

Changamoto ni kuwa sio kila kwenye simu inahitaji refresh rate kubwa

Kama muda wote utakuwa unatumia refresh rate kubwa basi betri itawahi kuisha kwa haraka

infinix zero 30 5g display

Kwenye infinix kuna chaguo la kubadirisha na kuiweka ndogo mpaka 60Hz

Pamoja na uzuri wa kioo kitu kimoja kinachokesekana ni teknoljia ya HDR10

HDR10 huboresha muonekano wa kitu kwa kuongeza kina cha rangi kwenye skrini

HDR10 hujaribu kuonyesha kitu kwa rangi halisi kama kinavyoonekana kwenye uharisia wake

Hata hivyo hii simu kioo chake bado ni kizuri ukizingatia resolution yake ni kubwa ambayo ni 1080 x 2400 pixels

Nguvu ya processor Mediatek Dimensity 8020

Meditek dimensity 8020 ni processor ya simu ambayo imeingia sokoni mwaka 2023

Kila kitu unachofanya kwenye infinix zero 30 5g kinawezeshwa na processor ya dimensity 8020

Chip hii imegawanyika katika sehemu mbili kama ilivyo kawaida ya processor nyingi za simu

Sehemu yenye nguvu kubwa kuna idadi ya core zipatazo 4, na kwenye nguvu ndogo kuna core zipatazo 4

Kwenye swala la nguvu kiutendaji, dimensity 8020 imashajaribiwa kwenye simu ya Motorola Edge 40

Katika app ya geekbench app ina alama 1124 kwenye core moja

Alama ni nyingi japo inazidia zaidi ya mara mbili na processor ya Apple A17 Pro iliyotumika kwenye matoleo ya iPhone 15 Pro

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya infinix zero 30 5g ina uwezo wa kupeleka umeme wa wati 68 kwenye betri

Ndani ya dakika 51 chaji inajaza betri kutoka 0% hadi 100%

Kwa nyakati hizi za umeme kukatika mara kwa mara chaji ya haraka inafaa zaidi

Betri yake inaweza kuchukua mpaka masaa 13 simu kuisha chaji ukiwa unatumia intaneti muda wote

Kwa mantiki hii kama unatumia sana intaneti utalazimika kuichaji simu mara mbili kwa siku

Waya wake wa chaji ni USB Type C 2 (waya wenye kichwa kipana)

Ndio chaji nyingi siku hizi zinatumia tundu la aina hii

Ukubwa na aina ya memori

Kuna infinix zero 30 5g za aina mbili zenye ukubwa sawa wa memori na RAM zikiwa tofauti

Kuna yenye RAM ya GB 8 na nyingine ina GB 12

Zote zina ukubwa wa GB 256

Mfumo wake wa memori ni UFS 3.1

UFS 3.1 inaweza kusairisha data kwa kasi inayofika 2400 kwenye njia moja

Hii inachochea vitu vingine kufanyika kwa haraka na kwa muda mchache mfano kukopi vitu kwenda kwenye simu

Uimara wa bodi ya Infinix Zero 30 5G

Hii ni moja ya simu chache za infinix zenye kioo cha Gorilla 5

Gorilla 5 ni kioo stahimilivu kwani kinaweza kuepuka kupasuka kama ikianguka urefu wa mita mbili

Hivi vioo hulinda skrini kiasi cha kwamba unaweza usione umuhimu wa skrini protekta

Pia hii simu ina uwezo wa kuzuia maji kwa kiwango kidogo kama ilivyo kwa Tecno Camon 20

Kwani ina viwango vya IP53, uwezo wa kuzuia maji haupo sawa na Samsung Galaxy S23 Ultra

Ubora wa kamera

Infinix Zero 30 5G ina jumla ya kamera tatu

Kamera yake kubwa inatumia teknolojia ya ulengaji ya PDAF

PDAF inazidiwa na dual pixel pdaf kwenye utambuzi wa kinachopigwa picha kwa haraka

Ubora wa picha nyakati za mchana ni wa kuvutia kwa kiwango kikubwa

infinix zero 30 5g camera

Uhalisia wa rangi katika kamera kwa kiasi kikubwa unaakisi jinsi kitu kinavyoonekana kwenye mazingira yake

Ila kuna hali ya kuzidisha rangi hasa unapotumia HDR

Hii kamera inaweza kurekodi mpaka video za 4K

Ubora wa Software

Infinix Zero 30 5G inakuja na Android 13 na XOS 13

XOS 13 ina mpangilio mzuri wa battan na app kitu kinachomsaidia mtumiaji kutumia simu kwa uwepesi

XOS inakuja na app zingine ambazo unaweza usizihitaji na huwezi kuzitoa kiurahisi

Infinix wameiunganisha hii na mfumo wa akili bandia unaoitwa ChatGPT

ChatGPT ni akili bandia unayoweza kuuliza kitu chochote na ikakujibu

Uzuri ni kuwa inasapoti maswali ama mjadala kwa njia ya sauti

Washindani wa Infinix Zero 30 5G

Sokoni, infinix itabidi ionyeshe umwamba mbele ya Samsung Galaxy 34, iPhone 15 na hata matoleo ya Redmi na Oppo

Bei ya infinix zero 30 5g inaendana na hizo simu tajwa na kama kuna tofauti ni ndogo

Kwa bahati mbaya ama nzuri nyingi ya hizo zina vitu vingine vya ziada

Kwa maana ni rahisi kwa mtu anaefuatilia kununua simu toka kampuni nyingine

Hitimisho

Pamoja na uboreshaji wa matoleo ya Infinix kadri muda unavyoenda, bado kuna vitu vinapaswa kuboreshwa zaidi

Isingekuwa mbaya kama infinix hii ingeboreshwa uwezo wake wa kuzuia maji na kuwa na viwango vya IP68 badala ya IP53

Na hata kamera dual pixel na laser AF hizi ni teknolojia nzuri zaidi ya PDAF kwa sasa

Wazo moja kuhusu “Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix mpya thumbnail

Simu za Infinix zinazotamba na bei zake (2024)

Mwishoni mwa mwaka 2023 na mwanzoni mwa 2024 kuna matoleo mapya ya infinix yalitoka Matoleo hayo mengi ni ya daraja la kati na la chini yaani yamegusa kila mtu kulingana […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

No Featured Image

Bei ya Infinix Hot 40 Pro na Ubora wake

Simu ya Infinix Hot 40 Pro ni simu janja ya daraja la kati ambayo imetoka pamoja na simu ya infinix hot 40 Hot 40 Pro ina ubora wa ziada kwenye […]

infinix hot 40

Bei ya Infinix Hot 40 na Sifa Zake Muhimu

Kuelekea mwishoni mwa mwaka 2023 infinix walitoa toleo jingine la simu aina ya Infinix Hot 40 Hili ni baada ya toleo la infinix hot 30 ambvalo limetoka mwaka 2023 pia […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram