SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Bei ya Simu ya iPhone 11 Pro Max na Sifa Zake (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

June 21, 2022

Simu ya iPhone 11 Pro Max ni simu ya iphone ya daraja la juu ambayo imetoka 2019

Ubora uliotumika kuiunda hii simu inafanya bei ya iphone 11 pro max kuzidi milioni 1.3 mpaka sasa 2022

Japokuwa ni moja ya simu bora ya mwaka 2019 ila kuna simu chache zinazoweza kuizidi iphone 11

muonekano wa apple iphone 11 pro max

Ila inaweza kuzidiwa na simu nyingi za sony mpya

Kwa kulinganisha bei yake na sifa zake itakupa sababu kwa nini bado gharama yake ni kubwa hata yenye memori ndogo

Bei ya iPhone 11 Pro Max ya GB 64

Bei ya iPhone 11 Pro Max ambayo ukubwa wake ni GB 64 na RAM yake ni GB 4 ni shilingi 1,500,000/= hapa Tanzania

Ila hii bei ni kubwa sana

Kwa sababu mtandao wa amazon wanauza iphone 11 pro max kwa shilingi 1,300,000/=

Kwa kutazama matoleo ya Pro Max ya 2020 na 2021, hii ya 2019 ina bei ndogo

Unafuu huo wa bei unaendana kwa kiasi kikubwa na sifa zake ambazo zimeambatanishwa kwenye jedwari chini

Sifa za simu ya iPhone 11 Pro Max

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A13 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.65 GHz Lightning
  • Core Za kawaida(4) – 4×1.8 GHz Thunder
  • GPU-Apple GPU
Display(Kioo) Super Retina XDR OLED,
Softawre
  • iOS 13
  • Inakubali iOS 15 na iOS 16
Memori  NVMe, 256GB,128GB,64GB,512GB na RAM 4GB
Kamera Kamera tatu (iphone macho matatu)

  1. 12MP, dual pixel PDAF(wide)
  2. 12MP(ultrawide)
  3. 12MP , PDAF (Telephoto)
Muundo Urefu-6.5inchi
Chaji na Betri
  • 3969mAh-Li-Po
  • Chaji-20W
Bei ya simu(TSH) 1,500,000/=

Ni Upi ubora wa iPhone 11 Pro Max?

iPhone 11 Pro Max ina utendaji wenye nguvu kutokana na kutumia chip yenye uwezo wa kuchakata vitu vingi kwa urahisi

Ina screen inayoonyesha vitu kwa rangi zinazoendana kwa uhalisia kwa kiwango kikubwa

Kamera zake zinatoa picha nzuri nyakati zote (iwe usiku au mchana)

iphone 11 pro max summary

Ina mfumo wa memori ambao una kasi kubwa ya kusafirisha data

Simu inaweza kupokea matoleo mapya ya mfumo endeshi wa iOS

Ukifuatilia uwezo wa simu kuanzia network mpaka software utaona kuwa ni simu yenye mapungufu machache kwa kulinganisha na simu mpya zilizotoka 2020 hadi 2022

Uwezo wa Network

Mtandao wenye kasi kubwa zaidi kwenye hii simu ni 4G kwa sababu haina 5G

Aina ya 4G simu inayotumia ni LTE Cat 18

Kama mtandao wa simu una kasi inayoendana na LTE Cat 18 basi simu inaweza kudownload faili la ukubwa wa 1500MB kwa sekunde kumi

iphone 11 pro max network

Lakini kwa Tanzania hakuna laini ya simu ambayo inatoa kasi ya 1200Mbps

Mitandao yote ya simu nchini inakubali intaneti ya LTE

Kwani simu ina masafa karibu ya kila nchi upande 3G na 4G

Ubora wa kioo cha iPhone 11 Pro Max

Kioo cha iPhone 11 Pro Max ni cha aina ya Super Retina XDR OLED

Super Retina XDR ni neno la kimasoko la apple lakini kiujumla ni kioo cha OLED kama tu vioo vilivyotumika kwenye baadhi ya simu za huawei

Kama ilivyo ada, oled huonyesha rangi nyeusi kama inavyoonekana na jicho la binadamu

Vioo vya oled huwa vina contrast kubwa kitu kinachoipa screen uwezo wa kuonyesha rangi nyingi za aina tofauti tofauti

Ustadi wa kioo chake unachangiwa na simu kuwa na HDR10

HDR10 hufanya screen ionyeshe vitu kwa namna jicho la binadamu linavyoona kwenye mazingira halisi

Kuelewa kiundani ufanyaji kazi wa hdr pitia: maana ya hdr kiundani

Nguvu ya processor Apple A13 Bionic

Kwa miaka mingi kampuni ya apple imekuwa ikitengeneza processor za simu zenye nguvu kubwa kiutendaji kuliko kampuni yoyote

Hii imekuwa ikiifanya kuwa moja ya kampuni bora duniani za simu

Tazama: orodha ya kampuni bora zinazotengeneza simu

Kwa kuzingatia data za app ya geekbench inayopima ubora wa processor Apple A13 Bionic ina alama 1319 kwenye core moja

apple a13 bionic

Ndio maana hii chip inaweza kucheza gemu linalohitaji nguvu la PUBG Mobile kwa resolution kubwa na kwa kasi 57fps

Kikawaida processor ikiwa na nguvu huwa inatumia umeme mwingi

Kitu kinachopelekea betri kuwahi kuisha

Lakini matumizi ya umeme kwenye apple a13 bionic ni madogo ukilinganisha na chip iliyotumika kwenye iPhone XR

Kwa mujibu wa apple, kuna ongezeko la utendaji kwa 20% kwenye core mbili zenye nguvu

Na pia core zinazotumia umeme mdogo zimepunguza matumizi ya umeme kwa 40% ikilinganishwa na Apple A12 Bionic

Uwezo wa betri na chaji

Kwa kutazama kwa macho betri ya iphone 11 pro max ni dogo

Kwani lina ukubwa wa 3969mAh

Lakini namba zisikudanganye kwani hii ni moja ya iphone inayokaa na chaji masaa mengi hata kwenye intaneti

Kwa mujibu wa GSMArena, iPhone 11 Pro Max inaweza kukaa na chaji masaa 102 simu ikiwa inatumika mara chache.

Ikiwa inaperuzi intaneti masaa mengi mfululizo, inaweza chukua masaa 15 mpaka chaji kuisha

Ni masaa ambayo simu kama ya Redmi Note 10 hayafikii ikiwa inaperuzi intaneti

Wakati simu ya Redmi ina betri kubwa la 5000mAh

Upande wa chaji kasi yake ni ya wastani

Kwani chaji yake inapeleka umeme wa wati 20

Ukubwa na aina ya memori

Memori za simu ya apple ni tofauti na zile kwenye simu za android

Apple hutumia memori aina ya NVMe wakati android hutumia eMMC, au UFS

NVMe huwa unausafirishaji mkubwa wa data zaidi ukilinganisha na aina zingine

Usafirishaji mkubwa wa data huifanya simu kuwa nyepesi na app kufunguka kwa haraka

Kiujumla kuna iphone 11 pro max za matoleo matatu upande wa memori

Ukiwa na bajeti ndogo utapata yenye GB 64

Ila kama bajeti ni kubwa unaweza ukapata ya GB 256 au GB 512

Uimara wa bodi ya iPhone 11 Pro Max

Mara nyingi bodi ya simu za apple huwa ni ngumu kuvunjika ama kuchunika

Hii inatokana na simu kutengenezwa na kioo cha gorilla upande wa mbele na nyuma

Na pia kuwekewa chuma upande wa pembeni

iPhone huwa zinakuja na viwango vya IP68

iphone 11 pro max bodi

IP68 inaonyesha uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi

Kama simu ikidumbukia kwenye maji ya kina cha mita 4 kwa muda wa nusu saa maji hayatopenya

Tazama hii video inayoonyesha maji yakishindwa kuingia ndani ya hii simu

Kiujumla hii ni simu ambayo haihitaji kava wala screen protector ya ziada

Ni simu chache sana za android ambazo za daraja la kati zinazoweza zuia maji ya kiwango cha mita 4

Hata simu mpya ya bei kubwa ya Xiaomi 12 Pro haina IP68

Ubora wa kamera

Hii ni iphone ya macho matatu yenye kamera aina ya telephoto, ultrawide na wide

Hivyo simu inaweza kupiga eneo pana sana la nyuzi 120

Uwepo wa kamera ultrawide unaiwezesha simu kuzoom kitu cha mbali kwa kutumia lenzi ambazo ubora wa picha haupotei

Ubora wa kamera ya hii simu unaongezwa na kutumika kwa ulengaji aina ya dual pixel autofocus

iphone 11 pro max camera

dual pixel pdaf hulenga na kutambua eneo linalopaswa kupigwa picha kwa haraka

Kamera ya iPhone 11 pro max inarekodi mpaka video za 4K  kwa kasi inayofika 60fps

Uzuri ni kuwa kamera ya telephoto na wide zina OIS

OIS hutuliza mitikisiko kwenye video wakati wa kurekodi

Ubora wa Software

Simu inatumia mfumo endeshi wa iOS 13

iOS ufanyaji kazi wake hauendani na Android

japokuwa iOS uko “optimized” kitu kinaachofanya simu kuwa nyepesi

iphone 11 pro max software

Lakini ule uhuru unaopatikana kwenye android haupo kwenye mfumo endeshi wa apple

Hivi karibuni apple imezindua toleo jipya la iOS 16

iPhone 11 Pro Max ni moja ya simu itakayopata mfumo endeshi mpya kabisa

Yapi Madhaifu ya iPhone 11 Pro Max

Kasoro kubwa ni simu kutokuwa na mtandao wa 5G

Lakini pia simu haina sehemu ya kuweka memori kadi

Kama utanunua simu ya GB 64 ikiwahi kujaa unakuwa hauna mbadala zaidi ya kupunguza mafaili kama unataka kuweka faili jipya

Pia simu haina redio wala sehemu ya kuweka earphone

Neno la Mwisho

Kiujumla bei ya iphone 11 pro max sio kubwa kwa kutazama ubora wa simu kwa nyanja nyingi

Ila ukinunua hii simu Tanzania tarajia bei kuwa kubwa kuliko uhalisia

Kama utaipata chini ya shilingi milioni na laki mbili ni jambo zuri

Vinginevyo ni bora kutazama simu mbadala kama iphone se 2022

 

Maoni 6 kuhusu “Bei ya Simu ya iPhone 11 Pro Max na Sifa Zake (2022)

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram