SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Infinix Note 30 na Sifa Zake Muhimu

Simu Mpya

Sihaba Mikole

June 8, 2023

Kwenye wiki ya nne ya mwezi wa tano 2023 infinix waliingiza sokoni toleo jipya la simu

Toelo hilo ni Infinix Note 30

Ni toleo la daraja la kati hivyo kuna ubora kwenye maeneo ya kamera, chaji, kioo na hata muonekano wa simu

infinix note 30 showcase

Kitu kinachofanya bei ya infinix note 30 kuzidi laki tano

Sifa zake nyingi ni za wastani kiasi cha kwamba haiwezi kuwa kwenye kundi moja na Tecno Camon 20 Premier

Fuatilia kila kuifahamu note 30 kiundani

Bei ya Infinix Note 30 ya GB 256

Infinix yenye ukubwa wa GB 256 utaipata kwa kiasi cha shilingi 600,000/=

Memori ya simu ni kubwa sio rahisi kupata simu yenye ukubwa huu kwa kiwango hiko

Kwa maana hayo kuna baadhi ya vitu ni lazima viwe na ubora wa kawaida kama utakavyoona

Kwa maana hata simu shindani zenye bei chini ya laki sita huwa na memori za GB 128 na 64

Hata kama bei yake ni kubwa infinix wanakupa pia chaguo la GB 128

Sifa za Infinix Note 30

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G99
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.2 GHz Cortex-A76
  • Core Za kawaida(6) – 6×2.0 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G57 MC2
Display(Kioo) IPS LCD, Refresh rate:120Hz
Softawre
  • Android 13
  • XOS 13
Memori UFS 2.2, 256GB,128GB na RAM 8GB
Kamera Kamera nne

  1. 64MP,PDAF(wide)
  2. 2MP(depth)
  3. QVGA
Muundo Urefu-6.78inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-45W
Bei ya simu(TSH) 600,000/=

Upi ubora wa Infinix Note 30

Simu inakuja na skrini yenye resolution kubwa tofauti na simu za bei nafuu zinazotumia vioo vya ips lcd

Utendaji wa simu ni wa kiwango cha kuridhisha kutokana na aina ya chip iliyotumika

Inatumia mfumo mpya kabisa wa android kitu kinachokupa uhakika wa matumizi ya miaka mingi

Betri yake ni kubwa na chaji yake ina kasi kubwa ya kujaza simu kwa muda mfupi

Kioo chake kina refresh rate kubwa inachangia uwepesi na ulaini wakati wa kutachi

Inakuja na memori kubwa na yenye kasi

Kamera inatoa picha nzuri kama utakavyoona baadae

Uwezo wa network

Infinix Note 30 inasapoti mpaka mtandao wa 4G kama kiwango cha juu

Aina ya 4G inayotumika na simu ni LTE Cat 13

Kama hufahamu kasi ya juu ya kupakua mafaili kwenye LTE Cat 13 ni 650Mbps ambayo ni sawa 81MBps

Hii inamaanisha kama unapakuwa gemu la Dream Soccer 2023 ambalo lina ukubwa wa MB 560 basi simu italidownload kwa sekunde 70 sawa na dakika 1 na sekunde 10

Kwa Tanzania mitandao mingi kasi ya 4G huwa ipo kati ya 20Mbps mpaka 75Mbps

Kwa maana sio rahisi kuipata kasi ya 650Mbps hapa nchini

Kuhusu masafa, simu ina masafa yote yatumikayo ni mitandao ya simu nchini

Kuna baadhi ya simu huwa yanakosa masafa yote ya 4G mfano mzuri ni baadhi ya vishikwambi walivyopewa walimu vinakosa masafa ya 4G ya halotel

Ubora wa kioo cha Infinix Note 30

Kioo cha infinix note 30 ni aina ya ips lcd chenye refresh rate inayofika120Hz

Mbali na kutumika kwa aina hii ya kioo ila ina resolution kubwa ya 1080 x 2460 pixels

Refresh rate ya 120Hz huleta uwepo na ulaini kwenye simu unapokuwa unaperuzi au kucheza gemu

infinix note 30 display

Kwa mfano ukiwa una-scroll kuangalia picha mbalimbali kwenye simu yako utaona simu ni nyepesi na inabadirika kwa uzuri

Kutokana na resolution kuwa kubwa muonekano wa vitu pia ni mzuri kwenye hii infinix

Inapokuja kwenye uangavu simu inafika mpaka nits 600

Hii inamaanisha kioo kitaonyesha vizuri pale unapokuwa unaitumia juani

Kikawaida kwenye jua kali skrini huonekana kwa shida kama kiwango cha uangavu wa simu ni kidogo

Nguvu ya processor Mediatek Helio G99

MediaTek Helio G99 ndio chip inayotumika na infinix note 30 kufanya kazi zake

Ni processor ya daraja la kati hivyo utendaji wake ni wa wastani

Imegawanyika katika sehemu mbili huku sehemu yenye nguvu zaidi ikitumia muundo wa Cortex A76 katika core zote mbili

Utendaji wa Cortex A76 ni wa kuridhisha na matumizi madogo ya umeme japo si sawa kama ilivyo kwa Cortex A78

Kwenye app ya kupima nguvu za processor ya geekbench inaipa hii simu alama 555

Kwa maana kiuwezo inaendana na simu ya Redmi Note 10 ya 2021

Kwa kifupi ni kuwa ina uwezo wa kufungua vitu kwa wakati mmoja na pia kucheza gemu kubwa bila shida ya kukwama kwama

Japo kwa baadhi ya gemu utalazimika kupunguza ubora wa “graphics”(muonekano wa picha)

Kwa sababu kwenye kama PUBG Mobile kwenye resolution kubwa inachezeka kwa kiwango cha 30fps (ni ndogo)

Ila kwenye resolution ndogo inazidi 40fps

Uwezo wa betri na chaji

Chaji ya Infinix Note 30 ina kasi ya wati 45 kwa ajili ya kujaza betri yake ya 5000mAh

Chaji yake inajaza betri kwa dakika 57 kutoka 0% mpaka 100%

Ukaaji wa chaji kutoka kwenye betri unadumu takribani masaa 14 ukiwa unaperuzi intaneti muda wote

infinix note 30 chaji

Ni masaa mengi ambayo yanakupa uhuru wa kutumia simu muda mrefu bila kuwa na mashaka ya chaji kuwahi kuisha

Kwa kasi ya kujaa kwa simu inaamanisha kwa siku unaweza kuichaji mara mbili tu na ukawa unatumia intaneti au kucheza gemu muda wote

Ikizingatia muda wa kucha ni dakika 57, hivyo utachaji masaa mawili kwa siku na kutumia kwa masaa 28

Ukubwa na aina ya memori

Kwenye memori kuna matoleo ya aina mbili

Kuna yenye ukubwa wa GB 128 na nyingine ya GB 256 zote zina memori ya GB 8 ambayo inaweza kuongezwa

Aina ya memori inayotumika ni UFS 2.2 ambayo huwa ina kazi kubwa ya kusafirisha data

Kasi ya UFS 2.2 inafika 1200MBps kwa njia moja wakati ufs huwa ina njia mbili

Hii inaongeza ufanisi kwenye utendaji wa simu na kufanya simu kufungua apps kwa haraka

Uimara wa bodi ya Infinix Note 30

Kimuonekano wa nyuma simu inafanana na iphone 14

Kiasi unachoweza kudhani ina glasi lakini si hivyo

Infinix note 30 ina bodi ya grassi mbele na nyuma na kwa pembeni ndio ina plastiki

Uzuri wa bodi za glasi inazuia michubuko ya rangi kwa kipindi cha muda mrefu

Hivyo ule muonekano wa simu haupotezi ubora kwa kipindi cha miaka mingi

Haijaainishwa kama simu inaweza kuzuia maji ya kuchuruzika kupenya ndani kwani haina viwango vya IP.

Uwezo wa Kamera

Infinix Note 30 unaweza kuita infinix macho matatu

Kwa maana ina jumla ya kamera zinapatazo tatu

infinix note 30 camera

Ila kiuharisia kuna kamera moja kwa sababu kamera iliyoandikwa depth haipigi picha

Bali huwa inapima umbali wa kitu kinacholengwa kupigwa picha

Inatumika zaidi kupiga picha zinazotenganisha upande wa nyuma wa kitu kinachopigwa

Kiujumla ubora wa picha ni mzuri sana japo kuna kukolea kwa rangi kitu kinachopunguza muonekano halisi wa kitu

infinix note 30 photo quality

Ila kwa watu wa instagram na mitandao ya kijamii itawafaa maana hutohitaji filter

Ina uwezo wa kurekodi video za full hd pekee

Ubora wa Software

Simu inatumia toleo la Android 13 na mfumo wa XOS 13

Kwenye XOS 13 kuna vitu vingi vinavyoambatana na simu

Moja ya utakachokutana nacho ni app ya XARENA inayokupa uwezo wa kuzuia shughuli zingine wakati unacheza gemu

infinix note 30 software

Mara nyingi unaweza ukakuta notification zinatokea au simu zinapigwa wakati akili yako ipo kwenye gemu

Basi xarena inakupa uwezo wa kuzuia hilo

Na pia simu inakuja na voice assistant inaitwa Forax Voice Assistance ambayo inaweza kusoma kwa sauti vitu kama sms nk

Washindani wa Infinix Note 30

Washindani wa Infinix Note 30 wapo wa aina mbili

Kuna ushindani kutokana na bei na pia ushindani kutoka kwenye simu zinazoendana sifa

Moja ya mshindani wake ni Samsung Galaxy A24 4G

Simu ya Galaxy A24 4G ina kamera ya kupiga eneo pana na inatumia kioo kizuri zaidi cha super amoled

Bei ya galaxy a24 4g ya gb 128 ni shilingi 480,000/=

Na mshindani mwingine ni Poco M5 na pia simu ya Vivo V27e, hizi zote bei zake ni pungufu ya infinix

Neno la Mwisho

Kwa muhitaji wa simu nzuri za infinix daraja la kati infinix note 30 ni chaguo sahihi

Bei yake inaendana kwa kiasi kikubwa na ubora wa simu ukizingatia inakuja na memori kubwa

Na sio tu ujazo wa memori ila inakupa memori yenye kasi kubwa kusafirisha data

Pia sio mbaya ukatizama simu zinazoendana kisifa ujue vitu vya ziada vilivyopo kwa washindani wengine

Maoni 23 kuhusu “Bei ya Infinix Note 30 na Sifa Zake Muhimu

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

infinix note 30 vip thumbnail

Bei ya Infinix Note 30 VIP na Sifa Zake

Infinix kwa mwaka 2023 wameachia matoleo mengi yakiwemo ya note series Moja ya toleo hilo ni Infinix Note 30 VIP ambayo imetoka mwezi Juni Haina tofauti sana na infinix note […]

infinix zero 30 5g thumbnail

Ubora na Bei ya Infinix Zero 30 5G (Infinix Kali)

Ni infinix kwa mara nyingine inajaribu kutengeneza hisia chanya juu ya ubora wa simu zao Unaweza kuliona hili kwa toleo jipya la Infinix Zero 30 5G Hii ni simu kali […]

TECNO CAMON 20 WATERPROOF

Uimara wa Tecno Camon 20 Kuzuia Maji (Waterproof)

Kama umefuatilia sifa na bei ya Tecno Camon 20, utaona kuwa ina viwango vya IP53 IP53 ni nini hasa? Kwanza neno IP kirefu chake ni Ingress Protection Inaasharia kiwango cha […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram