SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Uimara wa Tecno Camon 20 Kuzuia Maji (Waterproof)

Miongozo

Sihaba Mikole

September 24, 2023

Kama umefuatilia sifa na bei ya Tecno Camon 20, utaona kuwa ina viwango vya IP53

IP53 ni nini hasa?

Kwanza neno IP kirefu chake ni Ingress Protection

Inaasharia kiwango cha uimara wa simu kuzuia maji na vumbi kuingia ndani ya kifaa cha umeme mfano simu

IP53 ni kiwango kinachoashiria uimara wa simu kuzuia maji ya kiwango kunyunyuruzika

Sio kiwango kinachomaanisha uwezo simu kuhimili kutopitisha maji kama ikizama kwenye ndoo ya lita ishirini

Hivyo Tecno Camon 20 inaweza kuzuia maji kwa kiwango fulani na kwa muda mchache kama inavyoonekana kwenye hii video

Je Camon 20 haipitishi maji ikizama kwenye swimming pool

Tegmemea simu kufa iwapo itadumbukia katika maji ya kiwango hiko

Achilia mbali kuzama kwenye swimming pool, simu inaweza kuathirika kwa haraka hata ikizama kwenye jagi

Jinsi tecno camon 20 ilivyoundwa imeleka kuwa imara kwenye maji yenye kasi ndogo

Kwa maana hata kama ukiwa unatumia kwenye mvua kubwa sana itakulazimu kuwa makini vile vile

IP53 inalenga kuzuia vumbi na maji yenye kasi ndogo kwa kingeleza wanasema splash resistant

Kiwango cha maji simu inaweza kuhimiri ni maji ya levo isiyozidi sentimita mbili ndani ya muda mfupi na kwenye eneo dogo

Ukizidisha hapo maisha ya simu yatakuwa mashakani

Hivyo unapokuwa unafanya kwenye mazingira yenye maji ni muhimu kuwa mwangarifu.

Kwani hii simu haina uwezo wa iPhone 15 Pro inayoweza kuzuia maji kwa muda wa nusu saa kwenye kina cha mita sita(6).

Muda wa kuhimiri kutopitisha maji

Kama ilivyotanguliwa kuelezwa hapo awali, camon 20 ikiingia kwenye maji haiwezi kustahamili kwa muda wa nusu saa

Unapaswa uwahi simu ndani ya dakika mbili

Hali ni tofauti na simu za madaraja ya juu mabazo zimetetengenezwa kuhimili kutopitisha maji kwa dakika nyingi tena kwenye eneo kubwa

Kwa mfano Samsung Galaxy S23+ ikizama kwenye maji mengi ya kina cha mita 1.5 maji hayatoingia na unaweza itumia simu hata ndani ya maji

Ndio maana bei ya samsung galaxy s23+ ni kubwa zaidi kuliko camon 20

Kitu ambacho hutokuwa na wasiwasi nacho kuhusu camon 20 ni nyakati za mvua za rasha rasha

Unaweza kutoa simu yako na kisha ukawa unaangalia mambo mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii au kutazama video youtube

Na bado simu inaweza isiathiriwe na maji

Ila mvua ikiwa kubwa hapo ndipo unapopaswa kuilinda simu kwa kutoitumia kwenye hiyo mvua

Cha kufanya pindi camon 20 ikiingia majini

Kitu cha kwanza ifute simu maji kutumia kitambaa kisafi

Zingatia muda ambao simu imekuwapo ndani ya maji

Kwa sababu kwa kiasi fulani tecno camon 20 ni himilivu kwenye kina kidogo

Jaribu kuona kama simu inafanya kazi

Anza kujaribu tachi, kuchaji, sehemu ya earphone, tazama sehemu ya laini kama haina maji

Ukiona kila kitu kipo sawa basi simu inaweza kutumika vizuri

Iwapo simu imezama kwenye kina kikubwa na ukagundua haifanyi kwenye vitu vingi

Basi simu inapaswa ifunguliwe na vizuri ukamuona mtaalamu ya simu kuharibika kila kitu

Je Camon 20 haipitishi maji kabisa?

Simu ya tecno camon 20 haiwezi kuwekwa kwenye kundi la simu zisizopitisha maji

Kiwango cha IP53 ni kiwango kidogo

Hivyo ni upotoshaji kuita simu kuwa inaweza kuzuia maji

Kikawaida simu zisizopitsha maji zinaweza kuhimili dakika nyingi na kwenye mazingira tofauti

Camon 20 inaweza kuingiza maji kama ikizama katika kina cha mita 1, tena hata dakika moja inaweza isichukue

Hii inamaanisha nini?

Kuna kiwango cha maji Camon 20 inaweza kuzuia na kingine inashindwa kabisa

Kwa mara nyingine, umakini ni muhimu.

Simu zingine zisizopitisha maji

Simujanja nyingi za daraja la juu hutengenezwa kuwa na uwezo wa waterproof

Mifano michache wa smartphone za aina hiyo ni matoleo mengi ya iphone na samsung matoleo ya S-series

Mfano wa simu hizo ni iphone 14, iphone 14 Pro, iPhone 14 Pro Max, Samsung Galaxy S23, Samsung Galaxy S23+, Samsung Galaxy S23 Ultra, Google 7 Pro, Google Pixel 6 Pro na nyinginezo nyingi

Utofauti ni kuwa hizi simu chache nilizotaja  zenyewe zina viwango vya IP68

Hiki ni kiwango kikubwa kinachoashiria uwezo wa simu kutopitisha maji hata ikizamisha kwenye kina cha kuanzia mita 1.5 kwa muda wa nusu saa

Kwa mtu ambaye kazi zake ni za shambani kwenye umwagiliaji aina hii ya simu inamfaa zaidi

Changamoto kubwa ya simu zisizopitisha maji kabisa ni bei kubwa

Hapa ndipo matoleo ya Tecno Camon 20 yanapokuwa kimbilio kwa kuwa na uwezo wa kiasi kidogo cha kuzuia maji

Utajuaje uwezo wa simu kuzuia maji

Mara nyingi kampuni husika huanisha aina ya IP(Ingress Protection) iliyonayo

Na njia nyepesi kutambua ni kusoma sifa mbalimbali za simu husika

Kwani vitu huwekwa wazi

Na kwa kujihakikishia unaweza kutazama video mbalimbali za majaribio za simu husika

Kama simu haina kiwango chochote cha IP huwa haisemwi

Hitimisho

Kwa watu wenye bajeti ya wastani na wanahitaji simujanja isiyopitisha maji Camon 20 inaweza kuwa chagua zuri

Ila bahati mbaya simu haiwezi kustahimili kupitisha kwenye kina kikubwa, mvua kubwa na kwa muda mrefu

Hii simu inahimili maji ya kiwango kidogo sana tena kwa muda mfupi

Haipo sawa na matoleo ya simu za mbaya ambazo hutengenezwa kwa uimara mkubwa

Ila hizo simu ni kwa ajili ya watu wenye pesa ya kutosheleza ambazo watanzania hawawezi kumudu

Mbali na camon pia kuna matoleo ya OPPO na Redmi yenye IP53.

Wazo moja kuhusu “Uimara wa Tecno Camon 20 Kuzuia Maji (Waterproof)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 30 thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 na Sifa Zake Muhimu

Kwenye wiki ya nne ya mwezi wa tano 2023 infinix waliingiza sokoni toleo jipya la simu Toelo hilo ni Infinix Note 30 Ni toleo la daraja la kati hivyo kuna […]

No Featured Image

Bei ya Tecno Camon 20 na Sifa Zake Muhimu

Tecno Camon 20 ni simu ya mwaka 2023 ambayo imeingia sokoni mnamo mwezi Mei Kiubora ni simu inayoweza kuwekwa kwenye kundi la kati hivyo bei yake sio sawa na matoleo […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram