SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G na Sifa zake muhimu

Sifa za simu

Sihaba Mikole

May 10, 2024

Kwenye matoleo bora ya simu kutoka Tecno, matoleo ya Tecno Camon huja na ubora katika vipengele vingi

Hata bei za matoleo ya Camon huzizidi bei za Tecno Spark na Tecno Pop

Na hivyo jua kuwa bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G GB 512 kwa hapa Tanzania ni shilingi 995,000/= (laki tisa na elfu tisini na tano)

tecno camon 30 premier showcase

Ubora mkubwa wa Camon 30 Premier unapatikana kwenye nyanja za

  • Kamera
  • Utendaji wa processor
  • Kioo(skrini)
  • Kasi ya chaji

Na pia sifa zingine za hii simu zina ubora mzuri kama inavyoonekana kwenye jedwari

Sifa za Tecno Camon 30 Premier 5G

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Mediatek Dimensity 8200 Ultimate
  • Core Zenye nguvu sana(1) – 1×3.1 GHz Cortex-A78
  • Core zenye nguvu(3)-3×3.0 GHz Cortex-A78
  • Core Za kawaida(4) – 4×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G610 MC6
Display(Kioo) LTPO AMOLED, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 14
  • HiOS 14
Memori 512 GB na RAM 12GB
Kamera Kamera TATU

  1. 50MP,PDAF(wide)
  2. 50MP(periscope telephoto)
  3. 50MP(ultrawide)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-70W
Bei ya simu(TSH) 995,000/=

Uwezo wa network

Tecno Camon 30 Premier ni simu inayosapti mtandao wa 5G

Haisapoti eSIM kama ilivyo baadhi ya simu za daraja la kati zilizotoka miaka ya karibuni

Haishangazi sana kwa sababu mwitikio wa matumizi ya eSIM kwa Tanzania na Afrika kiujumla sio mkubwa

Camon 30 premier inaweza kutumia 5G za Stand Alone(SA) na Non Stand Alone(NSA)

tecno camon 30 premier network

Ila kwa hapa Tanzania miundombinu inayotumiwa na mitandao ya simu ni NSA

Aina ya 4G simu inayokuja nayo ni LTE Cat 21 yenye kasi ya kupakua faili inayofika Gbps 4.1

Kama mtandao unasapoti Cat 21 utakuwa unapakuwa mafaili kwa sekunde chache

Ni ngumu kwa Tanzania upande wa 4G

Ubora wa kioo cha Tecno Camon 30 Premier

Kioo cha Tecno Camon 30 Premier 5G ni cha aina ya LTPO Amoled

Kioo chake kina resolution ya 1264 x 2780 pixels

Kwa maana kinaonyesha picha zikiwa mkorezo mzuri wa rangi zenye kuonekana kwa ustadi

Vioo vya Amoled huwa na utajiri wa rangi na huonyesha rangi zenye uhalisia

tecno camon premier display

Kwa mfano, kioo cha amoled huonyesha rangi nyeusi halisi kabisa

Mbali na hayo kioo cha hii simu kina refresh rate ya 120Hz

Refresh rate huchakata fremu nyingi kwa muda mfupi

Hivyo simu inakuwa nyepesi na muonekano mzuri pindi unapo-scroll(kutachi simu kwa kuipeleka juu  au chini)

Lakini refresh rate kubwa hula umeme mwingi hivyo kuna njia vioo vya siku hizi hutumia kupunguza refresh pindi ikiwa hahiitajiki

Na hapo ndipo teknolojia LTPO(Low-Temperature Polycrystalline Oxide) inapokuja kudhibiti refresh rate

Nguvu ya processor Mediatek Dimensity 8200 Ultimate

Tecno Camon 30 Premier inatumia processor ya dimensity 8200 ultimate kufanya kazi zake

Dimensity imegawanyika katika sehemu tatu ila sehemu yenye nguvu sana inatumia muundo wa Cortex A78

Cortex A78 inaweza kufanya mizunguko mpaka GHz 3(mizunguko bilioni 3 kwa sekunde), na kila mzunguko mmoja unachakata kazi nne

tecno camon 30 premier processor

Ndio maana katika test za app ya geekbench, hii processor inaweza kufungua peji 108 kwa sekunde

Tofauti na processor ya Helio G99 inayofungua peji 50 kwa sekunde, na kwa apple a17 bionic ni 160 kwa sekunde

Kiujumla premier 30 inaweza fanya vitu vingi bila kukwama kwama ikiwemo upande wa magemu

Uwezo wa betri na chaji

Simu inatumia betri ya ukubwa wa 5000mAh

Inakaa na chaji masaa 13 kwenye matumizi tofauti tofauti

Ukiwa unacheza gemu muda wote simu inachukua takribani masaa 8 mpaka betri kuisha

Upande wa kasi ya chaji ni kuwa chaji yake inapeleka umeme mwingi unaofika wati 70

tecno camon 30 premier chaji

Kiasi hiki cha umeme kinaijaza betri kwa dakika 40 toka asilimia sifuri hadi mia

Kiujumla uwezo wa utunzaji chaji ni mkubwa kiasi cha kukaa masaa mengi kwa matumizi ya kawaida

Na nyakati hizi za umeme kukatika mara kwa mara hutohitaji kusubiri masaa matatu simu ijae

Ukubwa na aina ya memori

Kuna toleo la aina moja tu la Camon 30 Premiere upande wa memori

Na toleo hilo ukubwa wake ni GB 512

Hii ni nafasi kubwa inayochukua mafaili mengi na app za kutosha

Labda ndio maana Tecno na wenyewe wameamua kuondoa sehemu ya kuweka memori kadi

Mtindo wa kuondoa memori kadi uliasisiwa na iPhone, na wengine wakafuata

Aina ya memori ya simu ni UFS 3.1

Kwa maana kama unakopi kitu kwenda kwenye simu kitamalizila kwa muda mfupi

Uimara wa bodi ya Tecno Camon 30 Premier

Kama nilivyotangulia kueleza, simu za Camon ni matoleo bora ya Tecno

Bodi ya hii simu nyuma imewekewa aluminiam na sio plastiki

Pia ni simu yenye viwango vya IP54, ikimaanisha ina uwezo maji ya kiwango cha manyunyu(kuchuruzika)

Ila haiwezi zuia maji kama ikizama kwenye kina kikubwa

tecno camon premier bodi

Kioo chake kina skrini protekta ya Corning Gorilla Glass 5

Gorilla Glass 5 husifika kwa ugumu wa kutopasuka kirahisi kwenye kimo cha mita mbili

Hata hivyo kuwa na skrini protekta nyingine ni muhimu

Ubora wa kamera

Kama unataka Tecno macho matatu basi hii ni moja wapo

Ina kamera aina za ultrawide, wide na telephoto

Hapa nitazungumzia kamera moja tu ya wide(zingine kwenye mada inayojitegemea ya kamera)

Kamera ya kuu(wide) ina megapixel na upigaji wa picha ni mzuri kwenye mwanga na mwanga mdogo

tecno camon premier 30

Kwa nyakati za mchana hakuna kiwango kikubwa cha noise kinachoweza kuonekana kwa uwazi

Muonekano wa rangi unaendana na muonekanao wa vitu kwenye mazingira halisi

Hii inachagizwa na ukubwa wa lenzi pia aina ya processor(ISP) ya simu

Ubora wa Software

Camon 30 premier inatumia Android 14 na HIOS 14

Siku hizi simu zimezidi kuongeza matumizi ya AI(Artificial Intelligence) ama akili mnemba kwa kiswahili

HIOS 14 na yenyewe imefuata mwendo huo hasa kwenye kamera

Kwani imewekwa mfumo wa kuitakasa picha ikiwa haijatokea vizuri

Pia AI yake inamuwezesha mtumiaji kuondoa vitu asivyovitaka kwenye picha

Washindani wa Tecno Camon 30 Premier

Hii ni simu ya daraja la kati hivyo basi ipo kwenye kundi lenye washindani wengi

Kwa mwaka huu wa 2024 kuna matoleo ya Samsung Galaxy A55 na Samsung Galaxy A35, Oppo Reno 11 Pro na bila kusahau Xioami 13T

Bei ya Samsung Galaxy A55, Oppo Reno 11 Pro na Xiaomi 13T hazitofautiani sana na Camon 30 Premier

Ila Samsung Galaxy A55 ndio tishio kwa Tecno zaidi kutokana na aina ya bei

washindani

Galaxy A55 bei yake ni milioni moja na laki moja na inazidi premier kwenye maeneo ya kioo(skrini), uimara, ubora wa software na upokeaji wa maboresho ya android kwa miaka minne

Haitoshi pia Samsung A55 ina eSIM

Hivyo kuna vitu vinaweza mshawishi mteja kuchagua samsung kuliko Camon 30 Premier

Neno la Mwisho

Kwa sifa za hii simu kwenye vipengele vingi, inatosha kusema kwamba bei ya Tecno Camon 30 Premier inaendana na ubora wake

Kwa wale ambao wanapendelea tecno zenye kamera nzuri hili ni chaguo zuri

Kikubwa Tecno inabidi waongeze baadhi ya vitu vinavyopatikana kwenye matoleo mengine ya daraja la kati ili kuhimili ushindani

Maoni 10 kuhusu “Bei ya Tecno Camon 30 Premier 5G na Sifa zake muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

display

[VIDEO]: Simu za tecno zenye kamera nzuri zaidi

Tazama ubora wa picha zilizopigwa na simu za Tecno Camon 30, Camon 30 Premier, camon 20 premier na nyininezo

tecno camon premier 30

Ubora wa simu za Tecno Camon 30 na bei zake(Pro, Premier)

Tangu mwezi wa nne kampuni ya walitoa matoleo ya Tecno Camon 30 Matoleo ya Camon 30 yapo matatu ambayo ni ya daraja la kati yaani mid range Ubora wa kiujumla […]

tecno camon 30 thumb

Bei ya Tecno Camon 30 Pro na Sifa Muhimu

Simu ya Tecno Camon 30 Pro ilitangazwa mwezi februari ila imetoka rasmi mwezi wa nne 2024 Ni simu ya daraja la kati(midrange) hivyo bei yake sio sawa na Tecno matoleo […]

Bei ya Tecno Spark 20 Pro+ na Sifa zake

Simu ya Tecno Spark 20 Pro+ ilitoka rasmi desemba ya mwaka 2023 ila kwa Tanzania imeanza kupatikana miezi ya karibuni Kwa Tanzania bei ya juu kabisa ya Tecno Spark 20 […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani
TUFUATE
Youtube Facebook Instagram twitter

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company