SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sifa za simu mpya ya Apple iPhone SE (2022)

Sifa za simu

Sihaba Mikole

April 4, 2022

Simu ya apple iphone se(2022) ni simu ndogo yenye kamera moja upande wa nyuma.

Simu mpya ya Apple iPhone SE ni iPhone ya bei nafuu japo bei itakushangaza

Kwa sababu ukilinganisha na simu zingine, iPhone se bado ni simu ya gharama

Simu ina sifa nyingi za iPhone 13

Japokuwa SE imepunguza ubora wa kioo.

Sifa za simu ya Apple iPhone SE(2022)

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g and 5g
Processor(SoC)
  • CPU – Apple A15 Bionic
  • Core Zenye nguvu(2) – 2x 3.223 GHz – Avalanche
  • Core Za kawaida(4) -4x 1.82 GHz – Blizzard
  • Apple GPU
Display(Kioo) Retina IPS LCD
Softawre
  • iOS 15.4
Memori NVMe, 64GB,128GB,256GB na RAM 4GB
Kamera Kamera MOJA

  1. 12MP,PDAF(wide)
Muundo Urefu-4.7inchi
Chaji na Betri
  • 2018 mAh-Li-Ion
  • Chaji-18W
Bei ya simu(TSH) 995,280/=

Upi ubora wa simu mpya ya iPhone SE(2022)?

Simu iPhone SE inatumia processor bora ya simu duniani kwa sasa.

Uimara wa processor unachangia bei yake kuwa juu

Simu hii inatumia memori zenye kasi zaidi kuliko memori za simu ya android

Network ya 5g inakubali spidi ya kasi sana.

Na mtandao wake wa 4g unakubali karibu bands zote duniani.

Hivyo simu inaweza tumika popote

iPhone SE inaweza kutumia mtandao bila laini ya simu.

Huduma hii hupatikana endapo kampuni ya simu ina huduma ya eSim

Network

Simu mpya ya iPhone SE(2022) inaweza kutumia 4G au 5G kuperuzi mtandao.

Jambo la kustahabisha,

5G yake inakubali masafa marefu yenye kasi zaidi.

Ukiona bands za simu zimeandikwa A2783, A2784, A2785 na A2782

Basi hiyo simu inadownload file kwa spidi kubwa zaidi ya 5g

Na upande wa network ya 4G inakubali mitandao yote ya hapa Tanzania

Ubora wa kioo cha iPhone SE(2022)

iPhone SE imetengenezwa kwa kioo cha IPS LCD.

Apple wanakiita Retina IPS LCD

Sifahamu utofauti wa ips ya apple na za simu zingine.

Ila IPS LCD havitoi rangi iliyokolea ukilanganisha na vioo vya Amoled au OLED

Resolution ya SE(2022) ina ubora wa kati

Kutokana na kuwa na ukubwa wa 750 x 1334 pixels

Moja ya kitu kinachokosekana kwenye hii simu ni HDR10

HDR10 hurekebisha muonekano wa rangi wa display na kufanya vitu vionekane kiuhalisia.

Nguvu ya processor Apple A15 Bionic

Mpaka kufikia sasa hakuna chip yoyote ya simu inayofikia Apple A15 Bionic.

Apple A15 Bionic inaizidi kwa kiasi kidogo processor mpya ya Snapdragon 8 gen 1

Matoleo mapya ya simu za samsung s-series zinatumia Snapdragon 8 gen 1

Kiujumla apple a15 bionic ina core sita

Core sita zimegawanyika mara mbili.

Zipo core kubwa na ndogo.

Uwezo wa core kubwa

Core zenye nguvu zipo mbili.

Hizi hufahamika kama Avalanche

Kila core kubwa ina spidi inayofikia 3.223GHz

Ongezeko la spidi limekuza utendaji kwa karibu 8% ukilinganisha Apple 14 ya iPhone 12.

Geekbench inaipla A15 Bionic alama 1739

Wakati Antutu ni 804813

Processor nyingi zilizowahi kufafanuliwa hapa hazifikii alama 800

Chipset mpya ya apple ina utumiaji mzuri wa umeme

Hii inamaanisha ukiwa unacheza gemu kwa masaa mengi mfululizo simu itachelewa kuisha chaji

Uwezo wa core ndogo

Kuna core sita zenye nguvu ndgo.

Hizi ni aina ya processor mahsusi kwa matumizi madogo ya umeme

Kazi ndogo ndogo zinafanyika ndani ya simu hutumia core ndogo

Kila core ina spidi inayofikia 2.0GHz

Na hizi core kwenye iPhone huitwa Blizzard

Uwezo wa betri na chaji

Simu ya iPhone SE 2022 ina betri yenye ujazo mdogo.

Betri yake ni aina ya Li-Ion yenye ukubwa wa 2018mAh

Ukubwa huo wa betri unaweza kujazwa kwa 50% na chaji ya wati 20

Ila hii ni simu inayokaa na chaji muda mfupi

Ukubwa na aina ya memori

Simu nyingi za iPhone huja na memori aina ya NVMe.

NVMe ina spidi ya kasi sana linapokuja swala la kusoma na kuandika faili.

Hivyo data husafirishwa kwa kasi.

Spidi yake kwa maana ya bandwidth inafika 42.7 Gbit/s

Ram za SE 2022 zina ukubwa wa 4GB pekee

Na kuna aina tatu za hii simu upande wa memori 64GB, 128GB na 256GB

Uimara wa bodi ya iPhone SE(2022)

Hii ni simu fupi ya iphone yenye urefu wa inchi 5.4

Urefu unaojaa kwenye mkono

Simu ni ngumu, na maji hayawezi penya kirahisi ikidumbukia kwenye kina cha mita moja

Kwa sababu simu ina viwango vya IP67

Upande wa nyuma na mbele unalindwa kwa vioo

Haijaainishwa aina ya vioo.

Frame za apple iphone se ni za aluminium

Kiujumla bodi ya simu ni imara kwa kiasi chake.

Ubora wa kamera

Kamera ya iPhone se 2022 ipo moja kila upande(mbele na nyuma)

Kamera zinatumia teknolojia ya ulengaji wa moja kwa moja aina ya PDAF.

PDAF si nzuri sana kama dual pixel pdaf ila bado ni teknolojia inayotoa picha nzuri

Video itatokea vizuri tu pale unaporekodi video wakati ukiwa unatembea.

Kwa sababu kamera ina OIS

Ubora wa video

Simu inarekodi aina mbili za video

iPhone se inaweza kurekodi video za 4k na full hd

Uzuri wa kamera hii ni kurekodi video kwa spidi kubwa inayofikia 240fps

Nini maana ya 4k?

4K ni aina ya video ambazo zina pixels 3840(4000) kutoka kushoto kwenda kulia na pixel 2160 kutoka juu kwenda chini.

Pixel ni vinukta vidogo sana ambavyo huwa na mchanganyiko wa rangi tatu

Rangi hizo ni nyekundu, blue na kijani.

Hivyo vinukta(pixel) ndivyo vinavyounda picha unazoziaona kwenye simu, tv nk

Pixels zinapokuwa nyingi zinaunda picha nzuri zaidi.

Ubora wa Software

iPhone SE 2022 inatumia mfumo endeshi wa iOS 15.4

Kwenye iOS 15.4 kuna emoji mpya 38

iPhone se 2022 emoji

Mfumo una face id inayotambua sura hata ukieka barakoa

Baadhi ya simu za android zina face lock yenye ufanisi mdogo

Simu kama redmi note 10 haiwezi kuitambua sura kama mwanga ni mdogo

Zitazame emoji zote za iOS 15.4 : emoji za apple

Bei ya iPhone SE(2022) Tanzania

Bei ya iphone se 2022 inaweza kuzidi 996,000/= kwa Tanzania.

Maduka mengi ya Tanzania wanauza iPhone mpya kwa bei ya juu kidogo

Bei ya hii simu inanunua simu kali ya android kuliko hii

Kuna simu za oppo, samsung, realme, oneplus zenye “premium feature” za kutosha

Yapi Madhaifu ya iPhone SE(2022)

iPhone SE 2022 haijatumia kioo bora cha Super Retina OLED

Simu haina kamera ya telephoto, ultrawide, macro

Apple hawajaweka autofocus ya dual pixel pdaf

Hii simu ni fupi sana kwa watu wengine haiwapi burudani

Simu ina betri ndogo inayokaa na chaji masaa machache

Inaweza ikakulazimu kununua power bank

Simu inakosa sehemu ya kuweka memori card

Neno la Mwisho

Apple ni brand ya simu yenye wapenzi wengi.

Kwa wapenzi wa apple wenye bajeti ndogo simu mpya ya iPhone SE itakupa vitu vingi vinavyopatikana kwenye iPhone zingine.

Lakini kwa wale ambao hawajali kuhusu brandi wanaweza wakaangalia machaguo mengine ya iPhone za zamani au simu mpya za android.

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

iphone 15 pro max camera thumbnail

Ubora wa iPhone 15 Pro Max Upande wa Kamera[hatari tupu]

Apple iPhone 15 Pro Max ni simu yenye kamera tatu upande wa mbele na kamera moja ya mbele (selfie kamera) Ukifuatilia ubora wake wa kamera utagundua sababu ya kuuzwa bei […]

iphone 15 pro max thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro Max na Sifa Zake

Apple iPhone 15 Pro Max ni toleo jipya la iphone kwa mwaka 2023 Ni simu ya kwanza kutoka Apple kutumia chaji aina ya USB Type C ambazo hutumika na simu […]

iphone 15 pro thumbnail

Bei ya iPhone 15 Pro na Sifa Zake Muhimu

Kama ilivyotarajiwa hapo awali kuhusu ujio wa simu mpya za iphone kwa mwaka huu 2023 Moja ya simu hiyo ni iPhone 15 Pro ambayo imeongezewa utendaji Kiumuonekano hauwezi kutofautisha sana […]

iphone 15 muonekano

Ujio wa Simu mpya za iPhone 15 Septemba 2023

Kwenye tarehe 12 mwezi wa tisa 2023 kwenye ukumbi wa Steve Jobs makao makuu ya apple kutakuwa kuna uzinduzi wa bidhaa kutoka kwa kampuni ya apple Tukio hili litarushwa moja […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram