SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

Sifa za kipekee za simu ya Samsung Galaxy A22

Bei Nafuu

Sihaba Mikole

April 2, 2022

Moja ya sifa za kipekee ya simu ya samsung galaxy a22 ni uwezo wa simu kukaa na chaji muda mrefu

Kiukweli ukaaji wa chaji wa Samsung Galaxy A22 unaizidi simu mpya ya samsung galaxy s22 ultra

Simu ina sifa chache nzuri ila zinashawishi kuimiliki

Ni moja ya simu nzruri ya samsung iliyotoka mwishoni mwa mwaka 2021

Sifa zingine hazina upekee mkubwa kiasi cha kwamba inafanya simu kuwa ya kawaida.

Ni simu nzuri ya tabaka la chini kutoka samsung kwa kuangalia ubora wa sifa.

Sifa za Samsung Galaxy A22

Sehemu Za Simu Sifa za Simu
Network 2g, 3g, 4g
Processor(SoC)
  • CPU – MediaTek Helio G80 
  • Core Zenye nguvu(2) – 2×2.0 GHz Cortex-A75
  • Core Za kawaida(6) – 6×1.8 GHz Cortex-A55
  • GPU-Mali-G52 MC2
Display(Kioo) Super AMOLED, Refresh rate:90Hz
Softawre
  • Android 11
  • One UI Core 3.1
Memori eMMC, 128GB,64GB na RAM 6GB,4GB
Kamera Kamera nne

  1. 48MP,PDAF(main)
  2. 8MP(ultrawide)
  3. 2MP(macro)
  4. 2MP(depth)
Muundo Urefu-6.4inchi
Chaji na Betri
  • 5000mAh-Li-Po
  • Chaji-15W
Bei ya simu(TSH) 501,753.78/=

Upi ubora wa Samsung Galaxy A22

Ubora wa kioo cha super amoled ni ubora mkubwa wa samsung galaxy A22

Simu ya samsung galaxy A22 ina utendaji wa kuridhisha kutokana na kuwa na chipset yenye utendaji mkubwa

Betri yake ni kubwa ambayo inakaa na chaji muda mrefu sana.

Ni simu chache za samsung zinaweza kutunza moto muda mrefu kama Galaxy a22

Moja ya kamera yake ina teknolojia ya kutuliza kamera kutikisika

Network

Samsung galaxy a22 inakubali aina zote za mtandao isipokuwa 5G.

4G ya simu ni ya kundi la 7 (lte cat 7)

Spidi ya juu kabisa ya cat7 ya kudownload ni 301.5Mbps ambayo ni sawa na 37.68MBps

Spidi hii inadownload file la ukubwa wa 1300MB kwa sekunde 35, inategemea na aina ya mtandao

Simu hii ya samsung ina network bands za 4G kumi.

Bands hizo ni 1, 3, 5, 7, 8, 20, 28, 38, 40 na 41

Hivyo laini zote za simu zinakubali intaneti ya 4g hapa Tanzania

Ubora wa kioo cha Samsung Galaxy A22

Kioo cha samsung galaxy a22 ni aina ya super amoled.

Resolution ya kioo ni 720 x 1600 pixels

Na uangavu wake unafikia 600nits

600nits huweza kuonyesha vitu vizuri simu ikiwa inatumika juani

Vioo vya amoled vina rangi zinaofikia bilioni moja.

Idadi kubwa ya rangi hufanya kioo kuonyesha rangi za vitu kwa usahihi wa juu

Ila resolution ya hii simu ni ya kawaida

Bei ya kioo cha samsung aina ya super amoled ni gharama, kuwa makini utumiapo simu

Nguvu ya processor MediaTek Helio G80

Processor ya MediaTek Helio G80 ndio ubongo wa Samsung galaxy a22.

Ni processor yenye core nane(octacore)

Core zenye nguvu zipo mbili na zenye nguvu ndogo zipo sita.

Chip ya helio g80 ina utendaji wa wastani kwenye simu nyingi zinazotumia hii processor

Hilo linatokana na namna core zilivyoundwa

Uwezo wa core zenye nguvu kubwa

Kila core yenye nguvu ina spidi inayofikia 2.0GHz

Core zenye nguvu za Helio g80 zimeundwa kwa kutumia Cortex A75

Cortex A75 inaweza kusukuma gemu nyingi unazozifahamu kiurahisi

Kwa sasa utendaji wa Cortex A75 unazidiwa na Cortex A77 ambao una matumizi mazuri ya umeme

Kiujumla muundo huu unakuwezesha kucheza gemu la Mobile Legends: Bang Bang kwa spidi ya 57fps kwa resolution kubwa

Ni core zenye kasi kubwa

Uwezo wa core zenye nguvu ndogo

Core zenye nguvu ndogo zimeundwa kwa kutumia muundo wa Cortex A55

Cortex A55 inatumia umeme mdogo sana pale simu inpofanya kazi ndogo ndogo.

Kama unapenda kupiga simu tu simu inakaa na chaji muda mrefu

Kila core ina kasi ya 1.8GHz

Cha kufurahisha Cortex A55 ina utendaji mkubwa kidogo ukilinganisha na cortex a53 iliyopo kwenye simu ya Nokia G20 yinayotumia chip ya simu ya Helio g35

Alama za antuntu na geekbanch

antuntu na geekbench hizi ni app zinazopima uwezo wa processor za simu

Processor ya Helio G80 inachuana na snapdragon 680 4g kwenye alama za antuntu n geekbench

Chip ya Helio g80 ina alama 353 kwenye core moja(geekbench)

Wakati Antutu inaonyesha alama 66,889

Kwa kuzingatia hizo point Helio g80 inazidiwa na Snapdragon 680 iliyopo kwenye simu ya Samsung galaxy A23

Uwezo wa betri na chaji

Betri ya samsung galaxy a22 ina ukubwa wa 5000mAh

Na chaji yake inapeleka umeme wa wati 15

Kiasi hiki cha umeme kinajaza betri si chini ya masaa mawili

Betri yake infanya simu kukaa na chaji masaa 121 simu ikiwa imetulia (gsmarena)

Kwa mujibu wa GSMarena Samsung galaxy a22 inakaa na chaji masaa 17 simu ikiwa inatumia intaneti yaani data ikiwa ON masaa yote

Ukubwa na aina ya memori

Samsung galaxy a22 inatumia memori aina ya eMMC.

Kasi ya eMMC ni ndogo ukilinganisha na memori aina ya UFS

Na aina ya ram iliyotumika ni LPDDR4x zinazotumia umeme mdogo kusafirisha data

Zipo aina tatu za simu ya samsung galaxy a22

  • 128GB ROM na 4GB RAM
  • 128GB ROM na 6GB RAM
  • 64GB ROM na 4GB RAM

Bei ya simu inatofautiana kulingana na ukubwa wa memori

Uimara wa bodi ya Samsung Galaxy A22

Bodi ya simu imeundwa kwa plastiki upande wa pembeni na nyuma.

Ina ulinzi wa kioo lakini sio aina ya gorilla

Simu ni nzito kidogo kwa maana ina gramu 186

Ina urefu wa inchi 6.4 na inajaa kwa kiasi kikubwa kwenye mkono

Bodi za plastiki zina changamoto ya kuchunika rangi

Hivyo utahitaji kava ya simu kuzuia hilo

Ubora wa kamera

Simu ya samasung galaxy a22 ina kamera nne.

Katika kamera nne inakosekana aina moja ya kamera ya Telephoto

Kama ni kuzoom simu itategemea app ya kamera

Kamera kuu ina OIS ambayo inafanya video kutotikisika kutokana na kutisika kwa mkono

Ubora wa picha

Ubora wa picha zinazopigwa na samsung galaxy a23 si wa kuvuitia.

Ukipitia baadhi ya picha kutoka samsung galaxy a23 za gsmarena utaona kamera haipigi picha nzuri usiku.

Wakati wa usiku kamera inazalisha picha zenye texture mbaya

Noise(vichengachenga) zinaonekana kwa wazi ukiizoom picha kiogo

Ubora wa rangi ni mzuri kwa kiasi kikubwa wakati wa mchana

Ubora wa video

Kamera za hii simu zinaweza kurekodi video za aina moja.

Ukiwa unachukua video kwa kutumia galaxy a22 utapata video za full hd kwa spidi ya 30fps

Haiwezi kurekodi video za 4k na 8k zenye resolution kubwa zaidi.

Spidi ya 30fps si nzuri sana hasa ukiwa unarekodi kitu kinachokimbia kwa kasi

Ubora wa Software

Samsung a22 inakunaja na android 11 na One UI Core 3.1

Software ya One Ui 3.1 ina video call inayoruhusu kuweka ukungu(brul) kwenye background

Kuna onegezeko la video effects kwa simu za video

Mtumiaji wa simu anaweza pia kuondoa data zinazoonyesha eneo wakati wa kupiga picha

One ui inaweza kuchuja mwanga wa blue ambao huumiza macho

Bei ya Samsung Galaxy A22 Tanzania

Kwa baadhi y maduka kariakoo bei ya samsung a22 inafika 520,000 kwa samsung ya 64GB

Na kwa samsung a22 ya 128GB bei inafika shilingi 580,000/=

Kuna simu aina ya redmi zenye kamera na chip bora zaidi za dimensity zinazopatikana chini ya 500,000

Simu ya vivo t1 5g ina nguvu kuliko galaxy a22

Lakini bei ya vivo t1 5g haifiki 500,000/=

Yapi Madhaifu ya Samsung Galaxy A22

Samsung galaxy a22 haina viwango vya IP ratings vinavyoainisha uwezo wa simu kuzuia maji na vumbi

Kamera zake hazitoi picha nzuri nyakati za usiku kwenye mwanga mdogo

Bei yake ni kubwa ukilinganisha na ubora wa simu

Kioo chake kina resolution ndogo

Spidi ya juu ya 4g sio kubwa sana

Neno la Mwisho

Samsung galaxy a22 ni simu inayokaa na chaji muda mrefu sana

Kwa mtumiaji anayetumia intaneti sana hii simu itamsaidia pakubwa.

Hautakuwa na haja ya kuchaji mara kwa mara.

Kwa hilo na kioo cha amoled basi galaxy a22 ni ya kuimiliki

Lakini kama unazingatia utendaji na ubora wa kamera galaxy a22 haitokufaa

 

Maoni 2 kuhusu “Sifa za kipekee za simu ya Samsung Galaxy A22

Maoni na Maswali

Email yako haitochapishwa, kwenye alama * lazima pajazwe ili ukomenti

Fuatilia Zaidi

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A15 na Sifa Muhimu

Mwezi wa desemba 2023 ni mwezi ambao Simu ya Samsung Galaxy A15 ilizinduliwa Ni simu ya daraja la kati ambayo ina vitu vichache vinavyopatikana kwenye samsung za bei kubwa Ndio […]

No Featured Image

Bei ya Samsung Galaxy A55 na Ubora wake

Samsung Galaxy A55 imetoka mwezi machi mwaka 2024 na ni simu ya daraja la kati Bei ya Samsung Galaxy A55 kwa Tanzania ni shilingi milioni moja na laki moja na […]

thumbnail

Bei ya Samsung Galaxy A35 na Sifa zake

Samsung Galaxy A35 ni toleo jipya la samsung lilotoka mwezi machi 2024 Ni simu ya daraja la kati iliyochota baadhi ya sifa muhimu kutoka kwenye galaxy yenye bei kubwa Ndio […]

simu mpya

Simu mpya kali 20 na bei zake kwa mwaka 2024

Hii ni orodha ya simu mpya ambazo zimetoka mwaka 2024 ama mwishoni mwa mwaka 2023 kutoka kwa kampuni zipatazo 11 Ni orodha inayohusisha simu za daraja la kati na la […]

SimuNzuri

Zigundue Sifa Za Simu Bora Kiundani

E-mail : simunzuriblog@gmail.com

Simu: +255 683 420 543

Whatsapp: +255 756 077 262

Kabila, Magu

Mwanza, Tanzania

Company

Find Us On

FB Twitter Instagram